Dawa za kulevya: Viongozi wa dini sasa wajisalimisha; Wakiri kufanya biashara hiyo muda mrefu

Viongozi wa dini sasa wajisalimisha

*Wakiri kufanya biashara hiyo muda mrefu
*Watoa ushuhuda mbele ya kamati ya maadili

Na Mwandishi wa Jeshi la Polisi, Zanzibar

VIONGOZI sita wa madhehebu ya dini ambao wanajihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya nchini, wamejitokeza mbele ya Kamati ya Maadili ya Viongozi wa
Dini na Haki za Jamii na kukiri kujihusisha na biashara hiyo kwa muda mrefu sasa.

Ofisa Uhusiano wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Inspekta Mohammed Mhina, amesema baada ya viongozi hao kuhojiwa, waliiomba kamati hiyo kutowataja hadharani au madhebebu yao wakihofia kubezwa.

Akizungumza mwishoni mwa ziara yao visiwani humo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mchungaji William Mwamalanga wa Kanisa la Pentekosti Tanzania, alisema orodha hiyo na wengine 18 wakiwemo wafanyabiashara wakubwa na wanasiasa ambao wanajihusisha na biashara hiyo, itafikishwa kwa Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Dawa za Kulevya nchi.

Mchungaji Mwamalanga alisema ongezeko la dawa za kulevya nchini pia linazihusu nchi mbalimbali duniani ambapo kamati hiyo itakutana na kamati nyingine kama hizo za nchi za Maziwa Makuu kuzungumzia ufumbuzi wa tatizo hilo.

“Mkutano huu pia utapendekeza wabunge wa nchi hizo na Bunge la Afrika ya Mashariki, kutunga sheria za kuwafilisi wale wote waliojilimbikizia mali kutokana na biashara ya dawa za kulevya kwa nchi wanachama,” alisema Mchungaji Mwamalanga na kupongeza juhudi za Jeshi la Polisi kukabiliana na ongezeko la dawa hizo.

Akizungumzia kero ya dawa za kulevya visiwani hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, ACP Aziz Juma Mohammed, alisema kuwa jeshi hilo limekuwa likiwakamata wafanyabiashara na watumiaji wa dawa hizo na kuwafikisha mahakamani.

Kamanda Mohammed ametoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali wa usalama, kusaidiana na jeshi hilo kwa kutoa taarifa za wale wanaojihusisha na mtandao wa dawa hizo.

Wiki iliyopita watu wawili wakazi wa Dar es Salaam, walikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar kwa nyakati tofauti wakitokea nchini Brazil ambapo kila mmoja alipatikana na kiasi kikubwa cha madawa ya kulevya aina ya Cocaine.

Wataje au ondoa uchafu jamvini. Akina RACHEL wanateswa sana. Kila mmoja ana haki yake hakuna cha kiongozi wa--------
 
Mpaka hapo watakapotajwa hadharani na kufikishwa kwenye vyombo vya dola habari hii ni UDAKU tu!! Kwani wanaficha majina yao kwa faida ya nani?
 
kiongozi wa dini ni binadamu, dini ni imani hatuabudu binadamu, kama kiongozi wa dini anahusika atajwe coz kumficha ni kwamba atawaharibu na waumini wake wenye kuangalia mtu kwa ushawishi [mzazi alimfuata yesu aende kumponya mwanae, yesu alisema hakuna kinachoniudhi kama hiki kizazi kilichokosa imani, yesu aliwapa uwezo wanafunzi wake kuponya na kuna siku mtoto alikuwa akiumwa sana na hapo ndipo wanafunzi wa yesu walimwombea lkn mtoto hakupona coz waliamini ni yesu pekee anayeweza kuponya] kwa ushawishi

Kwa kuwa JK ni Rais Muislam hatoweza kuwataja majina hao wauza wa unga wa Kichungaji wa Kikiristo kwa sababu kutakuwa na conflict ambayo kuna watu watachukulia kama anawaonea kwa kutumia njia ya dini. Ndiyo maana pale alipotoa hotuba kwa Mapadre na akawaambia kwamba kuna Mapadre ambao wanauza unga, kuna watu fulani wakamuona kama ni mdini.
 
Nchi imevamiwa na wauza unga. Sasa kama viongozi wa dini wanauza unga, je watu wanaokwenda kufanya hiyo ibada itakuwaje?
 
Hao Viongozi wa dini kama wanafanya hiyo biashara basi ujue wao ni kivuli tu,wahusika wakubwa watakuwa ni viongozi wa kubwa wa Serikali,na ndiyo sababu hawathubutu kuwapeleka mahakamani kwani wakifanya hivyo wataumbuka,hayana tofauti na yale ya EPA,uliona wapi katika nchi hii muhalifu akashauriana na Polisi!!! Aibu tupu.
 
Hao Viongozi wa dini kama wanafanya hiyo biashara basi ujue wao ni kivuli tu,wahusika wakubwa watakuwa ni viongozi wa kubwa wa Serikali,na ndiyo sababu hawathubutu kuwapeleka mahakamani kwani wakifanya hivyo wataumbuka,hayana tofauti na yale ya EPA,uliona wapi katika nchi hii muhalifu akashauriana na Polisi!!! Aibu tupu.

Kama viongozi wa dini wataweza kutumiwa na serikali kuuza unga, nani aliebakia tumuamini sasa? Hii inaonesha kuwa nchi imejaa Wauza Unga kila sehemu.
 
Wataje au ondoa uchafu jamvini. Akina RACHEL wanateswa sana. Kila mmoja ana haki yake hakuna cha kiongozi wa--------

Sasa uchafu unaozungumzia wewe uko wapi hapa? sasa ukweli ndiyo huo. Hawa viongozi wa dini wanatumia mwanya kuuza madawa ya kulevya. Wanatumia hizo hela kujenga shule za Saint, Makanisa. Sasa wewe huoni kwamba hilo ni tatizo?
 
Mpaka hapo watakapotajwa hadharani na kufikishwa kwenye vyombo vya dola habari hii ni UDAKU tu!! Kwani wanaficha majina yao kwa faida ya nani?

Majina yao tayari yanajulikana, ndiyo maana wameamua kujisalimisha wenyewe.
 
Hakuna viongozi wa dini waliojisalimisha, kama ingekuwa kweli basi mjina yangewekwa hadharani, huu ni usanii wa Vasco da Gama ili watu waamini madai yake ya mwanzo!
 
Ninawasiwasi na mwenyekti asije akatajwa!!!!!!! hivi akitajwa anavuliwa apishe uchunguzi au!!!!
 

Ofisa Uhusiano wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Inspekta Mohammed Mhina, amesema baada ya viongozi hao kuhojiwa, waliiomba kamati hiyo kutowataja hadharani au madhebebu yao wakihofia kubezwa.

Naweza sasa kuona scenario katika mahakama zetu mbakaji wa kitoto kidogo akijitetetea "Mheshimiwa hakimu naomba uniachie huru ili wakwe zangu wasije wakajua wakaninyima binti yao maana nina miezi 4 kabla ya arusi yangu" Mheshimiwa hakimu anasema "kwa hoja hiyo muhimu ya kukwepa kuvunja uchumba ninakuachia bila masharti"
 
Hakuna viongozi wa dini waliojisalimisha, kama ingekuwa kweli basi mjina yangewekwa hadharani, huu ni usanii wa Vasco da Gama ili watu waamini madai yake ya mwanzo!

Vipi ile kauli ya polisi? Hawa jamaa wamejisalimisha kwa kuuza unga. Jamii yetu inatakiwa ipinge vikali kuhusu hawa viongozi wa dini wanaouza unga Makanisani, hii ni aibu kwa taifa.
 
MIMI NINAULIZA.

1) Je hii habari ya ukweli au la?

2) Kama ni ya uongo na ni siasa; ni nani mkosa? Mhariri, Polisi?

3) JK anahusika vipi na hii?

Naomba majibu yatakoyonielimisha hayo maswali yangu.
 
Majina yao tayari yanajulikana, ndiyo maana wameamua kujisalimisha wenyewe.

Kama yanajulikana kwa nini hawatajwi? Kwa nini hawajakamatwa na kushitakiwa? Wanaficha majina yao kwa faida ya nani? Ni lini nchi hii tumeanza kuwa na sheria ya kuficha wahalifu eti "kulinda" heshima yao ktk jamii? Hakuna kitu hapo...USANII mtupu!!
 
Sasa hapo siasa juu ya siasa ipo wapi? JK aliposema ukweli kuhusu viongozi wa Kanisa wanafanya biashara ya madawa ya kulevya, watu wa hiyo dini walimuona anaowaonea, sasa ukweli ndiyo huo. Leo tunajua hela za kujenga shule za Saint zinapotoka.
Lakini bado nashangaa kwa nini hizo shule zinaendelea kuitwa Saint wakati zimejengewa na hela za madawa ya kulevya!!


Una agenda ya UDINI-harufu naiona katika mawazo yako. Hoja ya msingi ilikuwa jk awataje na kuwachukulia hatua. hakuna mtu aliyejuu ya sheria 'awe ni sheikh, mchungaji, askofu, mbunge, au waziri'. mkuu wa nchi hapaswi kuogopa, maana tumempa mamlaka sisi atwange wala asiogope. Hiyo ndo hoja iliyopaziwa sauti na watu wengi, wakiwemo viongfozi wa dini!!!!
 
Muuzaji wa madawa ya kulevya ni mhalifu tu kama wahalifu wengine na hakuna haja ya kumfichia siri pale anapokamatwa na kukiri makosa yake. Utaratibu mzuri ni kuwafungulia mashtaka mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake. Na hili halibagui viongozi wa dini, watumishi wa serikali, wanasiasa, wafadhili wa chama na yeyote atakayefanya biashara hii kwani wote ni wahalifu. Sioni sababu ya Polisi kujadiliana na wahalifu na kukubaliana kuwa wasiwataje majina yao na ya makanisa wanayoyaongoza. Makubaliano haya hayana tofauti na makubaliano kati ya serikali na wezi wa fedha za EPA walioruhusiwa kurudisha kimyakimya fedha walizoiba bila ya kuchukuliwa hatua zozote za kisheria. Kwa ufupi anayevunja sheria na anayemsaidia mhalifu kuficha uhalifu wake wote ni wakosaji hata kama mmoja wao ni polisi.
 
Kwa mtazamo wangu mtu hawezi kuendelea kuwa kiongozi wa dini anapoanza kufanya biashara haramu kama ya kuuza madawa ya kulevya. Mara anapoanza kufanya biashara hiyo anakuwa mhalifu wa sheria na anatakiwa ashughulikiwe kama mhalifu wa sheria na siyo kama kiongozi wa dini. Hivyo kuendelea kutangaza kuwa viongozi wa dini wanafanya biashara kunahalalisha biashara yenyewe hasa kwa wafuasi na waumini wa viongozi hao. Kwani kuna uwezekano wa waumini na wafuasi wao kuamini kuwa maadamu kiongozi wao anafanya biashara hiyo na hachukuliwi hatua basi siyo kosa kuifanya.
 
Watu wanaweza kusema mengi, lakini nadhani matatizo yote haya yameletwa na serikali hasa kuchukua misingi mibovu iliyopo ndani ya ccm. Nasema hivi kwa sababu, seheria za nchi haziangalii cheo chochote cha mtu au nafasi yake kumpa nafasi ya kutenda uhalifu. "Hakuna nafasi kabisa kuwa atavua gamba". Sio kweli kuwa mwizi atapalekwa tu kwenye sheria andapo ni mtu mdogo ("minor"). Hii imedhihirika sana sehemu nyingi, na bahati mbaya hata wahanga wa wananchi kujichukulia sheria mkononi ni hawa hawa wasiokuwa na nafasi (say) ndani ya jamii. Kweli leo hii hao wanaoitwa majina yote mabaya kwa kulifikisha taifa hapa, wananchi wasingekuwa wamechukua sheria mikononi juu yao? Sasa hii janja ya ccm na serikali yake kutokusimamia haki ndio inayoifikisha nchi mahali pabaya, na matokeo yake kutafuta visingizio vya kipuuzi kama hivi vya kuotojana na wala kutowafikisha mbele ya vyombo vya seheria. Ieleweke, MHALIFU NI MHALIFU TU, bila kujali wadhifa wake au nafasi yake ndani ya chombo chochote cha kiserikali au kijamii.

Hizi double standards zitaisha lini? ndizo zinazolimaliza taifa hili! Shule kuanzai chakechea, afya, polisi, mahakama n.k ni double double, sasa hata makanisa na misikiti naona navyo vitakuwa double double
 
JF siku zote naiaminia sana kwa kuwahi kupa correct info, ivi kwa hili la majina ya drug dealer limeshindikanaje? kwanini majina hayabandikwi hapa? tukisubiri seriakli iyataje naona itachukua karne, tuifanye ilazimike kuyataja kwa wao kujikuta tayari jamii na media zinayataja.
 
Sasa uchafu unaozungumzia wewe uko wapi hapa? sasa ukweli ndiyo huo. Hawa viongozi wa dini wanatumia mwanya kuuza madawa ya kulevya. Wanatumia hizo hela kujenga shule za Saint, Makanisa. Sasa wewe huoni kwamba hilo ni tatizo?
Wewe term 'viongozi wa dini' unaichukuliaje? Kwamba ni WAKRISTO bila shaka! Katika hilo you're DEAD WRONG, mkuu.
 
Back
Top Bottom