oba
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 310
- 65
Nimekuwa nikifuatilia mijadala mbalimbali juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuwa Tanzania na kugundua kuwa japo muungano ni mzuri na wa kudumishwa kwa nguvu zote una mapungufu.
Mapungufu hayo yamezua hoja nyingi na kupelekea wengine kupendekeza muungano uvunjwe. Mapungufu hayo ni pamoja na lile la kuwa na serikari ya zanzibar na ile ya muungano bila kuwa na serikali ya Tanganyika, iweje nyumba ijengwe ndani ya nyumba nyingine?iweje kuwe na serikari huru ndani ya serikari nyingine?
Maoni yangu ni kuwa, muungano ni mzuri na unapaswa kudumishwa; sikubaliani na hoja ya kuuvunja!napendekeza mabadiliko ya muundo wa muungano yatakayovunja serikari ya mapinduzi ya Zanzibar na kuwa na kuwa na serikali moja tu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Jamhuri igawanywe katika majimbo; pemba liwe jimbo, unguja liwe jimbo na bara igawanywe kwenye majimbo kama itakavyoonekana kuwa bora
Kila jimbo liwe na utawala wa ndani chini ya gavana na mabunge ya majimbo kwa ajili ya kuendesha serikari za majimbo.
Kuwe na central government itakayoongozwa na raisi wa jamhuri, iwe na wizara nne; wizara ya ulinzi, mambo ya nje, fedha na mambo ya ndani. Kuwe na bunge la muungano lenye wajumbe kutoka kila jimbo. HAPO MUUNGANO WETU UTADUMU.
Hayo yote yanawezekana kama yatajumuishwa kwenye katiba mpya.
Naomba kuwasilisha! I stand to be corrected.
Mapungufu hayo yamezua hoja nyingi na kupelekea wengine kupendekeza muungano uvunjwe. Mapungufu hayo ni pamoja na lile la kuwa na serikari ya zanzibar na ile ya muungano bila kuwa na serikali ya Tanganyika, iweje nyumba ijengwe ndani ya nyumba nyingine?iweje kuwe na serikari huru ndani ya serikari nyingine?
Maoni yangu ni kuwa, muungano ni mzuri na unapaswa kudumishwa; sikubaliani na hoja ya kuuvunja!napendekeza mabadiliko ya muundo wa muungano yatakayovunja serikari ya mapinduzi ya Zanzibar na kuwa na kuwa na serikali moja tu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Jamhuri igawanywe katika majimbo; pemba liwe jimbo, unguja liwe jimbo na bara igawanywe kwenye majimbo kama itakavyoonekana kuwa bora
Kila jimbo liwe na utawala wa ndani chini ya gavana na mabunge ya majimbo kwa ajili ya kuendesha serikari za majimbo.
Kuwe na central government itakayoongozwa na raisi wa jamhuri, iwe na wizara nne; wizara ya ulinzi, mambo ya nje, fedha na mambo ya ndani. Kuwe na bunge la muungano lenye wajumbe kutoka kila jimbo. HAPO MUUNGANO WETU UTADUMU.
Hayo yote yanawezekana kama yatajumuishwa kwenye katiba mpya.
Naomba kuwasilisha! I stand to be corrected.