makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Wana JF na Watanzania wenzangu,
Naandika kwa uchungu sana topic hii. Kwamba hapa tulipofikia sasa lazima Watanzania TUSEME ENOUGH IS ENOUGH na tuchukue hatua kama ndugu zetu wa Tunisia walivyoamua juzi kwa KUFANYA MAANDAMANO NCHI NZIMA KUPINGA UTAWALA WA KIFISADI NA KIUONEVU WA DIKTETA BEN ALI AMBAYE KWA SASA AMEIKIMBIA NCHI.
Tanzania ya sasa ilipofikia hakuna tofauti na yale yaliyokuwa yakifanyika Tunisia. Kwamba DIKTETA BEN ALI alikuwa ameigeuza nchi kuwa ni sehemu yake BIASHARA na kujitajirisha. Aliingia kwa mbwembwe nyingi huku akisaidiana na Mkewe na kuanzisha sera ya ubinafishaji. Kwa kutumia sera hii aliweza kubinafsisha na kuuza Mashirika ya umma na Makampuni ya Serikali HUKU YEYE NA MKEWE AIDHA WAKIJIUZIA AU KUCHUKUA HISA KUBWA KWENYE MASHIRIKA AU MAKAMPUNI HAYO.Kama alivyofanya MKAPA na vigogo wenzake akiwa madarakani.
Hali hii ilipelekea hali ya uchumi wa nchi kudorora na hivo kupelekea hali za kimaisha na kiuchumi za Wananchi wengi wa Tunisia kuwa ngumu sana! Kupanda kwa gharama za maisha na ukosefu wa ajira kwa vijana wengi wanaomaliza vyuo vikuu na vyuo vya kati. Ukosefu wa ajira miongoni mwa wa TUNISIA hasa graduates uliwalazimisha kuanza biashara za kubangaiza ikiwemo umachinga!.
Ni kijana mhitimu wa chuo kikuu(graduate)aliyekuwa akifanya biashara ya kuuza mboga za majani mitaani ndiye aliyewasha MOTO WA MAANDAMANO YA NCHI NZIMA hatimaye kupelekea kung'olewa kwa Dikteta Ben Ali. Graduate huyu tayari ni marehemu kwa sasa LAKINI YEYE ATABAKIA KUWA SHUJAA(HERO)KATIKA MAISHA YA WA TUNISIA WOTE KWA MAANA YEYE NDIYE AMEKUWA MWANZILISHI WA UKOMBOZI WA NCHI NZIMA. Habari zinasema Polisi walimvamia mitaani akiuza mboga zake na kumunyang'anya bidhaa na meza yake. Uamuzi aliochukua ilikuwa KUJIUA kupinga manyanyaso ya polisi wa Ben Ali. Huo ukawa ndiyo mwanzo wa maandanano na mapambano na polisi.
Ukiangalia kwa undani utagundua kwamba yale yaliyotukia TUNISIA na yanayotukia TANZANIA kwa sasa hakuna tofauti. CCM hawana tofauti na chama cha Ben Ali kinachoitwa CDR(Constitutional Democratic Rally). Kama sera za Ubinafsishaji CCM awamu ya Mkapa walitia fora na wameendelea kutia fora kwa KUBINAFSISHA KILA kitu.Ilifikia mahali mpaka wakaanza kubezwa kuwa watabinafsisha mpaka magereza! Ukosefu wa ajira kwa vijana wanaomaliza vyuo vikuu inatisha.Hali za maisha kwa Watanzania zinazidi kuwa ngumu kila siku iendayo kwa Mungu. Bei ya Umeme JUU,bei ya PETROLI na DIZELI iko juu. THAMANI YA SHILINGI inazidi kuporomoka!! CCM iko likizo inakula kuku!
Serikali ya CCM imeshindwa kutatua kero hata moja kati ya zote hizi kwa kisingizio kuwa haina pesa. Wakti serikali ikidai haina pesa tunashuhudia Tshs.Bilioni 94/- tayari zinafanyiwa mchakato wa kulipwa kwa Kampuni hewa ya DOWANS tena kwa nguvu au lazima. CCM wameshindwa KUJALI AU KUSIKILIZA MALALAMIKO YA WANANCHI AMBAO NDIYO WENYE FEDHA kwa maana ya WALIPA KODI. Hii ni dharau kwa WANANCHI waliowapa ridhaa ya kuwaongoza. Huu ni uhuni!
Kama hili la DOWANS halitoshi CCM vilevile wameziba masikio kwa makusudi kuhusiana na KUPANDA KWA GHARAMA ZA UMEME. Serikali imetia pamba masikioni kana kwamba haisikii wala haielewi kuwa KUPANDISHA KWA GHARAMA ZA UMEME KWA 18% kutapandisha gharama za kila kitu kwa maana umeme ndiyo chanzo cha uzalishaji wa bidhaa kwa maana ya vyakula,mavazi,vipuri,vifaa vya nyumbani n.k vyote vinatoka viwandani.
Kuna hili la MAUAJI YA WATU 3 WASIOKUWA NA HATIA HUKO ARUSHA. CCM kupitia CC yao hawakutoa tamko lenye kutoa mwelekeo wa kumaliza mgogoro huo!. Badala yake wametumia ubabe na udikteta ule ule wa kusema anayeona uchaguzi haukuwa halali aende mahakamani. Hii ni jeuri ya chama cha CCM! Kwa CCM watu kupoteza maisha kwa mgogoro huo ni sawa tu maana walishinda kihalali. This is purely dictatorship ruling.
Kwa kuhitimisha hebu niseme hivi.Kwama CCM kinathibitisha kuwa kimegeuka kuwa chama cha KIDIKTETA. Kwamba CCM kwa sasa hakitaki kusikia MAONI wala USHAURI kutoks kwa VIONGOZI,WANACHAMA na WANANCHI kwa ujumla! Inashangaza CCM kupitisha uamuzi wa kuwalipa Kampuni hewa ya Dowans wakti kuna Mawaziri ndani ya CCM wameshauri Dowans wasilipwe! Kuna vijana wa CCM-UVCCM wametoa tamko kuhusu Dowans kuwa wasilipwe! CCM wamepuuza maoni na ushauri huo. M/kiti Kikwete anajifanya kuweka pamba masikioni wakti ukweli wote anaujua kuhusu Dowans.
Kitu ambacho ni dhahiri hapa ni kwamba CCM WALITUMIA MABILIONI YA SHILINGI WAKTI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU 2010. KWAMBA WALIKOPA AU WALIFADHILIWA HIYO PESA NA MTU KAMA ROSTAM AZIZ-RA. Kwa hiyo wanachofanya kwa sasa ni kutafuta PESA KWA NGUVU HATA KAMA NI KWA KUIBA,KUUA,KUDHULUMU au KUWABEBESHA MZIGO WATANZANIA ili wawalipe waliowakopesha au kuwafadhili kwenye Uchaguzi Mkuu. Hivi unafikiri gharama ya zile Helikopta 2 zilizokuwa zinamsafirisha Dikteta Kiwete wakti wa kampeni zilitoka wapi???Yale mabango yaliyotapakaa kila kona ya nchi hii nani aliyagharamia???Ni wazi kuwa MALIPO YA DOWANS NI KULIPIA GHARAMA HIZO ZA CCM. Huo ndiyo ukweli.
CCM wameshindwa kusoma alama za nyakati. Wameshindwa kupata somo kutoka TUNISIA. Kwa hili la DOWANS CCM wamejichimbia shimo jingine la kifo. Hizi Bilioni 94 zitawa-cost kisiasa huku mbeleni. It is gonna determine their political destiny. Kukataa ushauri,maoni,mawazo ya watu unaowaongoza ni tabia ya vijiserikali vya KIFISADI na KIDIKTETA. Hapa ndipo walipotufikisha CCM. Dawa yake ni kung'olewa kwa MAADAMANO YA KUSHINIKIZA NCHI NZIMA.
Mungu ibariki Tanzania.
Nawasilisha.
Naandika kwa uchungu sana topic hii. Kwamba hapa tulipofikia sasa lazima Watanzania TUSEME ENOUGH IS ENOUGH na tuchukue hatua kama ndugu zetu wa Tunisia walivyoamua juzi kwa KUFANYA MAANDAMANO NCHI NZIMA KUPINGA UTAWALA WA KIFISADI NA KIUONEVU WA DIKTETA BEN ALI AMBAYE KWA SASA AMEIKIMBIA NCHI.
Tanzania ya sasa ilipofikia hakuna tofauti na yale yaliyokuwa yakifanyika Tunisia. Kwamba DIKTETA BEN ALI alikuwa ameigeuza nchi kuwa ni sehemu yake BIASHARA na kujitajirisha. Aliingia kwa mbwembwe nyingi huku akisaidiana na Mkewe na kuanzisha sera ya ubinafishaji. Kwa kutumia sera hii aliweza kubinafsisha na kuuza Mashirika ya umma na Makampuni ya Serikali HUKU YEYE NA MKEWE AIDHA WAKIJIUZIA AU KUCHUKUA HISA KUBWA KWENYE MASHIRIKA AU MAKAMPUNI HAYO.Kama alivyofanya MKAPA na vigogo wenzake akiwa madarakani.
Hali hii ilipelekea hali ya uchumi wa nchi kudorora na hivo kupelekea hali za kimaisha na kiuchumi za Wananchi wengi wa Tunisia kuwa ngumu sana! Kupanda kwa gharama za maisha na ukosefu wa ajira kwa vijana wengi wanaomaliza vyuo vikuu na vyuo vya kati. Ukosefu wa ajira miongoni mwa wa TUNISIA hasa graduates uliwalazimisha kuanza biashara za kubangaiza ikiwemo umachinga!.
Ni kijana mhitimu wa chuo kikuu(graduate)aliyekuwa akifanya biashara ya kuuza mboga za majani mitaani ndiye aliyewasha MOTO WA MAANDAMANO YA NCHI NZIMA hatimaye kupelekea kung'olewa kwa Dikteta Ben Ali. Graduate huyu tayari ni marehemu kwa sasa LAKINI YEYE ATABAKIA KUWA SHUJAA(HERO)KATIKA MAISHA YA WA TUNISIA WOTE KWA MAANA YEYE NDIYE AMEKUWA MWANZILISHI WA UKOMBOZI WA NCHI NZIMA. Habari zinasema Polisi walimvamia mitaani akiuza mboga zake na kumunyang'anya bidhaa na meza yake. Uamuzi aliochukua ilikuwa KUJIUA kupinga manyanyaso ya polisi wa Ben Ali. Huo ukawa ndiyo mwanzo wa maandanano na mapambano na polisi.
Ukiangalia kwa undani utagundua kwamba yale yaliyotukia TUNISIA na yanayotukia TANZANIA kwa sasa hakuna tofauti. CCM hawana tofauti na chama cha Ben Ali kinachoitwa CDR(Constitutional Democratic Rally). Kama sera za Ubinafsishaji CCM awamu ya Mkapa walitia fora na wameendelea kutia fora kwa KUBINAFSISHA KILA kitu.Ilifikia mahali mpaka wakaanza kubezwa kuwa watabinafsisha mpaka magereza! Ukosefu wa ajira kwa vijana wanaomaliza vyuo vikuu inatisha.Hali za maisha kwa Watanzania zinazidi kuwa ngumu kila siku iendayo kwa Mungu. Bei ya Umeme JUU,bei ya PETROLI na DIZELI iko juu. THAMANI YA SHILINGI inazidi kuporomoka!! CCM iko likizo inakula kuku!
Serikali ya CCM imeshindwa kutatua kero hata moja kati ya zote hizi kwa kisingizio kuwa haina pesa. Wakti serikali ikidai haina pesa tunashuhudia Tshs.Bilioni 94/- tayari zinafanyiwa mchakato wa kulipwa kwa Kampuni hewa ya DOWANS tena kwa nguvu au lazima. CCM wameshindwa KUJALI AU KUSIKILIZA MALALAMIKO YA WANANCHI AMBAO NDIYO WENYE FEDHA kwa maana ya WALIPA KODI. Hii ni dharau kwa WANANCHI waliowapa ridhaa ya kuwaongoza. Huu ni uhuni!
Kama hili la DOWANS halitoshi CCM vilevile wameziba masikio kwa makusudi kuhusiana na KUPANDA KWA GHARAMA ZA UMEME. Serikali imetia pamba masikioni kana kwamba haisikii wala haielewi kuwa KUPANDISHA KWA GHARAMA ZA UMEME KWA 18% kutapandisha gharama za kila kitu kwa maana umeme ndiyo chanzo cha uzalishaji wa bidhaa kwa maana ya vyakula,mavazi,vipuri,vifaa vya nyumbani n.k vyote vinatoka viwandani.
Kuna hili la MAUAJI YA WATU 3 WASIOKUWA NA HATIA HUKO ARUSHA. CCM kupitia CC yao hawakutoa tamko lenye kutoa mwelekeo wa kumaliza mgogoro huo!. Badala yake wametumia ubabe na udikteta ule ule wa kusema anayeona uchaguzi haukuwa halali aende mahakamani. Hii ni jeuri ya chama cha CCM! Kwa CCM watu kupoteza maisha kwa mgogoro huo ni sawa tu maana walishinda kihalali. This is purely dictatorship ruling.
Kwa kuhitimisha hebu niseme hivi.Kwama CCM kinathibitisha kuwa kimegeuka kuwa chama cha KIDIKTETA. Kwamba CCM kwa sasa hakitaki kusikia MAONI wala USHAURI kutoks kwa VIONGOZI,WANACHAMA na WANANCHI kwa ujumla! Inashangaza CCM kupitisha uamuzi wa kuwalipa Kampuni hewa ya Dowans wakti kuna Mawaziri ndani ya CCM wameshauri Dowans wasilipwe! Kuna vijana wa CCM-UVCCM wametoa tamko kuhusu Dowans kuwa wasilipwe! CCM wamepuuza maoni na ushauri huo. M/kiti Kikwete anajifanya kuweka pamba masikioni wakti ukweli wote anaujua kuhusu Dowans.
Kitu ambacho ni dhahiri hapa ni kwamba CCM WALITUMIA MABILIONI YA SHILINGI WAKTI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU 2010. KWAMBA WALIKOPA AU WALIFADHILIWA HIYO PESA NA MTU KAMA ROSTAM AZIZ-RA. Kwa hiyo wanachofanya kwa sasa ni kutafuta PESA KWA NGUVU HATA KAMA NI KWA KUIBA,KUUA,KUDHULUMU au KUWABEBESHA MZIGO WATANZANIA ili wawalipe waliowakopesha au kuwafadhili kwenye Uchaguzi Mkuu. Hivi unafikiri gharama ya zile Helikopta 2 zilizokuwa zinamsafirisha Dikteta Kiwete wakti wa kampeni zilitoka wapi???Yale mabango yaliyotapakaa kila kona ya nchi hii nani aliyagharamia???Ni wazi kuwa MALIPO YA DOWANS NI KULIPIA GHARAMA HIZO ZA CCM. Huo ndiyo ukweli.
CCM wameshindwa kusoma alama za nyakati. Wameshindwa kupata somo kutoka TUNISIA. Kwa hili la DOWANS CCM wamejichimbia shimo jingine la kifo. Hizi Bilioni 94 zitawa-cost kisiasa huku mbeleni. It is gonna determine their political destiny. Kukataa ushauri,maoni,mawazo ya watu unaowaongoza ni tabia ya vijiserikali vya KIFISADI na KIDIKTETA. Hapa ndipo walipotufikisha CCM. Dawa yake ni kung'olewa kwa MAADAMANO YA KUSHINIKIZA NCHI NZIMA.
Mungu ibariki Tanzania.
Nawasilisha.