Kipandauso (migraine): Chanzo, Dalili, Tiba na jinsi ya kujikinga na tatizo hili

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,843
2,664
Migraine.jpg

Huu ugonjwa upo sana na utambuzi wake ni mgumu. Naomba kupata empirical data na evidence kuhusu kipandauso pamoja na dawa (za kienyeji na kisasa) pamoja na wapi matibabu yanapatikana. Kuna mdau anahisi anacho.


MASWALI YA WADAU WENGINE KUHUSU UGONJWA HUU
Nimekuwa na tatizo hilo tangu 2003, kadiri siku zilivyokuwa zikienda mbele ndiyo tatizo lilikuwa likikuwa na kuwa hatari kwa afya yangu.

Nimekuwa nikitumia sumatriptan 100 mg toka 2010, na Mwaka huu nimenadilishiwa dawa, dawa hizo ni jamii ya triptan, zinaitwa RIZACT-10. Nimetumia anti pain/pain killers Kama Panadol na Hedex mpaka nimechoka. Kuna Dr. Alinishauti nichome sidano za Botox kwani ndiyo treatments for chronic migraine, nilienda India, Apollo Hospital na kuchoma hizo sindano lakini hakuna nafuu yeyote toka nichome hizo botox mapema Mwaka huu. Nilienda India January 2013. Mpaka sasa bado natumia hizo RIZACT-10 lakini nafuu ni ya mda mchache tu.

Wanajamvi naamini ninyi mnaweza kuwa msaada kwa huu ugonjwa wangu ulionisumbua kwa miaka 10 sasa. Kiswahili chake huitwa kipanda USO. Ki ukweli nimekuwa mimekuwa non productive kwa shughuli zangu za kila siku. Kila mda kichwa kinauma tena sana, wakati mwingine natapika sana mpaka nichome sindano za pain killer ndo napata nafuta.

Yeyote anayejua dawa ya haya maumivu makali ya kichwa tafadhali nisaidieni tena kwa gharama yeyote kwani ninateseka sana. Tafadhali nisaidieni ndugu yenu ninsteseka mno na haya maumivu mskali ya kichwa.
Habari za asubuhi wapendwa,

Kwa yeyote ajuae dawa ya kipanda uso naomba aniambie maana uvumilivu umenishinda!.

Huwa nasumbuliwa sana na kichwa, maumivu huwa nayasikia kuanzia utosini mbka kwenye paji la uso ambayo husababisha macho yaume pia.

Nimejaribu kunywa pain killers ila ndo kwanza kimezidi!
Habarini, naomba msaada kwa hili tatizo; mi ninapata mumivu makali sana ya kichwa katika paji la uso pale ninapo tizama vitu vyenye mwanga hususani mkali, vitu hivyo ni luninga, computer, simu ya mkononi n.k , nikitizama vitu hivi kwa muda fulani mwanga wake unanitanya macho kuuma ikiambatana na maumivu makali sana ya kichwa katika paji la uso.

Pia mimi ni mkandarasi hivyo asilimia 100% ya muda wangu wa kazi ni juani na ninapokaa juani kutwa nzima napatwa na maumivu makali ya paji la uso, khari hii imedumu kwa takribani miaka 10 na wakati mwingi nashindwa kufanya kazi kwasababu ya tatizo hili, na tangu 2004 mpaka sasa nimekuwa na tatitizo la maimivi makali ya kichwa maeneo ya kisogoni nimefanya CT scan na MRI muhimbili hazikuona tatizo katika kichwa na kutumia dawa za nerves bila mafanikio pia miwani nimevaa kwa muda wa miezi 6 bila mafanikio, imefikia wakati hata mwajili wangu kutaka kuni simamisha kazi kwa ajili ya tatizo hili,jamani kwa mwanye kujua tiba ya tatizo hili anisaidie.
Hello!

Jaman nasumbuliwa na haka kaugonjwa kanaitwa "kipanda uso" yaani kunakuwa na maumivu ya kichwa upande mmoja hasa usoni. Mwenye kujua dawa zinazotibu au kupunguza tatizo hili anisaidie.

Natanguliza shukrani.


MICHANGO YA WADAU
Kuumwa na kichwa kumegawanyika sehemu kuu nyingi sana japo kuwa 1% yake ni ashirio la matatizo ya kiafya ambayo yame-advance. Kama vile concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia inawezatokana na matatizo ya taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi. Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.

Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo:

  • Mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
  • Baadhi ya neva za fahamu zilizoko usoni

Misuli ya kichwani
Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishu za ubongo kwa zenyewe haziumi kwani hazina mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.

1: Nervous tension headaches;
Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , ounguza au acha matumizi ya sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye mazoezi yakutosha.

2: Cluster headaches;
Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.

3: Hangover headaches;
Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache pombe.

4: Exertion headaches;
Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.

5: Caffein headaches;
Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.

6: Sinus headaches;
Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya maana saa zingine hii utkana na maambukizi.

7: Bilious headaches;
Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.

8: Hunger headaches;
Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda. Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .

9: Eyes ram headaches
Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi zimepotea nuru au la.

10: Menstrual headaches;
Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka. Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.

11: Arthritis headaches;
Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.

12: Hypertension headaches;
Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.

Kabla ya kukupa dawa na ushauri wangu nina maswali nikuulize unijibu.

Je unapata Usingizi wa kutosha? Unalala usiku masaa mangapi? Je, unakunywa maji ya kutosha? Una miaka mingapi? Unapata haja kubwa ya kutosha? Nenda pia kapime macho yako na ukapime tena kwenye mishipa yako ya fahamu huenda una matatizo. Na kitu kingine unakuwa upo juani uwe unavaa kichwani kofia.
DALILI ZA KIPANDA USO
Kipanda uso (Migraine) ni ugonjwa au maumivu makali ya kichwa anayokuwa nayo mtu baada ya mshipa wa damu (Enlargement of Artery ) kutanuka katika kichwa chake.

Baada ya kutanuka kwa mishipa hii ya damu, pia kuna kemikali ndani ya mwili zinazozalishwa na kuizunguka mishipa hii na kupelekea mtu apate maumivu makali ya kichwa na kutanuka zaidi kwa mishipa.

Maumivu makali ya kichwa hupelekea mfumo wa utendaji kazi wa mwili pia ubadilike, mtu atapatwa na kichefuchefu, kutapika, kuharisha, katika utumbo chakula hakitanyonywa vizuri kiingie mwilini, mtu atashindwa kuona vizuri maeneo yenye mwanga na kutopenda kukaa mazingira yenye sauti au kelele.

Vipo vitu mbalimbali vinavyoweza kuchangia mtu apate tatizo la kipanda uso, vitu hivi haimaanishi kuwa ni lazima kusababishe upate na hata kama haupo katika mazingira ya vitu hivi haimaanishi kuwa huwezi kupata tatizo la kipanda uso, miongoni mwa vitu hivyo ni kama vile: sauti kali au kelele, harufu kali, aleji, mwanga mkali, kuvuta sigara, matatizo ya kukosa usingizi, kukaa bila kula kwa muda mrefu, pombe, kubadilika badilika kwa siku za mwanamke (menstrual cycle fluctuations).

Inawezekana ukawa na tatizo hili la kipanda uso, miongoni mwa vitu vinavyowasaidia watu wenye kipanda uso ni kutumia dawa mbalimbali ukijumuisha dawa za maumivu zenye mchanganyiko na caffeine, pia utumiaji wa chai au kahawa umesaidia baadhi ya watu kuwapa nafuu ya maumivu makali ya kichwa.

Tunaweza kupunguza hatari (risk) ya kupata kipanda uso kwa kubadilisha staili ya maisha yetu ya kila siku, kuepuka vitu vyenye harufu kali, kuepuka utumiaji wa tumbaku (sigara), kupata muda wa kutosha kuupumzisha mwili (kulala), kufanya mazoezi, kutokaa bila kula kwa muda mrefu, kunywa maji ya kutosha.Je, unalo tatizo la kipanda uso (Migraine), dalili zako ni zipi na ni vitu gani ukitumia unapata nafuu?
KUUMWA NA KICHWA / KIPANDAUSO
Maumivu ya kawaida ya kichwa huweza kutulizwa na dawa za kuzuia maumivu za aina ya Panadol au aspirini.Iwapo unahisi hayo maumivu kwenye kipji cha uso wako, mashavuni na sehemu zilizo karibu na macho zikifura, kuna uwezekano kuwa umeambukizwa sehemu za kukaza pumzi puani.Iwapo utashikwa na maumivu makali ya kichwa ambayo hayapoi, haikosi kuna uwezekano kuwa umeanza kushikwa na ule ugonjwa sugu wa kipandauso.

Kipandauso (migraine) kina maumivu zaidi kuliko kuumwa kichwa kwa kawaida.Kipandauso huathiri upande mmoja wa kichwa na kuleta kisunzi,au kutaka kutapika.Iwapo unahisi kipandauso unaweza kuona vimulimuli kutokana na muangaza.Pia unaweza kuhisi maumivu makali kwenye jicho moja mara kwa mara.

Ukipatwa na kipandauso, muone daktari wako akuchunguze ili akupe ushauri .Unapopatwa na kipandauso lala chini palipo na utulivu katika chumba kilicho giza kuzuia miale ya jua yanayosababisha kichwa kiume zaidi.

Jaribu usinywe kakao, pombe ama kinywaji chochote kilicho na kakao.Hivi vinaweza kusababisha kipandauso, kunywa maji mengi kila siku.

Utahitajika kumuona daktari ikiwa:
  • Unaumwa na kichwa na hakipoi kwa muda wa juma moja ingawa umemeza dawa za kuzuia maumivu.
Utahitajika kwenda kwa chumba cha dharura ikiwa:
  • Una matatizo unapozungumza, au unasikia kizunguzungu, miguu haina nguvu. Kuna uwezekano kwamba umeanza kupatwa na ugonjwa wa pigo.
MAUMIVU YA KICHWA HUSABABISHWA NA AINA YA MAISHA TUNAYOISHI NA KUFANYA KAZI KILA SIKU

Jaribu kuepukana na mambo yafuatayo:

1. Msongo wa mawazo
2. Matumizi ya kompyuta kwa muda mrefu.
3. Kufanya kazi ktk mazingira ya kelele nyingi.
4. Kutumia vilevi vikali

Pendelea:

1. Kupata muda wa kutosha kupumzika/kulala
2. Kunywa maji mengi ya kutosha.
3. Kunywa juice ya zabibu zilizoiva vizuri.
AINA KUMI NA MBILI ZA KUUMWA NA KICHWA

Kuumwa na kichwa kumegawanyika sehemu kuu nyingi sana japo kuwa 1% yake ni hashirio la matatizo ya kiafya ambayo yameadvance. Kama vile concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia inawezatokana na matatizo ya taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi. Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.

Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo.mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
Baadhi ya neva za fahamu zizlizoko usoni
Misuli ya kichwani

Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishuu za ubongo kwa zenyewe haziumi kwani hazna mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.

1: Nervous tension headaches;
Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , ounguza au acha matumizi ya sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye mazoezi yakutosha.

2: Cluster headaches;
Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.

3: Hangover headaches;
Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache pombe.

4: Exertion headaches;
Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.

5: Caffein headaches;
Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.

6: Sinus headaches;
Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya maana saa zingine hii utkana na maambukizi.

7: Bilious headaches;
Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.

8: Hunger headaches;
Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda. Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .

9: Eyes ram headaches
Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi zimepotea nuru au la.

10: Menstrual headaches;
Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka. Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.

11: Arthritis headaches;
Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.

12: Hypertension headaches;
Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.

Ushauri wangu nenda hospitali kapime damu unayo damu ya kutosha? Nenda kapime macho? Je unapata Usingizi wa kutosha? Je unatapa choo laini kwa wiki unakwenda haja kubw amara ngapi? Je uanyo mawazo au Stress? Kapime Mapigo ya Moyo wako (High blood Pressure ) Yanakwenda sawa? Kisha uje hapa unipe majibu yako.@DANIEL MWITA

Dawa ya Maradhi ya Kichwa Fanya hivi: Fikicha (Sugua) Tangawizi kwa maji na weka kwenye paji la uso. pia hii ni dawa kwa maumivu ya jino na maumivu ya sikio kwa maumivu ya sikio dondoshea tone moja kwenye sikio.

Ukiwa na Swali au Tatizo lolote linalokukera usikose kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano

KIPANDA USO (MIGRAINE) NI DALILI YA UGONJWA WA KIHARUSI

Kwa ufupi

Zipo sababu za ugonjwa huu. Wagonjwa tofauti wanaweza kuhisi moja ya kati ya nyingi zilizopo. Unaweza kutokana na kufinywa au kupungua kwa upenyo wa mishipa ya damu inayopeleka damu sehemu ya mbele ya ukuta wa jicho au au mabadiliko kwenye mshipa wa fahamu wa jicho (optic nerve).

By Dk Isaack Maro

Kipanda uso cha macho ni maradhi yanayosababisha maumivu ya kichwa yakiambatana na matatizo ya macho. Maumivu haya huweza kutokea bila dalili zilizozoeleka za kipanda uso na mara nyingi husababisha kuona kwa shida au kutoona kabisa kwa kipindi kinachozidi saa moja.

Zipo sababu za ugonjwa huu. Wagonjwa tofauti wanaweza kuhisi moja ya kati ya nyingi zilizopo. Unaweza kutokana na kufinywa au kupungua kwa upenyo wa mishipa ya damu inayopeleka damu sehemu ya mbele ya ukuta wa jicho au au mabadiliko kwenye mshipa wa fahamu wa jicho (optic nerve).

Yaweza pia kutokana na maradhi yanayohusisha mfumo wa damu kama vile seli mundu au mwanga mkali unaomulika ghafla machoni. Pengine ikawa harufu kali ya marashi au sauti kubwa.

Msongo wa mawazo, wasiwasi na unywaji wa pombe kupita kiasi ni sababu nyingine. Hata unywaji wa kiasi kikubwa cha kahawa nayo husababisha bila kusahau mabadiliko ya hali ya hewa.

Ugonjwa huu unaweza kumpata yeyote lakini wenye historia ya kuugua wapo kwenye hatari zaidi. Tafiti za kisayansi zinaonyesha maradhi haya hurithiwa. Hii ina maana familia ambazo zina historia ya watu waliowahi kupata maradhi haya huwa kwenye hatari zaidi.

Kipanda uso cha macho kina uhusiano na homoni ya kike inaiitwayo Oestrogen hivyo kumaanisha huonekana zaidi kwa wanawake kuliko wanaume. Siyo tu huonekana zaidi kwa wanawake bali kwenye vipindi fulani kutokana na kuongezeka au kupungua kwa homoni hizo, mfano kipindi cha hedhi.

Kipanda uso cha macho huwa na dalili zinazofanana na kipandauso cha kawaida kama vile kichwa kuuma, kupata kizunguzungu, kusikia kichefu chefu na mara nyingine kutapika.

Ingawa dalili nilizotaja hapo juu huwa zinaonekana kabla au wakati wa maumivu makali ya kipanda uso si mara zote hutokea kwenye kipanda uso cha macho.

Kuumwa kichwa unapotazama mwanga mkali au kusikia sauti ya juu ni dalili nyingine ya ugonjwa huu. Lakini dalili kubwa ya kipanda uso cha macho ni kuona taswira ya vitu kama nyota au mwanga mkali wa mistari mistari.

Wengine huona giza muda mfupi kabla tatizo kutokea. Dalili ya kuona mwanga mkali wenye nyota nyingi ni dalili inayoripotiwa na wagonjwa wengi zaidi. Hali hii hudumu kwa kipindi kifupi kisichozidi dakika sitini au saa moja.

Tafiti zinabainisha dalili za maradhi haya mara nyingi hufanana na za maradhi mengine hivyo mgonjwa anatakuwa amuone daktari ili vipimo vitakavyothibitisha.

Historia ya maradhi na vipimo vikionyesha kuwa kweli tatizo la mgonjwa ni kipanda uso cha macho basi atapewa dawa za kutuliza maumivu ya kichwa na kuzuia kuongezeka kwa shinikizo la damu kwenye macho.

Yapo madhara ya kipanda uso cha macho ambacho mara nyingi husababisha maumivu makali ynayaomfanya mgonjwa kushindwa kufanya shughuli zake za kawaida ingawa huwa haudumu kwa muda mrefu.

Mara nyingi kipanda uso cha macho huwa ni ishara ya maradhi mengine makubwa na yenye matokeo mabaya zaidi. Ugonjwa huu unaweza kuambatana na majeraha au uvimbe kwenye ubongo.

Pengine waweza kuwa dalili ya kiharusi au kutanuka kwa mishipa ya damu kwenye ubongo (aneurysm) kama siyo maradhi ya mishipa ya damu inayosambaza damu kwenye ubongo.

Yaweza kuwa ishara ya maumivu ya mishipa ya fahamu au kichwa kikubwa (hydrocephalus) hasa kwa watoto. Wakati mwingine humaanisha upungufu katika maumbile ya fuvu la kichwa.

Chanzo: Kipanda uso ni dalili ya ugonjwa wa kiharusi
THEORIES ZINAZOELEZEA JINSI TATIZO HILI LINATOKEA
Kuna theories nyingi zinazoelezea pathophysiology (mechanism) ya jinsi tatizo hili linatokea,lakini hakuna hata moja iliyokubalika universally. Lakini pia hakuna dawa hata moja iliyothibitika kutibu/kumaliza tatizo hili universally. Ila kuna vitu kadhaa vinavyokubalika universally juu ya ugongwa huu.

1. Watalamu wote wanakubaliana kwamba hakuna uhakika wa nini hasa kinasababisha ugonjwa huu (kuna theory nyingi).

2 .Walamu wote wanakubaliana kwamba hakuna dawa ya uhakika inayotibu/inayomaliza tatizo hili kwa wagonjwa wote.

3. Watalamu wote wanaclassify type 2 za migraine headache: Typical na Atypical-Typical migraine ina classical signs & symptoms ("Zigzag silvery" vision dakika kadhaa kabla ya kichwa kuanza kuuma, unilateral headache yaani kichwa kinauma upande mmoja wa uso, kichefuchefu na mdomo kujaa mate au kutapika kabisa, photophobia yaani mgojwa hapendi kuona mwanga, kichwa kuuma kwa masaa hadi siku kadhaa kisha maumivu yanapotea kabisa) Kwa upande wa Atypical migraine, dalili hizo nilizotaja sio lazima zionekane zote kwa wakati mmoja.

4. Watalamu wanakubaliana kuwa kichwa kikishaanza kuuma hakuna dawa yoyote ya kumeza ya maumivu inayofanya kazi vizuri. Hii ni kutokana na kwamba kunakuwa na slow down ya gut movement na decreased absorption tumboni (stomach & intestines). Dawa utameza lakini haitafanya kazi vizuri kama inavyotegemewa.

5. Watalamu wanakubaliana kuwa kupona kwa maumivu hakutegemei dawa, kwa maana kwamba hata usipotumia dawa muda ukifika maumivu yanaondoka yenyewe.

6. Kuna utafiti umeonesha kwamba kadiri umri unavyozidi kwenda,frequency ya attacks inapungua! Pia wengine wanasema hata intensity ya maumivu hupungua,ingawa hii haijakubalika sana.

7. Hakuna data wala ushahidi unaoonesha kuwa migraine inaweza kupelekea mtu kupata uchizi, wala kifafa,wala kifo! Isipokuwa kuna taarifa za kuwepo idadi ndogo sana ya wagonjwa waliopata matatizo ya kuona ingawa bado haijathibitika kama ni kwa sababu ya migraine.

8. Pia takwimu zinaonesha kuwa,ungonjwa huu unaanza kuonekana baada ya kipindi cha utoto kupita.Mara nyingi watu huanza kuupata ukubwani, na inaonekana wanawake wanaathirika kwa wingi kuliko wanaume kiuwiano.

9. Pamoja na kwamba ugonjwa huu unaanza kuonekana zaidi ukubwani,lakini watalamu wanasema huu ni ugonjwa wa kurithi.Kwa hiyo ndugu yangu kama ndio hivyo, inawezekana tatizo hili lipo kwenye familia yenu! Mimi kwetu upo!

10. Watalamu pia wanasema kwa kuwa hakuna uhakika hasa ni nini sababu ya tatizo hili, wanasema, upo uwezekano wa tatizo hili kupotea bila tiba yoyote ya maana. Hapa ndipo kidogo kuna ukakasi, maana wapo watu wameombewa wakapona, wapo waliotumia dawa za wamasai wakapona nk, nk, nk. sasa huko siwezi kwenda zaidi!

Kwa nini nimetoa mchango wangu hapa? Mimi pia ni mhanga wa tatizo hili tangu nikiwa na umri wa miaka 14. Binafsi mimi ni mwanachuo ktk chuo kikuu fulani cha udaktari hapa nchini. Na kiukweli, kwa jinsi ugonjwa huu ulivyonitesa, naweza kusema, ndicho kichocheo kikubwa kilichonifanya nisome kozi hii.

Kwa sasa frequency imepungua sana;mwanzo nilikuwa napata attacks hata mara mbili hadi tatu kwa wiki,ila siku hizi ninaweza kukaa hadi miezi minne sijapata attack kabisa. Hata intensity nahisi imepungua tofauti na mwanzo;ingawa inawezekana labda ni kwa sababu nimeishazoea. Usually mimi maumivu huwa masaa 2-3 baada ya hapo nakuwa mzima kabisa na ninaendelea na shuguli zangu as usual.

But all in all maumivu ni makali jamani, asikwambie mtu. Every shughuli is shut down; huwezi kufanya chochote.

Nise tu pole kwenu ndugu yangu, maana na mimi naufahamu muziki huo!
 
Huu ugonjwa upo sana na utambuzi wake ni mgumu. Naomba kupata empirical data na evidence kuhusu kipandauso pamoja na dawa (za kienyeji na kisasa) pamoja na wapi matibabu yanapatikana. Kuna mdau anahisi anacho

Kuumwa na kichwa / kipandauso

Maumivu ya kawaida ya kichwa huweza kutulizwa na dawa za kuzuia maumivu za aina ya Panadol au aspirini.Iwapo unahisi hayo maumivu kwenye kipji cha uso wako, mashavuni na sehemu zilizo karibu na macho zikifura, kuna uwezekano kuwa umeambukizwa sehemu za kukaza pumzi puani.Iwapo utashikwa na maumivu makali ya kichwa ambayo hayapoi, haikosi kuna uwezekano kuwa umeanza kushikwa na ule ugonjwa sugu wa kipandauso.

Kipandauso (migraine) kina maumivu zaidi kuliko kuumwa kichwa kwa kawaida.Kipandauso huathiri upande mmoja wa kichwa na kuleta kisunzi,au kutaka kutapika.Iwapo unahisi kipandauso unaweza kuona vimulimuli kutokana na muangaza.Pia unaweza kuhisi maumivu makali kwenye jicho moja mara kwa mara.

Ukipatwa na kipandauso, muone daktari wako akuchunguze ili akupe ushauri .Unapopatwa na kipandauso lala chini palipo na utulivu katika chumba kilicho giza kuzuia miale ya jua yanayosababisha kichwa kiume zaidi.

Jaribu usinywe kakao, pombe ama kinywaji chochote kilicho na kakao.Hivi vinaweza kusababisha kipandauso, kunywa maji mengi kila siku.

Utahitajika kumuona daktari ikiwa:
  • Unaumwa na kichwa na hakipoi kwa muda wa juma moja ingawa umemeza dawa za kuzuia maumivu.
Utahitajika kwenda kwa chumba cha dharura ikiwa:
  • Una matatizo unapozungumza, au unasikia kizunguzungu, miguu haina nguvu. Kuna uwezekano kwamba umeanza kupatwa na ugonjwa wa pigo.
 
Wadau mke wangu ana matatizo ya kuumwa kichwa kwa miaka mingi, awali nilifikiri ni kwa sababu ya matatizo ya macho, Kweli alipimwa na baadae kupewa miwani.

Sasa tatizo hilo limekuwa kubwa kiasi kwamba akitumia computer kwa muda fulani tu hali inajirudia kiasi kwamba hata kunyanyua kichwa inakuwa ngumu Wadau dawa gani nitumie maana kila hospitali ya hapa jijini ametibiwa lakini wapi.

Msaada plze.
 
Pole sana kwa matatizo, your wife needs to be assessed by a neurologist to make a proper diagnosis. Nenda Muhimbili yupo na pia KCMC yupo. Epuka kutumia madawa bila kujua tatizo ni nini.
 
Kugundua chanzo cha tatizo ni hatua moja ya kulitatua. Mshauri apunguze matumizi ya computer au weka kioo maalum cha kupunguza mionzi ya screen, ama punguza screen contrast kidogo ya cp yako ama tumia LCD/ LED screens. Akifanya haya kidogo anaweza pata nafuu baadae
 
Umejuaje km ni kipanda uso kabla ujaenda hospital?
 
Use vasograin tabs. Make sure umechunguza kwanza kama hana matatizo ya Pressure bcoz pia huumiza kichwa esp kama imepanda sana.
 
Mkuu Miwatamu pole kwa hayo matatizo ya shemeji yangu kuumwa na Kichwa Upande mmoja mimi nitachangia dawa yangu ya asili ni hii hapa :

Grapes juice: Juice ya zabibu zilizoiva ndio dawa ya migrane, utumie kiwango kidogo cha juice hiyo atumia hadi atakapo ona kuwa amepata nafuu! Inshallah itamsaidia shemeji atumie kisha uje hapa unipe Feedback.

Grape Juice Juisi ya Zabibu Dawa ya Ugonjwa wa Kipanda uso Migraine. Chanzo. MziziMkavu Mtafiti wa Dawa za Mitishamba.
 
Last edited by a moderator:
  • Severe migraines with visual disturbances, known as aura, are the second biggest risk factor
  • Only high blood pressure was a bigger factor
  • Findings come from 15 year study of 27,860 women
article-2263178-08BB277B000005DC-599_468x286.jpg

Women who suffer from severe migraines accompanied by visual disturbances may be at an increased risk of

heart attacks and stroke. Scientists have said only high blood pressure was a bigger indicator of a stroke or

heart attack than migraines with aura, as the condition is known when accompanied by vision problems

including flashing lights.The landmark 15-year study followed 27,860 women, of who 1,435 had migraine with aura.

While previous studies have suggested migraine with aura is linked to a doubling of the risk of a stroke or heart attack, never before has it been named as the second biggest factor.

Over the years there were 1,030 cases of heart attack, stroke or death from a cardiovascular ailment,

according to the report from the American Academy of Neurology.

Study author Dr Tobias Kurth said: 'After high blood pressure, migraine with aura was the second strongest single contributor to risk of heart attacks and strokes.

'It came ahead of diabetes, current smoking, obesity, and family history of early heart disease.'

Dr Kurth, of the Brigham and Women's Hospital in Boston and the French National Institute of Health, is also a fellow of the American Academy of Neurology.

He said the risk for migraine-plagued women with aura was three times greater than for those with migraines that lacked this disturbance.

A second study released by the same academy said women who had migraines with aura and took hormonal contraceptives were more likely to have blood clots.

Both studies will be presented at the academy's annual meeting in March in San Diego, California.

Source : UK Home | Daily Mail Online
 
Nimekuwa na tatizo hilo tangu 2003, kadiri siku zilivyokuwa zikienda mbele ndiyo tatizo lilikuwa likikuwa na kuwa hatari kwa afya yangu.

Nimekuwa nikitumia sumatriptan 100 mg toka 2010, na Mwaka huu nimenadilishiwa dawa, dawa hizo ni jamii ya triptan, zinaitwa RIZACT-10. Nimetumia anti pain/pain killers Kama Panadol na Hedex mpaka nimechoka. Kuna Dr. Alinishauti nichome sidano za Botox kwani ndiyo treatments for chronic migraine, nilienda India, Apollo Hospital na kuchoma hizo sindano lakini hakuna nafuu yeyote toka nichome hizo botox mapema Mwaka huu. Nilienda India January 2013. Mpaka sasa bado natumia hizo RIZACT-10 lakini nafuu ni ya mda mchache tu.

Wanajamvi naamini ninyi mnaweza kuwa msaada kwa huu ugonjwa wangu ulionisumbua kwa miaka 10 sasa. Kiswahili chake huitwa kipanda USO. Ki ukweli nimekuwa mimekuwa non productive kwa shughuli zangu za kila siku. Kila mda kichwa kinauma tena sana, wakati mwingine natapika sana mpaka nichome sindano za pain killer ndo napata nafuta.

Yeyote anayejua dawa ya haya maumivu makali ya kichwa tafadhali nisaidieni tena kwa gharama yeyote kwani ninateseka sana. Tafadhali nisaidieni ndugu yenu ninsteseka mno na haya maumivu mskali ya kichwa.
 
Pole sana Mkuu.

Ngoja Madokta waje lakini usikate tamaa, ipo njia na tatizo litakwisha.
 
Hata mimi kilinisumbua sana lakni kimekwisha chenyewe! Ila nafikiri ni baada ya kuanzisha utaratibu wa kunywa sana Maji.

Kabla ya hapo nikiona dalili fulani machoni najua ndiyo chenyewe nakunywa Panadol haraka kinakata, but dawa mpaka sasa sijajua.

Kuna option nyingine nilikuwa natumia: Kutumia dawa za asili za Wamasai (zipo kwenye hali ya unga) ukinusa tu unapiga chafya na kinakata hapohapo. Kuna mtu aliniambia ukipiga chafya unastua mishipa ya kichwani na kuruhusu damu kutembea kwa urahisi (sina hakika sana na maelezo yake).

Ngoja tusubiri wataalam
 
Ninawajua watu kadhaa waliowahi kupatwa na matatizo kama haya. nakiri kuwa wengi walitumia approach tofauti, ila wote (watu 6 wamepona).

1. Tatizo la Allergy: rafiki yangu alikuwa na tatizo hili la migraine, baada ya kuwa ametumia dawa sana za maumivu akaja kugundua kuwa ilisababishwa na allergy. Akatibiwa na akapona.

2. Mdogo wangu alikuwa na tatizo la kuumwa na kichwa sana. baada ya kula sana dawa za maumivu (yeye alishauriwa atumie steroids) lakini baadae hakupata nafuu. Alikwenda UK na wakagundua alikuwa na shida ya uvimbe kichwani, hii ilikuwa 1999. Akatibiwa kwa wiki 3, hajawahi tena kuumwa na kichwa.

3. Jamaa yangu mwingine alikuwa na shida ya kuumwa na kichwa kisichosikia dawa, pamoja na maumivu ya kifua. Akatumia kila dawa lakini hakuwahi kupata nafuu. Lakini baadae alikuja kugundua alikuwa na rheumatic heart disease (a form of rheumatism).

Uncle wangu (Civil engineer - mbishi!!!!!) alikuwa na maumivu ya kichwa kisichoisha. Yeye alikuwa UK, alitumia dawa zote lakini hakupata nafuu, baadae aliombewa kanisani, this is in 2007 na hakuwahi kuumwa tena na kichwa.

Ndugu yangu nimeandika haya yoote nikiwa na lengo la kuonyesha kuwa wengi wamekuja gundua kuwa matatizo yao hayakuwa hicho walichofikiria mwanzoni. Na kama hutapata daktari akawa na muda na wewe (akakufanyia uchunguzi - a doctor who will explore all possibilities.

Some of these problems has a very simple solution.
 
Ninawajua watu kadhaa waliowahi kupatwa na matatizo kama haya. nakiri kuwa wengi walitumia approach tofauti, ila wote (watu 6 wamepona).

1. Tatizo la Allergy: rafiki yangu alikuwa na tatizo hili la migraine, baada ya kuwa ametumia dawa sana za maumivu akaja kugundua kuwa ilisababishwa na allergy. Akatibiwa na akapona.

2. Mdogo wangu alikuwa na tatizo la kuumwa na kichwa sana. baada ya kula sana dawa za maumivu (yeye alishauriwa atumie steroids) lakini baadae hakupata nafuu. Alikwenda UK na wakagundua alikuwa na shida ya uvimbe kichwani, hii ilikuwa 1999. Akatibiwa kwa wiki 3, hajawahi tena kuumwa na kichwa.

3.Jamaa yangu mwingine alikuwa na shida ya kuumwa na kichwa kisichosikia dawa, pamoja na maumivu ya kifua. Akatumia kila dawa lakini hakuwahi kupata nafuu. Lakini baadae alikuja kugundua alikuwa na rheumatic heart disease (a form of rheumatism).

Uncle wangu (Civil engineer - mbishi!!!!!) alikuwa na maumivu ya kichwa kisichoisha. Yeye alikuwa UK, alitumia dawa zote lakini hakupata nafuu, baadae aliombewa kanisani, this is in 2007 na hakuwahi kuumwa tena na kichwa.


Ndugu yangu nimeandika haya yoote nikiwa na lengo la kuonyesha kuwa wengi wamekuja gundua kuwa matatizo yao hayakuwa hicho walichofikiria mwanzoni. Na kama hutapata daktari akawa na muda na wewe (akakufanyia uchunguzi - a doctor who will explore all possibilities.

Some of these problems has a very simple solution.

Ubarikiwe kwa kunijuza hayo yote, naamini hata mimi ipo siku nitapona na kusahau.
 
wapi madaktari wa jamii forum?

Hii inshangaza kidogo lakini ni kweli mwaka 1990 nilkuwa nasumbuliwa na kichwa cha ajabu sana!

Nilkuwa siwezi kusoma kwa dk 30 akaja ndugu mmjoja akamwelekeza baba dawa! Baba alisita kwa sbb ya kidini lakini mama alimlainisha.

Dawa yenyewe ni hivi: Aliambiwa akchimbe mzizi wa jeopatra au mbono kaburi atafuta mzizi uliolala...aukate ,then akanichanja kichwani kidogo na kunipaka utomvu wake afu akaurudisha ule mzizi pale alipoutoa na kuunganisha vile2 nakufukia!

Masharti yake niliambiwa nisile kichwa cha mnyama yoyote tangu wakati ule sijawahi kusumbuliwa na hali hiyo tena hizi ndio dawa za kiafrika ni tukio ninalolitafakari mpaka leo!

Je, ni ushirikina au ni tiba ya kawaida? Ila yote tisa kumi nilipona na sikuona athari yoyote!
 
Kuna theories nyingi zinazoelezea pathophysiology (mechanism) ya jinsi tatizo hili linatokea,lakini hakuna hata moja iliyokubalika universally. Lakini pia hakuna dawa hata moja iliyothibitika kutibu/kumaliza tatizo hili universally. Ila kuna vitu kadhaa vinavyokubalika universally juu ya ugongwa huu.

1. Watalamu wote wanakubaliana kwamba hakuna uhakika wa nini hasa kinasababisha ugonjwa huu (kuna theory nyingi).

2 .Walamu wote wanakubaliana kwamba hakuna dawa ya uhakika inayotibu/inayomaliza tatizo hili kwa wagonjwa wote.

3. Watalamu wote wanaclassify type 2 za migraine headache: Typical na Atypical-Typical migraine ina classical signs & symptoms ("Zigzag silvery" vision dakika kadhaa kabla ya kichwa kuanza kuuma, unilateral headache yaani kichwa kinauma upande mmoja wa uso, kichefuchefu na mdomo kujaa mate au kutapika kabisa, photophobia yaani mgojwa hapendi kuona mwanga, kichwa kuuma kwa masaa hadi siku kadhaa kisha maumivu yanapotea kabisa) Kwa upande wa Atypical migraine, dalili hizo nilizotaja sio lazima zionekane zote kwa wakati mmoja.

4. Watalamu wanakubaliana kuwa kichwa kikishaanza kuuma hakuna dawa yoyote ya kumeza ya maumivu inayofanya kazi vizuri. Hii ni kutokana na kwamba kunakuwa na slow down ya gut movement na decreased absorption tumboni (stomach & intestines). Dawa utameza lakini haitafanya kazi vizuri kama inavyotegemewa.

5. Watalamu wanakubaliana kuwa kupona kwa maumivu hakutegemei dawa, kwa maana kwamba hata usipotumia dawa muda ukifika maumivu yanaondoka yenyewe.

6. Kuna utafiti umeonesha kwamba kadiri umri unavyozidi kwenda,frequency ya attacks inapungua! Pia wengine wanasema hata intensity ya maumivu hupungua,ingawa hii haijakubalika sana.

7. Hakuna data wala ushahidi unaoonesha kuwa migraine inaweza kupelekea mtu kupata uchizi, wala kifafa,wala kifo! Isipokuwa kuna taarifa za kuwepo idadi ndogo sana ya wagonjwa waliopata matatizo ya kuona ingawa bado haijathibitika kama ni kwa sababu ya migraine.

8. Pia takwimu zinaonesha kuwa,ungonjwa huu unaanza kuonekana baada ya kipindi cha utoto kupita.Mara nyingi watu huanza kuupata ukubwani, na inaonekana wanawake wanaathirika kwa wingi kuliko wanaume kiuwiano.

9. Pamoja na kwamba ugonjwa huu unaanza kuonekana zaidi ukubwani,lakini watalamu wanasema huu ni ugonjwa wa kurithi.Kwa hiyo ndugu yangu kama ndio hivyo, inawezekana tatizo hili lipo kwenye familia yenu! Mimi kwetu upo!

10. Watalamu pia wanasema kwa kuwa hakuna uhakika hasa ni nini sababu ya tatizo hili, wanasema, upo uwezekano wa tatizo hili kupotea bila tiba yoyote ya maana. Hapa ndipo kidogo kuna ukakasi, maana wapo watu wameombewa wakapona, wapo waliotumia dawa za wamasai wakapona nk, nk, nk. sasa huko siwezi kwenda zaidi!

Kwa nini nimetoa mchango wangu hapa? Mimi pia ni mhanga wa tatizo hili tangu nikiwa na umri wa miaka 14. Binafsi mimi ni mwanachuo ktk chuo kikuu fulani cha udaktari hapa nchini. Na kiukweli, kwa jinsi ugonjwa huu ulivyonitesa, naweza kusema, ndicho kichocheo kikubwa kilichonifanya nisome kozi hii.

Kwa sasa frequency imepungua sana;mwanzo nilikuwa napata attacks hata mara mbili hadi tatu kwa wiki,ila siku hizi ninaweza kukaa hadi miezi minne sijapata attack kabisa. Hata intensity nahisi imepungua tofauti na mwanzo;ingawa inawezekana labda ni kwa sababu nimeishazoea. Usually mimi maumivu huwa masaa 2-3 baada ya hapo nakuwa mzima kabisa na ninaendelea na shuguli zangu as usual.

But all in all maumivu ni makali jamani, asikwambie mtu. Every shughuli is shut down; huwezi kufanya chochote.

Nise tu pole kwenu ndugu yangu, maana na mimi naufahamu muziki huo!
 
Nakushauri ukafanye kipimo cha CT Scan , kabla ya kufata shauri nyingi zitakuchanganya
 
Back
Top Bottom