Dawa ya asili kwa wenye pumu/athma!

Mzee23

JF-Expert Member
Oct 9, 2014
1,696
3,472
PUMU NI NINI?

Ni ugonjwa unaoathiri njia ya hewa kwenda/kutoka katika mapafu.
Mtu mwenye pumu huwa na mcharuko-mwili sugu(chronic inflammation) katika mirija yake ya kupitishia hewa unaosababisha kuvimba kwa kuta za mirija ya hewa na kujaa ute kamasi hivyo kuminya njia ya hewa na kusababisha mtu kupumua kwa shida!

DALILI ZA PUMU

-Kuishiwa pumzi na kupumua kwa shida
-Kutoa sauti kama mluzi(wheezing)
-Kukohoa sana usiku/asubuhi
-Kubanwa kifua mara kwa mara
-Anayepatwa na shambulizi kubwa hushindwa kuongea na kuonesha kuchanganyikiwa
TANBIHI:
Mwenye pumu sugu siku zote huwa na njia nyembamba ya hewa na huzidi kuwa nyembamba kadiri anavyopata shambulio la pumu!

FANYA HIVI..

1. Tembelea duka la viungo/sokoni, nunua unga wa mdalasini, unga wa tangawizi na unga wa uwatu. Kisha tafuta asali mbichi. Changanya uwatu,mdalasini kwa uwiano sawa halafu miminia asali inayotosha kulainisha huo mchanganyiko vizuri, kisha changanyia unga wa tangawizi kidogo kidogo hadi uhisi ukali unaostahimili wewe wa tangawizi. kisha lamba kijiko kikubwa kutwa mara 3 kwa wiki 3.

2. pamoja na hiyo, tafuta karafuu ukishapata kila siku jioni chukua punje 6-8 toa vichwa halafu loweka ktk maji nusu kikombe, funika usiku mzima. Kesho yake asubuhi unywe maji yake tu kwa wiki 3.
 
Kuna thread moja alikuja nayo jamaa humu ya tiba ya ugonjwa huu..dawa yake ilinisaidia sana mpka leo nko pouwa..ila kinachonisikitisha nlipoteza mawasiliano nae...inaniuma mno....
 
Kuna thread moja alikuja nayo jamaa humu ya tiba ya ugonjwa huu..dawa yake ilinisaidia sana mpka leo nko pouwa..ila kinachonisikitisha nlipoteza mawasiliano nae...inaniuma mno....
Mtaje jina la ID yake huenda ninayo namba. Maana nakumbuka kuna mmoja humu mwaka jana niliwasiliana naye. Sema waliokuwa wanaunwa walileta mapozi
 
ID name yake nmeisahau,ila jamaa aliepost uzi huo nlimtafuta akanipa dawa alikuwa anaishi Turiani mkoani morogoro
 
ID name yake nmeisahau,ila jamaa aliepost uzi huo nlimtafuta akanipa dawa alikuwa anaishi Turiani mkoani morogoro
Vizuri kama dawa yake ilikusaidia mkuu,kwani unamtafuta kumpa mrejesho huu au kuna mgonjwa mwingine? Ugonjwa huu unatibiwa kiasili na kupona kabisa ndiyo maana nami nmeweka uzi huu kwani ninayo dawa pia.
 
Unadawa ya kutibu allerg inayopelekea mafua ya mara kwa mara yasiyoisha na pua kuziba mara kwa mara pia na inazidi kuwa hali inakuwa sio shwari ninapokutana na harufu kali mfano manukato
 
Unadawa ya kutibu allerg inayopelekea mafua ya mara kwa mara yasiyoisha na pua kuziba mara kwa mara pia na inazidi kuwa hali inakuwa sio shwari ninapokutana na harufu kali mfano manukato
Pole mkuu, kwa hili tatizo la mzio/allergy na mafua fanya hivi..

Nunua malimao kama matano hivi, asali mbichi hata robo rita tu,

kila siku asubuhi na jioni,pata maji vuguvugu kikombe kimoja,kamulia limao moja halafu ongeza kijiko kimoja cha chakula cha asali mbichi,koroga kunywa. Fanya hivi kwa angalau siku 15. Utakuwa vizuri

Maelezo ya tiba;
Limao na asali vina nguvu ya kuzuia/kukinga vimelea vya maradhi kama bacteria,virusi n.k pia vina uwezo mkubwa wa kuongeza nguvu ya kinga ya mwili kupambana na vimelea vya mzio/allergy na mafua.
 
Pole mkuu, kwa hili tatizo la mzio/allergy na mafua fanya hivi..

Nunua malimao kama matano hivi, asali mbichi hata robo rita tu,

kila siku asubuhi na jioni,pata maji vuguvugu kikombe kimoja,kamulia limao moja halafu ongeza kijiko kimoja cha chakula cha asali mbichi,koroga kunywa. Fanya hivi kwa angalau siku 15. Utakuwa vizuri

Maelezo ya tiba;
Limao na asali vina nguvu ya kuzuia/kukinga vimelea vya maradhi kama bacteria,virusi n.k pia vina uwezo mkubwa wa kuongeza nguvu ya kinga ya mwili kupambana na vimelea vya mzio/allergy na mafua.
Asante kwa sana nitafanya hivyo mkuu
 
Asali ya aina gani kaka,nyuki wadogo au wakubwa?
Asali ni mbichi,ya nyuki wakubwa limao kama mkipata saizi kubwa mtumie mkamulie kipande kimoja yaani limao moja kwa siku,kata nusu asubuhi,nusu jioni bali kama limao saizi ndogo tu,basi mkamulie lote mara moja.

Pamoja na mzio/allergy na mafua, limao na asali ktk maji vuguvugu ni dawa na kinga kwa madhaifu zaidi ya 50 mwilini,hivyo mtapata faida za ziada!
Asante kwa sana nitafanya hivyo mkuu
 
Kama una Pumu ya ngozi, tumia mafuta ya nazi
3e2793bf3b82bc38e88fe93553fa07b7.jpg
 
Mtaje jina la ID yake huenda ninayo namba. Maana nakumbuka kuna mmoja humu mwaka jana niliwasiliana naye. Sema waliokuwa wanaunwa walileta mapozi
Wanataka sindano za hospitali labda mkuu ambazo ni za kutuliza shida kwa mda!
 
Pole mkuu, kwa hili tatizo la mzio/allergy na mafua fanya hivi..

Nunua malimao kama matano hivi, asali mbichi hata robo rita tu,

kila siku asubuhi na jioni,pata maji vuguvugu kikombe kimoja,kamulia limao moja halafu ongeza kijiko kimoja cha chakula cha asali mbichi,koroga kunywa. Fanya hivi kwa angalau siku 15. Utakuwa vizuri

Maelezo ya tiba;
Limao na asali vina nguvu ya kuzuia/kukinga vimelea vya maradhi kama bacteria,virusi n.k pia vina uwezo mkubwa wa kuongeza nguvu ya kinga ya mwili kupambana na vimelea vya mzio/allergy na mafua.

Mkuu Mimi nilipima nikaambiwa Nina allergy ya vumbi, moshi na harufu Kali sasa napata matatizo sana ya kuumwa kichwa kila nikiwa mitaani huko kusaka mkate wa kila siku, nikifika Nyumbani nikitulia afadhali kinapoa Ila nikiwa tu mjini kichwa kinavuta sana nakisikia kizito mno
Mkuu ntapata tiba gani? Au ndo basi tena?
 
Mkuu Mimi nilipima nikaambiwa Nina allergy ya vumbi, moshi na harufu Kali sasa napata matatizo sana ya kuumwa kichwa kila nikiwa mitaani huko kusaka mkate wa kila siku, nikifika Nyumbani nikitulia afadhali kinapoa Ila nikiwa tu mjini kichwa kinavuta sana nakisikia kizito mno
Mkuu ntapata tiba gani? Au ndo basi tena?
mkuu tumia tiba hii ya limao na asali utaona badiliko
 
Back
Top Bottom