Dawa mpya kwa wagonjwa wa Ukimwi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,314
33,108
120629135659_arvs_hiv_304x171_bbc_nocredit.jpg


Baadhi ya dawa za kukabiliana na makali ya Ukimwi

Huenda wagonjwa wa Ukimwi wakanufaika na dawa mpya ambayo itawawezesha kutumia tembe moja kwa siku. Hii ni kwa mujibu wa utafiti mpya nchini Marekani.

Jarida la Afya Lancet limesema tembe hiyo inajumlisha dawa zote nne zinazokabiliana na makali ya ukimwi na kwamba ni salama.Utafiti unasema hii itawarahisishia wagonjwa katika kuhakikisha wanafuata maagizo ya madaktari wao.

Ukimwi hauna tiba lakini watafiti wameweza kutoa dawa za kukabiliana na maradhi nyemela.
Watafiti pamoja na kampuni za dawa wamechanganya dawa nne na kutengeneza tembe moja ili kurahisisha utumizi wa dawa hiyo miongoni mwa wagonjwa.

Tembe inayofanyiwa majaribio na ambayo imechanganywa dawa nne inauwezo wa kudhibiti virusi vya HIV kuongezeka mwilini.

Paul Sax mtafiti mkuum katika Hospitali ya Wanawake ya Brigham huko Boston,Massachussetts ambaye pia ni mwanazuo wa ziada wa taasisi ya afya ya Harvard ameelezea umuhimu wa tembe hii kwa kuimarisha afya ya wagonjwa.

Dk. Sax ameongoza utafiti huu ambapo pia wamefanyia majaribio tembe hii kwa wagonjwa 700 na kusema inafanya kazi, japo kulitokea matatizo ya figo miongoni mwa waliotumia.

Licha ya mafanikio ya sasa watafiti wanasema raia wengi hawafahamu hali zao ambapo wameendelea kuishi na maambukizi bila kujua.BBC Swahili - Habari - Dawa mpya kwa wagonjwa wa Ukimwi
 
Mbona wanasema uko dawa wamesha ipata au ni longo longo hawa wamarekan bna.
Mkuu Justin Dimee Wamarekani Uchumi wao umekufa sasa wanatanga tanga wanatafuta mbinu za kuweza kupata pesa hizi ni mbinu zao za kila siku wakishindwa huku wanatafuta kule Wamarekani ni kama vile sungura wa porini huwezi kuwakamata kirahisi .
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom