Dawa gani hizi?

Columbus

JF-Expert Member
Nov 5, 2010
2,002
648
Unakuta mwanaume ana nyumba ndogo na jamaa anaelekea kuitelekeza nyumba kubwa(yaani mke wa ndoa) baada ya kuuliza inakuwaje hivi unaambiwa jamaa kalishwa dawa, hivi hizi dawa gani na kweli zipo? na wewe mlengwa utagunduaje umeshalishwa?naomba kuwasilisha wanajamvi.
 
mliowahi kuwa nyumba ndogo leteni maujuzi,who knows na sie nyumba kubwa twaweza zitumia mkose soko lol
 
Asilimia pengine 99 ya watu kama hao anakuwa amepewa mapenzi mazuri tu, sio dawa. Hilo la dawa nalisikia lakini kwa siku hizi ni malavidavi tu...
 
Hakuna dawa Pauline, mapenz tu...

mbona saa nyengine unakuta mtu hata huko nyumba kubwa mapenzi anapata sana tu....nini kinachomfunga huko nyumba ndogo au kuna kuzidiana kete??? mie nahisi na dawa zimo sana tu
 
Mimi nakaribia kuamini hivi,
Kama mwanaume hana hofu ya Mungu,
yani hachukulii swala kama hilo ni dhambi kwa Mungu wake
Na akawa na mipaka kwa tamaa ya nafsi yake na mwili wake.

Hawezi kuridhika na mwanamke mmoja, hata mke wake.
Wanaoa ili maisha yaendelee tu, jamii iwatambue, apate mahali pakuja kulala,
na watoto, na heshima kwa jamii kwamba ana familia, na ni bab, lakini.
Wanatoka nje kama kawaida..................

Yani mi nakaribia kuamini hivo., nakaribia kukubaliana na hiyo.
Nimebaki na lile kundi la wale watu ambao wana hofu ya Mungu kweli kweli tu..............
 
Lisemwalo lipo,ukirogwa unakuwa hujui kama umerogwa ila wengine ndio wanaoweza kuona ya kuwa umerogwa. Hakuna linaloshindikana chini ya jua
 
hapo hamna dawa ni mapishi tuu si unajua wanawake wengi wakishaolewa wanajisahau wanazani kwamba wamemaliza kila kitu kumbe ndio wako vitani na ikitokea mmwanaume kaonja nje chakula tu anataka kulinganiasha na mapishi ya mkewe anagundua kwamba mkewe hujui kupika ndipo inakua tabu lakini kama mama atapika vizuri siku baba akila chakula kwa jirani kwa bahati mbaya ikikuta mapishi siyo sawa na ya mkewe lazima atarudi nyumbani tuu.
wakima dada amkeni kwa hilo
nawasilisha
 
huwa nyumba ndogo wanaweka yule mjusi wa nyumba kwenye chakula basi hutabanduka!au nyama ya maini inawekwa kwenye na nihiino siku 7 kisha unawekewa kwenye mboga
 
mbona saa nyengine unakuta mtu hata huko nyumba kubwa mapenzi anapata sana tu....nini kinachomfunga huko nyumba ndogo au kuna kuzidiana kete??? mie nahisi na dawa zimo sana tu

Kuzidiana kete kupo sana. Unajua baadhi ya wake wanadhani kuwa 'mapenzi ni kumridhisha, na kumhudumia' mwanaume kwa nguvu zao zote. No, vipo vitu vingi na strategies kadhaa. Hivi unajua kuwa ugomvi ni kiungo fulani katika kukoleza mapenzi. baadhi ya wanawake wanadhani, styles za kitandani (wengine wanatoa hata tigo), kupika vizuri, kuongea vizuri na kwa uchangamfu, kukubali kila unachoambiwa. eti ni mapenzi tosha kwa mwanaume, NO. Akili, tumia akili kuomuonyesha mumeo kuwa wewe ni mtu wa maana, ali ajivunie kuwa na wewe...
 
huwa nyumba ndogo wanaweka yule mjusi wa nyumba kwenye chakula basi hutabanduka!au nyama ya maini inawekwa kwenye na nihiino siku 7 kisha unawekewa kwenye mboga

Utamuua tu mumeo na mauchafu, hayo. Mapenzi (sio tendo la ndoa tu) ndiyo dawa...
 
Shetani yupo na ana nguvu pia kwa wasioenda kwa mataka ya mwenyezi Mungu, kwa maana hiyo wapo wanaotumia hiyo mittishamba kwa kuwashika waume za watu na kuwafanya kama mandondocha yao, na ukifanyiwa hivi wanasema sio rahisi kujijua ni watu wanaokuzunguka ndio watakujua, wewe utajiona upo poa sana.
Pia mume akitoka nje na kupata hawara sio lazima awe amelishwa limbwata wengine ni mambo tu ya mahaba yamewachanganya kwa hao mahawara wao. unajua mahawara wanakuwa hawana majukumu mengi kama wake muda mwingi wanakaa wakitafuta mbinu za kuwaridhisha wanaume wao, huku home mke anakuwa na majukumu kibao, watoto labda wanne wamefatana, anafuga kuku, anafanya kazi anapika kwa ajili ya familia, akilala anakuwa mchovu, hapa mume akitoka na demu yuko single, anaishi mwenyewe, nyumba muda wote ipo neat, mazingira yale yanamlewesha mume anashinda hukohuko, akirudi home ni kulala. Kw hiyo bwana mkubwa unaweza pewa limbwata likakukolea na unaweza usipewe ukapagawa tu mambo ya mahaba unayofanyiwa na kimwana wa pembeni
 
Unakuta mwanaume ana nyumba ndogo na jamaa anaelekea kuitelekeza nyumba kubwa(yaani mke wa ndoa) baada ya kuuliza inakuwaje hivi unaambiwa jamaa kalishwa dawa, hivi hizi dawa gani na kweli zipo? na wewe mlengwa utagunduaje umeshalishwa?naomba kuwasilisha wanajamvi.

ukilishwa utajua!!!!
 
Lisemwalo lipo,ukirogwa unakuwa hujui kama umerogwa ila wengine ndio wanaoweza kuona ya kuwa umerogwa. Hakuna linaloshindikana chini ya jua
Kwa nyongeza, kuna bosi wangu mmarekani kabisa amekolea nyumba ndogo ya kiswahili ni balaa hapa ofisini hatumuelewi hata utendaji wake wa kazi umepungua.Tunamuombea tu asije akadhurika na hayo madawa kiafya.
 
hakuna dawa wala nin ni upendo 2 na tamaa za muda mfup ndoa ndoa2 kwan we unawaswas gan kulala nje ndo hawez ataruka we lakn mwsho wa siku anarud mchukulie poa 2 ndo utafka sawa enhee (au anampa ndogo nin ambyo wew utoagi emb fnya ivyo afu tuone)
 
hapo hamna dawa ni mapishi tuu si unajua wanawake wengi wakishaolewa wanajisahau wanazani kwamba wamemaliza kila kitu kumbe ndio wako vitani na ikitokea mmwanaume kaonja nje chakula tu anataka kulinganiasha na mapishi ya mkewe anagundua kwamba mkewe hujui kupika ndipo inakua tabu lakini kama mama atapika vizuri siku baba akila chakula kwa jirani kwa bahati mbaya ikikuta mapishi siyo sawa na ya mkewe lazima atarudi nyumbani tuu.
wakima dada amkeni kwa hilo
nawasilisha

na hayo mapishi ya jirani uliyafuatia nini in the first place??????
 
Dawa zipo na mara nyingi wanawawekea wanaume wenye hela kwa ajili ya kuwasaidia kimaisha. unakuta upendo wa kweli hakuna
 
1.wanaume wa dar tulishabugia sana hizo dawa bila kujua, ila akili kichwani mwako.
2.unadhani waganga wa kienyeji nao wakale wapi? Huwauzia akina mama dawa za namna hiyo.
3'dawa nzuri ya mapenzi ni kumpa mwenzio kile atakacho,kumheshimu,kumjali,kutomuudhi na kumtunza.
4.hapo kila mtu atasema umempa dawa.
 
Huenda ni kweli kuna dawa,lakini si vizuri kutoka nje ya ndoa enyi wanandoa.kama mwenzio ana tatizo mwambie,ikishindikana muombe MUNGU kwake hakuna lisilowezekana.
 
Hahahahah imani hizi huko wanakotoa hizi dawa kuna sharti la kuwa nyumba ndogo nini,maana tangu nimeanza kusikia nyumba kubwa nazo zingekuwa juu....kuna kitu tunajisahau tu bwana au ni hila za wanaume:washing:
 
Back
Top Bottom