FirstLady1
JF-Expert Member
- Jul 29, 2009
- 16,792
- 5,373
siasa za bongo
Sakata la matangazo ya jengo la Machinga Complex. David Jairo analazimisha kampuni yake ipewe Tenda.
Ni nani huyo? David Jairo!!!
sasa nani msafi?JK ni Saigon, Zungu ni Sagon pia na Iddi Simba alikuwa Saigon. Jairo sio mwanamtandao wa JK, bali ma close pals, sasa inapokuja mgongano wa kimaslahi kati ya Saigoni na ma pals, JK atakumbatia ma pals kwa sababu Saigon haina nguvu tena kama ilizokuwa nazo, kama Simba aliangunguka, itakuwa Zungu, mtaji pekee wa Zungu Ilala yeye ni mtu wa watu, Simba aliwategemea sana wapambe, Zungu ni mwenyewe mpambe.
Hiki kilio cha Zungu dhidi ya Jairo, ni dalili ya mfamaji na hakitamsaidia Zungu, sana sana kitatifua tuu maroroso yote ya Machinga Complex ambayo Zungu ndiye main player. Masikini wamachinga, hilo jengo lao, wao wataishia kuliona kwa macho tuu.