Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Hivi tukisha letewa picha ndipo tutapata majibu kuwa Ballali aliidhinisha vipi zile pesa za Meremeta, Tangold na EPA?
sasa uongo uko wapi? ungejiuliza maswali hayo badala ya kuuliza maswali wrong usingetatizika na kinachoendelea sasa. Jmushi, tulia na jifunze kuuliza maswali ya msingi itakusaidia sana uko mbeleni. Na kuonesha kuwa unakwepa maswali muhimu huja highlite kipengele "D" labda kingekufanya ufikiri kidogo na kuona uzito wa nilichokisema... but that is not you!
jMushi,
Maswala mengine mkuu huna haja ya kuingia darasani. Balali alikuwa mwajiriwa wa serikali yetu kama Mtaalam wale tuliokuwa tukiwaita TX... Leo kumetokea swala la Usalama wa Taifa unafikiri kweli Balali angefahamu umuhimu wa fedha hizo kutoka kabla ya mama Meghji waziri wa fedha nchini!...
Hiyo Barua aloandika Balali kupitisha hizi fedha mbona hizo habari zimekuja baada ya Balali kuondoka Bongo kwenda tibiwa Marekani, muda wote bungeni mama Meghji huyo huyo alikuwa akisema hakuna ufujaji wa fedha benki kuu na mwenyewe alisema uchuguzi wa EPA unafanyika, kwa nini asiseme siku hizo kwa sababu alijua alichokifanya yeye..
Je kweli huo ndio Utaratibu wa kutoa fedha benki kuu yaani amri inatoka kule BoT kuidhisha fedha inayotakiwa kwa barua kutuma barua inayosisitiza sahihi ya kiongozi..Hata kama huyo Meghji asiwe na supporting document isipokuwa barua ya balali wakati hufahamu hizo fedha analipwa nani na kwa kazi gani hata kama ni Usalama wa Taifa... Mkuu Meghji alichemsha na ndio maana yupo nje hivi sasa tatizo kubwa ni JK kutowawajibisha hawa watu...
Hata Lowassa na kundi lake wote kina Karamagi, Msabah, Mwanyika, Donald Chidowu wote hawa wamefahamika kuhusika wazi na Richmond.. tumefganya nini zaidi!
na wote wanajitetea kutohusika na Richmond hadi kufa kwao, hivi kweli wewe unaamini hadi apatikane huyo Mhindi wa Houston ndipo tupate ukweli?.. Hivi sasa tunashindwa kitu gani kumvuta huyo mhindi kupitia vyombo vya serikali kama shahidi wa Richmond!..au naye tunasubiri avute kisha tuanze kusema huyo ndiye fisadi..
Toka report ya Mwakyembe umesikia hatua gani JK kazichukua kuhusiana na ubadhilifu ule zaidi ya wao kujiuzuru ama kuwaondoa madarakani wakati wa kuvunja baraza... Kuvunja kule hakuna maana yoyote kwani wapo mawaziri ambao hawakuhusika na deal lolote wamepoteza wadhifa, hivyo hadi leo upelelezi wa Richmond haujazaa matunda yoyote..
Mkuu kubali tu NDIVYO TULIVYO... siku zote sisi hutafuta mchawi wakati wachawi ni ni ndugu zetu wenyewe tunaokula na kulala nao.
MKJJ hapa bado huoni kuwa Ballali alitakiwa kuwa shahidi wa kwanza kwasababu alimdanganya Mama Meghji aandike barua ya kutoa pesa kwa kisingizio kuwa Kikwete ndio alimwambia?
Yani Kikwete hakuona umuhimu wa kummuliza Ballali kwanini amemtungia uongo?
Kwani ni siri kuwa umekuwa upande wa Ballali na Kikwete?
Mimi sipotezi kumbukumbu hovyo hata kama sija quote nakumbuka conversation zote muhimu ambazo tumeshawahi kuwa nazo hapa jf
NB:Unaposhinikizia kipengele D ndipo hapo unapo onyesha uana siasa wako.
Mushi ana hasira na mafisadi ndo maana kaamua kuendesha vita ya fikira nao, ndo maana kawa mkali tangia balali alipokufa.
Baada ya Balali kufa,Je nini kinafuatatatizo amekuwa mkali tangia Ballali alipokufa.... na anampigia kelele maiti..
mara kwanini afe?
Kwanini afe wakati anakaribia kukamatwa?
Kwanini afe mtu huru?
Kwanini afe bila kuaga?
Kwanini Kikwete amuache Ballali afe?
tatizo amekuwa mkali tangia Ballali alipokufa.... na anampigia kelele maiti..
mara kwanini afe?
Kwanini afe wakati anakaribia kukamatwa?
Kwanini afe mtu huru?
Kwanini afe bila kuaga?
Kwanini Kikwete amuache Ballali afe?
Wakuu,
Mimi nipeni hata sababu tano kwanini mnaamini Balali kafa?
Naona sasa upande wa Ballali umeingia kwenye kampeni kali kupitia vyombo vya habari, kampeni ya kutafuta mchawi wa Ballali.
Hivi kweli ulishwe sumu, unamjua aliyekulisha, umekimbia nje ya nchi, mungu amekusaidia kuishi miezi tisa mpaka ukapata nafuu, una documents zote, una mamilioni ya watu wanaotaka kukusaidia kama utatoka clean, BADO UNASHINDWA KUMKABILI HUYO MBAYA WAKO?
Naona Anna Muganda na hao mawifi zake sasa wako kwenye kampeni ya kuwadanganya Watanzania. Kama wanataka tuwaamini, basi waombe msaada kwa serikali ili mwili wa Ballali urudishwe kwao Iringa, watueleze Watanzania ilikuwaje mpaka wakashindwa kutangaza kifo cha mpenzi wao mpaka baada ya siku tano? Watueleze ni kwanini wamemzika kimya kimya kama kibaka? MUHIMU zaidi watuambie alilazwa hospitali gani? baada ya kufa ni hospitali ipi imetoa death certificate yake?
Naona sasa Anna Muganda na hao mawifi zake wanaanza kutumia ukaribu wao na mmiliki wa Tanzania Daima ili kuendelea kampeni ya kuwadanganya Watanzania.
Ndio wengine tunamchukia hasa Rostam Aziz na tungependa mwisho wake kwenye siasa ufike haraka. Kama Ballali alikuwa anamtuhumu huyu jamaa kumlisha sumu, alishindwa nini kuanika waziwazi kuhusika kwa Rostam kwenye EPA. Naamini kila mtu anajua Rostam ni mhusika mkuu sana kwenye EPA na laiti Ballali angeamua kutoka clean, angetusaidia Watanzania kumfunga kamba huyu jambazi.
Mimi nitakuwa wa mwisho kumwamini Anna Muganda maana inaelekea naye ni fisadi tu ambaye alitumia ukaribu wake na Mkapa kumwingiza matatizoni msomi wetu Ballali. Huyu mama laiti asingelimficha Ballali kutoka kwa wana familia, naamini wangemshaur vizuri juu ya namna ya kujitoa kwenye mtego aliokuwa ameunasa.
Najua sasa juhudi kubwa zitafanywa ili kumpakazia JK badala ya Mkapa ambaye ndiye hasa alikuwa mhusika mkuu kwenye EPA. msitegemee hata siku moja huyo mama atoe documents zinazomhusu Mkapa. Wanaona JK ameshindwa kuwalinda na sasa wanataka kutumia kifo cha Ballali kumkabili JK. Sawa JK ana makosa mengi sana kwenye hili lakini EPA ni ya Mkapa na hao mawaziri na wasaidizi wake wengine. JK kama mgombea urais alikuwa hana nguvu kabisa ya kuchota mapesa.