Daraja la Kigamboni au Reli ya kati? Kipi kina kipaumbele?

binafsi naona reli ya kati ingeshuhulikiwa ingekuwa vyema kuliko kuanza na kigamboni
ila nahisi kigamboni kuna vitega uchumi vya wakubwa flani,ndo maana wanapeleka fikra zote huko
 
kaka siasa tu, kigamboni kuna nini cha kumvutia mtalii? Yaani bado tunaishi kwa ndoto? Nani siku hizi akujengee mji ndugu yangu? Trilion 13 zinahitajika kama ukikuwa hujui ili kukamisha huo mji serikali yako inazo?

hivi nivichekesho kweli eeti watalii ni mtalii gani aje aangalie daraja la kigamboni wakati kunamadaraja duniani makubwa kuliko hilo!
 
Mbona jibu rahisi,
Kwa kuwa wakubwa wengi hawana biashara mwanza na Arusha inayo hitaji reli, na
Kwa kuwa wakubwa wengi wanakaa masaki na Beach ya ku-enjoy ni kigamboni, na
Kwa kuwa foleni ya kuingiza vx zao kwenye pantoni za kigamboni zinawachelewesha, na
Kwa kuwa wakubwa wanajengewa mji wa kisasa na Bush huko baada ya kuwatimua maskini, na
Kwa kuwa foleni hiyo inawaletea harufu ya samaki inayokera ya biashara ya mamantilie, na
Kwa kuwa kwenda mikoani kwa likizo au kikazi wanakwenda na vx zao bila kuulizwa na mtu, na
Kwa kuwa umaskini unaoletwa na reli kwa wananachi hauwahusu wakubwa wetu,

Kwa hiyo, basi, Kipaumbele ni Daraja la kigamboni na siyo Reli.
 
Jibu zuri sana BIG up kaka nadhani mleta mada atakuwa amekuelewa na kufunguka macho naomba tufunge mjadala.

Tuache siasa za majitaka katika kujenga uchumi wa nchi hii! Reli ya kati ndiyo uti wa mgongo wa nchi hii. Kwa kuiimarisha reli hii barabara zetu zitadumu kwa muda mrefu, ajali barabarani zitapungua kwa sababu mizigo mingi na mikubwa yote itasafirishwa kwa reli badala ya malori ambayo yanaongeza msongamano (foleni), nchi itapata kipato kikubwa kutoka kwa majirani zetu(Congo, Rwanda, Burundi, Uganda, Sudani ya Kusini) kupitishia mizigo yao na hivyo kuwezesha nchi kununua vivuko vingi zaidi kwa ajili ya watu wa Kigamboni, kukuza utalii kwa maeneo ya kati na magharibi mwa nchi yetu na faida zingine chungu nzima ambazo nikiziorodhesha hapa wote walioidhinisha kujengwa kwa daraja hili wanatakii wajipeleke wenyewe mahakamani kwa kosa la kuhujumu uchumi.
 
Jibu zuri sana BIG up kaka nadhani mleta mada atakuwa amekuelewa na kufunguka macho naomba tufunge mjadala.

Wewe mohamed na gango2 kweli hamnazo, na wasi na u great thinker wenu. Utawezaje kulinganisha kamji ka kigamboni eti ka utalii na reli ya kati?! Nyie ndo watanzania halisi, sie watanganyika hatufikiri kama nyie.
 
Kwanza ni kweli kabisa sekta ya reli haijapewa kipaumbele chochote kile na Serikali yetu.Kuna ushindani mkubwa kati ya sekta ya reli na barabara.Kuhusu bajeti kubwa inayotengwa kila mwaka kwa ujenzi wa barabara za lami hali inayopelekea wingi wa malori mengi ya mizigo yanayomilikiwa na wafanyabiashara wenyewe ama vigogo wa Serikali au makampuni na mashirika ya umma .

Kuua reli hii ni kuwanufaisha watu wachache wasio na uchungu na nchi hii,hawa ni wat hatari sana wasiowapenda Watanzania maskini walio wengi ambao mategemeo yao makubwa ni reli isiyofanya kazi na inayoendelea kudorora kila uchwao.Kuimarishwa kwa sekta hiyo kungesaidia kuokoa barabara zetu za lami kwa usafiri wa mizigo mizito na hata abiria wanaoisho maeneo ya mbali mahali ambako hakuna barabara hizi.

Ni wazi kuwa ufisadi ndio chanzo kikubwa cha kuua reli na kuona umuhimu wa kujenga daraja la Kigamboni ambalo litasaidia watu wachache tu.Reli bado no muhimu kwa maendeleo ya TAIFA hilli.

MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU IOKOE TANZANIA YETU NA UFISADI HUU.

 
Hivi tumepoteza billions ngapi, Jiulize-umiza kichwa
mara Rada, mara ndege ya Rais,Mara EPA, mara .............
kama hizi pesa zingewekezwa tungekuwa wapi iwapo Daraja la Kg ni 213bil pekee?
Watasha wanatuona sie wajjjingaax tu kila kukicha hodi tunaomba saaada
 
hivi vyote ni muhimu kwa maeneo yake, lakini kama unataka kipaumbele kati ya vitu hivyo, hakuna ubishi kuwa kuimarisha reli ya kati inazidi umuhimu wa kujenga daraja la kigamboni. Lakini hiyo haimaanishi kuwa daraja la kigamboni si muhimu.
Tatizo lipo miongoni mwa wanaofanya maamuzi. Tungeweza kuimarisha reli ili ituletee fedha za kutosha kuweza kujenga si tu daraja la kigamboni, bali na madaraja mengine pia. Sidhani kama daraja la kigamboni linaweza kuzalisha fedha za kutosha kuimarisha reli ya kati
yote yana umuhimu wa kipekee na hayashirikiani ila cha kutazama kwanza kinatakiwa kiwe wapi kuna shida zaidi au wapi wanateseka zaidi na uchumi na shughuli za kijamii unaathirika kwa kiasi gani. We inalinganisha daraja la kigamboni na reli hebu linganishana kujenga kiwanja cha ndege kikubwa pale msalato dodoma kwa sasa kama kuna mahitaji muhimu lukilinganisha na reli ya kati.
 
Sasa jamani si na mkuu wa sasa lazima apate mradi mkubwa wa kupewa jina lake atakapoondoka?
 
Swala la lipi ni muhimu kati ya daraja la Kigamboni na Reli ya Kati bila shaka reli ndio muhimu sana. Hata hivyo ieleweke kuwa reli ni biashara na daraja ni huduma kwa jamii. Daraja litatoza gharama za kuvuka na deni likisha la kujengea itakuwa bure kupita. Ngarama za daraja bila shaka ni ndogo kuliko kuimarisha usafiri wa reli yetu.

Serikali pekee haina uwezo wa kuimarisha hiyo reli. Makampuni ya ubia yamekuja na kuondolewa. NSSF nayo kwa maslahi yake ndio wamewekeza kwa daraja kwa 60%.

Tujue mambo hubadilika usafiri wa reli utakuja kuwa ya bei ghali kuliko mabasi. Tujipange upya na tuyakubali matokeo. Pesa za kugharamia kujenga daraja zitarudi bila tatizo.
 
Zote ni huduma kwa jamii na zipo sawa kabisa pasi na moja kuwa juu ya nyengine bali inategemea vipaumbele vya Serikali katika kutoa huduma kwa jamii ya watu wake.


Nilikuwa natafuta post ya namna hii mkuu. Zote ni huduma kwa jamii na hakuna mtanzania zaidi.
Kuhusu kipaumbele reli ya kati ipo kitambo na serikali imeendelea kuiendesha kwa muda wote huo, ni hivi karibuni tu uendeshaji umekuwa ni wa kusuasua. Hata hivyo haijatangazwa kufuta huduma hiyo na ndiyo kusema huduma ipo. Kuhusu daraja la Kigamboni, hilo ndiyo kwanza linataka kujengwa kwa hiyo kama ni vipaumbele basi daraja ni cha pili.
Nasikia harufu ya wivu hapa, kwa mwamba ngoma kuvutia ngozi kwake.
Lakini serikali inaweza kuyafanya yote hayo, siyo lazima iache kujenga daraja ili kuboresha usafiri wa reli, siyo lazima hata kinyume chake. Siyo lazima ukae Kigamboni kujua umuhimu wa daraja wala si lazima uwe mtu wa mikoa ya kati na magharibi ili kujua umuhimu wa reli ya kati.
Labda tungepaza sauti zetu kukemea matumizi ya anasa na ufisadi kuliko kuendeleza 'wivu wa kimasikini'
 
Daraja la kigamboni ni lakipaumbele ukiangalia Marginal Social Benefit kwakuwa watu wengi wana cross hapo kwa mwaka.
 
Back
Top Bottom