Dar yakithiri kwa rushwa, vurugu

armanisankara

JF-Expert Member
Jul 15, 2011
283
49
Taasisi ya utafiti na kuibua matatizo yanayowakabili wakazi wa Jiji la Dar es Salaam (Sikiliza) imebaini kwamba jiji hilo limekithiri kwa rushwa, vurugu, pamoja na wizi kwa asilimia 55.

Akitoa tathmini hiyo jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa Sikiliza, William Kihula, alisema mambo hayo yanaendelea kukua kwa kasi jijini humo.

Alisema sehemu kubwa ya matokeo ya utafiti huo, inaonyesha kuwa kati ya matukio manne yaliyokithiri, ni ya rushwa, ambayo yanasababishwa na askari wa usalama barabarani.

Pia alisema utafiti huo umebaini kuwa sio tu kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri wa barabarani, bali hata kwa wasiomiliki.

Kihula alisema wizi na vurugu ni miongoni mwa aina za uhalifu wa mara kwa mara unaoathiri maisha ya mamilioni ya wakazi wa jiji hilo.




SOURCE: NIPASHE

 
sababu kubwa ni unemployment na si kingine. watu wamejazana mjini halafu hawana kazi, wewe unafikiria kitu gani kitatokea. kama mikoani kuna ajira ya nguvu, nasi wakazi dar watapungua na wizi na umalaya na vurugu navyo vitapungua kwa kasi. wewe angalia kati ya mikoa 35 ya tanzania, ni mkoa minne tu ina toa ajita nayo ni Mbeya, mwanza, Arusha na Dar Es Salaam.

Hii yote ni ile sera ya kuchukia mabepari na kuzichukia western Europe , marekani na Israel. Haya ndiyo mataifa makuu yatoayo soko la ajira duniani. Ukiona raisi wako anajifanya kuyachukia tuu mataifa hayo, basi ujue kakuletea Njaa nyumbani.
 
Back
Top Bottom