kimatire
JF-Expert Member
- Nov 27, 2008
- 371
- 93
Swali hili najiuliza mara kwa mara na sipati m jibu muafaka, kama kweli Jiji kwa maana ya City Council na Manispaa zake yani Ilala,Temeke na Kinondoni,Wanatimiza wajibu wake kwa Wananchi wake katika nyanja zote wanazotakiwa?
Nia hasa ya kuligawa JIJI la Dar Es Salaam katika Manispaa tatu ilikuwa ni kurahisisha utendaji wa kazi kwa watendaji wake pamoja na kuhakikisha mapato yanakusanywa kikamilifu.Lakini inashangaza jinsi mambo yanavyokwenda kienyeji kila kona ya Jiji,Si taka,wala mitaro ya maji machafu,Ujenzi wa kiholela,barabara mbovu achilia biashara kila pahala!
Kwamba hakuna mipango,au iliyopo haina mikakati ya kuifanikisha?
Wizara yenye dhamana sawa iko Dodoma lakini haya yote watoa maamuzi wako wapi?Usafi wa mazingira , fukwe kuvamiwa,vyoo vichafu kila kona ya Jiji-Uchafu nk
Kila kukicha porojo mpya kuhusu mwendelezo wa JIJI na harakati zake kumwezesha raia kuishi mahali safi ,salama,na kupata huduma nzuri iwe ya matibabu au shule au usafiri kutoka mahali pamoja kwenda mahali pengine nk.HIVI HIVI MPAKA WAPI NA LINI????Halafu tunajigamba Eti BANDARI SALAMA??Vivutio vya utalii ni uchafu uliozagaa kila mahali au ni bonde la Jangwani lilojaa mifuko ya plastiki?
Nia hasa ya kuligawa JIJI la Dar Es Salaam katika Manispaa tatu ilikuwa ni kurahisisha utendaji wa kazi kwa watendaji wake pamoja na kuhakikisha mapato yanakusanywa kikamilifu.Lakini inashangaza jinsi mambo yanavyokwenda kienyeji kila kona ya Jiji,Si taka,wala mitaro ya maji machafu,Ujenzi wa kiholela,barabara mbovu achilia biashara kila pahala!
Kwamba hakuna mipango,au iliyopo haina mikakati ya kuifanikisha?
Wizara yenye dhamana sawa iko Dodoma lakini haya yote watoa maamuzi wako wapi?Usafi wa mazingira , fukwe kuvamiwa,vyoo vichafu kila kona ya Jiji-Uchafu nk
Kila kukicha porojo mpya kuhusu mwendelezo wa JIJI na harakati zake kumwezesha raia kuishi mahali safi ,salama,na kupata huduma nzuri iwe ya matibabu au shule au usafiri kutoka mahali pamoja kwenda mahali pengine nk.HIVI HIVI MPAKA WAPI NA LINI????Halafu tunajigamba Eti BANDARI SALAMA??Vivutio vya utalii ni uchafu uliozagaa kila mahali au ni bonde la Jangwani lilojaa mifuko ya plastiki?