FYATU
JF-Expert Member
- Dec 7, 2011
- 5,392
- 4,468
Kuna bwana anomba msaada wa ushauri.
Miaka kama kumi na saba iliyopita, akiwa kidato cha tatu, jamaa alipewa taarifa na Dada wao wa kazi kuwa ni Mja mzito....baada ya Dada kuona jamaa anakodoa macho kodo akamwambia 'usishtuke Wewe soma siwezi kukuingiza kwenye majukumu mazito mapema hii'...kama utani na kweli Dada wala hakumuuliza tena.
Jamaa anakiri kuwa ni kweli kwa wakati huo wote mapenzi kati yake na Dada yalikuwa moto moto ile mbaya, wanakula na kupakuwa hapo ndani kama Wenye nyumba.
Ila kwa wakati huo huo kulikuwa na Kijana aliyekuwa anaishi jirani yao, alikuwa ni Kijana kufikia, na tofauti kati yake na Watoto wa familia ile ilikuwa dhahiri...alionekana zaidi kama House boy pale.
Kijana wa Watu alikuwa anamsumbua sana Dada, na Dada na Jamaa walikuwa kama vile wanashirikiana kumdhihaki Kijana yule, Jamaa alikuwa anavizia njiani na kumuita dada, basi Dada anamtolea nje alafu anakuja na kumuadithia Jamaa hivyo huishia kucheka sana. Kijana yule alikuwa tayari na umri wa kuoa, hivyo alikuwa seriou na hakukata tamaa kwa Dada, alikuwa Mlokole na Mchapa kazi kwelikweli na wala hakuhitaji kutembea na Dada yeye alikuwa anataka wakapange Nyumba waishi....Kufupisha hii stori ni kuwa Dada aliishia kuishi na yule Kaka.
Baada ya miaka kama kumi na hivi Jamaa alifanya utafiti na kugundua Dada anapoishi na yule Bwana, wakati huo tayari Dada na Bwana wake wana Watoto Watatu..Jamaa akafanya jitihada kukutana na Dada a.k.a x wake, akajaribu kumkumbusha kuhusu lile suala la Mimba Dada alimchenjia balaa, akamwambia hakuna kitu kama hicho na wala hakuwahi kumwambia kama ana mimba yake, na kumuonya Jamaa asimfuatilie tena...Sasa yapata miaka kama kumi na saba na Jamaa anatamani japo aambiwe tu kama yule Mtoto ni wake, Ndoa ya Dada ni imara na Wameshajijenga kimaisha mambo yao safi, Wana Nyumba kadhaa, Usafiri n.k..Jamaa bado ni Mlokole na Mke naye alishakuwa Mlokole.
Inavyoonyesha dada hana imani kama akimwambia yule ni mwanae yataishia hapo hapo...sasa afanyeje na DAMU NI NZITO? na jamaa na uhakika wa asilimia tisini kuwa yule Binti mrembo ni wa kwake.
Miaka kama kumi na saba iliyopita, akiwa kidato cha tatu, jamaa alipewa taarifa na Dada wao wa kazi kuwa ni Mja mzito....baada ya Dada kuona jamaa anakodoa macho kodo akamwambia 'usishtuke Wewe soma siwezi kukuingiza kwenye majukumu mazito mapema hii'...kama utani na kweli Dada wala hakumuuliza tena.
Jamaa anakiri kuwa ni kweli kwa wakati huo wote mapenzi kati yake na Dada yalikuwa moto moto ile mbaya, wanakula na kupakuwa hapo ndani kama Wenye nyumba.
Ila kwa wakati huo huo kulikuwa na Kijana aliyekuwa anaishi jirani yao, alikuwa ni Kijana kufikia, na tofauti kati yake na Watoto wa familia ile ilikuwa dhahiri...alionekana zaidi kama House boy pale.
Kijana wa Watu alikuwa anamsumbua sana Dada, na Dada na Jamaa walikuwa kama vile wanashirikiana kumdhihaki Kijana yule, Jamaa alikuwa anavizia njiani na kumuita dada, basi Dada anamtolea nje alafu anakuja na kumuadithia Jamaa hivyo huishia kucheka sana. Kijana yule alikuwa tayari na umri wa kuoa, hivyo alikuwa seriou na hakukata tamaa kwa Dada, alikuwa Mlokole na Mchapa kazi kwelikweli na wala hakuhitaji kutembea na Dada yeye alikuwa anataka wakapange Nyumba waishi....Kufupisha hii stori ni kuwa Dada aliishia kuishi na yule Kaka.
Baada ya miaka kama kumi na hivi Jamaa alifanya utafiti na kugundua Dada anapoishi na yule Bwana, wakati huo tayari Dada na Bwana wake wana Watoto Watatu..Jamaa akafanya jitihada kukutana na Dada a.k.a x wake, akajaribu kumkumbusha kuhusu lile suala la Mimba Dada alimchenjia balaa, akamwambia hakuna kitu kama hicho na wala hakuwahi kumwambia kama ana mimba yake, na kumuonya Jamaa asimfuatilie tena...Sasa yapata miaka kama kumi na saba na Jamaa anatamani japo aambiwe tu kama yule Mtoto ni wake, Ndoa ya Dada ni imara na Wameshajijenga kimaisha mambo yao safi, Wana Nyumba kadhaa, Usafiri n.k..Jamaa bado ni Mlokole na Mke naye alishakuwa Mlokole.
Inavyoonyesha dada hana imani kama akimwambia yule ni mwanae yataishia hapo hapo...sasa afanyeje na DAMU NI NZITO? na jamaa na uhakika wa asilimia tisini kuwa yule Binti mrembo ni wa kwake.