Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,110
Kwa maana hiyo, yatupasa wote tuliopo katika uhusiano, kabla ya kuendelea na kufanya maamuzi fulani tuwe tunatazama pia dalili za hatari.
Kwa upande mkubwa dalili hizi zimeegemea kuwasaidia zaidi jinsia ya kike kujua au kuwafahamu wanaume.Hii ni kwa sababu wanawake ndio ambao wamekuwa wakiumizwa zaidi na kukatishwa tamaa na mabadiliko ya tabia za wanaume mara wanapozama katika dimbwi la mapenzi, ingawa pia wapo wanaume wanaoumizwa kutokana na mabadiliko ya tabia za wapenzi wao, nao pia waweze kuzitazama dalili hizi.
Dalili:
1.Mpenzi wako anakuwa na wivu sana kwa ule muda unaotumia kuwa na wafanyakazi wenzako, marafiki na hata ndugu zako, ingawa siyo kwamba anakuhitaji kwa muda huo.
2.Anapenda kukuudhi na kukutawala, anaangalia sana kutoka na kuingia kwako, nyendo zako na hata matumizi yako ya fedha, ukimuuliza kwanini anafanya hivyo, anajiteteta kuwa anakusaidia kufanya maamuzi sahihi.
3.Taratibu anakutenga na wote waliokaribu na wewe. Pia anajaribu kukutenga na wale wanaoonekana kuwa msaada kwako kama vile, wale unaowasiliana nao kwa simu, wafanyakazi wenzako na hata ndugu zako wa karibu.
4.Huwa na tabia ya kuwalaumu sana wengine kwa matatizo anayoyapata. Mfano anapokosa kazi, anaposhindwa shuleni nk. Kila kitu ni kosa la mtu mwingine na siyo yeye.
5.Hukasirishwa na kuudhiwa na vitu vidogo vidogo na vya kawaida katika maisha ya kila siku, mfano akiambiwa afanye kazi zaidi ya muda wa ofisi, akiombwa amwangalie mtoto, anapopingwa katika kitu kidogo nk.
6.Anakuwa na tabia za kikatili kwa wanyama (wafugwao) na hata kwa watoto. Haumizwi pale anapoona maumivu au kuteseka kwa wanyama au watoto.
Anaweza kujiona anacheza au kutania bila kujua anaumiza mtoto au mnyama.
7.Ana tabia ya mabavu hususan katika tendo la ndoa, hajali hisia zako, umelala usingizini au unaumwa, bali hujali zaidi kuzitimiza haja zake.
8.Ana maneno makali ya kuumiza na kushusha hadhi, huweza kukuamsha usingizini ili akutukane au kukugombeza. Akianza malumbano hakupi upenyo wa kwenda kulala, anaweza kulalama usiku mzima.
9.Hatabiriki, ana hisia za kubadilika badilika, mara muda huu ana furaha na kuonyesha mapenzi, mara ghafla kakasirika na kutaka kumuadhibu mtu.
10.Anaweza kuwa na historia ya tabia za kikorofi na kigomvi, labda amewahi kuwa na matukio ya kuwapiga marafiki zake, akijitetea kuwa alipitiwa tu na hasira.
11.Ni mwenye vitisho na tabia za kuashiria fujo, mfano kupenda kutishia akisema Nitakuzaba vibao Nitakuua, Nitakuvunja Shingo nitakufanyia kitu mbaya n.k.
12. Ana tabia ya kupiga au kugonga vitu kwa hasira, kuvunja vitu vyako, kukurushia vitu wewe au watoto kwa hasira.
13.Hutumia nguvu anaposisitiza hoja yake, mfano, kukushika nguo au kukukandamiza ukutani na mara nyingine kukusukuma.
Tafiti zimegundua kwamba, kama mtu anaonyesha tabia za fujo na kijeuri wakati wa urafiki au uchumba kuna uwezekano mkubwa wa kuwa hatari zaidi mara atakapoingia kwenye ndoa. Kamwe usijidanganye na kujifariji kwamba hiyo vitabia anayoionyesha sasa eti atabadilika tu mara mkioana.
Kumbuka , fujo huzaa fujo, na ujeuri huzaa ugomvi na kwa haraka, vyote hivi huua mapenzi kwa wale wanaopendana.
Kwa upande mkubwa dalili hizi zimeegemea kuwasaidia zaidi jinsia ya kike kujua au kuwafahamu wanaume.Hii ni kwa sababu wanawake ndio ambao wamekuwa wakiumizwa zaidi na kukatishwa tamaa na mabadiliko ya tabia za wanaume mara wanapozama katika dimbwi la mapenzi, ingawa pia wapo wanaume wanaoumizwa kutokana na mabadiliko ya tabia za wapenzi wao, nao pia waweze kuzitazama dalili hizi.
Dalili:
1.Mpenzi wako anakuwa na wivu sana kwa ule muda unaotumia kuwa na wafanyakazi wenzako, marafiki na hata ndugu zako, ingawa siyo kwamba anakuhitaji kwa muda huo.
2.Anapenda kukuudhi na kukutawala, anaangalia sana kutoka na kuingia kwako, nyendo zako na hata matumizi yako ya fedha, ukimuuliza kwanini anafanya hivyo, anajiteteta kuwa anakusaidia kufanya maamuzi sahihi.
3.Taratibu anakutenga na wote waliokaribu na wewe. Pia anajaribu kukutenga na wale wanaoonekana kuwa msaada kwako kama vile, wale unaowasiliana nao kwa simu, wafanyakazi wenzako na hata ndugu zako wa karibu.
4.Huwa na tabia ya kuwalaumu sana wengine kwa matatizo anayoyapata. Mfano anapokosa kazi, anaposhindwa shuleni nk. Kila kitu ni kosa la mtu mwingine na siyo yeye.
5.Hukasirishwa na kuudhiwa na vitu vidogo vidogo na vya kawaida katika maisha ya kila siku, mfano akiambiwa afanye kazi zaidi ya muda wa ofisi, akiombwa amwangalie mtoto, anapopingwa katika kitu kidogo nk.
6.Anakuwa na tabia za kikatili kwa wanyama (wafugwao) na hata kwa watoto. Haumizwi pale anapoona maumivu au kuteseka kwa wanyama au watoto.
Anaweza kujiona anacheza au kutania bila kujua anaumiza mtoto au mnyama.
7.Ana tabia ya mabavu hususan katika tendo la ndoa, hajali hisia zako, umelala usingizini au unaumwa, bali hujali zaidi kuzitimiza haja zake.
8.Ana maneno makali ya kuumiza na kushusha hadhi, huweza kukuamsha usingizini ili akutukane au kukugombeza. Akianza malumbano hakupi upenyo wa kwenda kulala, anaweza kulalama usiku mzima.
9.Hatabiriki, ana hisia za kubadilika badilika, mara muda huu ana furaha na kuonyesha mapenzi, mara ghafla kakasirika na kutaka kumuadhibu mtu.
10.Anaweza kuwa na historia ya tabia za kikorofi na kigomvi, labda amewahi kuwa na matukio ya kuwapiga marafiki zake, akijitetea kuwa alipitiwa tu na hasira.
11.Ni mwenye vitisho na tabia za kuashiria fujo, mfano kupenda kutishia akisema Nitakuzaba vibao Nitakuua, Nitakuvunja Shingo nitakufanyia kitu mbaya n.k.
12. Ana tabia ya kupiga au kugonga vitu kwa hasira, kuvunja vitu vyako, kukurushia vitu wewe au watoto kwa hasira.
13.Hutumia nguvu anaposisitiza hoja yake, mfano, kukushika nguo au kukukandamiza ukutani na mara nyingine kukusukuma.
Tafiti zimegundua kwamba, kama mtu anaonyesha tabia za fujo na kijeuri wakati wa urafiki au uchumba kuna uwezekano mkubwa wa kuwa hatari zaidi mara atakapoingia kwenye ndoa. Kamwe usijidanganye na kujifariji kwamba hiyo vitabia anayoionyesha sasa eti atabadilika tu mara mkioana.
Kumbuka , fujo huzaa fujo, na ujeuri huzaa ugomvi na kwa haraka, vyote hivi huua mapenzi kwa wale wanaopendana.