Dalili/viashiria vya mwanzo kabla ya ya biashara yako kufa/kufilisika

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Jun 4, 2011
7,789
8,914
Niukweli usipingika kwamba Biashara haiwezi kufa kama ajari vile yaani leo ilkuwa katikakiwango cha juu halafu kesho imekufa.

- Biashara mpaka kufikia kufa nikwamba kuna muendelezo wa dalili nyingi sanaambazo hupelekea biashara au mfanya biashara kufilisika, ni kama vita, vitakablya kuanza huwa kuna viashiria vingi sanaambavyo huonyesha dalili za vita kuzuka.

VIASHILIA VYA MWANZO KABLA YA BIASHARA YAKOKUFA NI KAMAHIVI HAPA CHINI


1. WAFANYA KAZI WAKO HAWANA ARI NA KAZI,

Kitendo cha wafanya kazi kukosamalali/hamasa ya kufanya kazi ni moja ya dalili za mwanzo kabisa kabla yakampuni yako haijafikia mwisho, hapa mara nyingi wafanya kazi wanakuwa hawanaari ya kazi, na hawajitumi kufanya kazi kama mwanzo, na hii husababishwa namambo mengi sana, na madhara ya hii, huhamia kwenye wateja na mali za kampuni

2.WAFANYA KAZI WAKO HAWAONGEI NA WATEJAVIZURI

H
apa wafanya kazi hufikia hata steji ya kuwagombeza wateja na hata kupiganana wateja wako

3. WATEJA KUACHA KUONGELEA MAZURI YAKAMPUNI YAKO/BIASHARA YAKO

- Wateja mara nyingi ndo hutumikakutangaza biashara yako, ila hiki kipindi wateja wanakuwa wanaongelea mabaya yakampuni yako na si mazuri ya kampuni yako tena, na mara nyingi hapa watakuwawakilalamika kuhusu huduma zako au bidhaa zako,
Hapa jujikita kuongelea mazuri yamshindani wako na mabaya yakwako

4. SPEED KUBWA YA KUONDOKA KWA WAFANYA KAZIWAKO MUHIMU,

Ukiona kila kukicha wafanya kazi wakowalio muhimu wanaondoka jua ni moja ya dalili za biashara yako kuelekea kufa,hapa unakuwa unaondokewa na wafanyakazi ambao ni tegemeo kwa kampuni yako

5. WASAMBAZAJI WA VFAA MBALIMBALI NA VITUVINGINE WANAANZA KUKUGOMEA

Ha
pa wale walio kuwa wakikusambazia vitu muhimu wanaaza kuacha na kuanzishamgomo kama wa madakitari vile, hii ni moja ya dalili mbaya sana,wasambazaji wako hufikia mahali wakaacha kukusambazia bidhaa/huduma

6.Kupungua kwa faida/ Hakuna faida
Hapa ni biashara kujiendesha kwafaida na ghalama za uendeshaji huwa juu kuliko mapato,

7. Kushindwakulipa bili mbalimbali kama kodi ya mapato,Bili ya umeme, maji na kazalika
Hii huwa ni moja ya dalili mbaya kwabiashara yako, inapofikia ukashindwa kulipa bili mbalimbali ni alama ya kampuniyako kufikia mwisho wake, make matokeo ya kutolipa hizo bili nazani unayafahamumwenyewe

8. Washindanikuwa wengi sanakuliko mwanzo,
Unapo ona washindani wengi sana katika secta yako au katikakazi ulizo kuwa unafanya ni dalili mbaya sanakwakampuni yako na hapa usipo chukua hatua za kutosha ni kufunga kampuni ndosuluhisho la mwisho

  1. SOKO/MASOKO ULIYO KUWA UNAYATEGEMEA YAMEONDOKA
- Kuna kipindiutakuta masoko yako yote hayapo tena, mahali ulipo kuwa ukiuzia kuku wako kwasasa wahitaji kuku wako tena, ulipo kuwa ukiuza maziwa kwa sasa hawahitajimaziwa yako tena kwa sababu wana msambazaji mwingine, hii ni dalili mbaya sanakwako ya biashara yako kufa
-
  1. WATEJA WAKO MUHIMU WANAHAMIA KWA WASHINDANI WAKO
- Wateja ulio kuwa ukiwauzia kuku kwa sasa hawachukui tena kuku wakobali wanachukua kwa mfugaji mwingine, wateja wa hoteli yako kwa sasa hawalikwako wanakula hoteli nyingine kabisa, wateja wa gest yako wamehamia gestnyingine.
- HII NI MOJA YA DALILI KUU KABISA ZA BIASHARA YAKO KUFIKIA MWISHO

  1. MALALAMIKO JUU YA BIDHAA/HUDUMA ZAKO YAMEZIDI
Utakuta kila kukicha watu wanao kulalamikia kuhusu bidhaa zako/huduma yakowanazidi,

  1. WATEJA WAKO MUHIMU/TEGEMEO KUPUNGUZA KIWANGO CHA MANUNUZI KWAKO
. MFANO
: wateja wako muhimu kupunguza ununuzi kwako, walikuwa wananunua kuku 500sasa wananua kuku 100 tu, walikuwa wananunua bidhaa za karibia lako moja kwawiki dukani mwako sasa wananunua za elfu 30,000 tu,
Mteja wako muhimu na tegemeo alikuwa ananunua lita 30 za maziwa kwa sikukwako sasa ananunua lita 5 tu,
Mteja wako muhimu alikuwa akinunua trey 100 za mayai kwa mwezi kutoka kwakosasa ananunua trey 20 tu

  1. HUWAJALI WATEJA WAKO TENA
  1. Unarudia makosa yaleyale
Ukiona kila mara unaludia makosa yaleyale ujue ni dalili mbaya sanakwako

  1. KUWALIPA WATU/KAMPUNI/TAASISI ZINAZOKUDAI NJE YA MUDA MLIO KUBALIANA
, Ukianza kuwalipa watu wanao kudai nje ya muda wa makubaliona ni isharambaya sana kwani kitakachafuata ni hao wadeni wako kushindwa kufanya kazi tena na wewe

  1. KUSHINDWA KULIPA MIKOPO YA BENKI

  1. Kuanza kuuza baadhi ya mali za kampuni yako ili kukidhi mahitaji yako.
Ikifikia ukaanza kuuza badhi ya malizakampuni yako ili kuendeshea kampuni yako ujue ndo mwanzo wa kampuni yakokuingia kwenye matatizo

18 KUBADILIJINA LA KAMPUNI GHAFULA
Hii ni moja ya dalili mbaya sanakwako

  1. KUENDELEA KUPATA HASARA KWENYE KAMPUNI YAKO

Wakuu kwakifupi hizo ni chache kati ya dalili nyingi sanaambazaohuanza kutokea kabla ya wewe kufunga lasimi kampuni yako
Narudiakusema kampuni haifi kwa siku moja ila kuna dalili kama tu dalili za mgonjwa
 
Kwahiyo mtu akiona hizo dalili inabidi afanyaje?

Inatakiwa uchukue hatua, na moja ya hatuazinaweza kuwa ni either kufunga kampuni yako kabisa au kuona utawezaje kuiokoakampuni yako,

- Biashara inapo kuwa mbaya zaidi uamuzi wa kufunga nao waga ni mzuri kulikouendelee kun'ga'n'gania na mwisho wa siku unongeza madeni bure,

 
Inatakiwa uchukue hatua, na moja ya hatuazinaweza kuwa ni either kufunga kampuni yako kabisa au kuona utawezaje kuiokoakampuni yako,

- Biashara inapo kuwa mbaya zaidi uamuzi wa kufunga nao waga ni mzuri kulikouendelee kun'ga'n'gania na mwisho wa siku unongeza madeni bure,


sasa komandoo, hakuna entrepreneur anaanza business akiexpect kufail. Lets say nina company na nimeshanote signs zote hizo za kuloose customers, employees wangu hawana morale ya kazi na wengine wanaquit, cashflow inasoma negative & other signs, kama nimekufata for advice or wewe ni advisor wa my company, what would u advice me? Nifunge company? Huoni kufunga company ni dalili ya kushindwa wakati sikuanza ili nishindwe.? Do u mean companies zikiexperience situation kama hiyo hakuna strategies zozote wanawezafanya wakarudi kwenye mstari kabla ya kufikia hatua ya kuamua kufunga?
 
sasa komandoo, hakuna entrepreneur anaanza business akiexpect kufail. Lets say nina company na nimeshanote signs zote hizo za kuloose customers, employees wangu hawana morale ya kazi na wengine wanaquit, cashflow inasoma negative & other signs, kama nimekufata for advice or wewe ni advisor wa my company, what would u advice me? Nifunge company? Huoni kufunga company ni dalili ya kushindwa wakati sikuanza ili nishindwe.? Do u mean companies zikiexperience situation kama hiyo hakuna strategies zozote wanawezafanya wakarudi kwenye mstari kabla ya kufikia hatua ya kuamua kufunga?

Mkuu kuna wakati unaweza kuta solution pekee ya kunusuru kampuni yako ni kuiuza au kuifunga kabisa, na hii ni ili ikunusuru na madeni zaidi, make unaweza kuta the more unavyo operate ndo the more unavyo pata hasara na kutengeneza madeni mengi sana ambayo yatakuja kukuwia vigumu kuyalipa,

Washauri wanaweza kukuambia hapa no way out ni kufunga au kuuza kampuni, unaweza kuta kampuni iko katika hali ambayo haitaweza kukuposheka kamwe, wala kujiendesha tena wewe utafanyaje? competetitor wanakuwa wengi sana, wateja wamekukumbia, wafanyakazi wameondoka karibia wote, umeshindwa kurudisha mikopo ya mabenki.

Hata makampuni makubwa yanayo filisika si kwamba unakuta hayana kitu kabisa bali hufikia hapo ili kujinusuru na matatizo zaidi,

Kufunga biashara si kushindwa, unafunga unakaa unatafakari unakuja na mbinu mpya, na hii huwa moja ya sehemu ya kujifunzia ili usije fanya makosa tena

 
Back
Top Bottom