Si umeona eeh?Wadau, huku barabarani naona mkusanyiko mkubwa wa watu na pikipiki za kutosha. Nilisikia kutakuwa na mgomo, je ndio huu? shida ni nini?
Si umeona eeh?
Kwa ufupi hali ni mbaya sana barabarani.
Abiria wanapata shida isiyo kifani, maana ni route-march iliyoenda shule!
Sababu:
Madereva na makondakta wa vifodi wanalalamikia suala la wao kukamatwa kila wakati na kuswekwa ndani kwa makosa yasiyo na maelezo ya kuridhisha!
Mfano, dereva akishusha abiria mahali, anakamatwa na kupigwa faini au kutupwa selo, wakati barabara za Arusha nyingi hazina vituo official!
Kuna madereva wasiopungua 5 wapo Kisongo Gereza la mkoa, na hivyo madereva wote wameamua kuwa hawatatoa huduma ya usafiri hadi hao wenzao watakapoachiliwa huru bila masharti yoyote!
Hakika watoto wa wa shule za Saint Kayumba Kiswahili Medium wako kwenye wakati mgumu sana. Leo barabarani zinatamba gari za watu binafsi, gari za rangi ya Njano za shule za Watakatifu(St. PakaJimmy) na bodaboda!kwa kweli polisi wa barabarani Arusha huwa ni waonevu sana......sasa madhara yanaenda kwa wananchi.........watoto wa shule ndio wanaoteseka zaidi........
Mji wa Arusha lea ni balaa tupu, usafiri wa watu wa kawaida comon man hakuna. Watu wa daladala wamegoma hivyo kwenda kazini leo itakuwa shida. Madai yao nikwamba wananyanyaswa na trafiki polisi na kuonewa watu wao wanawekwa ndani bila sababu. Bila shaka imechangiwa na frustrations za maisha, kupanda ovyo kwa mafuta na gharama za maisha yote hiyo inachangia!!!!!! Ngoja tuone hadi mchana itakuwaje???????????
katika mji wa Arusha leo asubuhi watu wanaotumia daladala kama usafiri wa kuwapeleka ktk shughuli zao wamejikuta wakikumbana na adha ya kutokuwa na usafiri baada ya madereva hao kugoma kutoa huduma hio wakishinikiza wenzao waliokamatwa na polisi wa barabarani wawaachilie wenzao. Mji mzma wa Arusha raia wamebidi watumie boda boda na wale wasio na uwezo wa kumudu usafiri uwo wa bodaboda imewabidi watembee umbali mrefu kufika makazini na shuleni.
Nawasilisha