Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENTS OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Daktari wa Rais Kikwete awa Profesa
Daktari Mkuu Binafsi wa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Janabi amepandishwa daraja la usomi wa utibabu na kuwa Profesa wa Chuo cha Utibabu cha South Carolina (MUSC) kitengo cha magonjwa ya moyo nchini Marekani kuanzia Oktoba Mosi, mwaka huu, 2010.
Dk. Janabi (47) amekubali kupandishwa daraja hilo ambako atakuwa Profesa Mshiriki wa Tiba katika Idara ya Utibabu, Sehemu ya Tiba ya Moyo, kwenye chuo hicho kilichoko mjini Charlestown.
Hata hivyo, Dk. Janabi ambaye ni mmoja wa Watanzania wachache wenye sifa na ujuzi mkubwa zaidi katika udaktari, anaendelea kuwa Daktari Mkuu Binafsi wa Rais Kikwete.
MUSC ni chuo kikuu kikubwa zaidi na maarufu zaidi kuliko kingine chochote katika Jimbo la South Carolina na anakuwa Mtanzania wa kwanza kupata utambuzi na heshima ya namna hiyo kwenye chuo hicho ambacho amekuwa nao kikazi tangu mwaka 2003.
Dk. Janabi alipata Shahada ya Uzamivu (PhD) mwaka 2000 nchini Japan katika fani ya magonjwa ya moyo. Mbali ya kuwa Daktari Mkuu Binafsi wa Rais Kikwete, mtaalam huyo wa magonjwa ya moyo pia ni mtaalam bingwa wa masuala ya moyo kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Mkufunzi wa Heshima katika Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi cha Muhimbili (MUHAS).
Dk. Janabi pia ni Mwanasayansi Mwandamizi katika Utafiti wa Chanjo ya Ukimwi na Mkurugenzi Mwakilishi (Tanzania) wa Taasisi ya Kimataifa ya Madaktari wa Africa.
Amekuwa Daktari Mkuu Binafsi wa Rais Kikwete tokea 2006.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
22 Oktoba, 2010