Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,109
Kituko cha mwaka kimeibuka katika hospitali ya wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, baada ya daktari mmoja wa upasuaji hospitalini kumuacha mgonjwa kwenye kitanda cha upasuaji na kukimbilia dukani kununua kifaa kilichokosekana kwa zoezi hilo.
Ni tukio lisilo la kawaida pengine kutokea hapa nchini, likionyesha jinsi sekta ya afya ilivyoelemewa katika usambazaji wa vifaa muhimu vya huduma katika hospitali za serikali.
Daktari huyo(jina linahifadhiwa kwa sasa), alibaini kukosekana kwa moja ya vifaa muhimu wakati wa upasuaji huku akiwa tayari ameshaanza upasuaji na haraka akatimkia dukani kununua kifaa hicho chenye thamani ya sh.1,000/ tu.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni katika hospitali hiyo, ambapo daktari huyo (jina limehifadhiwa) alichukua hatua hiyo
baada ya juhudi za kupata kifaa hicho chenye thamani ya Sh.1,000/- kushindikana.
Kituko hicho kiliibuliwa juzi na Mkurugenzi wa Manispaa wa Temeke, Magreth Nyalile baada ya kuitisha kikao cha dharura cha madaktari wa hospitali hiyo, akitaka maelezo ya kina kwanini utoaji huduma kwenye hospitali hiyo umedorora sana mwaka jana.
Habari za uchunguzi kutoka kwenye hospitali hiyo zinasema daktari huyo siku ya tukio alikuwa kwenye chumba cha upasuaji kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura.
Akiwa katikati ya zoezi hilo, aligundua kifaa hicho kimekosekana ndipo alipotoa taarifa kwa mtu anayehusika na ununuzi wa vifaa vya dharura.
Jambo la kusikitisha ni kwamba mfanyakazi huyo anayehusika na ununuzi aligoma kwenda kununua kifaa hicho kwa maelezo kwamba sharti kwanza apewe hati ya ununuzi (invoice) inayoonyesha gharama halisi ya kifaa hicho.
Kufuatia jibu hilo, daktari huyo kwa ujasiri aliamua kumuacha mgonjwa wake kitandani na kisha alikimbilia moja ya maduka yaliyo nje
ya hospitali hiyo kwenda kununua kifaa hicho na kuokoa maisha ya mgonjwa huyo.
Akionekana kuchukizwa na tukio hilo, Nyalile alisema mtu aliyesababisha kutokea kwa tukio hilo hatakuwa na msamaha kwani lazima
achukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wafanyakazi wasiowajibika.
Hata hivyo alimpongeza daktari aliyechukua hatua hiyo na kumuelezea ni mtu ambaye anafuata maadili yake ya kazi na hakutaka mgonjwa apoteze maisha yake kwa kutokuwepo kwa kifaa chenye gharama isiyozidi Sh.1000/-.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Kasheshe kweli Hospitali zetu tutakwisha sana namna hii Hata vifaa hakuna?
Ni tukio lisilo la kawaida pengine kutokea hapa nchini, likionyesha jinsi sekta ya afya ilivyoelemewa katika usambazaji wa vifaa muhimu vya huduma katika hospitali za serikali.
Daktari huyo(jina linahifadhiwa kwa sasa), alibaini kukosekana kwa moja ya vifaa muhimu wakati wa upasuaji huku akiwa tayari ameshaanza upasuaji na haraka akatimkia dukani kununua kifaa hicho chenye thamani ya sh.1,000/ tu.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni katika hospitali hiyo, ambapo daktari huyo (jina limehifadhiwa) alichukua hatua hiyo
baada ya juhudi za kupata kifaa hicho chenye thamani ya Sh.1,000/- kushindikana.
Kituko hicho kiliibuliwa juzi na Mkurugenzi wa Manispaa wa Temeke, Magreth Nyalile baada ya kuitisha kikao cha dharura cha madaktari wa hospitali hiyo, akitaka maelezo ya kina kwanini utoaji huduma kwenye hospitali hiyo umedorora sana mwaka jana.
Habari za uchunguzi kutoka kwenye hospitali hiyo zinasema daktari huyo siku ya tukio alikuwa kwenye chumba cha upasuaji kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa dharura.
Akiwa katikati ya zoezi hilo, aligundua kifaa hicho kimekosekana ndipo alipotoa taarifa kwa mtu anayehusika na ununuzi wa vifaa vya dharura.
Jambo la kusikitisha ni kwamba mfanyakazi huyo anayehusika na ununuzi aligoma kwenda kununua kifaa hicho kwa maelezo kwamba sharti kwanza apewe hati ya ununuzi (invoice) inayoonyesha gharama halisi ya kifaa hicho.
Kufuatia jibu hilo, daktari huyo kwa ujasiri aliamua kumuacha mgonjwa wake kitandani na kisha alikimbilia moja ya maduka yaliyo nje
ya hospitali hiyo kwenda kununua kifaa hicho na kuokoa maisha ya mgonjwa huyo.
Akionekana kuchukizwa na tukio hilo, Nyalile alisema mtu aliyesababisha kutokea kwa tukio hilo hatakuwa na msamaha kwani lazima
achukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wafanyakazi wasiowajibika.
Hata hivyo alimpongeza daktari aliyechukua hatua hiyo na kumuelezea ni mtu ambaye anafuata maadili yake ya kazi na hakutaka mgonjwa apoteze maisha yake kwa kutokuwepo kwa kifaa chenye gharama isiyozidi Sh.1000/-.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Kasheshe kweli Hospitali zetu tutakwisha sana namna hii Hata vifaa hakuna?