Daktari Kitila Mkumbo haya ndiyo uliyoyatabiri Uingereza au kuna Mengine Yaja.....

Meitinyiku L. Robinson

JF-Expert Member
Aug 29, 2011
412
90
Ikiwapendaza wakuu;

Magazeti ya leo yamesheheni juu ya Kauli ya Zitto Zuberi Kabwe na nia yake ya Urais ikielezwa kuwa kauli hiyo inaelekea kukigawa Chama Binafsi bado sijaona tatizo lolote liwalo lile kwa kauli hiyo manake kimsingi kinachoonekana kukwaza ama viongozi wa chama au makada ni swala la muda. Ati huu si muda muafaka nimejaribu kujiuliza muda muafaka ni upi aidha ulioainishwa ndani ya Katiba ama kwenye Sheria nyinginezo ni upi bila kupata majibu.

Ushawishi unaojengwa ni kwamba ati muda huu Chama kiko busy na Kampeni Arumeru Mashariki bado hii haiwezi kuwa hoja manake kama ushindi ni wa Chadema basi utakuwa na kama si Chadema bado itabaki kuwa hivyo hakuna haja ya kuendekeza woga mtu mmoja alishawahi kusema mtu mwoga hufa kabla hata ya siku yake kufikia. Labda ingejengwa hoja kwamba Zitto hashikiri Kampeni na badala yake anajikita na vyombo vya habari hapo tungeweza kufikiria mara mbili lakini Zitto alikuwa Mwanza, Arumeru amekuwepo, sijui Uzini na kwingineko.

Hili ndilo lililonifanya kuwaza na kufikiri kuwa labda yale aliyoyasema Dr. Mkumbo kule Uingereza yakawekwa humu juu ya mpasuko ndani ya Chama ndiyo hayo yanayoanza kuonekana manake tatizo si nia ya Zitto bali Kauli na majibu kutoka kwa viongozi wengine; mathalan Katibu Mkuu ambaye naye anajitahidi kujificha chini ya Mwamvuli wa muda akisema huu si muda muafaka. Yeye anaonekana kuwa mmoja kati ya wanaoungwa mkono kugombea sasa hizi kauli angeacha zitolewa na wanaowatazama manake ni rahisi sana kufikiri kuwa kaamua kusema hivyo kwa sababu naye ni mmoja kati ya wanaoutaka.

Ni wazi kwamba Mshauri Mkuu wa CHADEMA anajua mengi na nahisi aliamua kusema hayo huko kwa sababu yalimfika shingoni aidha kuna ushauri aliotoa juu ya pande hizo zitakazo Uraisi ila ushauri wake ukapuuzwa ama naye kaanza kuandamwa baada ya watu humu kumshauri naye agombee Uraisi.

WanaCDM mtakuwa wakali ila mazee mpende msipende lazima changamoto mzipata, mzikubali na mtafute namna ya kuzitatua lakini mkijifanya kila kitu kiko sawa ama hamtaki yenu yajadiliwe madhara yake ipo siku ya Sirini yatatandazwa nje mchana kweupe......... Na huo ndio mwanzo tu!

Accept critiques and let the same be your best friend and consequently your fault will be easily determined
 
Hebu PASTE hapa kauli ya Dr Kitila Mkumbo aliyosema akiwa huko Uingereza kwanza!

Mkuu kuna kauli inasemekana aliitoa huko ughaibuni kwamba kuna minyukano na makundi ndani ya CDM yakilenga Urais wa 2015. Kauli hiyo iliwekwa humu wiki iliyopita na Dr. Mkumbo hakuikubali wala kuikanusha japo alikuwa akifuatilia post kwenye ule uzi.
 
Tuache mambo ya kugesi..hebu tuambie Dr Mkumbo alisema nini? Halafu ndio uje useme wewe unasema nini juu ya kauli ya Dr Mkumbo..nakubaliana na hoja yako kuwa ishu ya uraisi lazima itakuwa hot,na si kwa CHADEMA karibia kwa vyama vyote vyenye demokrasia ndani yake.Ila natamani kujua Dr Mkumbo alisema nini huko UK kabla ya kuanza kuchangia kwa kina hii hoja yako.
 
Tuache mambo ya kugesi..hebu tuambie Dr Mkumbo alisema nini? Halafu ndio uje useme wewe unasema nini juu ya kauli ya Dr Mkumbo..nakubaliana na hoja yako kuwa ishu ya uraisi lazima itakuwa hot,na si kwa CHADEMA karibia kwa vyama vyote vyenye demokrasia ndani yake.Ila natamani kujua Dr Mkumbo alisema nini huko UK kabla ya kuanza kuchangia kwa kina hii hoja yako.


Mshauri mkuu wa chadema ndugu, Kitila Mkumbo alitembelea Uingereza katika miji ya London na Readings kuanzia tarehe 5 Machi na 6 Machi 2012 na kuondoka tarehe 10 Machi, 2012.


Miongoni mwa mambo aliyotueleza ni kuwepo kwa mpasuko wa nani anasitahiri kubeba/kupeperusha bendera ya chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kati ya Freeman Mbowe na Dk. Slaa. Mkumbo anasema kuna kambi mbili zinazopingana ndani ya chadema kuhusu suala hilo.

Wanaomuunga mkono Dk. Slaa wanasema kwamba ni mtu anayejua kujenga hoja, ana mvuto, wananchi wanamwamini kuliko Mbowe lakini pia kwamba Dk. Slaa alishinda uchaguzi mkuu wa 2010 kabla ya kuchakachuliwa. Kwa sababu hiyo akipewa nafasi tena 2015 na chadema ikisimamia vyema uchaguzi huo Dk. Slaa anaweza kuwa Rais ajaye.



Kambi ya mbowe inasema kwamba alitumia asilimia 72 ya pesa yake katika kufanikisha kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010, wapo wanaodai chama kirudi mikononi mwa Mbowe kwa sababu hivi sasa ameimarika zaidi kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu ujao. My take: Kuendeleza huo mpasuko kutaisaidia ushindi wa CCM katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.


Wadau nimeleta kwenu tusaidiane namna ya kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kambi mbili hizi ili chadema kiendelee kuwa chama kikuu cha upinzani na pengine kushika dola mwaka 2015. Source: Nilikuwa Uingereza miongoni mwa wafuasi wa chadema tuliohudhuria kikao cha kamanda wetu Kitila.

Habari ndio hiyo,haya changia sasa.
 
This is a big Joke!!

Hii kampeni ya makusudi ya kumuongelea mtu badala ya issue.........Yani Zitto ndio mjadala sasa hivi?? Kweli?
Labda tumelogwa!!

Huyu Zitto na mwenzake January ni wapuuzi sana, tena sana, and I dare talk openly about upumbavu wao.
Wakati huu ambao tupo kwenye mchakat wa katiba mpya, wao wanataka issue ya umri wa kugombea uraisi ushushwe kwasababu wao ni vijana, kwasababu wao wanataka kugombea??

1) Issue ya Umri sio swala la msingi hata kidogo, tnahitaji kuongelea majukumu na nguvu za rais ndani ya katiba. Rais yeyote ajaye, awe na miaka 20 au 60, tunataka majukumu yake yawe haya, na nguvu yake kisheria iwe hiii......HIYO NDIO ISSUE.

2) Kwasababu tu ZItto na Makamba ni vijana chini ya miaka 35 kwa sasa, basi wanataka umri ushushwe huku wakiwa wamesema wanautaka urais?? huu ndio unafiki na ubinafsi wa Zitto and Co. Je, mtu wa namna hii, akifikisha miaka 60, na akawa rais, si anaweza akabadilisha tena katiba isomeke 'hakuna kugombea urais kama huna miaka 60''??

Be careful na huu mchezo unaondelea people!!!:attention:
 
Habari ndio hiyo,haya changia sasa.

Mshauri mkuu wa chadema ndugu, Kitila Mkumbo alitembelea Uingereza katika miji ya London na Readings kuanzia tarehe 5 Machi na 6 Machi 2012 na kuondoka tarehe 10 Machi, 2012.
Miongoni mwa mambo aliyotueleza ni kuwepo kwa mpasuko wa nani anasitahiri kubeba/kupeperusha bendera ya chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kati ya Freeman Mbowe na Dk. Slaa. Mkumbo anasema kuna kambi mbili zinazopingana ndani ya chadema kuhusu suala hilo.

Wanaomuunga mkono Dk. Slaa wanasema kwamba ni mtu anayejua kujenga hoja, ana mvuto, wananchi wanamwamini kuliko Mbowe lakini pia kwamba Dk. Slaa alishinda uchaguzi mkuu wa 2010 kabla ya kuchakachuliwa. Kwa sababu hiyo akipewa nafasi tena 2015 na chadema ikisimamia vyema uchaguzi huo Dk. Slaa anaweza kuwa Rais ajaye.



Kambi ya mbowe inasema kwamba alitumia asilimia 72 ya pesa yake katika kufanikisha kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010, wapo wanaodai chama kirudi mikononi mwa Mbowe kwa sababu hivi sasa ameimarika zaidi kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu ujao. My take: Kuendeleza huo mpasuko kutaisaidia ushindi wa CCM katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.


Wadau nimeleta kwenu tusaidiane namna ya kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kambi mbili hizi ili chadema kiendelee kuwa chama kikuu cha upinzani na pengine kushika dola mwaka 2015. Source: Nilikuwa Uingereza miongoni mwa wafuasi wa chadema tuliohudhuria kikao cha kamanda wetu Kitila.

Utoto huu!
Hii ni thread aliyopandisha mwanajamvi hapa!
Kinachotakiwa ni Kauli original, au HyperLink inayoquote alipoongea Live toka huko alikokuwa!
Uswazi wa nini?
 
Yaani watu wako so busy.. trying 2 create chaos & misunderstandin ndani ya CDM..! Mnadhani mkifanya hivyo ndo maisha ya watanzania yataboreka..? Kuna wanaoshabikia hapa wakifika majumbani mwao wanakunywa maji ya kisima.. Biashara zao zinakufa kwa kukosekana umeme.. Bei ya vyakula imepanda kiasi amepunguza kula milo mitatu kwa cku.. Kwa ujinga wao wanaamini Mungu ndo ametaka tuwe hivi.. Wananchi wameamka sasa.. Kama Zito ametamka haya bila ya kusukumwa sawa.. Lakini kama atakuwa anatumika katika hili la kuleta mfarakano.. Basi ajue atashindwa..
 
Kitila Mkumbo anasemekana kutabiri mpasuko wa chadema akiwa uingereza kama hali hiyo haitathibitiwa kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015.

Wakati kila mtu kaelekeza macho, mdomo na masikio yake Arumeru Zitto anakuja na nia yake ya kugombea Urais.
 
hakuna mpasuko wowote.... ni kwamba watu wanataka kuonysha nia ya kugombea

nimewaza nikagundua ni bora wafanye mapema ili kama ni vita iende na ipoe kuliko waanze vijembe in 2014

na kwa jinsi hali inavyokwenda, we may fail to differentiate nia ya hasa ya mgombea yoyote yule zaidi ya personal fulfilmemt

sioni kwa zitto wala slaa mtu anayetaka kugombea ili asaide wananchi... ni ile self actualization tu
 
This is a big Joke!!

Hii kampeni ya makusudi ya kumuongelea mtu badala ya issue.........Yani Zitto ndio mjadala sasa hivi?? Kweli?
Labda tumelogwa!!

Huyu Zitto na mwenzake January ni wapuuzi sana, tena sana, and I dare talk openly about upumbavu wao.
Wakati huu ambao tupo kwenye mchakat wa katiba mpya, wao wanataka issue ya umri wa kugombea uraisi ushushwe kwasababu wao ni vijana, kwasababu wao wanataka kugombea??

1) Issue ya Umri sio swala la msingi hata kidogo, tnahitaji kuongelea majukumu na nguvu za rais ndani ya katiba. Rais yeyote ajaye, awe na miaka 20 au 60, tunataka majukumu yake yawe haya, na nguvu yake kisheria iwe hiii......HIYO NDIO ISSUE.

2) Kwasababu tu ZItto na Makamba ni vijana chini ya miaka 35 kwa sasa, basi wanataka umri ushushwe huku wakiwa wamesema wanautaka urais?? huu ndio unafiki na ubinafsi wa Zitto and Co. Je, mtu wa namna hii, akifikisha miaka 60, na akawa rais, si anaweza akabadilisha tena katiba isomeke 'hakuna kugombea urais kama huna miaka 60''??

Be careful na huu mchezo unaondelea people!!!:attention:

Haihitaji degree kujua Zito anamtumikia CCM. Coverage za leo zikishafika Arumeru zitasema kumbe hiki chama wanagombana basi wanapiga kura za hasira kwa CCm. zito anajua fika mwisho wa huu mchezo ni nini! J.K nyerere hakuhitaji kutumia nguvu ili awe Rais. Wazee waliona kijana anafaa. Ukiangalia average age ya kina nyerere wakati wanashika nchi ilikuwa ni miaka 40 kushuka. Ndio maana waandishi wa riwaya za WILLY GAMBA na JORAM KIANGO walipokuwa wakiwakilisha lugha ya picha ya TISS walikuwa wanawaonesha wapelelezi wao kama vijana wa miaka 28 tu! Leo vijana wanaomba kwa nguvu kupewa madaraka huku masikioni wameweka IPOD!

 
Ikiwapendaza wakuu;

Magazeti ya leo yamesheheni juu ya Kauli ya Zitto Zuberi Kabwe na nia yake ya Urais ikielezwa kuwa kauli hiyo inaelekea kukigawa Chama Binafsi bado sijaona tatizo lolote liwalo lile kwa kauli hiyo manake kimsingi kinachoonekana kukwaza ama viongozi wa chama au makada ni swala la muda. Ati huu si muda muafaka nimejaribu kujiuliza muda muafaka ni upi aidha ulioainishwa ndani ya Katiba ama kwenye Sheria nyinginezo ni upi bila kupata majibu.

Ushawishi unaojengwa ni kwamba ati muda huu Chama kiko busy na Kampeni Arumeru Mashariki bado hii haiwezi kuwa hoja manake kama ushindi ni wa Chadema basi utakuwa na kama si Chadema bado itabaki kuwa hivyo hakuna haja ya kuendekeza woga mtu mmoja alishawahi kusema mtu mwoga hufa kabla hata ya siku yake kufikia. Labda ingejengwa hoja kwamba Zitto hashikiri Kampeni na badala yake anajikita na vyombo vya habari hapo tungeweza kufikiria mara mbili lakini Zitto alikuwa Mwanza, Arumeru amekuwepo, sijui Uzini na kwingineko.

Hili ndilo lililonifanya kuwaza na kufikiri kuwa labda yale aliyoyasema Dr. Mkumbo kule Uingereza yakawekwa humu juu ya mpasuko ndani ya Chama ndiyo hayo yanayoanza kuonekana manake tatizo si nia ya Zitto bali Kauli na majibu kutoka kwa viongozi wengine; mathalan Katibu Mkuu ambaye naye anajitahidi kujificha chini ya Mwamvuli wa muda akisema huu si muda muafaka. Yeye anaonekana kuwa mmoja kati ya wanaoungwa mkono kugombea sasa hizi kauli angeacha zitolewa na wanaowatazama manake ni rahisi sana kufikiri kuwa kaamua kusema hivyo kwa sababu naye ni mmoja kati ya wanaoutaka.

Ni wazi kwamba Mshauri Mkuu wa CHADEMA anajua mengi na nahisi aliamua kusema hayo huko kwa sababu yalimfika shingoni aidha kuna ushauri aliotoa juu ya pande hizo zitakazo Uraisi ila ushauri wake ukapuuzwa ama naye kaanza kuandamwa baada ya watu humu kumshauri naye agombee Uraisi.

WanaCDM mtakuwa wakali ila mazee mpende msipende lazima changamoto mzipata, mzikubali na mtafute namna ya kuzitatua lakini mkijifanya kila kitu kiko sawa ama hamtaki yenu yajadiliwe madhara yake ipo siku ya Sirini yatatandazwa nje mchana kweupe......... Na huo ndio mwanzo tu!

Accept critiques and let the same be your best friend and consequently your fault will be easily determined

Mkuu,
Hoja ya Zitto kutokushiriki campaign haiwezi kujengwa maana anashiriki campaign kikamilifu na wanalijua hilo.. alishiriki Arumeru kwenye uzinduzi na baada ya hapo akaendeleza mapambano sehemu mbalimbali kwenye udiwani, kama ulivyosema alishiriki uzinduzi wa Mwanza pamoja na Vijibweni-Kigamboni. Na wiki hii atakuwa kwenye campaign za lala salama Songea, Mbeya, Tanga and Mwanza.
Kuhusu comment ya katibu mkuu thats the best you should expect from him kwa kuzingatia kwamba washauri wake wanashinda humu jamvini, ungetegemea maoni gani zaidi ya hayo kwamba si muda muafaka!
 
Zitto anaweza kuwa Rais lakini si wanchi labda anaweza kuwa Rais wa TFF. Huyu kwa taarifa yenu hata ubunge jimboni kwake mwaka 2015 kupita inatakiwa ifanyike kazi ya ziada, anaefikiria habari ya Urais kwa Zitto anapoteza muda wake bure. nadhani anatamani kuwa kama alivyo Amaan Walid Kaborou kwa sasa ambaye alikuwa katibu mkuu wa CHADEMA na akatingisha ipasavyo.
Kaburi la Zitto kisiasa wala haliko mbali ni swala la muda tu litakaloamuwa na wala sio CHADEMA bali ni wapiga kura wa Kigoma jimboni kwake. mwenye note book na aandike maneno haya.
 
Utoto huu!
Hii ni thread aliyopandisha mwanajamvi hapa!
Kinachotakiwa ni Kauli original, au HyperLink inayoquote alipoongea Live toka huko alikokuwa!
Uswazi wa nini?
Au akanushe....kukaa kimya maana yake ni nini hivi hasa ukizingatia nae ni member mwenzetu humu na siku na siku thread unayoisema ilipopandishwa na jina lake lilionekana miongoni mwa member waliokua wakiufuatilia mjadala kwa muda mrefu bila kusema lolote,na wewe pia ulikua ni mmoja wapo na uliuliza suali hilihili na nilikukumbusha kitila mkumbo alikua pia online anasoma michango mbalimbali kwenye thread ile,hiyo inaashiria nini katika hali ya kawaida?acheni kujibaraguza chadema kuna tatizo tena si dogo.
 
Zitto anaweza kuwa Rais lakini si wanchi labda anaweza kuwa Rais wa TFF. Huyu kwa taarifa yenu hata ubunge jimboni kwake mwaka 2015 kupita inatakiwa ifanyike kazi ya ziada, anaefikiria habari ya Urais kwa Zitto anapoteza muda wake bure. nadhani anatamani kuwa kama alivyo Amaan Walid Kaborou kwa sasa ambaye alikuwa katibu mkuu wa CHADEMA na akatingisha ipasavyo.
Kaburi la Zitto kisiasa wala haliko mbali ni swala la muda tu litakaloamuwa na wala sio CHADEMA bali ni wapiga kura wa Kigoma jimboni kwake. mwenye note book na aandike maneno haya.
dua la kuku,hata uchaguzi uliopita mlisema hapiti ubunge kisa alimtest mchagga mwenzenu mbowe kwenye uenyekiti wa chama...!acheni ukabila nyie,fanyeni siasa.
 
dua la kuku,hata uchaguzi uliopita mlisema hapiti ubunge kisa alimtest mchagga mwenzenu mbowe kwenye uenyekiti wa chama...!acheni ukabila nyie,fanyeni siasa.
Kwanza kabisa ningependa kukuomba usinipe kabila ambalo siyo la kwangu, kama unapenda kujuwa kabila langu mimi ni Mkwerre.

Ukitaka kuwa Analyst mzuri basi jiepusha uropokaji na kupelekeshwa na utashi wako kulio fact, Zitto Kabwe uchaguzi wa mwaka 2005 alishinda kwa kura ngapi na mwaka 2010 alishinda kwa kura ngapi? ukipata jibu ndipo sasa urudi kujenga hoja yako je matokeo hayo kisiasa huyu umaarufu wake jimboni unaongezeka au unashuka. mimi huwa napenda Intellectual Argument only.

KIGOMA
WILAYA YA KIGOMA
KIGOMA KASKAZINI
Candidate
Political Party
Number of Votes
Percentage Votes
ZITTO KABWE ZUBERI
CHADEMA
23,366 48.57
LEMBO ROBINSON FULGENCE
CCM
18,352 38.15
OMARY MUSSA NKWARULO
CUF
4,839 10.06
CHONGERA HARUNA CHONGERA
CHAUSTA
264 0.55
MFAUME HAMISI MFAUME
APPT - MAENDELEO
108 0.22
AUGUSTINO PETER MBOLEGWA
SAU
88 0.18
GERMANI MAULIDI MLETE
DP
87 0.18
HAMISI FADHILI KISWAGA
NRA
47 0.1
MAUWA SHAURI KAMANA
JAHAZI ASILIA
19 0.04
TATU SAIDI HUSSEIN
UMD
8 0.02
SPOILT VOTES 927 1.93
TOTALS 48,105 100

 
Hizi ni porojo na propaganda za ccm. Dr Kitila ninayemjua mimi angehisi kitu kama hicho angepeleka hoja ya hiyo kwenye vikao vya Chama kama kamati kuu ambavyo yeye ni mjumbe. Mengine story za kujaza server za JF bure.
 
Zitto, Mbowe, Slaa etc..wote ni CDM na watapita kwenye mchujo kwa kanuni na taratibu za CDM kwa wakati muafaka utakapofika, atakayeshinda ndie atagombea sasa kuna kipi kigeni hapo? CCM wanahangaika sana kutaka kuwagombanisha au kuanzisha mgogoro ndani ya CDM kwa mbinu hizi za kipuuzi na kitoto na sidhani kuwa watafanikiwa kwani CDM ni makini kwa hilo
 
Back
Top Bottom