Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,038
- 2,199
wakuu je ni kweli Tanzania tumefikia mahala hapa?kuwatisha na kuwadhalilisha wataalamu wetu?hebu sikia kisa cha madaktari walioshiriki mgomo katika ule mji unaotambulika kuwa ni makao makuu ya ccm na serikali na pia ni mji ambao mara kwa mara hupokea wawakilishi wa wananchi kutoka Tanzania nzima.nini maoni yetu juu ya hili???
Serikali ifahamu kuwa kutumia mabavu na nguvu kubwa kupita kiasi si njia ya kufikia suluhu,naomba madaktari popote tulipo tukemee kitendo kilichofanyika Dodoma na mimi kama muathirika,tulikamatwa kwa nguvu bila hata kupewa nafasi ya kuwaaga wenzetu,tumehojiwa kwa masaa tisa huku tukiwa tumefungiwa na maafisa upelelezi,tumepekuliwa majumbani tunakoishi na baadhi kuzuiliwa vitu vyao vikiwemo laptop,moderm,frash,tumechukuliwa finger prints na picha,na kupewa ratiba ya kureport ofisini kwao 4hrly na baadae kutapper down follow up kwa simu 4hrly na kuchukua taarifa zetu utafikiri wezi huu ni udhalilishaji wa taaluma yetu...