Dai hili la wana UAMSHO lisipuuzwe, kwani lina harufu ya madhara makubwa hapo baadae

" mna upotoshaji kwenye makala yako .... tumesema na tutaendelea kusema, na hizo fitna mnazolishwa na kuziamini hata hazitaturudisha nyuma katika dai letu la msingi nalo ni "SOVEREIGN ZANZIBAR" twataka Zanzibar yetu yenye mamlaka kamili, hatuna haja ya maili 10 za Tanganyika wala nini, chukuweni hatuna haja nazo tena, japo zilikuwa ni milki yetu, yaonesha wengi wenu hata hiyo historia ya MRIMA (Tanganyika) hamuijui. Sisi huku mashaAllah wengi wetu tunaijua historia ya Dola ya Zanzibar, wapi ilipotoka, ilipo leo na inapoenda. Ya nini kuharibu bisu langu kwa nyama isiyoliwa!"


Nguruwe ni nguruwe tu, hata akiwekwa lip stick domo ake halibadiliki, na siku zote umaarufu wa jogoo ni kuchinjwa tu. Kisiwani kuna watu wenye akili na busara, tena hao ni wengi zaidi kuliko watu wenye uchu, baada ya mwafaka kuja sasa wanajaribu kutafuta adui mwingine, hata wakijitenga na bara wataanza kutafuta mwingine. Utumwa wa kimawazo na hasa umaskini wa akili, unajionesha sana siku hizi hapa JF. Inaonekana watu hawajui ni nini maana ya muungano, badala ya kutoa hoja zenye akili za kutaka uvunjwe na wanaleta mipasho kama watu wasioenda darasa hata la madrasa. Get a life!
 
Nguruwe ni nguruwe tu, hata akiwekwa lip stick domo ake halibadiliki, na siku zote umaarufu wa jogoo ni kuchinjwa tu. Kisiwani kuna watu wenye akili na busara, tena hao ni wengi zaidi kuliko watu wenye uchu, baada ya mwafaka kuja sasa wanajaribu kutafuta adui mwingine, hata wakijitenga na bara wataanza kutafuta mwingine. Utumwa wa kimawazo na hasa umaskini wa akili, unajionesha sana siku hizi hapa JF. Inaonekana watu hawajui ni nini maana ya muungano, badala ya kutoa hoja zenye akili za kutaka uvunjwe na wanaleta mipasho kama watu wasioenda darasa hata la madrasa. Get a life!
BWANA YESU ANAOKOA, KWA NINI MNAUMIZA AKILI HIVI?KWA NINI MNASONONEKA?KWA NINI MNAHANGAIKA NA HII DUNIA? MPE BWANA YESU MAISHA YAKO NA KUHAKIKISHIA HUTA JUTA,roho ya hasira,chuki na mambo mabaya yataondoka nawe utakuwa mwenye furaha muda wote.KARIBU KANISA LOLOTE LILILOKARIBU NAWE LINALOAMINI WOKOVU.
AU TUWASILIANE KWA EMAIL :johnhella2007@yahoo.com hiyo email naitumia hata facebook ukisearch kwa email hiyo utanipata
 
Hivi hawa waislamu nani kawaroga?!!!! Mahakama ya kadhi wanataka waanzishiwe na serikali!!!! Sensa wanataka wafanyiwe na serikali!!! Hadi mitihani wanataka serikali iwasaidie kupass!!!! Sasa nusu ya jiji la Dar es salaam ni sehemu ya Zanzibar... Huu nao ni uendawazimu mwingine!!

Mkuu taratibu, haya hayakusemwa na Waislamu, yamesemwa na wahuni fulani huko visiwani. Karume, Kawawa, Jumbe, Salim Ahmed Salim, Kikwete, Magembe, Shababi (Makamu wa Rais) na Mzee Ruksa wooote hawa nao ni waislamu, lkn kwa kuwa ni watu na akili zao, sidhani kama wana mawazo haya ya wacheza bao.

Ukisema WAISLAMU unakosea, kwani mhuni aliyesema haya hakukusanya maoni yao. Neno sahihi ni WAHUNI
 
Mkuu taratibu, haya hayakusemwa na Waislamu, yamesemwa na wahuni fulani huko visiwani. Karume, Kawawa, Jumbe, Salim Ahmed Salim, Kikwete, Magembe, Shababi (Makamu wa Rais) na Mzee Ruksa wooote hawa nao ni waislamu, lkn kwa kuwa ni watu na akili zao, sidhani kama wana mawazo haya ya wacheza bao.

Ukisema WAISLAMU unakosea, kwani mhuni aliyesema haya hakukusanya maoni yao. Neno sahihi ni WAHUNI

Mkuu ni kweli kwamba si wazanzibar wanaosema hivyo, lakini kuna wahuni wachehce kutoka Zanzibar ndio wanasema hayo kwa kutumia jina la Zanzibar na kwa kutumia jina la waislamu na uislamu, tatizo ni kwamba wale tunaofahamu kuwa ni wazaznibar wenye elimu, wenye akili na wenye busara wanapokaa kimya kupita kiasi na kuwaacha majuha, wabwabwaje na kubwatuka kwa jina la usialmu la Zanzibar hapo ndio kuna wasiwasi, na ndio tunaanza kujiuliza kuna nini? au ndio kwamba majuha wamekuwa na nguvu kuliko watuy wamaana kutoka Zanzibar?
 
Nakuuliza swali: Ikiwa UAMSHO nia yake ni uhuru wa Zanzibar, iweje isajiliwe kama taasisi ya dini na kutumia mihadhara ya dini kuleta chokochoko za kisiasa? Je, Wazanzibari wasio waislamu watashiriki vipi ukombozi wa Zanzibar yao?[/QUOTE]

Nadhani hujasoma vizuri hayo majadiliano, swali lako la DINI na SIASA amelijibu. lakini usijali ndugu nakuwekea tena uone alivyojibu;

JAMHURI: Taasisi ya kidini kwanini ijikite kwenye siasa?

Sheikh Farid: Hakuna tatizo lolote. Hakuna tatizo kikatiba, hakuna tatizo kidini yetu, hakuna tatizo kimtazamo sahihi wa wanasiasa. Kote hakuna tatizo. Mtazamo sahihi wa wanasiasa. Tumchukue Rais wetu wa hapa Zanzibar, Mheshimiwa Jumbe ameandika kitabu na kuna sura maalumu anaita “Dini na Siasa”. Kaeleza mengi. Kaeleza jinsi watu wengine walivyo katika dini zao, lakini akaelezea ama upande wa Uislamu huwezi kutenganisha dini na siasa. Hilo moja. Basi kama watu wanajua wanasiasa, huyu mwanasiasa anatamka kwenye kinywa chake. Alikuwa Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania. Alikuwa pia Makamu wa Mwenyekiti wa CCM na kaeleza wazi kabisa kwenye Uislamu huwezi kutenganisha na siasa.
Ukija kwenye Koran, Uislamu unahesabu kuwa dini ni mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu, ikiwamo sehemu ndogo inayoitwa “siasa”. Siasa kwenye Uislamu au kwenye lugha ya Kiarabu, neno hilo hilo siasa kama lilivyo, maana yake ni “uongozi”, kwa hiyo uongozi ni sehemu ndogo, ni mlango katika maisha ya mwanadamu au katika dini ya Kiislamu. Kwa hiyo sisi kuzungumza siasa ni sahihi kabisa.
 
Nakuuliza swali: Ikiwa UAMSHO nia yake ni uhuru wa Zanzibar, iweje isajiliwe kama taasisi ya dini na kutumia mihadhara ya dini kuleta chokochoko za kisiasa? Je, Wazanzibari wasio waislamu watashiriki vipi ukombozi wa Zanzibar yao?

Nadhani hujasoma vizuri hayo majadiliano, swali lako la DINI na SIASA amelijibu. lakini usijali ndugu nakuwekea tena uone alivyojibu;

JAMHURI: Taasisi ya kidini kwanini ijikite kwenye siasa?

Sheikh Farid: Hakuna tatizo lolote. Hakuna tatizo kikatiba, hakuna tatizo kidini yetu, hakuna tatizo kimtazamo sahihi wa wanasiasa. Kote hakuna tatizo. Mtazamo sahihi wa wanasiasa. Tumchukue Rais wetu wa hapa Zanzibar, Mheshimiwa Jumbe ameandika kitabu na kuna sura maalumu anaita “Dini na Siasa”. Kaeleza mengi. Kaeleza jinsi watu wengine walivyo katika dini zao, lakini akaelezea ama upande wa Uislamu huwezi kutenganisha dini na siasa. Hilo moja. Basi kama watu wanajua wanasiasa, huyu mwanasiasa anatamka kwenye kinywa chake. Alikuwa Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania. Alikuwa pia Makamu wa Mwenyekiti wa CCM na kaeleza wazi kabisa kwenye Uislamu huwezi kutenganisha na siasa.
Ukija kwenye Koran, Uislamu unahesabu kuwa dini ni mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu, ikiwamo sehemu ndogo inayoitwa “siasa”. Siasa kwenye Uislamu au kwenye lugha ya Kiarabu, neno hilo hilo siasa kama lilivyo, maana yake ni “uongozi”, kwa hiyo uongozi ni sehemu ndogo, ni mlango katika maisha ya mwanadamu au katika dini ya Kiislamu. Kwa hiyo sisi kuzungumza siasa ni sahihi kabisa.
[/QUOTE]

Baki hapo hapo kaka! Uislam na siasa sawa, lakini mnachotaka nyinyi ni kufanya nchi yenu iwe zaidi ya uislamu na siasa. Yaani Zanzibar iwe ya kiislamu tu. Hao wengine hamuwataki kabisa kuwepo katika kisiwa chenu, tena usiwasemee leo na kuwaonea huruma wakati juzi ulikuwa unashiriki harakati za kuchoma makanisa yao. Wewe si mmoja wao? Wewe si ndo ulikuwa unashangilia na kuona raha watu wakichomewa moto nyumba zao?
 
Usipofahamu historia ya zanzibar unaweza ukapata tabu sana, ndio kama wewe unaefananisha UAMSHO na BOKO HARAMU, sikulaumu maan tunao wengi mfano wako yaani "WAVIVU WA KUFUATILIA HISTORIA NA WAPAYUKAJI WASIOUSHAHIDI",Kwanza UAMSHO wana hati ya usajili, pili bado wanakwenda sambamba na katiba yao ya zanzibar,maana katiba initaka serikali kuitisha kura ya maoni katika mambo yote yanayohusu Muungano, ivi lipi walilovunja UAMSHO na kwa ushahidi gani?"NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK",ndio msemo utaokufunza. Kwa nini binaadamu mnakuwa wavivu wa kusoma vitabu hasa vya historia?,


Wewe hata ni chadema nini?, maana ndio wanaodai eti sasa serikali ziwe tatu na zanzibar iwe kamaJIMBO tu,Pia niwavivu wa kusom maandiko ya historia ndio maana wanasema tu kilichokaa mbele yao,mnatakiwa muwe na mizani mnapo sema ,aundio kuitafuta nchi hivo?"POLENI",mwisho nakueleza hivi ;Kama kitu hukielewi nyamaza kimya sio lazima kusema .
 
Nguruwe ni nguruwe tu, hata akiwekwa lip stick domo ake halibadiliki, na siku zote umaarufu wa jogoo ni kuchinjwa tu. Kisiwani kuna watu wenye akili na busara, tena hao ni wengi zaidi kuliko watu wenye uchu, baada ya mwafaka kuja sasa wanajaribu kutafuta adui mwingine, hata wakijitenga na bara wataanza kutafuta mwingine. Utumwa wa kimawazo na hasa umaskini wa akili, unajionesha sana siku hizi hapa JF. Inaonekana watu hawajui ni nini maana ya muungano, badala ya kutoa hoja zenye akili za kutaka uvunjwe na wanaleta mipasho kama watu wasioenda darasa hata la madrasa. Get a life!

nimekuwa nguruwe tena? ahsante, Allah akuwafu ndio ninalokuombea, ndugu yangu adui wetu mkubwa tokea day one ni huu muungano feki. sijui hoja gani tena unataka uzisikie, ikutoshe tu hata Karume Sr. mwenyewe wakati alipoondoka duniani hakuwa na mawasiliano na Nyerere, tatizo ni hili dudu muungano. Akaja mzee Aboud Jumbe sina haja ya kukueleza kilimfika nini na sababu inajulikana. Shk Idriss alituwachia usia mzuri tu kuhusu dudu hili muungano. Misukosuko iliyomfika Dr. Salmin Amour sote huku tunaielewa. Mwisho kipenzi cha dodoma Dr Amani Karume, si haba katuletea maelewano na KATIBA YETU MPYA ya Zanzibar.

wengi wa waTanganyika, jeuri, kibri, matusi ni hulka yenu, tutukaneni mtakavyo (narudia tena) ila dai letu lipo pale pale, wacha tusiwe na elimu yoyote.

Ni kweli wengi wetu hatujui nini maana ya muungano, hasa huu wa Tanganyika na Zanzibar, munaelewa ni nyinyi waTanganyika tu, maana hata jirani kina Kenya, Rwanda na wengineo hawajavutiwa kujiunga nao hata siku moja.

 
Usipofahamu historia ya zanzibar unaweza ukapata tabu sana, ndio kama wewe unaefananisha UAMSHO na BOKO HARAMU, sikulaumu maan tunao wengi mfano wako yaani "WAVIVU WA KUFUATILIA HISTORIA NA WAPAYUKAJI WASIOUSHAHIDI",Kwanza UAMSHO wana hati ya usajili, pili bado wanakwenda sambamba na katiba yao ya zanzibar,maana katiba initaka serikali kuitisha kura ya maoni katika mambo yote yanayohusu Muungano, ivi lipi walilovunja UAMSHO na kwa ushahidi gani?"NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK",ndio msemo utaokufunza. Kwa nini binaadamu mnakuwa wavivu wa kusoma vitabu hasa vya historia?,


Wewe hata ni chadema nini?, maana ndio wanaodai eti sasa serikali ziwe tatu na zanzibar iwe kamaJIMBO tu,Pia niwavivu wa kusom maandiko ya historia ndio maana wanasema tu kilichokaa mbele yao,mnatakiwa muwe na mizani mnapo sema ,aundio kuitafuta nchi hivo?"POLENI",mwisho nakueleza hivi ;Kama kitu hukielewi nyamaza kimya sio lazima kusema .

Ok! Maelezo yako mazuri sana. Lakini naomba unijibu swali langu dogo tu. Unaweza kuniambia sababu ya kuchoma makanisa ilikuwa nini?
 
nimekuwa nguruwe tena? ahsante, Allah akuwafu ndio ninalokuombea, ndugu yangu adui wetu mkubwa tokea day one ni huu muungano feki. sijui hoja gani tena unataka uzisikie, ikutoshe tu hata Karume Sr. mwenyewe wakati alipoondoka duniani hakuwa na mawasiliano na Nyerere, tatizo ni hili dudu muungano. Akaja mzee Aboud Jumbe sina haja ya kukueleza kilimfika nini na sababu inajulikana. Shk Idriss alituwachia usia mzuri tu kuhusu dudu hili muungano. Misukosuko iliyomfika Dr. Salmin Amour sote huku tunaielewa. Mwisho kipenzi cha dodoma Dr Amani Karume, si haba katuletea maelewano na KATIBA YETU MPYA ya Zanzibar.

wengi wa waTanganyika, jeuri, kibri, matusi ni hulka yenu, tutukaneni mtakavyo (narudia tena) ila dai letu lipo pale pale, wacha tusiwe na elimu yoyote.

Ni kweli wengi wetu hatujui nini maana ya muungano, hasa huu wa Tanganyika na Zanzibar, munaelewa ni nyinyi waTanganyika tu, maana hata jirani kina Kenya, Rwanda na wengineo hawajavutiwa kujiunga nao hata siku moja.


Mkuu kuna siku Augustine Mrema alisikia Nyerere akisema "i can not let my country go to the dogs", akasema kuwa wapinzani wamitwa mbwa, watu wakamuona mbumbumbu kabisa hata hakujua maana ya sentensi fupi ya Nyerere, labda tu hapo nikuombe radhi kwa kutumia lugha ya kigeni lakini hilo si tusi, ni kueleza tu hali fulani au state of mind ya baadhi ya watu, haina uhusiano na matusi.
 
Ok! Maelezo yako mazuri sana. Lakini naomba unijibu swali langu dogo tu. Unaweza kuniambia sababu ya kuchoma makanisa ilikuwa nini?

kwa kusaidia tu labda hapa, Uamsho na kila mpenda amani wa kweli (sio wale wanafik) kama jumuiya wamelaani kitendo hiki hadharani, na wakatoa ahadi watasaidia upelelezi ili wale waliohusika wafikishwe kwenye vyombo vya sheria, na kwa taarifa yako wamefanya hivyo. ila ni jukumu la jeshi la polisi kutoa taarifa ya nani na nani kahusika kwenye tukio hilo. bahati mbaya hadi sasa wapo kimya, kwa taarifa yako tu hujo siku za nyuma Uamsho imewahi pia kushutumiwa kwa kadhia ya uchomaji wa makanisa na maeneo mengine. nakumbyuka enzi za Mh Chiligati kama naibu waziri mambo ya ndani (kama sikosei) akaahidi yeye mwenyewe ataianika hadharani ripoti ya waliohusika. lakini kimyaaaa hadi leo!

Sijui unanipata nini nakusudia?
 
Habari yako ndungu, jiulize suali hili, wewe ukiwa kama muislam umeisaidiaje dini yako kuhahakikisha kuwa inasimama? Kumbuka ukiwa kama muislam ni wajibu wako kuhakikisha kuwa popote ulipo dola ya kiislam inasimama, sheria na miongozo ya kiislam inafuatwa, na hapo ndipo kila utakachokuwa unakifanya kitahesabiwa kuwa ni ibada. By the way, wana uamsho hoja zao ziko wazi na mimi naamini hakuna kiongozi wa kisiasa anaeweza kujibu hoja zao. Mwisho nikukumbushe kuwa, kwa waislam dini kwao ni mfumo mzima wa maisha, na uslam unakataza dhulma na hiyo ndiyo wanayoizungumzia, pamoja na matatizo mbalimbali ya wana jamii wakiwamo wana uamsho.
 
Muungano wanulilia sana wakristo hasa (wapenzi wa st. nyerinyeri(oooo) sijui kwa nini??

Waislamu wa Tanganyika tunawaombea kila la heri ili muweze kupata madai yenu na zanzibar iliyo huru kabisa..

InshAllah
 
Hakuna shida kwani alie jipa pwani ni nani? au huyo mwarabu alikuwepo berlin wakati wa kugawa makoloni! hofu yangu mimi dhidi ya kundi hili ni kuchoma makanisa na kuleta mgogoro wa kidini na kwa serikali DHAIFU kama hii inakua raisi kuenea na kujitokeza makundi mengine yanayochochewa na Redio Iman ku kashifu na kutukana Imani za watu wengine
 
we hujui hayo makundi yalianza kama huu UAMSHO? unaoupigia debe. huu UAMSHO ni kikundi cha maharamia na watakuja kusumbua sana ikiwemo kuteka meli, na washaanza kuchoma moto makanisa, hawa sio watu wema kabisa na washukuru hizi ni zama za baba MwanaAsha na Saidi Mwema waislamu wenzao ndio maana wanapumua,,, lakini huu nao ni upepo watapita haraka

wanauamsho na wazanzibar kwa ujumla wanaongea point kisheria,kwanini wana jf wanashindwa kupinga hayo madai kisheria na sio kuzurura mada?
 
Hii ndio moja ya sababu ya Zanzibar kubaki kuwa mali yetu daima!
Link http://www.tanzania.go.tz/history.html

Hili suala la maili 10, limekuwa 16 katika hii link. Tanzania National Website Jisomee uelewe, huenda hili likuwa sababu moja ya Mwalimu kutaka Muungano na Zanzibar.

Pia kubadili jina la Muungano baada ya mwaka mmoja ili kupoteza jina Tanganyika.

Kuna haja kupiga reverse gear kulirudisha jina la muungano la asili, Jamhuri ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Pande la ardhi lilioitwa Tanganyika leo linaitwa Bara. Sishangai kusikia badungu zinaua albino ili wapate utajiri.
Mambo ya ajabu ajabu yanatokea duniani.

Tanganyika kuitwa Bara. Ni mazingaombwe au kiini macho?

Kwa usanii wa watawala, Chai chapati maharage huenda wakabadilisha jina tena na kuita muungano huu
Jina jipya , Jamhuri ya Muungano ya Tanzania badala ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya muda tena itakuwa Jamhuri ya Tanzania.

Kwa watawala hiyo ndio maana ya kuimarisha muungano.

Kutufanyia kiini macho huku wakitugawia umaskini.
 
nadhani uelewa wako una matatizo, nimekwambia hebu ingia google ujisomee hao AL KAIDA na BOKO HARAM walianzaje? na wakapewa usajili kama uamsho?

mbona watanganyika hawatoi point zenye mashiko ya sheria kupinga hoja za wazanzibar?mm naona porojo tupu mwanzo mwisho.
 
mbona watanganyika hawatoi point zenye mashiko ya sheria kupinga hoja za wazanzibar?mm naona porojo tupu mwanzo mwisho.

You***** there is no such a thing as mtanganyika, hiyo nchi unayoiita Tanganyika ili cease ku-exist baada ya Muungano, huku bara kwa sasa hakuna mtanganyika, kama una maana watu wa bara kama vile wandegereko, wamakua, wamakonde etc hata huko wapo, kuna wazanzibar wengi wa makabila hayo ya huku bara, na kuna wabara wachahce wenye asili ya huko tunawaona wabara wenzetu, hatuwabagui kuwa kuwa wao wana asili ya Zanzbiar.

Point ni kwamba kwamba hakuna Tanganyika, hiyo nchi unayoitaja haitambuliwi popote pale hata na sheria za Tanzania haina watu, haaina ardhi na haiina kiongozi, sasa kuna Tanzania. Kama wewe unataka kuifanya Zanzibar isiwe sehemu ya Tanzania toa hoja za maana zilizoenda shule, usiongee kama mtu wa mtaani asiyejua a wala be.

You need to study the contents of "articles of union" and see what was the wisdom behind the decisions to be part of the union, you need to read between the lines and ask yourself whether Mzee Karume and members of revolution council were less smart than you, or the were fools and you are very smart than them all.

You need to look at issues around muungano, look at pros and cons of Muungano for the people of Unguja and to the people of Zanzibar in general. Look at them in terms of uchumi, siasa, jamii, usalama etc, then uje hapa na kuongea kama mtu anayejua. Usiongee kama watu wa uamsho, who are guided by a bedeviled theology of hatred, separation and killing, ambao hata shule sifuri. Lighten up.

Ni upumbavu kusema bara wanawazuzia wazanzibar kuwa ombaomba, ni upumbavu kusema bara wanatunyonya wakati huelezi ni kipi wabara tunawanyonya wazanzibar, ni ujinga kuchoma makanisa kwa kudhani kuwa wabara wote ni waislamu wakati kuna mamia ya wabara waislamu wanaenda kwenye misikiti ya Zanzibar, ni ujinga kusema wabara wanachukua kazi za wazanzibar wakati kuna mamia ya wazanzibar wanafanya kazi bara, ni ujinga kusema wabara tunaitegemea Zanzibar wakati kuna mamia ya matatizo yanayotukabili na tunayatatua bila kuomba senti kutoka SMZ. Ukiridi na pointi zinazoeleweka kwa wenye akili na busara, ndio utajibiwa kwa hoja zenye mashiko.
 
You***** there is no such a thing as mtanganyika, hiyo nchi unayoiita Tanganyika ili cease ku-exist baada ya Muungano, huku bara kwa sasa hakuna mtanganyika, kama una maana watu wa bara kama vile wandegereko, wamakua, wamakonde etc hata huko wapo, kuna wazanzibar wengi wa makabila hayo ya huku bara, na kuna wabara wachahce wenye asili ya huko tunawaona wabara wenzetu, hatuwabagui kuwa kuwa wao wana asili ya Zanzbiar.

Point ni kwamba kwamba hakuna Tanganyika, hiyo nchi unayoitaja haitambuliwi popote pale hata na sheria za Tanzania haina watu, haaina ardhi na haiina kiongozi, sasa kuna Tanzania. Kama wewe unataka kuifanya Zanzibar isiwe sehemu ya Tanzania toa hoja za maana zilizoenda shule, usiongee kama mtu wa mtaani asiyejua a wala be.

You need to study the contents of "articles of union" and see what was the wisdom behind the decisions to be part of the union, you need to read between the lines and ask yourself whether Mzee Karume and members of revolution council were less smart than you, or the were fools and you are very smart than them all.

You need to look at issues around muungano, look at pros and cons of Muungano for the people of Unguja and to the people of Zanzibar in general. Look at them in terms of uchumi, siasa, jamii, usalama etc, then uje hapa na kuongea kama mtu anayejua. Usiongee kama watu wa uamsho, who are guided by a bedeviled theology of hatred, separation and killing, ambao hata shule sifuri. Lighten up.

Ni upumbavu kusema bara wanawazuzia wazanzibar kuwa ombaomba, ni upumbavu kusema bara wanatunyonya wakati huelezi ni kipi wabara tunawanyonya wazanzibar, ni ujinga kuchoma makanisa kwa kudhani kuwa wabara wote ni waislamu wakati kuna mamia ya wabara waislamu wanaenda kwenye misikiti ya Zanzibar, ni ujinga kusema wabara wanachukua kazi za wazanzibar wakati kuna mamia ya wazanzibar wanafanya kazi bara, ni ujinga kusema wabara tunaitegemea Zanzibar wakati kuna mamia ya matatizo yanayotukabili na tunayatatua bila kuomba senti kutoka SMZ. Ukiridi na pointi zinazoeleweka kwa wenye akili na busara, ndio utajibiwa kwa hoja zenye mashiko.

Povu la nini ahali yangu.

Fanya uchunguzi wa kina sana kuhusu madai ya Uamsho ambayo ni ya kisharia zaidi na sio kisiasa.

Hebu soma hapo uwone dhulma za kiuchumi zinazobainishwa na wawakilishi barazani

Na Mwantanga Ame


HUKU wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakijadili bajeti ya mwaka wa fedha wa 2012/2013, kilio cha kero za Muungano kimetawala na kutikisa michango ya wajumbe wa Baraza hilo.


Wajumbe hao walisema kuwa kero za Muungano zimekuwa kero kubwa kwa uchumi wa Zanzibar na kwamba zinahitaji kurekebishwa hivi sasa badala ya kusubiri mchakato wa katiba mpya.


Akichangia bajeti hiyo, Mwenyekiti wa kamati ya Wenyeviti wa Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan Juma (Kwamtipura), alisema kuwa serikali inapaswa kuja na majibu mazuri juu ya namna ya kero za Muungano zitakavyomalizwa, kwani zinakandamiza uchumi wa Zanzibar.


Hamza alisema inasikitisha kuona serikali ya Muungano hivi sasa imekuwa na mambo mbali mbali ya serikali inayotakiwa kuyafanyia kazi lakini hakuna lililofanyika wakati serikali ya Muungano ikiwa inatekeleza vyema matakwa yake.


Mwenyekiti huyo alisema serikali ya Zanzibar inakosa majibu juu ya suala la mgao wa Muungano wa asilimia 4.5 ambao kwa muda mrefu yametolewa mapendekezo ya asilimia 11.5 lakini BOT bado halijatekelezeka hadi sasa.


Alisema jambo linaloshangaza kuona baada ya kupelekwa mapendekezo hayo serikali ya Muungano imeipatia gawio la asilimia 7.8 huku kukiwa hakuna muendelezo wa hatma ya suala hilo.


Alisema kuwapo kwa gawio hilo limeifanya serikali ya Zanzibar wakati ikisubiri suala hilo kumalizwa katika vikao vya kero za Muungano imekuwa ikikosa shilingi bilioni 7,000,000,000 kati ya shilingi bilioni 15, ambazo zilitakiwa kuingia katika mfuko wa hazina ya Zanzibar kama hilo lingekuwa limemalizwa.


Suali jengine linaloonesha kutokuwepo kwa utayari wa serikali ya Muungano kulifanyia kazi kwa haraka, ni kodi ya mishahara ya wafanyakazi wa Muungano ambao wanafanya kazi hapa Zanzibar ambapo inakosa shilingi bilioni 18.


Alisema kama mambo hayo yangeliweza kutolewa maamuzi ya haraka, kwa kiasi kikubwa zingeweza kuisaidia serikali ya Zanzibar kupata gawio lake kwa miaka mingi badala ya hivi sasa kuendelea kutolewa kwa fedha hizo kama ni huruma.


Aidha alisema kero pia ziko katika suala la elimu ya Juu ambapo serikali ya Zanzibar itapaswa kuona inadai serikali ya Muungano kwa mwaka ujao wa fedha kupatiwa asilimia ya gawio la Zanzibar ikiwa ni hatua itayoweza kujipanga vyema katika kutoa elimu ya juu.


Mwenyekiti huyo, aliikosoa bajeti hiyo, kwa kueleza kuwa kodi ya umeme ambapo alisema inaweza ikachangia kuongeza gharama za maisha kwa wananchi na kuiomba serikali kuiondoa hadi kamati ya Baraza la Wawakilishi litapomaliza kufanya uchunguzi wake katika shirika la Umeme.


Kutokana na hali hiyo Mwenyekiti huyo aliishauri serikali kufikiria kuwaangalia watendaji wake kwa kuhakikisha wanawatumikia wananchi huku serikali ikawachukulia hatua za kinidhamu wanaotajwa kuibia serikali.


Aidha, Mwenyekiti huyo pia alieleza dhamira ya Kamati hiyo kutaka kuwasilisha maombi ya kuifanyia uchunguzi Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) baada ya kujionesha baadhi ya Watendaji katika kitengo cha Bandarini kuonekana kujihusisha na uvujaji wa mapato.


Eneo jengine ambalo kamati hiyo imetishia kuizuia bajeti hiyo ni juu ya suala la ajira kwa vijana kutokana na hivi sasa kuwepo kwa taarifa za wageni kuajiriwa kwa wingi katika mahoteli ya kitalii huku Wazanzibari wakikoseshwa nafasi hizo.


Kwa upande wake, Mwakilishi wa Uzini (CCM), Mohammed Raza alisema uchumi wa Zanzibar unaweza ukakosa kunawiri ikiwa baadhi ya mambo yakiachiwa moja kwa moja kutekelezwa na serikali ya Muungano likiwemo suala la kujiunga na taasisi ya kimataifa ya Kiislamu (OIC).


Aidha Mwakilishi huyo alihoji juu ya suala la Afrika Mashariki nalo linahitaji kuangaliwa katika haki ambazo itaweza kuzipata kama Zanzibar bila ya kuingia kama ipo chini ya mwamvuli wa Tanzania.


Naye Mwakilishi wa Kitope Makame Mshimba Mbarouk alisema serikali itapaswa kujiangalia katika miradi ya uwekezaji kutokana na baadhi ya wawekezaji kufutiwa miradi yao ikiwa analipia gharama kubwa na kupewa watu wanaolipiwa kiasi kidogo cha fedha.


Alisema hivi sasa kuna watu wamekuwa wakiondolewa kwa chuki katika baadhi ya miradi hiyo jambo ambalo linapoteza imani ya wawekezeji kuwekeza Zanzibar na kuahidi kuizuiya bajeti hiyo hadi atapopewa maelezo ya kija juu ya suala hilo.


Nae Mwakilishi wa Chonga (CUF), Abdalla Juma Abdalla, aliiomba serikali kuona inatekeleza vyema bajeti hiyo na kuahidi kuwa hatoacha kuiziya hadi atapopewa maelezo ya kina kutokana na kujitokeza mambo mbali mbali katika serikali.


Mwakilishi wa Ziwani, Rashid Seif, akitoa mchango wake aliitaka serikali kuona inajipanga vyema katika suala la kusimamia sekta ya elimu kutoka an akuanza kuonekana eneo hilo huenda kukawa na wajanja wanaotumia vibaya nafasi zao.
 
Back
Top Bottom