Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,770
- 59,114
Kwa wale ambao bado hawajaolewa hua hawaishi kuonyesha na kuelezea namna gani wanaume walivyo wabaya hata kufanya swala zima la kuingia ndoani kuwa gumu. Walioolewa hawaishi kulalama namna waume zao walivyo wabaya ndoani hata kuona ndoa zao hazina furaha. Ila wote wanasahau kwamba kwa kiasi kikubwa wengi hua wanachangia ubaya wauonao kwa wanaume kama ambavyo wanaume huchangia ubaya (sio wote) wauonao kwa wanawake.
Kuna dada kaolewa miaka minne(4) iliyopita, na harusi yake ndo harusi pekee ambayo mimi nimewahi kuhidhuria mpaka leo hii. . .
Sina shaka kwamba alikubali mwenyewe kuolewa na siku ile aliifurahia maana alionekana mwenye furaha muda wote. Miaka minne baadae wamejaaliwa mtoto wa kike na maisha yao ni ya kawaida. Sasa wiki iliyopita alimuomba mumewe pesa ya mkaa, mume akawa hana. Alichofanya ni kwamba amemnyima chakula (anachonunua huyo huyo mume) mpaka leo hii. Yani "kwa eaha na shida (siku hizi inabidi mchungaji akisema . . . . na shida waseme "INATEGEMEA NI ZIPI" badala ya "NDIO NAKUBALI" za kinafiki) aliyotamka imekosa matendo.
Sasa mwanamke kama huyu, mume akimbadilikia au akimmwaga atamlaumu nani?Nae ataweza kusimama mahali na kusema wanaume ni watu wabaya? Kwanini asifanye shughuli ndogo ndogo nae awe anasaidia akiona mume mambo hayajamuendea vizuri sana kwenye shughuli zake?
Ahhhhh wanaume wengine mna kazi kweli aisee. . .nawapa pole wote mnaokaribia kupewa vichaa na wake/wapenzi wenu.
Kuna dada kaolewa miaka minne(4) iliyopita, na harusi yake ndo harusi pekee ambayo mimi nimewahi kuhidhuria mpaka leo hii. . .
Sina shaka kwamba alikubali mwenyewe kuolewa na siku ile aliifurahia maana alionekana mwenye furaha muda wote. Miaka minne baadae wamejaaliwa mtoto wa kike na maisha yao ni ya kawaida. Sasa wiki iliyopita alimuomba mumewe pesa ya mkaa, mume akawa hana. Alichofanya ni kwamba amemnyima chakula (anachonunua huyo huyo mume) mpaka leo hii. Yani "kwa eaha na shida (siku hizi inabidi mchungaji akisema . . . . na shida waseme "INATEGEMEA NI ZIPI" badala ya "NDIO NAKUBALI" za kinafiki) aliyotamka imekosa matendo.
Sasa mwanamke kama huyu, mume akimbadilikia au akimmwaga atamlaumu nani?Nae ataweza kusimama mahali na kusema wanaume ni watu wabaya? Kwanini asifanye shughuli ndogo ndogo nae awe anasaidia akiona mume mambo hayajamuendea vizuri sana kwenye shughuli zake?
Ahhhhh wanaume wengine mna kazi kweli aisee. . .nawapa pole wote mnaokaribia kupewa vichaa na wake/wapenzi wenu.