Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Huyu bwana mdogo ananiheshimu sana kutokana na anavyonijua.Ana mpenzi tangu anasoma form five, walikua na malengo ya kufika mbali.Kijana alimpoteza mama yake(alifariki) wakati yuko form one,hivyo ameishi na baba yake muda wote huu.Kijana mwaka jana amemaliza chuo,na muda huu anafanya kazi Nbc bank,kazi hii ana mwezi tu tangu aipate.Muda wa mwaka mmoja uliopita amekua akinilalamikia mpenzi wake kubadilika vituko haviishi,nimekua nikimshauri kuwa mvumilivu lakini kilichotokea juzi sijui hata nisemeje.Mpenzi wa kijana ana miaka 25 na kijana ana miaka 27,siku ya tukio majira ya saa 2 usiku alipigiwa simu na baba yake kuwa baba yake ana sapraizi.Kijana akaenda,akamkuta mpenzi wake yuko na baba yake,wakati hajajua kinachoendelea baba akamwambia kijana akae,akafanya hivyo,ndipo baba akamwambia kijana "unajua tangu mama yako atutoke nimekua mpweke sana,sasa huyu natarajia muda mfupi ujao awe nasi pale nyumbani,unasemaje?" Kijana akawa kwenye mshangao,ndipo alipokurupuka kutoka kwenye mshangao na kukubaliana na baba yake.Baadae kijana alimpigia simu mpenzi wake kumuuliza kulikoni binti akamwambia "kwanza naomb iwe mwisho kunipigia simu na kuanzia leo uniheshimu kama mama yako,mambo tuliyofanya huko nyuma yafanye historia.Sasa kijana amechanganyikiwa na anauliza,atawezaje kuishi na mama yake mpya wakati alikua mpenzi wake?Kijana hajui afanye nini,unaweza kumshauri afanye nini?