Dadake mbunge Munde Tambwe (CCM) akamatwa na dawa za kulevya!

[h=2]Monday, July 30, 2012[/h] [h=3]LISSU ATAJA WABUNGE WALA RUSHWA[/h]


Kuhusu majina ya wabunge wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya rushwa, Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, wabunge hao walipaswa kutaja masilahi yao kibiashara kwenye shirika hilo.
"Sasa wabunge hawa hawajawahi kufanya hivyo na wameendelea kuwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini na wengine kufanya biashara na TANESCO," alisema Lissu na kuwataja kuwa ni Munde Tambwe, Sara Msafiri, Mariam Kisangi wa Viti Maalumu, Yusuf Nassir (Korogwe Mjini) na Charles Mwijage Muleba Kaskazini.
Lissu alifafanua kuwa Tambwe na Msafiri wana tenda ya kuiuzia TANESCO matairi na kwamba hawajawahi kutangaza masilahi yao katika jambo hilo kwenye kamati zao.
"Mwijage ni mtaalamu mwelekezi wa Kampuni ya PUMA Energy iliyopewa tenda na Maswi kuiuzia mafuta TANESCO, hivyo kama mjumbe wa Kamati ya Nishati ana mgongano wa kimasilahi. Nassir na Kisangi hawa wanafanya biashara ya mafuta wanamiliki vituo vya mafuta na wana mgongano," alisema.

Kuhusu Christopher ole Sendeka, Lissu alidai kuwa amekuwa akizipigia debe kampuni tatu zilizonyimwa tenda ya kuiuzia mafuta TANESCO akiwashawishi wajumbe wa kamati kuwa serikali ilikiuka kanuni kuipa tenda Kampuni ya PUMA Energy.
Mbunge mwingine aliyetajwa ni Vicky Kamata wa Viti Maalumu ambaye alidaiwa kuwa na mgongano wa kimasilahi na Maswi.
"Tunampongeza Spika kwa kuivunja Kamati ya Nishati na Madini lakini tunataka azivunje pia zile za LAAC, inayoongozwa na Augustine Mrema (TLP) na POAC ya Zitto, kwa kuwa baadhi ya wajumbe wake wamekuwa wakitajwa sana kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Fukuto la kutajwa kwa majina ya wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa lilitawala mjadala wa Bunge jana, ambapo wabunge, Kangi Lugora (Mwibara), James Mbatia (Kuteuliwa), Ali Keisy (Nkasi), Joshua Nassari (Arumeru Mashariki na Salum Baruani (Lindi Mjini), waliomba mwongozo wa Spika wakidai wahusika wawekwe wazi.
Hata hivyo, katika mwongozo wake, Naibu Spika, Job Ndugai, alisema kuwa Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge inaendelea na uchunguzi kama ilivyoagizwa na Spika ndipo hatua nyingine zitafuata.
"Wabunge, baadhi mtaitwa kusaidia kamati hiyo lakini si kwamba ukiitwa kuhojiwa na kamati inamaanisha umepokea rushwa, ni katika hatua za mwanzo tu kufikia ukweli wa kile kinachochunguzwa. Labda niwaeleze kuwa Spika amekubali kuiangalia kamati hii ili wale wajumbe wenye mgongano wa kimasilahi waondolewe," alisema.
Alikataa kutaja majina ya watuhumiwa akisema kuwa Spika pamoja na yeye hawawajui wahusika ndiyo maana wanachunguza kuwabaini. Lakini aligusia kuwa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeanza kuwahoji baadhi ya wabunge.
Ndugai pia alitolea ufafanuzi mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Rage (CCM), aliyetaka kujua ni kwanini kiongozi wa upinzani alitaja majina ya watuhumiwa wa rushwa kutoka CCM wakati kwenye chama chake cha CHADEMA kuna watuhumiwa pia.
"Mimi ningewashauri kuwa katika jambo hili tuwe na subira na tukitaka kulizungumza tutende haki kwa pande zote, maana hakuna chama chenye sera ya kura rushwa, tusilifanye kisiasa kwa kuoneana," alisema Ndugai.
Watuhumiwa wajitetea
Tanzania Daima iliwasiliana na watuhumiwa kujua wana kauli gani dhidi ya tuhuma hizo ambapo Mwijage, Msafiri na Munde simu zao ziliita pasipo kupokewa wakati Ole Sendeka, Kisangi na Nassir walizikanusha.
Nassir alisema kuwa si kweli kuwa anafanya biashara ya mafuta bali aliwahi kufanya kazi katika Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) ambapo alipata ujuzi na hivyo kuwa na nia ya kutaka kuanza biashara ya gesi.
"Lissu ni mwanasheria lakini nashindwa kuelewa ni kwanini anafanya ‘generalization' katika jambo hili, mimi sifanyi biashara ya mafuta na TANESCO wala serikali kupitia wizara husika, nampuuza kwa madai yake na nitamchukulia hatua," alisema.
Kwa upande wake Kisangi alikiri kufanya biashara ya mafuta, akisema anamiliki vituo vya mafuta eneo la Mbagala Rangi Tatu, lakini akafafanua kuwa kila wakati alipochangia hoja ndani ya Bunge na kwenye Kamati ya Nishati na Madini alitangaza masilahi yake.
"Mimi niko vizuri sina wasiwasi, rejea kumbukumbu rasmi za Bunge utaona kuwa nimetangaza masilahi yangu, hivyo namshangaa huyu mwanasheria. Ina maana naye kuwa kwenye Kamati ya Sheria ni mgongano wa masilahi kwa vile ni mwanasheria?" alihoji.
Ole Sendeka naye alisema kuwa hakuwahi kuzipigia debe kampuni anazohusishwa nazo kwani alichokifanya kwenye kamati ni kuwaeleza wajumbe namna Maswi alivyovunja sheria ya manunuzi ya umma.
"Maswi ameichukua PUMA Energy kama mashati ya mitumba sokoni wala haikuwa kushindanishwa, sasa kama Lissu ambaye ni mwanasheria haoni hilo napata taabu," alisema.
na tanzania daima
 
Pasco, with the respect your have earned yourself in JF community. It is high time you start distancing yourself from some issues.

Ahaa Chadema na ukweli ni kama maji na mafuta!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Dada wa mbunge wa viti maalumu (CCM) Mh Munde Tambwe anayeitwa Khadija Tambwe alikamatwa jana na madawa ya kulevya ktk uwanja wa ndege wa JK Nyerere akiwa safarini kuelekea Uturuki.

Mpaka sasa polisi haijatoa taarifa ya tukio hili.

Ifahamike kuwa Munde ni mmoja wa wabunge wanaotuhumiwa kwa rushwa kamati ya bunge ya Nishati na Madini.

NIPASHE wamehabarisha "Uyo Mbunge inasemekana alishatangulia huko alikokua anakwenda uyo aliyekamatwa na hayo madawa kwa ajili ya kumpokea". check zaidi hapo chini kutoka nipashe ya 31.07.2012.


"Wanawake wawili wamekamtwa katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, wakiwa katika harakati za kusafirisha bangi ya kusindikwa.

Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya cha Jeshi la Polisi, Alfred Nzowa, aliwataja watu hao kuwa ni Hadija Tambwe Magesa (42) na Sasha Farhan Mnyeki (34), wote wakazi wa Shekilango, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Habari zaidi ambazo gazeti hili zimeipata zinasema kuwa Hadija, anadaiwa kuwa na mawasiliano na mbunge mmoja ambaye alikuwa ametangulia kumpokea huko alikokuwa anakwenda.

Kwa mujibu wa Nzowa, watuhumiwa hao walikamatwa usiku wa kuamkia Julai 29, mwaka huu, wakisubiri kusafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki kutoka Dar es Salaam kwenda Uturuki.

Alisema Hadija alikamatwa na bangi ya kusindikwa kilo 20, wakati Sasha alikamatwa na bangi hiyo kilo 20.

Nzowa alisema Hadija alikutwa na pasipoti ya kusafiria namba AB 151604, iliyotolewa Mei 16,2006, ambapo Sasha alikutwa na pasipoti namba AB 174099, iliyotolewa Septemba 7, 2006.

Aidha Nzowa aliongeza kwamba inaonyesha kuwepo na mtandao mkubwa unaotumia wanawake katika biashara ya dawa za kulevya na hivyo alitoa wito kwa wanawake kukataa kutumiwa katika biashara hiyo.

Hata hivyo, Nzowa alisema uchunguzi juu ya tukio hilo unaendela na pindi ukikamilika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani.

CHANZO: NIPASHE
 
Hii ni tabia ya wahalifu wengi kutumia CCM kama kichaka cha kujificha juzijuzi Tanga Mdogo wa Rostam aliachiwa kwenye kesi ya kukutwa na Madawa ya Kulevya, na sasa Dada wa Munde Tambwe kwa hiyo inaonyesha kichaka cha wauza madawa ya kulevya ni CCM, tunaomba safisheni hicho chama tunaangamia jamani.
 
Pascal wa PPR sorry Pasco wa JF mbona povu? Lazima atuambie huyu mtu ni nani,kusema kwamba ni dada yake na mb. Sio kosa bwana,tena na huyu mb anatajwa kuvuta mlungula!

Tambua kuwa muanzisha thread alitaka sisi tuchanganue wenyewe....inapotikeea ndugu wa karibu kajihusisha na shughulu kama hiyo....tunatakiwa kummulika kwa undani mheshimiwa tukioanaisha na issue iliyopo kama kwa jinsi moja au nyingine anahusika.

KWa mtazamo wangu...tulipaswa kuangalia mabadiliko ya kimaisha ya mbunge muhusika, yawezekana dada anatumiaga jina la Mh kupitisha mihadarati AU NI MUHESHIMIWA ANAMTUMIA MDOGO WAKE!!!!

Tutafakali sio kukurupuka tu!!!!!!
 
NIPASHE wamehabarisha "Uyo Mbunge inasemekana alishatangulia huko alikokua anakwenda uyo aliyekamatwa na hayo madawa kwa ajili ya kumpokea". check zaidi hapo chini kutoka nipashe ya 31.07.2012.


"Wanawake wawili wamekamtwa katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, wakiwa katika harakati za kusafirisha bangi ya kusindikwa.

Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya cha Jeshi la Polisi, Alfred Nzowa, aliwataja watu hao kuwa ni Hadija Tambwe Magesa (42) na Sasha Farhan Mnyeki (34), wote wakazi wa Shekilango, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Habari zaidi ambazo gazeti hili zimeipata zinasema kuwa Hadija, anadaiwa kuwa na mawasiliano na mbunge mmoja ambaye alikuwa ametangulia kumpokea huko alikokuwa anakwenda.

Kwa mujibu wa Nzowa, watuhumiwa hao walikamatwa usiku wa kuamkia Julai 29, mwaka huu, wakisubiri kusafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki kutoka Dar es Salaam kwenda Uturuki.

Alisema Hadija alikamatwa na bangi ya kusindikwa kilo 20, wakati Sasha alikamatwa na bangi hiyo kilo 20.

Nzowa alisema Hadija alikutwa na pasipoti ya kusafiria namba AB 151604, iliyotolewa Mei 16,2006, ambapo Sasha alikutwa na pasipoti namba AB 174099, iliyotolewa Septemba 7, 2006.

Aidha Nzowa aliongeza kwamba inaonyesha kuwepo na mtandao mkubwa unaotumia wanawake katika biashara ya dawa za kulevya na hivyo alitoa wito kwa wanawake kukataa kutumiwa katika biashara hiyo.

Hata hivyo, Nzowa alisema uchunguzi juu ya tukio hilo unaendela na pindi ukikamilika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani.

CHANZO: NIPASHE
Hawatafikishwa mahakamani kwa kuwa wanahusiana na Mbunge wa CCM kaka
 
Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya cha Jeshi la Polisi, Alfred Nzowa, aliwataja watu hao kuwa ni Hadija Tambwe Magesa (42) na Sasha Farhan Mnyeki (34), wote wakazi wa Shekilango, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Habari zaidi ambazo gazeti hili zimeipata zinasema kuwa Hadija, anadaiwa kuwa na mawasiliano na mbunge mmoja ambaye alikuwa ametangulia kumpokea huko alikokuwa anakwenda.

Wana JF ni sisi Watanzania tutakaoweza kuiokomboa nchi hii. Tukitengemea hivi vyombo vya dola vya CCM We are finish. Juzi amekamatwa mdogo wake Rostamu na madawa ya kulevya but POLICE wamemu exonerate.

To put thing in perspective Mwana JF aliyeko Dodoma tunaomba afanye uchunguzi kama Mh. Munde Tambwe yupo Bungeni Dodoma.

Kama hayupo Bungeni, tunaomba mwana JF yeyote aliyepo JKNI atueleze kama aliwahi kumuona Munde Tambwe akisafiri siku nje ya nchi siku za hivi karibuni, final destination ikiwa Uturuki.

Tukiweza kupata hizo information, then tukawenda VODACOME, Airtel, TIGO ku cross check kama simu ya aliyekuwa anawasiliane naye Hadija ni ya Dada yake Mh. Munde Tambwe.

Tukimaliza kukusanya hizi taarifa tutawapasha umma wa Tanzania jinsi baadhi ya vigogo wa CCM wanavyotumia vyeo vyao kufanya biashara ya mihadarati, ingawa pia tunafahamu walitumia chupi zao kupata hivyo vyeo.

CCM ni janga la kitaifa kila mtu kwa sehemu aliyepo atumia nafasi yake kufichua maovu ya CCM.
 
Mkuu Sangarara, nimekusikia, ila pia its a respetable professional mpaka kuna watu wanajipatia ajira rasmi tena very decent jobs kwa ajili hiyo!.

Hivi una taarifa enzi za vita kuu ya pili wanawake walikuwa hawaajiriwi jeshini, ilibidi hao wenye kazi hizo kukusanywa na nguvu na kupelekwa vitani kwa title za 'confort ladies"!. Baada ya kusainiwa The Universal Declaration of Human Right, 1948, ndipo kuwalazimisha wadada kutoa huduma hizo kukasitishwa na majeshi wakaamriwa wawaajiri rasmi kama askari wa kike!. Find out kwenye military book, hawa wadada wakisha ajiriwa ni lazima kwanza watumike kwa miaka mingapi ndipo waruhusiwe kuolewa!.

Kiukweli, kwenye biashara hii lawama na shutuma zote zinaelekezwa tuu kwa hawa wadada, lakini there are are customers ambao siku zote hawatajwi kabisa!. Biashara ipo na inashamiri kwa sababu wateja wapo na wanashamiri, cha ajabu, wanasumbuliwa tuu wadada, wateja wako ok!.

Tafuta uzi wangu kuhusu wabunge wapya wa viti maalum, wengi wamekuwa wakipata nafasi hizo kwa sifa kuu ya uwezo wa kutoa huduma hizo za kibinaadamu, na kuna wengine, amini usiamini, tangu wameingia bungeni, hawajawahi kuuliza swali wala kuchangia hoja yoyote!, wao ni huduma tuu!, angalau kuna baadhi yao ofcourse huduma lazima watoe, ila angalau hijitutumua kuuliza hata vijiswali na kuchangia vijimichango kwenye baadhi ya hoja!.

Pia tunatatizo kubwa la double standards humu, wakifanya biashara hiyo, nameless dada zetu ndio watajwe, wakifanya waheshimiwa...no wasitajwe tunawaheshimu sana!, tena mna bahati, ningeweza kumwaga humu listi ya mpaka mawaziri waliowahi!.

Hii nimeipenda mkuu
 
Mbunge wa CCM viti maalumu kutokea mkoani Tabora Munde Tambwe Abdallah,amehusishwa na uuzajiwa madawa ya kulevya aina ya Bangi..kutokana na kukamatwa kwa mdogo wake Air Port Dar es salaam huyo ndugu yake ajulikanaye kama Hadija Magesa ni nduguye lakini Jina lake halisi ni Hadija Tambwe Abdallah!...kwataarifa zilizopatikana zinaonyesha Munde aliondoka nchini kwa ndege ya shirika la emirates No EK 726 julai 28/2012 kwenda italia saa chache yeye na mwenzake Sasha Mnyake kukamatwa wakitaka kuondoka kwa ndege shirika la ndege la Uturuki namba TJ 604 julai 29/2012 kwenda Istambul uturuki.
Chanzo:Raia Mwema.
 
Ili ku-dilute uzito wa issue mbele ya jamii watasema na Zitto yumo.
 
Back
Top Bottom