Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Kwanza haijawahi kunitokea,huu ni ukweli.Alivyoniambia nilihisi miguu ikilegea! Nilikutana na dada huyu akaniambia ni Mkenya. . . Akaniuliza kama ni mwenyeji hapa Mwanza nikamwambia ndio.
Akaniomba nimsaidie kumpeleka baadhi ya maeneo fulani hivi, nilimpeleka. . . Wakati nakutanana nae jana ilikua saa 8 mchana.
Nilimpa msaada aliouhitaji kwani jana jumapili sikua na kazi nilimaliza mizunguko yangu mapema,na ilipofika saa 11 jioni akawa amekamilisha kazi yake akaniambia anataka akanywe juisi,nikampeleka,wakati tunakunywa ndipo akaniambia "(akinitaja jina kwani nilimwambia). . . .
Nakushukuru kwa msaada ila ningefurahi kama tungeenda ukani. . .(akataja tendo la ndoa bila tafsida) nitafurahi zaidi na nitaona nimekushukuru vizuri"!!!!
Kwanza juisi niliyotaka kuimeza ilinikaba,kisha nikaduwaa!Nilikosa la kusema kisha nikagundua miguu imelegea!Ilibidi nikurupuke. . . Eeeeee. . Mmmmmm thanks,usijali nimekusaidia tu dada!!
Alijitahidi kunisihi mwishowe ikabidi nimpe excuse ya ugonjwa akanielewa japokuwa hakuridhika!Nilitamani nimdanganye nimeoa lakini wakati tuko kwenye mizunguko aliniuliza kama nimeoa nilimwambia ukweli kuwa sijaoa!Dah nimejiuliza sana kwa taharuki ile ilisababishwa na nini sipati jibu.
Sijui ni kwa kuwa sipo kwenye mahusiano muda mrefu!Yaani na umri hu wa miaka 3.... kidogo nionekane katoto. . .Lol! Jamani wadada wamebadilika unapokutana nae jiandae kwa lolote!!!!Dada huyu anaondoka leo mchana na Akamba!!
Akaniomba nimsaidie kumpeleka baadhi ya maeneo fulani hivi, nilimpeleka. . . Wakati nakutanana nae jana ilikua saa 8 mchana.
Nilimpa msaada aliouhitaji kwani jana jumapili sikua na kazi nilimaliza mizunguko yangu mapema,na ilipofika saa 11 jioni akawa amekamilisha kazi yake akaniambia anataka akanywe juisi,nikampeleka,wakati tunakunywa ndipo akaniambia "(akinitaja jina kwani nilimwambia). . . .
Nakushukuru kwa msaada ila ningefurahi kama tungeenda ukani. . .(akataja tendo la ndoa bila tafsida) nitafurahi zaidi na nitaona nimekushukuru vizuri"!!!!
Kwanza juisi niliyotaka kuimeza ilinikaba,kisha nikaduwaa!Nilikosa la kusema kisha nikagundua miguu imelegea!Ilibidi nikurupuke. . . Eeeeee. . Mmmmmm thanks,usijali nimekusaidia tu dada!!
Alijitahidi kunisihi mwishowe ikabidi nimpe excuse ya ugonjwa akanielewa japokuwa hakuridhika!Nilitamani nimdanganye nimeoa lakini wakati tuko kwenye mizunguko aliniuliza kama nimeoa nilimwambia ukweli kuwa sijaoa!Dah nimejiuliza sana kwa taharuki ile ilisababishwa na nini sipati jibu.
Sijui ni kwa kuwa sipo kwenye mahusiano muda mrefu!Yaani na umri hu wa miaka 3.... kidogo nionekane katoto. . .Lol! Jamani wadada wamebadilika unapokutana nae jiandae kwa lolote!!!!Dada huyu anaondoka leo mchana na Akamba!!