Dada Dr. Pamela Sawa, tafadhali jirekebishe!

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,238
4,464
N.B: Nimeiweka hapa kwenye siasa, maana Tz kila kitu ni siasa tu!

Nimekuwa na rafiki zangu wazalendo kuliko mimi (kama watatu) ambao wamekutana na mama huyu pale Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Kama kawaida ya mama huyu wote walikuwa wakifika ofisini kwake wanaishia kuondoka wamekwazika, bila kujali malengo yao thabiti ya kuanzisha hospitali na vituo vidogo vya afya nchini Tanzania, kwa lengo la kuboresha maisha ya mtanzania. Hawa ni watanzania ambao wametumia mali zao ili kufungua vituo vya afya nchini, biashara ambayo kwa hakika si ya kuaminika kwa nchi yetu ya Tanzania lakini wakiwa wanaongozwa na dhamira njema ya kusaidia wenzetu nyumbani wamethubutu kujaribu (Mmoja Marekani, mwingine Afrika Kusini, na wa mwisho yupo nyumbani Tanzania). (Tunamshukuru Mungu ndugu zangu hawa wote wamepata usajili baada ya kusota kwa miezi kadhaa wakisubiri kupata usajili).

Naambiwa Dr. Pamella Sawa ni Msajili wa Vituo vya Afya Binafsi na Umma wizara ya Afya. Kitengo ambacho kwa hakika kimekuwa kinazidi kufungia vituo vya watu binafsi kwa maelekezo kwamba havijatimiza vigezo wakati huo huo wakiviacha vituo vya serikali visivyohitajika hata kuwapo kwa jinsi visivyokuwa na sifa za kutoa huduma kwa wananchi.

Kitengo hiki kimekuwa kikipokea rushwa nyingi wawapo kuchunguza utendaji kazi wa vituo vya afya Tanzania, na mara zote wamekuwa wanatengeneza mazingira ya rushwa hata kama huna kosa.

Mtanzania msomi, Dr Pamella anasifika sana kwa kuheshimu raia wa kigeni hususani wahindi wenye vituo vyao vya afya nchini kwetu, huku akiwadharau Watanzania vijana kwa wazee ambao wanajitolea kutoa huduma kama hiyo. Ni mara nyingi utaona mhindi anaruhusiwa kuingia ofisini kwake bila kusubiri foleni ya watanzania waliokaa nje ya ofisi yake.

Ukiingia ofisini kwa Dr. Sawa (Yameshawahi nikuta wakati namsindikiza jamaa yangu kufuatilia usajili wa hospitali yake) utapokelewa kwa moyo mkarimu na wasaidizi wake ambao pia hawaishi kunyanyaswa na dada huyu mrembo lakini ghafla ukashangaa anakutoa kwa ukali kwa kisingizio cha kwamba wana mkutano au subiri mtu mwingine atoke (japo kuna watu zaidi ya watatu wanaotoa huduma katika ofisi yake).

Dr. Sawa anasifika kwa maneno makali ambayo baadhi ya nyakati huleta aibu kwa watanzania wanaoingia ofisini kwake. Watumishi wengi wizara ya afya ambao wanahitaji huduma katika ofisi yake huenda kuongea naye kwa woga mkumbwa utadhani yeye ni Simba, ingawa ana umbile dogo na lenye mvuto.

Wengine wanadai kwamba ati Sawa hutumiwa na baadhi ya rafiki zake kutoruhusu kupitisha maombi ya watu wengine wanaonekana ni hatari kwa vituo vingine vya afya kuendelea kupata wateja (sina uhakika maana maombi hupitishwa na board, ingawa yeye huhusika na hatua zote za kupitia maombi na pia ana nguvu sana kikaoni).

Tunashukuru serikali kutoa fursa sawa kwa wote, maana hata mwanamke msomi kama huyu anaweza kupata nafasi nzuri wizara ya afya makao makuu bila shida yoyote, lakini mambo anayowafanyia watanzania wenye moyo safi wa kutaka kuisaidia jamii yetu yanamfanya aonekane asiyefaa na kwa kweli anatakiwa ajirekebishe haraka.

Kama ni tabia zake za asili basi ajitahidi kuziweka kando pindi awapo kazini.

Lakini Tutafika tu!!!
 
Kitengo ambacho kwa hakika kimekuwa kinazidi kufungia vituo vya watu binafsi kwa maelekezo kwamba havijatimiza vigezo wakati huo huo wakiviacha vituo vya serikali visivyohitajika hata kuwapo kwa jinsi visivyokuwa na sifa za kutoa huduma kwa wananchi. Kitengo hiki kimekuwa kikipokea rushwa nyingi wawapo kuchunguza utendaji kazi wa vituo vya afya Tanzania, na mara zote wamekuwa wanatengeneza mazingira ya rushwa hata kama huna kosa.

Bolded: double standards, kuna vitu vya afya vya serikali vinatia aibu kwa uchafu. vingine hakuna hata vyoo.
 
Kumbe we ulikuwa hujui kuwa wanawake wengi wakipata madaraka wanakuwa na roho za kinyama. Wapo wengi sana kama huyo.
 
Pamela Sawa nimewahi kumuona kwenye TV alipokuwa anafunga Hospital pale Stop Over... hana tofauti na yule Jinga wa NHC Raymond Mndolwa na Puppet wake mkubwa...ambaye juzi juzi alikuwa Mwanza hivi wanawatoa wapi hawa machiziiii...
 
Huyo Dr. Pamela hana kitu wala hasiwababaishe. Na sijui huo udaktari kaupatapataje huko Russia maana form 4 hapa Tanzania alipata division zero. Siku nyingine ukienda muulize jina lake la ukweli. Jina lake haswa ni Lulu Sawa; amesomea Muhimbili P/School na alikuwa anakaa Ocean Road, pale Sea View. Baade akaenda either Mzizima Secondary au Shaaban Robert. Yawezekana alichakachukua vyeti vya form 4 na 6.

Tatizo la Tanzania mtu akishakuja na cheti cha nje wanamshobokea na kumpa cheo kikubwa bila kuangalia background yake ikoje.
 
Lengo la wizara ni zuri ila dada anaatatizo ta tabia since akiwa shule

hilo la wahindi limenishtua
 
Hakuna tofauti ya waliosoma na wasiosoma! Rushwa na ubabe ofisini kwa watanzania wasomi ni jadi. Inauma sana, tena sana. Poleni ma Dr.
 
Je na hapo tutamlaumu JK? Maana huyo mwana dada Dr, is an individual ambaye amepewa dhamana na serikali, watanzania inabidi yubadilike kwanza as individual ndiyo tuikosoe serikali, bila hivyo anayepata rungu atapiga kila mahali, na mwingine akipata naye analipiza kisasi.
 
Kuwa daktari wa binadamu ni kitu very sensitive saana lakini TZ na wizara ya afya kila mara unasikia watu hawana uwezo wa kuitwa madaktari ilikuwa Kigoda na sasa huyu kulikoni wizara hiyo ? Hebu wekeni CV yake tuipitie jamani
 
Tatizo la nchi yetu ni kwamba tumefanywa tuamini kwamba ofisi za serikali hazipo kwa ajili ya kutuhudumia sisi, bali zipo kwa ajili ya ku-exercise authority juu yetu.
Ni lazima tubadili huu mfumo ili hao wanaokalia viti kwenye ofisi za serikali wajue kwamba wapo pale kwa ajili ya kutuhudumia sisi na si vinginevyo.
 
Je na hapo tutamlaumu JK? Maana huyo mwana dada Dr, is an individual ambaye amepewa dhamana na serikali, watanzania inabidi yubadilike kwanza as individual ndiyo tuikosoe serikali, bila hivyo anayepata rungu atapiga kila mahali, na mwingine akipata naye analipiza kisasi.

directly hapana, indirectly yes kwani yeye huteua wasiamizi wa watu kama dr sawa
 
Ndiyo matatizo ya watu kuitwa Dr bila kuwa na sifa za kuitwa Dr mara Dr. Kikwete yale yale!
Huyo Pamela pumbavu zake.!

hapo kwenye red kama unakosea vile aisee

Pamela ni daktari alisoma urusi/nchi za huko, alifanya intern miaka zaidi ya 12 iliyopita na post graduate (nadhani)... anastahili kuitwa Dr. na vituo anavyofunga vingi ni kweli vina matatizo, shida inakuja kwa serikali kwa ujumla kwamba vituo vyake (vya serikali) ndio vina hali mbaya zaidi kimajengo, vifaa na wafanyakazi, na yeye hana uwezo wa kufunga kwani yupo kusimamia private. ni muhimu tukubali kwamba kuna baadhi ya vituo vya fya binafsi lazima vifungwe

Upande wangu naona tatizo la huyu dada ni anavyotreat watu wanaohitaji huduma, she looks down at people mara nyingine na pia hilo la wahindi limenisikitisha kwani hakuwahi kuonyesha kama ni mla rushwa (issues zake ni mahusiano na watu tu)
 
Kumbe we ulikuwa hujui kuwa wanawake wengi wakipata madaraka wanakuwa na roho za kinyama. Wapo wengi sana kama huyo.

Tena humo kwenye mawizara ndo balaa kabisa! Mi nlishaacha kwenda maeneo hayo, huwa natuma mtu tu, unless nahitajika mimi mwenyewe personaly.
 
Mmh! Kuna mtu kama yeye aliondolewa kwenye ofisi kama hiyo nchi fulani maeneo ya kusini huku baada ya kuwa anawaletea nyodo wadau wa vituo kama hivyo. Wadau wa ofisi husika wakaandamana hadi kwa waziri husika kwamba huyu ndugu umemwajiri kwa ajili yetu, na sasa hawezi kutuhudumia sisi tunavyostahili; hatuoni kama kuna umuhimu wa wewe kuendelea kumlipa mshahara wakati hatupati huduma inayostahili toka kwake.
Nimepita pita pale wizarani bongo nikifuatilia nyaraka zangu za kufanya kazi ng'ambo, bahati nzuri sijawahi kumbana naye ila naamini kutakuwa na ukweli, hasa ukizingatia watumishi wengi wizarani makwetu, hususani wizara ya afya huzifanya ofisi za serikali kama za familia. Tujirekerebishe, hebu tuchape kazi.
 
inasikitisha sana, halafu tunalaumu nchi haisongi mbele wakati wazalendo hawapewi fursa. Je malalamiko haya yamefika eneo stahili? Hakuna utaratibu maalum wa kutoa malalamiko anagalau mhusika akapewa onyo! Isijekuwa watu wanaumia halafu yanaishia hapa tunasema tumwachie mungu! Mkuu nakushauri uandike barua ya malalamiko in general bila kuonyesha kuna lolote ambalo ni personal kwenda kwa katibu mkuu/waziri! Sina hakika kama ndio sehemu stahili.
 
inasikitisha sana, halafu tunalaumu nchi haisongi mbele wakati wazalendo hawapewi fursa. Je malalamiko haya yamefika eneo stahili? Hakuna utaratibu maalum wa kutoa malalamiko anagalau mhusika akapewa onyo! Isijekuwa watu wanaumia halafu yanaishia hapa tunasema tumwachie mungu! Mkuu nakushauri uandike barua ya malalamiko in general bila kuonyesha kuna lolote ambalo ni personal kwenda kwa katibu mkuu/waziri! Sina hakika kama ndio sehemu stahili.

Kuna mtu anamlinda pale wizarani. Hata ukiandika bado haitasaidia kitu
 
Wanawake badilikeni. Mnapopata nafasi nzuri onyesheni kwamba tunaweza na hamkupewa kwa upendeleo. Inanisikitisha sana kila mara wanawake wenye madaraka kulaumiwa kwa utendaji wao. Hebu tujirekebishe ili ile fursa sawa ionekane.
 
Back
Top Bottom