Uanachama wa CWT kwa walimu wa Shule za serikali ni lazima that's why tunakatwa michango directly hata bila kujiunga, unakumbuka wale walimu wa Kigoma ambao wamejaribu kujitoa hadi mahakamani wamebaunsi.... CWT ni mradi wa serikali kuwakandamiza walimu.. Vp auditing CWT MBONA haifanyiki?Sheria zipo. Tangu lini vyama vya hiari vimegeuzwa kuwa wanyang'anyi wa fedha ya mwl. bila hiyari.? Amini uanachama si lazima, pia kuanzisha chama kingine ruksa. Tuhamasike tujitoe ndipo CWT itajua kuwa ilijisahau kutetea walimu. Mwisho aminini kuwa hata mgomo huo unao hubiriwa na Mkoba ni viini macho vya kumfanya yeye avute mshiko. Mkoba na .......... damu damu!.
tutumie njia gani mkuu hawa CWT ni wanyonyaji hivi ni haki kila ofisi ya wilaya Kuwa na ESCUDO tena ambazo zimenunuliwa kwa bei ya kuruka, ni haki kwa makatibu na wenyeviti kulipana posho kwa kutimiza wajibu wao? Na je kuna uhalisia wa gharama halisi za mwalimu houses mikoani na tunavyoziona? Hivi zile billion 3 za kuanzisha mwalimu bank zimeenda wapi?Mkoba mnafiki,tuachane na CWT.Tujipange upya tupate haki zetu.