Seif Sharif Hamad keshaolewa uko ZNZ, hamuoni siku hizi yupo very smart jamani? Ananyoa ndevu, ananyoa nywele, anapika, anaosha vyombe, anafua nguo.
Wakuu kama nimelewa issue nadhani hapa issue si ndoa wala unyumba ndogo wa CUF bali walichosema kuhusiana na gamba Edward Lowassa. Kuna haja ya kuangalia ukweli au uongo au uzito wa waliyosema. Ni kweli CUF na CCM ni mke na mume. Hili halina mjadala. Hivyo mie naona hili lisingetupotezea muda vinginevyo hoja ijifie. Hoja ya CUF hata kama yaweza kuwa ya kinafiki ina mashiko kuwa Lowassa ni sehemu ya matatizo yanayosababisha umaskini kwa watanzania. Kwa ufupi ni kwamba wanampiga fumbo Lowassa hadi Kikwete kuwa wizi wao ndiyo unasababisha umaskini wetu.