Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
CUF watishia kwenda ICC Wednesday, 29 December 2010 20:52
Sadick Mtulya na Elias Sichalwe CHAMA cha Wananchi (CUF) kimetishia kwenda Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kuwashitaki viongozi wa Serikali kutokana na kile kinachodai kuwa ni ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na Jeshi la Polisi nchini.
CUF wanalalamikia polisi kuwakamata wafuasi wake 40 kwa tuhuma za kushiriki maandamano yaliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi kwa lengo la kuwasilisha rasimu sifuri ya Katiba kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani.
Maandamano hayo yalifanyika wakati kukiwa na marufuku ya Jeshi la Polisi inayozuia kutofanyika kwake na polisi hao kuyaita kuwa ni batili kutokana na kufanyika bila kibali chao.
Jana, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria wa CUF, Salim Bimani aliliambia Mwananchi kuwa Kama polisi wataendelea na ukiukwaji wa haki za binadamu, CUF ipo tayari kulifikisha suala hili ICC kuwashtaki viongozi wa nchi kwa ukiukwaji huo.
Kwa mujibu wa Bimani, polisi hawakuwa na mamlaka ya kuwakamata waandamanaji hao kutokana na ukweli kwamba maandamano ni haki ya kikatiba ya kila mwananchi.
Alisema katika maandamano hayo, watu 40 walikamatwa na kuhojiwa kwa saa kadhaa na wengine kuachiwa huru muda mfupi baadaye.
"Hadi saa 6:00 mchana wanachama 40 waliokamatwa, lakini wamachama 36 waliachiwa baadaye hivyo ninavyozungumza hapa bado kuna watu wanne wako mahabusu,"alisema Bimani.
Bimani alimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha kuvidhibiti vyombo vya usalama kwa kuwa vingi, vinafanya kazi kinyume na taratibu na vinakiuka haki za binadamu. Awali akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya CUF jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Julius Mtatiro alisema rasimu ya katiba iliyowasilishwa jana wizarani ina sura 16 na ibara 131.
Rasimu hiyo ya Katiba imeandaliwa na wadau mbalimbali ikiwamo kunakiliwa kutoka kwenye katiba zaidi ya 30 za nchi mbalimbali duniani zikiwemo za Afrika na Ulaya, alisema Mtatiro. Kwa mujibu wa Mtatiro, Sura ya tano, ibara ya 32 ya rasimu hiyo inahusu uwepo wa Rais wa Jamuhuri ya Shirikisho la Tanzania ambaye atakuwa mkuu wa nchi, kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.
Juzi majira ya saa 2:00 asubuhi polisi wenye silaha walifika ofisi za CUF kudhibiti maandamano ambapo waliwatangazia wananchi hali ya hatari na kuwataka wajifungie majumbani mwao huku wakifyatua risasi za moto na kurusha mabomo kuwatawanya.
Mara baada ya tangazo hilo, wananchi walianza kukusanyika kwa wingi nje ya makao makuu ya chama hicho wakiwa na mabango mikononi na vitambaa vilivyoandikwa ujumbe mbalimbali wa kudai katiba mpya. Baada ya hapo, magari hayo ya polisi yaliyokuwa yamesheheni askari wenye silaha nzito za moto na mabomu ya kutolea machozi, yaliondoka na kwenda kuegeshwa katika makutano ya barabara ya Uhuru na barabara ndogo inayoingilia Makao Makuu ya CUF eneo la Rozana.
Baadaye waandamanaji walianza maandamano na walipofika Rozana, magari ya polisi yaliondoka na kwenda kuegeshwa katika kituo cha mabasi cha Buguruni Malapa, ambako gari maalumu la kumwaga maji ya kuwasha maarufu kama deraya, lilikuwa limeegeshwa.
Baada ya kuona hivyo waandamanaji walijipa moyo na kuona labda polisi wanawaogopa na hivyo kuingia moja kwa moja katika Barabara Kuu ya Uhuru kuelekea mjini. Lakini, walipofika Malapa, walikumbana na kizuizi cha magari ya polisi zaidi ya sita ya FFU na deraya nyingine. Hapo ilikuwa kama mchezo wa kuigiza baina ya FFU na waandamanaji, baada ya kila upande kumtunishia msuli mwingine. Wakati polisi wakiwataka wanachama hao wasalimu amri na kusitisha maandamano yao, wanachama hao wanajibu "Kuandamana ni haki yetu kikatiba.
" Wakiwa wanatunishiana misuli katika kituo cha mabasi cha Malapa, gari moja la FFU lilikaa katikati ya barabara na dereva wake alitangaza tena Tafadhali hili gari usilipite, ukilipita hili gari unatafuta shari. Lakini pamoja na tangazo hilo, wanachama hao waliendelea kulipita gari hilo na mkuu wa operesheni ya polisi hao akaruhusu gari la maji ya kuwasha kuanza kuwarushia maji.
Wakati hayo yakiendelea, daladala na magari yote yanayotoka na kwenda Buguruni yalikuwa yamezuia kupita na kupaki pembeni ama kwa amri au kwa hofu yao wenyewe. Baada ya kuona kizuizi hicho waandamanaji hao waliamua kuingia mitaani na kwenda kuibukia katika mitaa ya Amana na Ilala Boma na kuendelea na safari ya kuelekea wizarani. Wakati huo polisi walikuwa wameachwa Malapa.
Polisi hao walisituka kwamba maandamano yanaendelea wakati waandamanaji hao walipokuwa tayari wamefika eneo la Karume na Mchikichini. Maandamano yalipofika kati ya mitaa ya Ilala Boma na Karume, polisi hao ambao walikuwa tayari wameshajawa na hasira kwa mchezo wa sinema waliokuwa wakichezewa na waandamanaji, waliamua kufyatua risasi za moto kuwatawanya.
Pia mabomu kadhaa ya kutoa machozi yalilipuliwa katika mitaa hiyo jambo ambalo lilisababisha waandamanaji hao kuanza kupoteza mwelekeo huku baadhi ya viongozi wao, wakifanikiwa kupita kwa gari la chama lenye bendera. Baadaye maandamano hayo yalifanikiwa kufika ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria ambako viongozi wa CUF walikabidhi rasimu yao ya katiba. Mwisho
Sadick Mtulya na Elias Sichalwe CHAMA cha Wananchi (CUF) kimetishia kwenda Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kuwashitaki viongozi wa Serikali kutokana na kile kinachodai kuwa ni ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na Jeshi la Polisi nchini.
CUF wanalalamikia polisi kuwakamata wafuasi wake 40 kwa tuhuma za kushiriki maandamano yaliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi kwa lengo la kuwasilisha rasimu sifuri ya Katiba kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani.
Maandamano hayo yalifanyika wakati kukiwa na marufuku ya Jeshi la Polisi inayozuia kutofanyika kwake na polisi hao kuyaita kuwa ni batili kutokana na kufanyika bila kibali chao.
Jana, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria wa CUF, Salim Bimani aliliambia Mwananchi kuwa Kama polisi wataendelea na ukiukwaji wa haki za binadamu, CUF ipo tayari kulifikisha suala hili ICC kuwashtaki viongozi wa nchi kwa ukiukwaji huo.
Kwa mujibu wa Bimani, polisi hawakuwa na mamlaka ya kuwakamata waandamanaji hao kutokana na ukweli kwamba maandamano ni haki ya kikatiba ya kila mwananchi.
Alisema katika maandamano hayo, watu 40 walikamatwa na kuhojiwa kwa saa kadhaa na wengine kuachiwa huru muda mfupi baadaye.
"Hadi saa 6:00 mchana wanachama 40 waliokamatwa, lakini wamachama 36 waliachiwa baadaye hivyo ninavyozungumza hapa bado kuna watu wanne wako mahabusu,"alisema Bimani.
Bimani alimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha kuvidhibiti vyombo vya usalama kwa kuwa vingi, vinafanya kazi kinyume na taratibu na vinakiuka haki za binadamu. Awali akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya CUF jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Julius Mtatiro alisema rasimu ya katiba iliyowasilishwa jana wizarani ina sura 16 na ibara 131.
Rasimu hiyo ya Katiba imeandaliwa na wadau mbalimbali ikiwamo kunakiliwa kutoka kwenye katiba zaidi ya 30 za nchi mbalimbali duniani zikiwemo za Afrika na Ulaya, alisema Mtatiro. Kwa mujibu wa Mtatiro, Sura ya tano, ibara ya 32 ya rasimu hiyo inahusu uwepo wa Rais wa Jamuhuri ya Shirikisho la Tanzania ambaye atakuwa mkuu wa nchi, kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.
Juzi majira ya saa 2:00 asubuhi polisi wenye silaha walifika ofisi za CUF kudhibiti maandamano ambapo waliwatangazia wananchi hali ya hatari na kuwataka wajifungie majumbani mwao huku wakifyatua risasi za moto na kurusha mabomo kuwatawanya.
Mara baada ya tangazo hilo, wananchi walianza kukusanyika kwa wingi nje ya makao makuu ya chama hicho wakiwa na mabango mikononi na vitambaa vilivyoandikwa ujumbe mbalimbali wa kudai katiba mpya. Baada ya hapo, magari hayo ya polisi yaliyokuwa yamesheheni askari wenye silaha nzito za moto na mabomu ya kutolea machozi, yaliondoka na kwenda kuegeshwa katika makutano ya barabara ya Uhuru na barabara ndogo inayoingilia Makao Makuu ya CUF eneo la Rozana.
Baadaye waandamanaji walianza maandamano na walipofika Rozana, magari ya polisi yaliondoka na kwenda kuegeshwa katika kituo cha mabasi cha Buguruni Malapa, ambako gari maalumu la kumwaga maji ya kuwasha maarufu kama deraya, lilikuwa limeegeshwa.
Baada ya kuona hivyo waandamanaji walijipa moyo na kuona labda polisi wanawaogopa na hivyo kuingia moja kwa moja katika Barabara Kuu ya Uhuru kuelekea mjini. Lakini, walipofika Malapa, walikumbana na kizuizi cha magari ya polisi zaidi ya sita ya FFU na deraya nyingine. Hapo ilikuwa kama mchezo wa kuigiza baina ya FFU na waandamanaji, baada ya kila upande kumtunishia msuli mwingine. Wakati polisi wakiwataka wanachama hao wasalimu amri na kusitisha maandamano yao, wanachama hao wanajibu "Kuandamana ni haki yetu kikatiba.
" Wakiwa wanatunishiana misuli katika kituo cha mabasi cha Malapa, gari moja la FFU lilikaa katikati ya barabara na dereva wake alitangaza tena Tafadhali hili gari usilipite, ukilipita hili gari unatafuta shari. Lakini pamoja na tangazo hilo, wanachama hao waliendelea kulipita gari hilo na mkuu wa operesheni ya polisi hao akaruhusu gari la maji ya kuwasha kuanza kuwarushia maji.
Wakati hayo yakiendelea, daladala na magari yote yanayotoka na kwenda Buguruni yalikuwa yamezuia kupita na kupaki pembeni ama kwa amri au kwa hofu yao wenyewe. Baada ya kuona kizuizi hicho waandamanaji hao waliamua kuingia mitaani na kwenda kuibukia katika mitaa ya Amana na Ilala Boma na kuendelea na safari ya kuelekea wizarani. Wakati huo polisi walikuwa wameachwa Malapa.
Polisi hao walisituka kwamba maandamano yanaendelea wakati waandamanaji hao walipokuwa tayari wamefika eneo la Karume na Mchikichini. Maandamano yalipofika kati ya mitaa ya Ilala Boma na Karume, polisi hao ambao walikuwa tayari wameshajawa na hasira kwa mchezo wa sinema waliokuwa wakichezewa na waandamanaji, waliamua kufyatua risasi za moto kuwatawanya.
Pia mabomu kadhaa ya kutoa machozi yalilipuliwa katika mitaa hiyo jambo ambalo lilisababisha waandamanaji hao kuanza kupoteza mwelekeo huku baadhi ya viongozi wao, wakifanikiwa kupita kwa gari la chama lenye bendera. Baadaye maandamano hayo yalifanikiwa kufika ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria ambako viongozi wa CUF walikabidhi rasimu yao ya katiba. Mwisho