CUF watishia kujilipua

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Kama hili ni kweli, basi hawa CUF wanataka kutuletea balaa kubwa sana

CUF watishia kujilipua

na Mwandishi Wetu, Pemba
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENENDO wa mambo visiwani Zanzibar unazidi kuwa wa mashaka, baada ya wafuasi wa Chama Cha Wananchi (CUF) kutangaza kuwa wataanza kujivisha mabomu ya kujitoa muhanga kama njia ya kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kusaini makubaliano ya mazungumzo ya muafaka.

Sambamba na hatua hiyo ya kutisha, pia wamewataka wafanyabiashara kutoka kisiwani Pemba kutosafirisha mazao ya chakula kwenda katika Kisiwa cha Unguja.

Hatua hiyo ni tishio kwa wakazi wa Unguja wanaotegemea chakula kutoka Pemba na iwapo itatekelezwa, itasababisha maelfu ya wakazi wa kisiwa hicho kukabiliwa na baa la njaa.

Wito wa kujitoa muhanga kwa wana CUF kama njia ya kukabiliana na manyanyaso waliyodai kuyapata kutoka Serikali ya Mapinduzi, ulitolewa na mwimbaji wa utenzi, Saidi Hamad, mbele ya viongozi wakuu wa chama hicho.

Huku akishangiliwa na umati wa wanachama hicho wakati akisoma utenzi baada ya kumalizika kwa maandamano ya amani ya kuishinikiza CCM kusaini makubaliano ya muafaka, Hamad alisema wana CUF wako tayari kujivika mabomu ya kujitoa muhanga kutokana na manyanyaso na maumivu ya ubaguzi wanayofanyiwa na serikali.

Baada ya Hamad kumaliza kusoma utenzi huo, Mbunge wa Viti Maalumu wa CUF, Rizik Omar, ambaye alisoma risala mbele ya viongozi wa CUF, alisema Wapemba wote wanapaswa kususia kupeleka chakula Unguja.

Katika risala hiyo, wanachama wa CUF wanawaonya wakazi wote wa Pemba kuwa, atakayekwenda kinyume cha uamuzi huo wa kutopeleka chakula Unguja, atatengwa kwa vile atadhihirisha kuwa hana umoja na wenzake na hajali maovu wanayofanyiwa Wapemba na SMZ.

Hatua hiyo iwapo itatekelezwa, inaweza kuwa madhara makubwa zaidi, kwa kuwa Kisiwa cha Unguja kinategemea sehemu kubwa ya mazao na matunda kutoka Pemba.

Sambamba na hilo, wafuasi wa CUF pia wametakiwa kutotumia meli za serikali za mv Mapinduzi na mv Maendeleo katika safari wanazozifanya kati ya visiwa vya Unguja na Pemba.

Ilidaiwa na msoma risala huyo kuwa, Wapemba wanapaswa kugoma kutumia usafiri wa meli hizo kwa sababu zimekodishwa kwa mama wa kiongozi mmoja wa SMZ na mkataba wake ni wa kutatanisha.

Madai mengine ya kuwepo kwa migomo hiyo yaliyosomwa katika risala hiyo, ni Wapemba kutengwa katika nafasi za ajira serikalini na kwenye taasisi za umma pamoja na kutopatiwa nafasi za masomo na uongozi kama vile wao si sehemu ya Zanzibar au Jamhuri ya Muungano.

Akizungumza katika mkutano huo, Makamu Mwenyekiti wa CUF, Machano Khamis, alisema anaunga mkono uamuzi wa wananchi wa Pemba ingawa atakuwa mmoja wa waathirika wa mgomo huo.

Alisema mgomo huo ni hatua nzuri kwa vile ni moja ya njia za mapambano ya kupigania haki na kukataa kudhulumiwa.

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alisema chama hicho kimefunga mlango wa mjadala na CCM juu ya suala la muafaka na kutangaza masharti yanayopaswa kutekelezwa kabla ya kurejea katika meza ya mazungumzo.

Aliyataja masharti hayo kuwa ni Rais Jakaya Kikwete kuwakutanisha na Rais Amani Abeid Karume, kama alivyofanya kwa Rais Mwai Kibaki na kiongozi wa upinzani, Raila Odinga, wakati aliposhiriki mazungumzo ya mgogoro wa kisiasa wa Kenya.

Alisema kumkubali Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ni kupoteza muda na kuendeleza fani ya usanii ya CCM kwa sababu Makamba hana kauli wala uamuzi katika chama hicho ambacho kila siku kinabadili kauli zake.

Alisema iwapo Rais Kikwete atashindwa kutimiza sharti la kwanza, basi anapaswa kuhakikisha makubaliano ya pande mbili zilizokuwa zikishiriki mazungumzo ya muafaka yanatekelezwa kwa kusainiwa na wahusika na utekelezaji wake kuanza mara moja.

Kwamba njia hizo ndizo pekee zinazoweza kuinusuru Zanzibar isitumbukie kwenye matatizo makubwa zaidi.

Kwa upande wake, Prof. Ibrahim Lipumba aliuambia umati wa waandamanaji hao kuwa, amesikitishwa na kitendo cha viongozi wa serikali waliolazimika kuachia madarakani kwa tuhuma za kukiuka maadili ya uongozi kupokelewa kwa mbwembwe majimboni kwao mfano wa mashujaa.

Alisema viongozi wa serikali na CCM wilaya, kumpokea aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, kwa karamu nono za nyama choma na pombe ni kuwakebehi Watanzania walioiweka serikali ya CCM madarakani.

Lipumba alisema katika nchi inayozingatia misingi ya utawala bora, viongozi wanaokabiliwa na shutuma za aina yoyote hawapaswi kurandaranda mitaani, bali wanapaswa kuwa chini ya uchunguzi na wanapothibitika kutenda kosa huwa wanafikishwa mahakamani mara moja.

Alimkumbusha Rais Kikwete kutekeleza ahadi aliyoitoa bungeni ya kuwashughulikia mafisadi na kuinusuru nchi na watu wenye nia ya kuhujumu rasilimali za nchi kwa kuweka mbele tamaa zao.

Wakati CUF wakiendelea kulia na CCM, Katibu Mkuu wa chama hicho tawala, Yusuph Makamba leo anatarajia kukutana na waandishi wa habari kuzungumzia maendeleo ya mazungumzo yao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (bara), George Mkuchika ilieleza mkutano huo ni muhimu kwa mustakabali wa Zanzibar na nchi kwa ujumla.

Wakati CCM wakitarajia kutoa maendeleo ya mazungumzo hayo, CUF wao walishaweka wazi msimamo wao kuwa hawatakubali kufanya mazungumzo na CCM kwani hatua waliyofikia ilipaswa iheshimiwe.

CUF walisema katika mazungumzo yaliyomalizika hivi karibuni walikubaliana namna ya kumaliza tatizo hilo, lakini kikao cha CCM kilichoketi Butiama kiligoma kukubali mapendekezo hayo.

CCM katika kikao chake iliweka wazi msimamo wake kuwa suala la muafaka au serikali ya mseto linapaswa kujadiliwa na wananchi wote na wala si chama au kundi la watu fulani.

Msimamo huo uliwakera zaidi CUF kiasi cha wabunge wao kuamua kutoka nje katika mkutano wa kumi na moja wa Bunge mjini Dodoma kwa lengo la kushinikiza CCM kukubali mazungumzo waliyokubaliana katika mkutano wa muafaka.

Aidha, CUF iliamua kufanya maandamano nchi nzima kupinga uamuzi wa Butiama na kuwataka wananchi washirikiane nao kama ishara ya kukuza demokrasia hapa nchini.

Zanzibar imekuwa na mgogoro wa kisiasa tangu kufanyika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 na makubaliano mawili ya muafaka ya hapo awali kukwama, huku watu kadhaa wakipoteza maisha katika machafuko yaliyowahusisha wafuasi wa CUF na vyombo vya dola
 
hayo ndio mambo ya akili kweli? hawa ndio tuwaachie nchi watawale?

sasa jee watawaambia pia wahame unguja warudi pemba?

maana wanachekesha sana hawa watu na wavae mabomu na vifaru

warudi kwenye mazungumzo wazungumze sio vitisho na upuuzi
 
siasa za vitisho hazijatatua matatizo; leo hii israel na palestina licha kulipuana na kuuana wamefikia karibu kwenye suluhisho la mgogoro wao kwa kiasi gani?

Kuna mambo mengine ni mazuri kutia hamasa lakini haya manufaa yoyote yale.
 
Kama hili ni kweli, basi hawa CUF wanataka kutuletea balaa kubwa sana

CUF watishia kujilipua

na Mwandishi Wetu, Pemba
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENENDO wa mambo visiwani Zanzibar unazidi kuwa wa mashaka, baada ya wafuasi wa Chama Cha Wananchi (CUF) kutangaza kuwa wataanza kujivisha mabomu ya kujitoa muhanga kama njia ya kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete kusaini makubaliano ya mazungumzo ya muafaka.

Sambamba na hatua hiyo ya kutisha, pia wamewataka wafanyabiashara kutoka kisiwani Pemba kutosafirisha mazao ya chakula kwenda katika Kisiwa cha Unguja.

Hatua hiyo ni tishio kwa wakazi wa Unguja wanaotegemea chakula kutoka Pemba na iwapo itatekelezwa, itasababisha maelfu ya wakazi wa kisiwa hicho kukabiliwa na baa la njaa.

Wito wa kujitoa muhanga kwa wana CUF kama njia ya kukabiliana na manyanyaso waliyodai kuyapata kutoka Serikali ya Mapinduzi, ulitolewa na mwimbaji wa utenzi, Saidi Hamad, mbele ya viongozi wakuu wa chama hicho.

Huku akishangiliwa na umati wa wanachama hicho wakati akisoma utenzi baada ya kumalizika kwa maandamano ya amani ya kuishinikiza CCM kusaini makubaliano ya muafaka, Hamad alisema wana CUF wako tayari kujivika mabomu ya kujitoa muhanga kutokana na manyanyaso na maumivu ya ubaguzi wanayofanyiwa na serikali.

Baada ya Hamad kumaliza kusoma utenzi huo, Mbunge wa Viti Maalumu wa CUF, Rizik Omar, ambaye alisoma risala mbele ya viongozi wa CUF, alisema Wapemba wote wanapaswa kususia kupeleka chakula Unguja.

Katika risala hiyo, wanachama wa CUF wanawaonya wakazi wote wa Pemba kuwa, atakayekwenda kinyume cha uamuzi huo wa kutopeleka chakula Unguja, atatengwa kwa vile atadhihirisha kuwa hana umoja na wenzake na hajali maovu wanayofanyiwa Wapemba na SMZ.

Hatua hiyo iwapo itatekelezwa, inaweza kuwa madhara makubwa zaidi, kwa kuwa Kisiwa cha Unguja kinategemea sehemu kubwa ya mazao na matunda kutoka Pemba.










Mh kuna kaharufu huko CUF, kuna mtu tu anataka kuwafanya CUF waonekane kama Terrorists, sasa kwa akili hii ndio wataweza kuongoza nchi kwa kweli. Hebu fungueni macho ninyi, nchi inauzwa nyie mnapoteza muda wenu kutaka kujiua, ili nani aumie sasa? ama kweli!!!!!
GIVE THEM THE LONGEST ROPE AND THEY'LL HANG THEMSELVES.
 
Hiyo ni danganya toto tu. Subutu, hawa jamaa wa CUF kamwe hawawezi kujilipua. Ndio kusema kama Ibrahimu Lipumba akiweka sera zake endapo atakapokuwa Raisi na wapinzani wa wakati huo watapinga uongozi wake, Lipumba kweli atajilipua kama hawa jamaa wanavyotaka kujilipua?
 
Nani ajilipue? Thubutu!

Labda kama wanazungumzia 'kujilipua' kwa kuchana passport na kuukana uraia, hiyo wanaiweza sana.
 
I am alittle bit confused about these guys(CUF) I am sorry, I sometimes consider them as terrorists and sometimes kama wapigania haki. Haiji kichwani kiongozi mkubwa kama huyo aanze kututishia kuwa CUF wanataka kujilipua. Kwanza kabisa huyu jamaa inabidi afunguliwe kesi ya jinai na pili watafutwe hao jamaa watakao jilipua na wawekwe ndaini na baadae hiki chama Kifutiwe kabisa usaji. Sababu uhaini kama huu hatuukalibishi kabisa hapa ktk visiwa vyetu vya ZNZ. Mie ningeshauri hawa CUF wakaungane na wenzao akina ALQAEDA akiongozwa na bosi wao OSAMA, wadituletee fujo hapa visiwani.INSHALLAR
 
nadhani wakitaka kujilipua wajifungue vyumbani mwao wao na watoto wao halafu waweke matangazo nje "tutajilupua saa fulani"
 
Siungi mkono sula la watu kujiua lakini kila mtu Tanzania yuko frustrated kivyake

JAMBO FORUMS mnko frustrated na mnatumia internet kuonyesha hilo

wapemba (CUF) nao wanatathmini jinsi gani watakavyonyesha frustration yao


Who knows maybe WATAWALA wetu wakiona damu inamwagika wanaweza kustuka kidogo


Upande wa wapemba nao nadhani its about time wakaachana na kujenga ma Ghorofa ya mabilionioni kariakoo na kuchangia serikali ya CCM mpaka dola milioni moja wakati kule pemba hakuna kitu cha maana wanachoijenga

ukweli ni kuwa si kazi ya wananchi kujenga hospitali au bara bara lakini surely kama wapemba wangaanza kujenga viwanda na nyumba kwao inamaana kutakuwa na employment kwa wakazi wake

kama wameamua kuwa kujilipua ndio njia iliyobasi then be it

mimi nishachoka na political system yetu ya ngojera kila kukicha

serikali inayo pesa za kulipia vita COMOROS lakini haina pesa za kujenga bara bara Pemba..halafu wakitaka kujitenga wanaambiwa eti wao ni wabaya

 
CUF watishia kujilipua

na Mwandishi Wetu, Pemba
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENENDO wa mambo visiwani Zanzibar unazidi kuwa wa mashaka, baada ya wafuasi wa Chama Cha Wananchi (CUF) kutangaza kuwa wataanza kujivisha mabomu ya kujitoa muhanga

Wito wa kujitoa muhanga kwa wana CUF kama njia ya kukabiliana na manyanyaso waliyodai kuyapata kutoka Serikali ya Mapinduzi, ulitolewa na mwimbaji wa utenzi, Saidi Hamad, mbele ya viongozi wakuu wa chama hicho.

Jarida hili linapotosha.

1. Wapi hapo inaonyesha 'wafuasi' wamesema hivyo zaidi ya mfuasi mmoja, muimba tenzi?

2. Huyo mwimbaji ana nguvu ya kutoa tamko la CUF au kutumbuiza?

3. Waandishi waliwauliza wasemaji wa CUF kuhusu hilo, au wameliachia achia jambo linaning'inia hewani ili waje kutudanganya 'CUF wametoa tamko?'

4. Pia, nipe nukuu ya hata sentensi moja ya maneno yake mwenyewe. Usinitafsirie peke yake. Tafadhali ndugu muhariri.

Jamani hawa waandishi ni waongo, wachovu. Hawana hiyo taaluma hata kama wameenda shule za uandishi. Mimi sio CUF lakini nataka ukweli kwanza, kabla sijajadili lolote. Bongo hakuna Media!
 
Siungi mkono sula la watu kujiua lakini kila mtu Tanzania yuko frustrated kivyake

JAMBO FORUMS mnko frustrated na mnatumia internet kuonyesha hilo

wapemba (CUF) nao wanatathmini jinsi gani watakavyonyesha frustration yao


Who knows maybe WATAWALA wetu wakiona damu inamwagika wanaweza kustuka kidogo


Upande wa wapemba nao nadhani its about time wakaachana na kujenga ma Ghorofa ya mabilionioni kariakoo na kuchangia serikali ya CCM mpaka dola milioni moja wakati kule pemba hakuna kitu cha maana wanachoijenga

ukweli ni kuwa si kazi ya wananchi kujenga hospitali au bara bara lakini surely kama wapemba wangaanza kujenga viwanda na nyumba kwao inamaana kutakuwa na employment kwa wakazi wake

kama wameamua kuwa kujilipua ndio njia iliyobasi then be it

mimi nishachoka na political system yetu ya ngojera kila kukicha

serikali inayo pesa za kulipia vita COMOROS lakini haina pesa za kujenga bara bara Pemba..halafu wakitaka kujitenga wanaambiwa eti wao ni wabaya


Hivi kwa nini tusiweze kusoma alama za nyakati?

Hivi katika migogoro katika visiwa vya zanzibar wamekufa wangapi?

Lisemwalo lipo kama halipo basi jueni linakuja.
 
Ujinga mtupu, hizi ndizo siasa za Seif Hamad toka nimfahamu...

Mkuu ni vizuri kusema lakini siasa za CCM ni mbaya sana hata kuliko hizo za CUF. huna haja ya kujiuliza kujua wenzako wamegafirika vipi ktk hili. Tutatue tatizo lililopo mbele yetu.

Hawa CUF wanataka haki. Haki ktk bahadhi ya nchi haiwezi kuja bila kuidai wakati mwingine kutumia nguvu. Kila mtu ana uhuru wa kusema lolote kulingana na jinsi anavyoguswa.
 
Swala hili ni very sensitive. I don't support hawa jamaa kujilipua kwani hawezi solve tatizo. Bali nashangaa kwa nini JK anaweza kuwa kinyonga na kugeuka maamuzi ya Mkamba na Seif?

Nimepata siki more than 95% ya wabunge wa pemba ni CUF, sasa najiuliza jee ni haki kwa chama chenye wabunge zaidi 95% ndani ya pemba kutokuwa na wawakilishi ndani ya serikali? Wakati JK and CCM plays politic Wapemba wanashindwa kupata matibabu, wanashindwa kupeleka watoto wao kwenye shule bura sababu tuu walichagua CUF kwenye general election.

Pemba hata Umeme ni tabu, mafuta ni tabu, na pemba ndio wakulima wakuu wa visiwani kule.

I support swala zima la kutokutuma chakula unguja, however i condem swala la kujilipua mabomu.
 
Ujinga mtupu, hizi ndizo siasa za Seif Hamad toka nimfahamu...

Kabla hujamlaani Seif, hebu kwanza take time kuisoma Pemba. If you can just travel to Pemba. I bet ukirudi utabadilisha imani yako nzima.

I don't support Maalim on certain things, lakini i do understand jinsi anavyoihangaikia zanzibar.
 
Mambo yatamshinda Kikwete amepandishwa mkenge na akina karume .ambae ameenda Marekani kuweka kampeni ya waUnguja nao wadai serikali yao ,kwa wanaoweza au kusikia habari za waUnguja nao wakidai Unguja iachane na Bara na Pemba ,watu wagawane mbao wafike pwani au jahazi litazama.
Habari tulizozipata kutoka sauti ya
amerika,voa,zikiwahoji maalwatani wa kiunguja/Zanzibar zimewafurahishwa na kuunga mkono hatua za wananchi wa pemba kwa kudai serikali kamili ya jamhuri ya jazira/pemba,pamoja na kuichimba petrol kwa nafasi yao
na kujiunga na opec na sisi waumguja tunawaunga mkono kwa hilo na tuko nyuma kufuata nyayo zao kwa kudai serikali kamili ya unguja/zanzibar bila ya shirikisho
la bara au pemba kwani hatua hiyo litaisaidia unguja katika kupunguza tatizo la ardhi,ambayo imevamiwa na wageni kwa fujo.
 
Na mimi mtanganyika naliunga mkono hilo. Ni lini mtatuondolea mzigo wa umeme na ruzuku toka kwenye hazina yetu, pemba na unguja sio sawa na arusha na mara. Cha msingi jamani jiondoeni wenyewe kwani nilikuwa nawaonea huruma kusema muungano uvunjike. Mmechukua biashara huku na mmechukua viwanja huku tanganyika, jitengeni mrudi kwenu mtuachie ardhi yetu. Ni afadhali mjiunge opec tanganyika tunawatia aibu kwa ngozi nyeusi.
 
Mkuu ni vizuri kusema lakini siasa za CCM ni mbaya sana hata kuliko hizo za CUF. huna haja ya kujiuliza kujua wenzako wamegafirika vipi ktk hili. Tutatue tatizo lililopo mbele yetu.

Hawa CUF wanataka haki. Haki ktk bahadhi ya nchi haiwezi kuja bila kuidai wakati mwingine kutumia nguvu. Kila mtu ana uhuru wa kusema lolote kulingana na jinsi anavyoguswa.

Nafikiri umefika wakati ambao watu wamefikia mwisho wa uvumilivu na hili linatokea kwa binadamu yeyote au kiumbe yeyote ,kwani hata paka unaweza kucheza nae lakini akishindwa kuvumilia na akaona unamchezea bila mpangilio atakuparura na kukutoa mikwaruzo na damu kukumwagika seuze binadamu ambae huweka tamaa kwamba pengine uchaguzi utakaokuja kutakuwa na amani lakini si hivyo makundi ya CCM-Zanzibar yamekuwa yakiwashukia wapemba chini ya ulinzi wa Vyombo vya dola wakiwatesa na kuwanajisi ndugu zao mbele ya wanafamilia jambo ambalo ni unyama wa mwisho ambao binadamu anaweza kuutenda kwa aliehai na anaetazama kinachofanyika ,hayo yamepita Pemba katika wakati wa Uchaguzi mkuu wa CCM ,na si jambo la siri waliokufa wapo ,waliowekwa vilema wapo walionajisiwa wapo na waliotizamishwa wapo ,sasa wewe unaekaa na kusema wanachotaka kukifanya hakitaleta matunda ,kwa hali ilivyo Wapemba hawana haja ya matunda safari hii msipoangalia watakufa na mtu kama walivyoondoka na mapolisi na wengine kuwakata vichwa basi kwa Wapemba hayo mambo ya kujilipuwa naamini kabisa si jambo linalowashinda kwani sasa wanamsemo hakuna walilobakisha ila hilo la kufa na mtu kwa mikanda ya baruti umesikia sasa wameshaambizana Mpemba atakaepanda meli za Serikali hiari yake.Wapemba ni fighters ambao ugonvi wanauweza kinachowatuliza ni hizo nguvu za chama cha CUF lakini CUF sasa inaonekana kubwaga manyanga.
Na hapa Tanganyika haya mambo ya unyanyasaji hayapo mbali si yameshaanza kwenye uchaguzi wa Kiteto hiyo ndio CCM inapolinda mlo kwa hali yeyote na Utawala wa CCM unajulikana wangapi wameangamia chini ya utawala wa CCM utasikia mtu kapelekwa Lugalo mbona wengine hawapelekwi huko wanasafirishwa nchi za nje tena kwa fedha ya serikali ,Pemba ni mwamko wa wanaoipinga dhulma ya CCM ndani ya Taifa hili Tajiri hakuna sababu ya Mtanzania kufana kulala na njaa na Pemba hilo ndilo wanalolipigania.
GOD will show them the light to fight to the last drop of their blood lakini CCM will never ever gain support to the peoples of Pemba Land.
 
Back
Top Bottom