Alaa mkuu wangu wewe vipi? Yaani Chadema waliokuwa na CUF toka mwaka 1995 dhidi ya CCM, ghafla CUF wamejitoa na wamekuja unda urafiki na CCM, ulitaka Chadema wakae upande gani?..Maalim Seif alikuwa na kila dalili za Ushindi Zanzibar mkaungana na CCM kugawana vyeo, wewe unataka Chadema washangilie hilo. Na mlipokwenda fanya Muafaka kwa nini msiwajuze Chadema ambao ni wabia wenu..
Mkuu wangu CUF imejiweka sehemu mbaya wenyewe kwa kudanganywa na CCM. Na niliyasema haya hapa hapa JF kabla hata muafaka haujamalizika ya kwamba CCM watahakikisha wanashika sehemu zote muhimu na wamefanya hivyo. Na kisiasa chama cha Upinzani hujenga kambi na vyama vinavyopingana na chama tawala na sio vile vilivyoshindwa viunde umoja. CUF, NCCR,TLP na vyama vingine vyote vilivyochukua nafasi chini ya pili wana takiwa kuchagua upande wanaoona unashabihiana na malengo yao.
Hivyo, huwezi kuunda kambi moja na CUF chama kinachoshabikia sera za CCM, na hata kutumika ktk aendeleo ya Zanzibar waliko na Ubia.. Hivi tulivyo leo ndivyo inavyotakiwa kuwa. CCM na CUF kisha unakuta Chadema na NCCR picha zinakwenda na ndivyo ilivyotakiwa. Mimi naweza kusema tu NCCR walitakiwa kupewa nafasi ktk kuunda kambi ya Upinzani lakini sio CUF wala TLP kwa sababu hivi vyama vinaunga mkono sera za CCM..And that is Politics mkuu wangu.