CUF waridhia uamuzi wa JK; Wampongeza kusaini muswada mabadiliko ya katiba na kumuunga mkono

Pumb&%%@$^ I expected that anyways! Wakumbuke malipo ni hapa hapa duniani
 
Ulitegemea CUF wapingane na uamuzi wa bosi wao? Hakuna nyumba ndogo yenye ubavu wa kupinga maamuzi ya bwana wake. Maana kuiacha hakuhitaji talaka wala kwenda mahakamani-ni rahisi kama ku-swat inzi. CUF wamefanikiwa kuwaridhisha mabwana zao-CCM na kuendelea kuwasaliti wapemba waliowaamini kuwa ni wakombozi wasijue ni watafuta riziki. Seif amesaliti ndugu zake kwa cheo cha makamu wa rais. Sijui wale ndugu wa wale waliouawa kwenye fujo alizoanzisha akiwaaminisha wapemba kuwa alikuwa anatafuta haki yao na si umakamu wa rais wakimuona anatanua wakati wao wanatanuliwa na shida tokana na kufiwa na wapendwa wao wanajisikiaje? Sipendi kufikiria hili-linaumiza na kukatisha tamaa sana. CUF wanapaswa kuelewa kitu kimoja-mshitiri wao ni wa hovyo na hana ahadi. Rejea walivyogeukwa akina Nape na Chiligati. Your time is coming soon-just soon and in a very disgraceful manner.
 
Nilijua cuf wamekwenda kumliwaza mume wake ccm baada ya cdm kusema watabaki na msimamo wa awali, ukweli ndo hivyo kulingana na mahusiano yaliyopo cuf na ccm, ila cdm bado ikomae na kama vipi tuanzishe maandamano yasiyo na kikomo tanganyika nzima.
 
Alaa mkuu wangu wewe vipi? Yaani Chadema waliokuwa na CUF toka mwaka 1995 dhidi ya CCM, ghafla CUF wamejitoa na wamekuja unda urafiki na CCM, ulitaka Chadema wakae upande gani?..Maalim Seif alikuwa na kila dalili za Ushindi Zanzibar mkaungana na CCM kugawana vyeo, wewe unataka Chadema washangilie hilo. Na mlipokwenda fanya Muafaka kwa nini msiwajuze Chadema ambao ni wabia wenu..

Mkuu wangu CUF imejiweka sehemu mbaya wenyewe kwa kudanganywa na CCM. Na niliyasema haya hapa hapa JF kabla hata muafaka haujamalizika ya kwamba CCM watahakikisha wanashika sehemu zote muhimu na wamefanya hivyo. Na kisiasa chama cha Upinzani hujenga kambi na vyama vinavyopingana na chama tawala na sio vile vilivyoshindwa viunde umoja. CUF, NCCR,TLP na vyama vingine vyote vilivyochukua nafasi chini ya pili wana takiwa kuchagua upande wanaoona unashabihiana na malengo yao.

Hivyo, huwezi kuunda kambi moja na CUF chama kinachoshabikia sera za CCM, na hata kutumika ktk aendeleo ya Zanzibar waliko na Ubia.. Hivi tulivyo leo ndivyo inavyotakiwa kuwa. CCM na CUF kisha unakuta Chadema na NCCR picha zinakwenda na ndivyo ilivyotakiwa. Mimi naweza kusema tu NCCR walitakiwa kupewa nafasi ktk kuunda kambi ya Upinzani lakini sio CUF wala TLP kwa sababu hivi vyama vinaunga mkono sera za CCM..And that is Politics mkuu wangu.

Nakuunga mkono na ninaongeza kidogo! Sababu rahisi iliyopelekea CUF kuunda kambi ya upinzania bungeni kwa pamoja na CHADEMA ni kwa sababu CUF hawakuweza kufikisha kiwango cha wabunge wanaohitajika kuunda kambi rasmi ya upinzani na CUF wanajua hilo. Hata huko tulikoiga utaratibu huu ndo wanavyofanya, kwa hiyo mheshimiwa alitakiwa ajue hivyo kabla ya kufyatua ''SIJUI'' zake jamvini. Sisi wengine hukaa kimya kama hatuna uhakika vinginevyo huuliza!
 
Back
Top Bottom