jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
La!! Hapana, kauli zangu zinakanyagana na zako. Kauli zangu ziko wazi kuwa CCM wamepandikiza mbegu ovu juu ya CUF (nataja CCM kwa kuwa haina mtetezi hapa jukwaani na naogopa kuanzisha kukanyagana kwengine nikiwataja wahusika wengine. wa kusambaza mbegu hizi).Mpaka hapo tutakapotoka kwenye kasumba hizo CUF hata ipate fedha kiasi gani haitaweza kuwa na nguvu Bara.
Ngekewa hapo umeniacha kapa mkuu,nimesoma posting hii zaidi ya mara tatu lakini sijaambulia kitu hapo,hata hivyo nadhani Ndege ya Uchumi alikuwa akimjibu Gozigumu.