Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Tofauti kubwa imeendelea kudhihirika kati ya CUF Zanzibar na CUF Tanzania, baada ya maoni ya Hamad Rashid juu ya muswada wa katiba kupingwa hadharani na Naibu Katibu Mkuu (Bara), Julius Mtatiro leo.
Akihojiwa kwanza kwa njia ya simu, Hamad alisema kuwa muswada hauna tatizo, na wabunge watafanya kaz yao vyema kuhakikisha kuwa Watanzania watapewa kitu wanachokitarajia. Muda mfupi baadae alihojiwa Mtatiro ambaye alisema muswada ni mbovu na msimamo wa CUF ni kuwa haufai. Alipoulizwa kuhusu maoni yaliyotolewa na Hamad kuwa hauna tatizo, Mtatiro alisema hayo yalikuwa maoni ya Hamad binafsi, na sio ya chama.
Nikabaki najiuliza; CUF wana jukwaa gani refu la kuongelea zaidi ya bungeni?
Kama jukwaa refu ni bungeni, CUF bungeni wanawakilishwa na Wazanzibar (ukiacha mh wa Lindi), na maoni ya Hamad, bila shaka ndiyo maoni ya CUF Zanzibar.
Alafu nikajiuliza maoni ya Naibu katibu mkuu ndiyo maoni ya Katibu mkuu mwenyewe?!!!
Akihojiwa kwanza kwa njia ya simu, Hamad alisema kuwa muswada hauna tatizo, na wabunge watafanya kaz yao vyema kuhakikisha kuwa Watanzania watapewa kitu wanachokitarajia. Muda mfupi baadae alihojiwa Mtatiro ambaye alisema muswada ni mbovu na msimamo wa CUF ni kuwa haufai. Alipoulizwa kuhusu maoni yaliyotolewa na Hamad kuwa hauna tatizo, Mtatiro alisema hayo yalikuwa maoni ya Hamad binafsi, na sio ya chama.
Nikabaki najiuliza; CUF wana jukwaa gani refu la kuongelea zaidi ya bungeni?
Kama jukwaa refu ni bungeni, CUF bungeni wanawakilishwa na Wazanzibar (ukiacha mh wa Lindi), na maoni ya Hamad, bila shaka ndiyo maoni ya CUF Zanzibar.
Alafu nikajiuliza maoni ya Naibu katibu mkuu ndiyo maoni ya Katibu mkuu mwenyewe?!!!