CUF ni Wasaliti, Watakufa Kisiasa

ibange

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
1,543
550
Kwa watu wanaofuatilia siasa za Tz kuna wakati CUF walikuwa wanatumia falsafa ya ngangari na kujifanya wanatetea watu. Kuna watu nchi hii wameteswa na kupata tabu kwa ajili ya CUF. CUF walikuwa wanadai serikali ya Tanganyika na katiba mpya na haki sawa kwa wote. Kupewa cheo huko Znz kisicho na meno ndio kumewabadilisha hivi? Sasa kumbe walikuwa wanapigania vyeo na vihela vidogo? Ukweli kwa vile wamejifunga na CCM watazikwa pamoja. Wananchi wengi waliokuwa CUF sasa wamejua ni chama cha aina gani?

Haki hailetwi kwa kushirikiana na CCM. Haki inaletwa na katiba inayotokana na wananchi. CUF wangetumia nafasi hii kuweka mambo sawa maana muungano na ccm si wa kudumu ila katiba ni ya kudumu. Hivi CUF hawajui kuwa mkakati Znz ni kuhakikisha CUF haitakaa ishinde urais?
 
Tangu lini mke akapingana na mumewe hadharani?!!
Unapogundua mchezaji mwenzenu amehongwa na mshamaliza "sub", dawa ni kumnyima pasi tu!!!!
 
Kwa kile nilichokiona na kukisikia toka HAMAD Rashidi na wenzio kuhusu mswada wa katiba mpya,yeyote alieko CUF ambaye ni mwanachama wa kawaida kama ataendelea kuwa huko hadi ijumaa basi huyo ni mgonjwa wa akili.CUF sio kitu tena kwa kauli zao hizo hao sio kabisa,kubaki huko kama mwanachama au kiongozi wewe i adui kwa wapenda haki na wavuja jasho wa nchi hii
 
Hivi chama hiki bado kipo? Aibu kupata 2100 Igunga!

CUF inamatatizo makubwa tu.Tatizo wao wenyewe hawawezi kuambiana ukweli!Lakini ki ukweli Lipumba na Seif chama kimewashinda siku nyingi.Wameshindwa kutengeneza mtandao bara,hawatembei kuangalia uhai wa chama matokeo yake ndio hayo tuliyoshuhudia Igunga,.
Wanahitaji kubadilisha uongozi wa juu.Seif na Lipumba wanatakiwa wawapishe wengine.Hamad Rashid anafaa kuwavusha kwa sasa kama watampa uongozi wa juu,tatizo lake mzimu wa kupoteza uongozi wa kambi ya upinzani bungeni bado unamsumbua badala yake hasira anaielekeza CDM!Vinginevyo anafaa kuwa kiongozi wa kitaifa kuokoa jahazi la CUF.
Kosa jingine ni hii ndoa yao ya bandia na CCM.Hii watakuja jutia maana CCM ni kama vinyonga!Hawaaminiki kabisaaaa!Vinyonga hao.
 
Kwa watu wanaofuatilia siasa za Tz kuna wakati CUF walikuwa wanatumia falsafa ya ngangari na kujifanya wanatetea watu. Kuna watu nchi hii wameteswa na kupata tabu kwa ajili ya CUF. CUF walikuwa wanadai serikali ya Tanganyika na katiba mpya na haki sawa kwa wote. Kupewa cheo huko Znz kisicho na meno ndio kumewabadilisha hivi? Sasa kumbe walikuwa wanapigania vyeo na vihela vidogo? Ukweli kwa vile wamejifunga na CCM watazikwa pamoja. Wananchi wengi waliokuwa CUF sasa wamejua ni chama cha aina gani?

Haki hailetwi kwa kushirikiana na CCM. Haki inaletwa na katiba inayotokana na wananchi. CUF wangetumia nafasi hii kuweka mambo sawa maana muungano na ccm si wa kudumu ila katiba ni ya kudumu. Hivi CUF hawajui kuwa mkakati Znz ni kuhakikisha CUF haitakaa ishinde urais?

Nia ya CUF si kushinda urais kama walivyo CHADEMA. Nia ya CUF ni kuleta maendelea kwa watanzania kwa kuyashabikia na kuyaendeleza mawazo ya watanzania wote hata wa chama tawala ikiwa pamoja na wapinzani. Ni mawazo potofu, tena potofu sana kufikiria kuwa huwezi kuleta maendelea au mabadiliko mpaka ushinde Urais. Dhana hii ndio inayowafanya wenzetu CHADEMA washindwe kuungana na chama chochote pinzani na kutoweza kuzungumza na chama tawala.

Madai yote ya CUF yametelkelezwa na chama tawala ikiwa pamoja na:
  • kuunda SERIKALI YA MSETO ZANZIBAR
  • Kutungwa kwa katiba mpya Zanzibar
  • Kuwa na Daftari rasmi la wapiga kura ikiwa pamoja na kitambulisho cha mpiga kura
  • Kuundwa kwa katiba mpya ya Muungano ambayo Mswada wake umeshawasilishwa Bungeni (CHADEMA wamegoma)
  • Uhuru wa Media; sasa hivi wapinzani mnaonekana katika Luninge kama CCM Ikiwa pamoja na JF
Hebu niambie sababu hata mbili za CUF kuikasirikia CCM katika madai yao waliyoyadai kwa usemi maarufu wa NGANGARI.

Hivi sasa imebakia na dai moja ambalo nyie CHADEMA mnalipinga, nalo ni kuunda SERIKALI YA MSETO YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. Nilichogundua ni kwamba wewe ndio huelewi msimamo wa CUF. CUF ni chama chenye program na ajenda za muda mrefu (Long term program). Mipango ya muda mrefu haihitaji papara, inahitaji uvumilivu, hekima, ueleo wa juu, masikilizano na ummoja. Vyote hivyo vipo CUF.

Ninachoionea huruma CHADEMA ni kuwa chama cha nguvu ya SODA. Wajua matokeo yake ni nini.
 
Nia ya CUF si kushinda urais kama walivyo CHADEMA. Nia ya CUF ni kuleta maendelea kwa watanzania kwa kuyashabikia na kuyaendeleza mawazo ya watanzania wote hata wa chama tawala ikiwa pamoja na wapinzani. Ni mawazo potofu, tena potofu sana kufikiria kuwa huwezi kuleta maendelea au mabadiliko mpaka ushinde Urais. Dhana hii ndio inayowafanya wenzetu CHADEMA washindwe kuungana na chama chochote pinzani na kutoweza kuzungumza na chama tawala.

Madai yote ya CUF yametelkelezwa na chama tawala ikiwa pamoja na:
  • kuunda SERIKALI YA MSETO ZANZIBAR
  • Kutungwa kwa katiba mpya Zanzibar
  • Kuwa na Daftari rasmi la wapiga kura ikiwa pamoja na kitambulisho cha mpiga kura
  • Kuundwa kwa katiba mpya ya Muungano ambayo Mswada wake umeshawasilishwa Bungeni (CHADEMA wamegoma)
  • Uhuru wa Media; sasa hivi wapinzani mnaonekana katika Luninge kama CCM Ikiwa pamoja na JF
Hebu niambie sababu hata mbili za CUF kuikasirikia CCM katika madai yao waliyoyadai kwa usemi maarufu wa NGANGARI.

Hivi sasa imebakia na dai moja ambalo nyie CHADEMA mnalipinga, nalo ni kuunda SERIKALI YA MSETO YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. Nilichogundua ni kwamba wewe ndio huelewi msimamo wa CUF. CUF ni chama chenye program na ajenda za muda mrefu (Long term program). Mipango ya muda mrefu haihitaji papara, inahitaji uvumilivu, hekima, ueleo wa juu, masikilizano na ummoja. Vyote hivyo vipo CUF.

Ninachoionea huruma CHADEMA ni kuwa chama cha nguvu ya SODA. Wajua matokeo yake ni nini.

sera ya ccm serikali mbili kuelekea moja unguja na pemba zikiwa mikoa. Sera ya cuf serikali tatu ndio basi?
 
We zawadi una jinsia gani, nataka nijue. kama mwanume basi nikununulie KY maana Cameroon anakuja kuonana na wadau wa CUF na kama mwanamke nikuombee ubunge wa kiti maalum kwa magamba, ila uwe tayari kushi Pemba au Tanga, sawa?
 
We zawadi una jinsia gani, nataka nijue. kama mwanume basi nikununulie KY maana Cameroon anakuja kuonana na wadau wa CUF na kama mwanamke nikuombee ubunge wa kiti maalum kwa magamba, ila uwe tayari kushi Pemba au Tanga, sawa?
cameroun anakuja kuònana na cuf au anakuja kuwaona mashoga zao chadema ambao wanapewa misaada na kina camerun tokea chadema ilipoanzishwa napia viongozi wa chadema wakienda kuchukua hiyo misaada kabla ya kupewa huchezewa sana masaburi kwa sababu wandoa nakina cameroun tokea cdm ilipoanzishwa, upo hapoo???
 
We zawadi una jinsia gani, nataka nijue. kama mwanume basi nikununulie KY maana Cameroon anakuja kuonana na wadau wa CUF na kama mwanamke nikuombee ubunge wa kiti maalum kwa magamba, ila uwe tayari kushi Pemba au Tanga, sawa?

cameroon na CUF wapi na wapi msiibambikie uchafu huo CUF,uchafu huo ni wa Chadema na mabwana zao consevertive. Cameroon bwanabasha,na mbowe bibie wake. Kila mtu analielewa hilo.
 
Idadi ya kura ambazo CUF wamepata Igunga pamoja na mtaji wa kura za mwaka 2010 waliokuwa nao sioni sababu ya kubisha kuwa chama hiki kinaelekea kufa Tanzania bara, labda kitakua zaidi huko Zanzibar. CUF wamepoteza mvuto kwa wapiga kura walio makini na hasa unapoangalia jinsi wanavyoshabikia kila linatotendwa na CCM. Katika nchi zilizoendelea upinzani ulio na nguvu unaikosoa serikali na kuifanya iwajibike kwa wananchi wake.Katika hali ya kawaida haiwezekani watu wenye itikadi na mitizamo tofauti kila siku mkakubaliana, ukiona hivyo hapo kuna tatizo lazima mmoja anaburuzwa kukidhi matakwa ya mwingine au itikadi zenu zinafanana
 
Back
Top Bottom