CUF na Operesheni "Zinduka"

Kweli inasikitisha. sasa hivi Wapemba wanayimwa kujiandikisha kupiga kura ili CCM wayachukue majimbo yao 2010 viongozi wao wako huku Bara wanatumikia agenda za RA dhidi ya maadui zake.

Profesa, tulikuamini sana, achana na hao akina Jussa na Maalim, pigania haki ya wazalendo hapa wanaoibiwa fedha zao kila siku na majambazi ya CCM. Achana kuikandia Chadema kwa agizo la RA, ungana na Chadema katika kuutokomeza ufisadi ndani ya CCM kwa lengo la kuleta utawala bora. Achana na tamaa ya pesa za wizi, pigania haki ya wazalendo hata bila malipo, kwani siasa za kweli ni kujitolea.

Kama kweli una uchungu wa nchi hii, adui yako inapasa awe CCM, na siyo Chadema. Unapotea sana. Utakimbiwa na wengi.

Yakhe Pemba hakuhitaji hata kampeni wala kiongozi wa CUF kwenda huko ,WaPemba mambo wanayaweza na wala yasikupe shida ,wameshaamka na wanajua nanmna ya kupambana na CCM ,ile viongozi wa CUF kufikia kusema ni wajibu wao tu,(wametimiza wajibu wao kuifahamisha jamii)

Adui sio CCM adui ni wale wote walio na wano ifisidi nchi hii wawemo CUF au Chadema au kwengineko kokote kule ,hao watakuwa maadui ,sasa tusiwe wenye kubabaika katika kuchagua viongozi au Chama kilicho bora kwa kuwa tu baadhi ya viongozi fulani wamekuwa mstari wa mbele katika kulipua mabomu ni lazima ukubali kuwa unaponyoonyeshea wenzio kidole basi kama hukuangalia vizuri vidole vingine tena vinne vitakuwa vinakuelekea mwenyeo , na kama haitoshi mara nyingi wanaolipua mabomu hutokezea mambo yakaenda kombo mabomu yakamlipukia mikononi.

Hivyo tusiwe katika msimamo usiotetereka ,inavyokuwa tunaisimamia haki na kuuchukia ufisadi basi hatuna budi kumuumbua yeyote yule ,ikiwa ni Lipumba au Seif au mwengine yeyote, tusione soo kusema au kukubali kuwa viongozi wa Chadema kumbe nao wamo katika kapu la ufisadi ,tusiwe na gatigati ,ugumu wa kuwaumbua kwa kuwa tu ,tunao au tupo pamoja nao ,hawa kama ni wahusika wa ufisadi kwa kweli watakuwa hawafai na hawatufai ,let us be sensible katika kupambana na wafujaji wa uchumi wa Taifa na Nchi hii ya Tanzania ,haiwezekani ikawa tunapigana na CCM peke yake wakati upnde wetu wapo wanaop fanana nao ,huko kutakuwa ni kutaka kwanza kuwadanganya wananchi na pili kuwaonea choyo CCM ni kwamba tunataka kuwaondoa CCM kwenye ulaji ili tukamate sisi ,CHADEMA imetuhumiwa kuwa hakuna viongozi wenye sifa zinazofaa kuongoza hilo sio jambo dogo ,kwa maana ingine ile kulipua yote ilikuwa ni kutembea na ngozi ya kondoo.

Lazima tuwajibike kwa hili kama hawa waliotuhumiwa na CUF ni wahusika wa ufisadi fulani fulani basi isiwe mbinde kuwachanganya na wale wa CCM na kama Lipumba nae anahusika nae mtajeni ila hadi leo sijaona ni wapi Lipumba amehusika au kuwa upande mmoja na akina Rostam huko itakuwa ni kumzulia au kutaka kumhusisha na mkumbuke tu siku zote ukweli unakuja juu ,sasa mnaweza mkaumbuka ,sijawasikia viongozi wa CHADEMA kulisema hilo kuwa Lipumba anahusika na kuwasaidia akina Rostam ,jamani na wao waseme tusikie kuwa viongozi wa CUF nao ni mafisadi hivi kama kuna ukweli itakuwa shida ,ila naona sasa kama mmebabaika baada ya kuumbuliwa kwa viongozi wa CHADEMA ,msiwe hivyo kubalini ukweli na msiseme Lipumba ameharibu upinzani ,bado hajaharibu kitu.

Naona kama CHADEMA nao wameshikwa pabaya.
 
TATIZO HATA PICHA ZA UFUNGUZI WA ZINDUKA MNASHINDWA KUTULETEA ,poleni sana.
 
TATIZO HATA PICHA ZA UFUNGUZI WA ZINDUKA MNASHINDWA KUTULETEA ,poleni sana.
Mwiba,
Pamoja na kuwa umequote uchaguzi wa marekani, huoni kuwa Mcain aliingiza uongo mwingi kuwa Obama sijui terrorist friend, sijui sio Mmarekani, Mwarabu, muislamu; hadi mambo yakamgeukia mwenyewe? If you have smear politics tactics you must be a clean man yourself. Then what you speak must be proved true. Hivi hawa FBI wa Tanzania sasa hivi wana kazi ya kufanya na kuimalizia kuhusu ile kuungua kwa BOT. Lipumba knows who burnt it. "Mr. Makani and Mtei because they stole money so they wanted to spoil evidence".

Serious allegations and a dirty game which can finish Mr. Lipumba. This guy got no datas, when the bank was burnt and when Mtei was a governor.

Also I was thinking in politics you may have "face"; CHADEMA and CUF were PARTNERS inn previous election; why all this eneminity; and coming from the Professor? I thought Professors are wiser! He has to know Professor Obama got the country (USA) by avoiding smear politics!
 
Kivipi mbona unataka kukwepa hoja nakuingiza udini?? labda wewe ndiyo umeanza udini??
Lipumba anaongelea mafisadi wote either wako chadema, wako CCM it doesn't matter?? ,Masikio yangu yako huru nasubiria kusikia chadema wakijibu hizo tuhuma kwa faida ya nchi!!

Mhh Chadema chama cha wasomi.
Hawezi kujibu pumba watu wasije kuona tofauti haipo!
 
Lipumba kesha katiwa , anaonyesha yale madai ya watanzania kwamba CUF kuna udini mie naongezea anasimama kumtetea Rostam kwa mshiko na kwa kuwa wote wanatoka Tabora .Mtu mwenye heshima na akili timamu hata ndani ya CCM they will never stand for Rostam trust me and at least not in the open like this .Lipumba kweli pumba .Kesha jua CIF imekufa visiwani sasa anaisaidia CCM bara .

Jamani mbona siamini kama Lipumba anaweza sema haya? labda nisikie audio kwa masikio yangu, yaani kaisha fisadiwa kiasi hiki?

Lakini hii ni habari njema kwakweli, make wengi tulikuwa tukilalamika kwamba Chadema ni wabinafsi kwanini wasiungane na wengine, sasa kumbe wa kuungana nao ndo hawa? wanao simama hadharani kutetea mafisadi mchana kweupe?
 
Lipumba ameshaona kashindwa kuendeleza CUF sasa anaona iliyobaki ni kuharibia wengine.Bora tu ajiunge na CCM ili akaseme vizuri kama kina Tambwe Hiza.Ni profesa lakini ana fikra kama za mtu wa shule ya msingi.
 
Mbunge Slaa aibua ufisadi katika mradi uliozinduliwa na Rais Kikwete
slaa.jpg

Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa (Chadema).
Ataka TAKUKURU nyingine iundwe kuchunguza iliyopo

Habel Chidawali,Dodoma

MBUNGE wa Karatu, Dk Willibrod Slaa (Chadema), ambaye ni maarufu kwa kuanika uovu, jana aliulipua mradi mkubwa wa kusambaza maji kwa wananchi wanaoishi kwenye miji ya Shinyanga na Kahama uliogharimu takriban Sh252 bilioni za walipakodi, akidai kuwa una harufu ya ufisadi.

Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana akiwa mchangiaji wa tatu katika hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa mwaka wa fedha 2009/10.

Alidai kigogo mmoja wa Mamlaka ya Maji safi na Majitaka wa Shinyanga kuwa alifanya ufisadi mkubwa, akishinikiza wenzake wakubali kupitisha fedha ambazo haziko katika utaratibu mzuri huku akionekana kuwekewa ulinzi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Dk Slaa alisema katika mradi, ambao unatoka ndani ya mradi mkubwa wa Ziwa Victoria, ameingia mdudu anayeonekana wazi, lakini wahusika hawaonyeshi kasi katika namna ya kumshughulikia.

"Ni lazima iundwe Takukuru nyingine kwa ajili ya kuichunguza Takukuru iliyopo hivi sasa, kwani inaonekana kuwa imeshindwa kabisa kutekeleza majukumu yake na inaingilia kazi ambazo zinaonekana wazi kuwa ni sehemu ya rushwa," alisema.

Aliitaka serikali iunde taasisi nyingine ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kwa ajili ya kuichunguza Takukuru iliyoko hivi sasa.

Alisema sababu za kutaka kuundwa kwa taasisi hiyo mpya ni kutokana na kile alichokieleza kuwa, Takukuru imeshindwa kabisa kutekeleza majukumu yake.

Akiongea kwa hisia kali, siku moja baada ya Spika Samuel Sitta kuruhusu watu kuonyesha hisia zao, mbunge huyo ambaye ni katibu mkuu wa Chadema, alizungumza huku akionyesha baadhi ya vielelezo vyake.

Alisema: "Tarehe 13 Machi mwaka huu, kigogo huyo alikwenda katika Hoteli ya Karena na kuongea na mkurugenzi wa Trans Ocean Supply Ltd na kukubaliana mambo ambayo ni wazi yanaonyesha kuwa kuna mianya ya kifisadi.

"Kama haitoshi siku iliyofuata alikwenda tena mkurugenzi huyo na kumchukua mgeni wake bila ya kujua walikuwa wanazungumza kitu gani, lakini kwa kutumia gari la serikali aina ya (Toyota)Prado namba STJ 6463 alimbeba na kumpeleka kwenye Uwanja wa Ndege wa Shinyanga."

Dk Slaa alifafanua kuwa siku chache baada ya kuondoka kwa mkurugenzi wa Trans Ocean Supply Ltd, Gulam aliwaita wenzake na kuwaeleza kuwa alikuwa na maagizo kutoka kwa wakubwa ili aweze kununua vifaa vya kufunga mitambo ya maji katika miji ya Shinyanga na Kahama.

Kwa mujibu wa Dk Slaa, mkurugenzi huyo alikataliwa na mkurugenzi wa fedha wa Shinyanga kwamba asingeweza kutoa fedha zozote kwa ajili ya manunuzi ambayo yalikuwa nje ya utaratibu, lakini alilazimishwa na kutishwa ili akubali kuidhinisha kiasi cha Sh 2.1 bilioni ambazo tayari zilikuwa zikidaiwa.

Mbunge huyo alifafanua zaidi kuwa, baadhi ya viongozi waliendelea kumtishia mkurugenzi wa fedha na hata kiasi cha kumwandikia barua ya kumsimamisha kazi huku Takukuru ikiingilia kati kwa kuwasaidia baadhi ya watu ili wambane mkurugenzi huyo wa fedha ambaye aliendelea kuweka msimamo na kugoma.

Aliongeza kuwa, mkurugenzi wa maji aliamua kutembeza karatasi kwa ajili ya kuwasainisha wajumbe wa bodi kwenye nyumba zao ili waidhinishe fedha hizo bila ya kufuata maoni ya mkurugenzi wa fedha.

Alisema wakati huo tayari mita 4,000 za maji zilishafika katika eneo hilo bila ya kujua tenda hiyo ilikuwa imepitishwa na nani na kwa muda gani.

Maelezo ya Dk Slaa yalisema kuwa, kutokana na msimamo wa mkurugenzi huyo, alipelekewa fedha katika bahasha na alipokana, aliitiwa watu wa Takukuru ambao walimchunguza na bila kupata kitu chochote, lakini waliendelea kumfuatilia bila ya kujua sababu zipi ziliwafanya wamfuatilie.

Pamoja na kuihusisha Takukuru katika masuala ya rushwa, Dk Slaa aliijia juu Wizara ya Maji na Umwagiliaji ambayo alisema imeonyesha udhaifu katika mradi huo baada ya kutumia fedha nyingi huku ikitambua kuwa bado kuna matatizo makubwa katika eneo hilo.

Alisema kuwa, taasisi hiyo haikutenda haki katika jambo hili kutokana na kuhusika moja kwa moja katika masuala mazima ya kushughulikia jambo hilo kwa kuwa iliwaacha wahusika kamili na kumfuata mtu mwingine tena kwa vitisho.

Alisema tayari ameshamfikishia Waziri wa Maji na Umwagiliaji taarifa zote na orodha ndefu ya majina ili aweze kushughulikia, vinginevyo hakuna haki inayotendeka kwa watumishi wenye misimamo ya kweli ndani ya wizara hiyo.

Kwa upande wa Maji, Dk Slaa aliibebesha lawama kwa kusema ilitumia kiasi cha Sh 700 milioni katika mradi huo huku itambua kuwa kuna tatizo kubwa katika mgogoro wa uendeshaji shughuli zake na kwamba, fedha hizo hazikutumika ipasavyo.

Dk Slaa alisema Sh700 milioni zingeweza kutosha kugharamia mradi mzima wa kusambaza maji katika miji ya Shinyanga na Kahama na kwamba kuidhinisha Sh2 bilioni ni sehemu ya ufisadi mkubwa usio na huruma kwa wananchi wa Tanzania. Katika hotuba ya makadirio ya matumizi, wizara hiyo iliomba Bunge lipitishe jumla ya Sh 264,933,617,000 ili ziweze kutumiwa katika miradi mbalimbali.


http://www.mwananchi.co.tz
 
Last edited by a moderator:
nadhani kichwa cha hii topic hakiendani na maneno aliyoyasema Lipumba at el huko mwanza, hiyo siri nzito wanayoitoa wana CUF ni hipi?
pili hata jina la kampeni yao haiendani na wanachofanya mimi nadhani wako bize kutafuta blanketi ili walale usingizi mzito na wala sio kuzinduka

kuna post yangu moja nilishaituma kuhusu huyu bwana Lipumba na CUF kwa ujumla ni kuwa ukweli kamili tutaupata kutoka kwa Bwana Lwakatare na Prof Safari, walichofanyiwa hawa Mabwana ni kitu kikubwa na sababu ni kupinga hizi sera za kufadhiliwa na watu wasio na nia njema kwa Tanzania,
Ndoto kubwa ya maalimu ni kuwa wao sio raia wa Tanzania na labda Africa, wanataka kurudi kwao, sasa maskini Lipumba hajuhi kuwa anacheza na timu ya wageni, Shariff, RA, Manji,Bakhresa hawa wote sio watanzania na wako hapa kwa malengo yao maalumu, sasa huyu Mmatumbi mwenzetu na elimu yake anashindwa kujua anapelekwa wapi, kweli elimu sio Madegree tu ni laazima ikusaide kukukwamua kwenye utumwa wa kiakili,
 
LUNYUNGU.
Maneno ya Mkandara unayakumbuka?kuwa wapinzani wasigombee ukoko.


Mkuu hizo line zinaweza kuwa zilinipita nirushie hapa ama sirini nipitie tena mkuu .Unajua nilikuwa sio jamvini muda sana .
 
Profesa amechemsha sana, nadhani ndiyo politics jinsi zilivyo, ukiishiwa hoja unakuja na siasa za maji taka ambazo kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa.

Mzee Edwin Mtei amekuwa Gavana wa BoT kutoka 1966 mpaka 1974. BoT iliungua zama za Nyirabu ambaye amekuwa Gavana kuanzia 1974 mpaka 1989. Sasa kusema kwamba Mtei alihusika na ufisadi na baadaye akachoma benki, hizo ni siasa za kuchafuana na mtu anaweza kushitaki kwa kuchafuliwa jina.

Bob Makani hajawahi kuwa Gavana wa BoT, aliondoka BoT akiwa Naibu Gavana, sina details za tenure yake. Pamoja na hayo claiming that Bob Makani alihusika na ufisadi na hatimaye kuchoma BoT nayo inaweza kuwa na utata kwa kuwa mwenye final say katika transactions zote ni Gavana. Halafu kwa mfumo wa BOT kwa miaka ile kabla ya hii sheria mpya ya mwaka 2007, Naibu Gavana alikuwa anashughulika na mambo ya administration zaidi, mambo yanayogusa uchumi pamoja na hizo transactions zenye ufisadi yako chini ya Gavana. Kwa sheria ya BoT ya mwaka 2007, kuna manaibu 3 (wa Admin, wa Uchumi na Sera, na wa kusimamia taasisi za fedha pamoja na ukuaji wa sekta ya fedha). Labda Profesa Lipumba aje aseme huo ufisadi wa Bob Makani ulikuwa wa namna gani, lakini kuja na blanket statement kwamba Bob Makani alifanya ufisadi na wakachoma BoT nauona kwamba ni uzushi mtupu?

Hao wengine aliowataja kwamba ni mafisadi mbona hajataja ufisadi wao ukoje ama waliufanya wapi?

Hizi ni dalili za mfamaji, anaweza kushika hata jani akitegemea kwamba labda linaweza kumuokoa na akajikuta amezama huku kashikilia jani.

Mafisadi nyangumi amemlenga Mengi, lakini hao wengine ambao ni wahindi na ambao kuna ushahidi wa ufisadi wao mbona hawataji? Kwa kifupi ni kwamba Lipumba anakubaliana na jinsi wahindi wanavyotuibia hela kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani, which means na yeye akiingia madarakani ataendeleza huo ushirikiano uliokuwepo kati ya wahindi na serikali na tutakuwa tumebadilisha kanzu tu lakini Sheikh ni yule yule na mawaidha yake yatakuwa ni yale yale tuliyoyazowea.

Wenye kutaka tenure za magavana waende kwenye link hii hapa: Bank of Tanzania: About the Bank - Former Bank of Tanzania Governors and Deputy Governors
Edwin Mtei hakuacha kazi 1974 ni mbele ya mwaka huo cheki details zako.
 
Yaani jamaa u-Profesa wake anaudhalilisha si kidogo. Maana hii ni wazi kabisa kuwa katumwa na RA kubomoa upinzani. Na hajui kuwa watu sasa wamechoka ni hizi porojo tu za kurushiana maneno bali wanataka mikakati hasa ya kulinusuru taifa kutoka kwenye lindi la umaskini ikiwemo kudhibiti wizi wa rasilimali za taifa na si hizo porojo za maneno. Arudi akajipange upya maana bara hakuendeshwi kwa jazba za chuki dhiki ya mtu fulani tu.

Maproffesa wengi wa Tanzania wengi wao walisoma sana kwa kukalili na kupasi mitihani yao na kupata A+ lakini kwenye practical ni F+. Enzi zile za ujamaa Mtu kama Proffesa alieshimika sana kwamba anajua mambo kumbe ni kwa sababu hapakuwa na utandawazi wa kuwagundua ubovu wao, leo hii mtu akisema kitu kama ni pumba unajua tu huyu mtu kachemsha, ni kama huyu anayejiita Prof Lipumba. Huyu jamaa atakufa kabla ya umri wake, maana alijua akiwa prof maisha yakuwa mazuri, kumbe yamekuwa kinyume chake, angalia sasa anavyopewa visenti kidogo tu na kuanza kupayuka utafiri mtu ambaye hata darasa la kwanza hakupita. Rostamu alisema Mengi ni Nyangumi, leo prof kasema tena Mengi ni nyangumi, jee hii imekaaje!!. Prof katetea turbine za Dowan/Rostamu zinunuliwe huku akijua wazi ni hiyo fraud. Jee watu kama hawa kweli hata akikufundisha utabaki kukalilishwa vitabu vya mwaka 47, mwisho wa yote kwenye practical life unakuwa kama ujaenda shule.

Ndo maana wasomi wengi Tanzania akisoma mpaka apate ajira, maana wanafundishwa kuajiiwa wakati huo, India, US, UK, JAPAN etc wanafundishwa kujiajili. Utakuta mtu na masters Degree au degree mojae anaajiliwa na mhindi wa darasa la saba hapo Dar. hiyo yote ni kwa sababu ya kufundishwa na hawa Maprof uchwara.
 
Maproffesa wengi wa Tanzania wengi wao walisoma sana kwa kukalili na kupasi mitihani yao na kupata A+ lakini kwenye practical ni F+. Enzi zile za ujamaa Mtu kama Proffesa alieshimika sana kwamba anajua mambo kumbe ni kwa sababu hapakuwa na utandawazi wa kuwagundua ubovu wao, leo hii mtu akisema kitu kama ni pumba unajua tu huyu mtu kachemsha, ni kama huyu anayejiita Prof Lipumba. Huyu jamaa atakufa kabla ya umri wake, maana alijua akiwa prof maisha yakuwa mazuri, kumbe yamekuwa kinyume chake, angalia sasa anavyopewa visenti kidogo tu na kuanza kupayuka utafiri mtu ambaye hata darasa la kwanza hakupita. Rostamu alisema Mengi ni Nyangumi, leo prof kasema tena Mengi ni nyangumi, jee hii imekaaje!!. Prof katetea turbine za Dowan/Rostamu zinunuliwe huku akijua wazi ni hiyo fraud. Jee watu kama hawa kweli hata akikufundisha utabaki kukalilishwa vitabu vya mwaka 47, mwisho wa yote kwenye practical life unakuwa kama ujaenda shule.

Ndo maana wasomi wengi Tanzania akisoma mpaka apate ajira, maana wanafundishwa kuajiiwa wakati huo, India, US, UK, JAPAN etc wanafundishwa kujiajili. Utakuta mtu na masters Degree au degree mojae anaajiliwa na mhindi wa darasa la saba hapo Dar. hiyo yote ni kwa sababu ya kufundishwa na hawa Maprof uchwara.

Mkuu huu ndo mshangao wangu, hivi kweli lipumba anaweza pumbazwa kiasi hiki? hivi RA anawapa pesa tu ama obiism? sijapata picha kwakeli!
 
Ama kweli ufisadi mbaya ,yaani CHADEMA wameingizwa ndani ya kapu ,Makada wa CHADEMA hapa JF wamepata kazi ya kujipapatua ila hakionekani wanachokipapatua ni kipi ,sasa baada ya kukanusha wanamsakama Lipumba ,jamani ujumbe ndio huo umefikishwa ,yaani mlizani atasimama pa Kikwete tu kumbe mambo ni mbele kwa mbele.

Yaani mafisadi tunao humu humu ,jamani sasa wajitokeze hapa kupinga hizo shutuma ,akina ZItto,Slaa naona wamezidiwa ,wanashindwa kufahamu kuwa siasa si lelemama.

Sasa wamelipuliwa kabisa ,yaani Majeshi ya CHADEMA yote yamemvaa LIpumba ,yanajaribu kutafuta pa kushika ,hamna, wanabaki kuzunguka papo kwa papo.

Huyu sie ,huyu si profesa ,wakati wa zamani hakuna mitandao ,yaani CHADEMA na wafuasi wao wamechanganyikiwa kweli,hawajui cha kufanya au sivyo ?

Yaani CUF wamelipua lile bomu lenyewe labisa la nyukliya ,sio mchezo ,wachadema wanatafutana.

Mnajua hapa mnakuwa hamna pa kushika ,ukiangalia utaona ni wenywewe kwa wenyewe mnapeana maliwazo na kujalibu kupeana moyo ,lakini ndio hivyo jamaa wamemwaga mboga kabisa ,aisee ,sasa sijui Lwakatale kule watamfanya nini ,kuna tetesi kuwa yeye ndie alikuwa na manyuklia haya na alikwisha kuyatoa kitambo ila alisahau ,sijui watamfanyeje,ila bora wakae kimya maana wakimgusa nae atawalipukia.

Ila kama hapa mpo kama WaTz ambao mmeamua kufanya kweli na mambo ndio yanawekwa hazarani ili kujua lipi bichi na lipi limeiva ,msidumae na kujaribu kuwakosha waliopopolewa ni kuwakimbia kama wenye marazi ya ukoma ,maana wao ni hatari kuliko hao CCM ,ei ndio maana yake ,haina haja ya kutafuta maana ingine ,hao kumbe nao ni mafisadi undercover through CHADEMA ,hiphop leaders ,inafaa wajiuzulu mara moja ili kuisafisha CHADEMA ,hii ni kashfa nzito kwa CHADEMA. Yaani mapigano yao katika medani ya kisiasa ni bure kabisa ,ikiwa tu hizo kashfa walizonadiwa nazo zimewaganda ,hakuna sababu ya wao kubakia kama viongozi wa CHADEMA ,they have to resign .

WAJIUZULU mara moja ,Je utamaduni huo upo TZ ?
 
Edwin Mtei hakuacha kazi 1974 ni mbele ya mwaka huo cheki details zako.

Niliweka link ya website ya BOT ambayo ina hiyo miaka, unless wewe uniambie kwamba una information tofauti na hizo ambazo ziko kwenye website ya BOT.
 
duh! waandishi wetu bwana!....habari nzima hakuna direct quote hata moja!
bora angesema kwa nilivyo mfahamu mimi lipumba alikuwa anaongelea hili"..............."
lakini kama hatupi maneno yake moja kwa moja, inakuwa tabu kuamini kasema kwa kutaja maneno hayo ya "nyangumi" moja kwa moja
 
"Nyangumi", "CCM B", zote ni kauli ambzo tume sha sikia sana. Nothing new. Seems like he is trying to recycle things so he can look relevant.
 
Sasa hivi Lipumba kachoka sana na azungumza pumba. Unapoona kiongozi wa siasa hana sera za kuuza kwa wananchi bali kushambulia wanasiasa wenzake huyo kafilisika. Sasa hivi anatumiwa na maadui wa maendeleo ya watanzania ili kuturudisha nyuma. Huyu ni kiongozi aliyefilisika kisiasa na kibaraka.

Ushauri mzuri ni kumdharau ili aibu yake ianguke kwenye kichwa chake mwenyewe
 
Maproffesa wengi wa Tanzania wengi wao walisoma sana kwa kukalili na kupasi mitihani yao na kupata A+ lakini kwenye practical ni F+. Enzi zile za ujamaa Mtu kama Proffesa alieshimika sana kwamba anajua mambo kumbe ni kwa sababu hapakuwa na utandawazi wa kuwagundua ubovu wao, leo hii mtu akisema kitu kama ni pumba unajua tu huyu mtu kachemsha, ni kama huyu anayejiita Prof Lipumba. Huyu jamaa atakufa kabla ya umri wake, maana alijua akiwa prof maisha yakuwa mazuri, kumbe yamekuwa kinyume chake, angalia sasa anavyopewa visenti kidogo tu na kuanza kupayuka utafiri mtu ambaye hata darasa la kwanza hakupita. Rostamu alisema Mengi ni Nyangumi, leo prof kasema tena Mengi ni nyangumi, jee hii imekaaje!!. Prof katetea turbine za Dowan/Rostamu zinunuliwe huku akijua wazi ni hiyo fraud. Jee watu kama hawa kweli hata akikufundisha utabaki kukalilishwa vitabu vya mwaka 47, mwisho wa yote kwenye practical life unakuwa kama ujaenda shule.

Ndo maana wasomi wengi Tanzania akisoma mpaka apate ajira, maana wanafundishwa kuajiiwa wakati huo, India, US, UK, JAPAN etc wanafundishwa kujiajili. Utakuta mtu na masters Degree au degree mojae anaajiliwa na mhindi wa darasa la saba hapo Dar. hiyo yote ni kwa sababu ya kufundishwa na hawa Maprof uchwara.

Mrugaruga umezungumza mavituz. Umenikumbusha mwaka juzi nilikwenda hospitali kutibiwa na Profesa mmoja ambaye alikua anatumia reference book (British National Formulary) ya edition ya mwaka 1982, tena alikua kaijaladia (kaweka jalada) maana ilikua too old. Hicho kitabu kinakuwa updated every 6 - 9 months... sasa jiulize hapo jinsi daktari profesa anavyolisha watu sumu..

Ukweli ni kwamba Profesa Liipumba hajazungumza lolote la maana. Ni pumba 100%
 
Back
Top Bottom