CUF maji ya shingo kesi ya kukaidi Amri Halali ya Mahakama

hasan124

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
716
128
Yaliyojiri Mahakama KUU Kanda ya Dar ES Salaam leo tar. 15-10-2012, Kesi ya Mhe. Hamad Rashid Mohamed (MB) jimbo la Wawi CUF na wenzake dhidi ya chama cha Wananchi CUF.
Katika ishara inayoonyesha kwamba hali ni tete Upande wa washitakiwa ie; CUF , Jaji Agustino Shangwa akiendesha kesi hii akasema yafuatayo:
1. Alimuagiza karani wa Mahakama akatafute Majaji wawili ashauriane NAo Kabla hajatoa hukumu.
2. Kwa kuwa kesi husika charges zake zinahitaji watuhumiwa WAFUNGWE JELA na SI vinginevyo, anaisogeza mbele ili apate kushauriana na Majaji wenzake Kabla ya hukumu.
3. Akashauri, kwa nini haya makundi mawili wasikae kutafuta suluhu na kuyamaliza nje ya Mahakama mpaka wanafikia kuhukumiana.
4. Mwisho, Jaji Shangwa akasema, Kwa kuwa Nchi ina joto/vuguvugu la kisiasa liko juu ameonelea aisogeze mbele hadi tar. 05-12-2012 ndio atatoa HUKUMU.


Katika hali inayoonyesha kuweweseka wakili wa CUF Job Kirario alionekana akizungumza na Kiongozi Mmoja Muandamizi wa chama kipya cha kisiasa cha ADC (mmoja kati ya viongozi waliojiengua CUF wakati timuatimua imeshika kasi) akiomba suluhu na suala husika lirudi chamani (CUF), wayamalize nje ya Mahakama.
Kwa ufupi mazingira Mahakamani pale kwa yeyote aliye timamu atakuwa ameona dhahiri ni jinsi gani hali ilivyo tete kwa chama hiki kikongwe cha Upinzani NCHINI Tanzania.
Kesi hii inaweza kuwa ni Fundisho kubwa katika suala zima la utii wa sheria bila shuruti na hakuna aliye juu ya Mahakama awe Rais, MAKAMU WA RAIS, Mbunge, Mfanyabiashara au Hata Mlalahoi huku Uswahilini kwetu.
 
Ina maana cuf hawana katiba ya chama? Viongozi wote waliotimuliwa si walitimuliwa kwa mujibu wa katiba yao ndani ya cuf? Na kama cuf walifuata taratibu zote za katiba kwanini mahakama itoe hukumu wakati cuf imeshaamua kulingana na katiba?
 
Ina maana cuf hawana katiba ya chama? Viongozi wote waliotimuliwa si walitimuliwa kwa mujibu wa katiba yao ndani ya cuf? Na kama cuf walifuata taratibu zote za katiba kwanini mahakama itoe hukumu wakati cuf imeshaamua kulingana na katiba?

Walitoa hukumu wakati kulikuwa na zuio la mahakama.Kwa kifupi walikaidi amri ya mahakama.
 
Ina maana cuf hawana katiba ya chama? Viongozi wote waliotimuliwa si walitimuliwa kwa mujibu wa katiba yao ndani ya cuf? Na kama cuf walifuata taratibu zote za katiba kwanini mahakama itoe hukumu wakati cuf imeshaamua kulingana na katiba?

Mahakama bado haijahukumu, ila kesi iliyo mahakamani ya kutaka viongozi CUF WAFUNGWE JELA ilifunguliwa na MHE. Hamad Rashid na washirika wake baada ya CUF kukiuka Amri ya Mahakama ambapo Baraza KUU CUF Taifa waliendelea na Kikao cha, na Kuwafukuza MHE. Hamad Rashid na wenzake ilhali Amri husika ilishawasilishwa katika ofisi za CUF Taifa.
Bwn. Apolinary, Unadhani Katiba ya Chama na Sheria za Nchi ni kipi kina Nguvu zaidi hapo? Fikiria chukua hatua.
 
Ahaa kumbe ndiyo maana Maalim Seif na Jussa hawataki muungano ha ha ha ha Segerea inanukia.
 
Ina maana cuf hawana katiba ya chama? Viongozi wote waliotimuliwa si walitimuliwa kwa mujibu wa katiba yao ndani ya cuf? Na kama cuf walifuata taratibu zote za katiba kwanini mahakama itoe hukumu wakati cuf imeshaamua kulingana na katiba?

mkuu mahakama ilizuia kikao ambacho kilikaa kumjadili mh.HAMAD kutokana na pingamizi ambalo aliliwasilisha katika mahakama hiyo,taarifa ilipelekwa chamani kabla siku ya kikao na hata siku ya kikao walionyeshwa hati ya mahakama kuzuia mkutano huo ila walipuuzia na wakaendelea na mkutano na kufikia maamuzi yao.HILO NDILO KOSA LENYEWE
 
Ina maana cuf hawana katiba ya chama? Viongozi wote waliotimuliwa si walitimuliwa kwa mujibu wa katiba yao ndani ya cuf? Na kama cuf walifuata taratibu zote za katiba kwanini mahakama itoe hukumu wakati cuf imeshaamua kulingana na katiba?

Hujaelewa maana yakudharau mahakama.
 
Kesi hii inaweza kuwa ni Fundisho kubwa katika suala zima la utii wa sheria bila shuruti na hakuna aliye juu ya Mahakama awe Rais, MAKAMU WA RAIS, Mbunge, Mfanyabiashara au Hata Mlalahoi huku Uswahilini kwetu.

Mbona hapo kwenye makamu wa Rais umeamua kutilia msisitizo kwa kuandika herufi kubwa???

By the way, Maalim seif na Mtatiro wanasubiriwa Segerea Desemba 5. Tunaandaa mapokezi na muda huu ni muafaka kusafisha marereza ili waingia kukiwa safi
 
mkuu mahakama ilizuia kikao ambacho kilikaa kumjadili mh.HAMAD kutokana na pingamizi ambalo aliliwasilisha katika mahakama hiyo,taarifa ilipelekwa chamani kabla siku ya kikao na hata siku ya kikao walionyeshwa hati ya mahakama kuzuia mkutano huo ila walipuuzia na wakaendelea na mkutano na kufikia maamuzi yao.HILO NDILO KOSA LENYEWE

Naomba ufafanuzi wadau, ikiwa mahakama itajiridhisha pasi na shaka kuwa washitakiwa wana hatia ni nani yupo responsible kwenda jela?
 
kafu na makafu yao hawaeleweki kwenye hii kesi haki sawa kwa wote waende segerea hata V4C Wamekopi toka ADC Mikakati wamekopi M4C washitakiwe kwenye mahakama za umma kama vile jamii forums magazeti kwa hoja waache uvivu
 
Vijana wa CDM wanachekesha kweli pale wanapo jipa moyo kwa kujifurahisha endeleeni kubaki mithili ya fisi kudhani mkono utadondoka yagujuuuu
 
Vijana wa CDM wanachekesha kweli pale wanapo jipa moyo kwa kujifurahisha endeleeni kubaki mithili ya fisi kudhani mkono utadondoka yagujuuuu

Mke anagombana na wanafamilia wenzake cha kushangaza Mme amekaa kimya, tunamshauri aingilie kati kuamua ugomvi huu wa mke wake.
 
Back
Top Bottom