CUF kupeleka katiba kwa maandamano

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,269
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Lipumba amesema chama chake kitawasilisha kwa Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, nakala ya rasimu sifuri ya mapendekezo ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Desemba 28 mwaka huu kwa maandamano ya amani yatakayoanzia Buguruni.
 
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Lipumba amesema chama chake kitawasilisha kwa Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, nakala ya rasimu sifuri ya mapendekezo ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Desemba 28 mwaka huu kwa maandamano ya amani yatakayoanzia Buguruni.
kitendo hiki ni cha kiungwana na kinachopaswa kuungwa mkono na mwanaharakati yeyote_mwanaharakati ni yule siku zote anatamani kuona mabadiliko bila kujali wala kutaka kujua yamesababishwa na nani_post hii imekaa muda mrefu bila kuchangiwa, wana jf vp?
 
kitendo hiki ni cha kiungwana na kinachopaswa kuungwa mkono na mwanaharakati yeyote_mwanaharakati ni yule siku zote anatamani kuona mabadiliko bila kujali wala kutaka kujua yamesababishwa na nani_post hii imekaa muda mrefu bila kuchangiwa, wana jf vp?
Labda wachagiaji wangekuwa wengi kama wangeona ni CDM wanajua wanaopeleka ni CCM-B inawezekana wametumwa kufanya hivyo ndiyo maana hata kibali cha kuandamana wameshapewa.
 
Hawa Ndondocha nao kwanini wasiungane na waislamu wenzao kuandaa katiba yao feki! CCM B at work
 
Hongereni Cuf piganieni kila mlichokua mnapigania toka mfumo wa vyama vingi umeanzishwa,nakumbuka mliwahi kutoa hata rasimu yakatiba mpya,sasa endelezeni mapambano na watz wote tuko nyumayenu natutashiriki maandamano hayo ya amani,ALUTA CONTINUA mpaka KIELEWEKE, Tunawaamini CUF mkiamua mnaweza kufikia malengo yakupata katiba mpya.
 
Hawa Ndondocha nao kwanini wasiungane na waislamu wenzao kuandaa katiba yao feki! CCM B at work
we kalagabaho kaakimya kama hujui kitu sio unakaa unaropoka pumbazako hapa,tunataka katiba mpya wacha kuleta udiniwako hapa.
 
Prof Lipumba anayo haki kufanya hivyo na CUF kinacho haki pia kuwashilisha maoni juu ya katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vile vile, najua kila mtu anasubiri kwa shauku kubwa jinsi Chama hiki ambacho kiliwahi kuonekana cha kidini zaidi namna gani wanavyoondokana na kicho kivuli kibaya.

Pili, mbali na CCM chama cha wananchi CUF ndicho chama kilicho na wabunge wengi Tanzania Bara na Visiwani. Jambo hili linamfanya kila mtu awe na shauku juu ya namna gani watakavyotoa mapendekezo yao juu ya muundo wa taifa letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwisho, tunasubiri kuona mapendekezo ya vikundi mbali mbali juu ya usimamizi wa rasilmali za taifa na upanuzi wa haki za binadamu nchini mwetu.
 
ukitaka kujua kuwa cdm si wanmapambano just wanataka ujiko angalia hapa

walitaka kuwadanganya wananchi kuwa wao ndio walioanzisha haya mapambano ya katiba mpya sasa hawatopenda kujiunga mkono kwa maana watu watajua kuwa mapambano hayo yalikuwepo muda mrefu na wao hawakuwa sehemu ya mapambano hayo
 
Hawa Ndondocha nao kwanini wasiungane na waislamu wenzao kuandaa katiba yao feki! CCM B at work
<br />
<br />
Umedhihirisha ambalo wengi hawataki kulikiri, shida hapa sio katiba mpya wala uchungu na TZ. Basi subiri, Askofu Malasusa, Kadinali Pengo, na Padri Slaa wanamalizia ya kwao itakayowasilishwa na chama chao CHADEMA
 
Si lazima CDM kupiga kelele barabarani kila siku ndio watu wajue kwamba wanafanya kazi kubwa kiasi gani kuhusu uwepo wa Katiba mpya nchini mwetu.

Mtu wa Pwani, wewe vuta tu subira utaona kazi inayofanyika pale CHADEMA. Pili, ikumbukwe kwamba CUF, TLP, CHADEMA na vyama vinginevyo vyote ni vyama vyetu sisi wenyewe Wa-Tanzania.

Hatuna sababu ya kutazamana kwa jicho la uchoyo kwani lengo letu ni moja kuboresha maisha ya nchi yetu na mteja wetu sote ni mwananchi wa nchi hii. Kwa msingi huu, mafanikio ya CUF au TLP kamwe hainiumi wala kushindwa kuyatolea pongezi penye ustahili huo.

Lakini kwa kufanya hivyo hakuniondoi CHADEMA hata kidogo. Na hata kuvikosoa vyama hivi haimaanishi kuna chuki isipokua FISADI na WAKUMBATIAJI WAO ni maadui wakubwa wa taifa letu.

Ukomavu kisiasa unahitajika.
 
KATIBA mpya ni LAZIMA... lkn CUF wamepoteza mwelekeo kwa walio wengi Tanganyika (ukiacha TA, Lindi na MT). MYTAKE: Isije kuwa wanatekeleza MARIDHIANO!!!
 
Kuna yoyote anayefahamu yaliyoko kwenye rasimu ya mapendekezo yao? Kama yupo atujuze kwanza tuelewe vizuri kuhusu mapenedekezo yao.
 
Kuna yoyote anayefahamu yaliyoko kwenye rasimu ya mapendekezo yao? Kama yupo atujuze kwanza tuelewe vizuri kuhusu mapenedekezo yao.

CCM wao wanapeleka rasimu yao lini???? Au kwao katiba hili kongwe kama chama chao chenyewe ni poa tu???
 
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Lipumba amesema chama chake kitawasilisha kwa Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, nakala ya rasimu sifuri ya mapendekezo ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Desemba 28 mwaka huu kwa maandamano ya amani yatakayoanzia Buguruni.



Hebu tuambie kama umeperuz kwenye hiyo rasimu yao ya Katiba yao kujua ni Mahakama ya Kadhi ipo section ngapi?
 
CUF kupeleka rasimu ya katiba? wanapeleka kwa nani? hii mbona inafanana na CCM kupeleka katiba.....CUF wameungana na CCM na hili limejionyesha hata kwenye chaguzi za mameya na wenyeviti wa Halmashauri. Ina maana katika hili hawapo na CCM? Au wanatuzuga ili kutupoteza dira?
 
Unajua Idd Simba alishawahi kusema watanzania wengi tena wasomi wana mtindio wa ubongo, mimi kwa haraka nilikubaliana naye kwa kuji-evaluate baada ya kutafuta ukweli nikagundua mtindio wa ubongo ni kusema na kuzngumza au kuandika vitu visivyo na tija wala kichwa wala mguu!

wachache sana wanaojua maridhiano ya CUF na CCM zanzibar, wngi hawajui indeep na leo hii CUF imefikia hapo baada ya vitu gani kutokea cuf siyo ccm b wenye mtindio tu ndiyo watasema hivyo

lets debate
 
Si lazima CDM kupiga kelele barabarani kila siku ndio watu wajue kwamba wanafanya kazi kubwa kiasi gani kuhusu uwepo wa Katiba mpya nchini mwetu.

Mtu wa Pwani, wewe vuta tu subira utaona kazi inayofanyika pale CHADEMA. Pili, ikumbukwe kwamba CUF, TLP, CHADEMA na vyama vinginevyo vyote ni vyama vyetu sisi wenyewe Wa-Tanzania.

Hatuna sababu ya kutazamana kwa jicho la uchoyo kwani lengo letu ni moja kuboresha maisha ya nchi yetu na mteja wetu sote ni mwananchi wa nchi hii. Kwa msingi huu, mafanikio ya CUF au TLP kamwe hainiumi wala kushindwa kuyatolea pongezi penye ustahili huo.

Lakini kwa kufanya hivyo hakuniondoi CHADEMA hata kidogo. Na hata kuvikosoa vyama hivi haimaanishi kuna chuki isipokua FISADI na WAKUMBATIAJI WAO ni maadui wakubwa wa taifa letu.

Ukomavu kisiasa unahitajika.

Usichoke kuelimisha
 
Maalim Seif (CUF) anatekeleza ilani ipi? Isijekuwa ni ile ya Kombani!! Tujuzeni yaliomo kwenye Rasimu ndio join hands.
 
CUF siku hizi si sehemu ya chama tawala, kinaweza kuitisha mkutano wa hadhara au kufanya maandamano wakati wowote bila kuingiliwa na polisi. Lakini CHADEMA ikidhubutu inakiona cha mtema kuni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom