Mwenyekiti wa CUF, Prof. Lipumba amesema chama chake kitawasilisha kwa Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, nakala ya rasimu sifuri ya mapendekezo ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Desemba 28 mwaka huu kwa maandamano ya amani yatakayoanzia Buguruni.