muhogomchungu
JF-Expert Member
- Jan 9, 2011
- 375
- 3
Kwa pamoja walifikishwa katika viwanja vya Mahakama Kuu majira ya 8:40 mchana wakiwa chini ya ulinzi mkali, huku Dk Slaa, Mbowe na Ndesamburo wakiwa kwenye gari dogo aina ya Landrover.
Watuhumiwa wengine walifikishwa mahakamani hapo kwa karandinga. Waliokuwa kwenye Karandinga hilo ni Selasini, Lema na washitakiwa wengine.
Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Zakaria Elisante alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Arusha Charles Magesa, kuwa watuhumiwa hao, wametenda kosa moja la kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.
Elisante alisema kwa kufanya kosa hilo, watuhumiwa hao, wamevunja sheria namba 74 na 75 kifungu cha 16 kama ilivyofanyiwa marekebishoa mwaka 2002 na pia sheria ya polisi sura 45 kifungu cha 322 ambayo pia ilifanyiwa marekebisho mwaka 2002.
wengine ni Goodluck Lema, Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, Mbunge wa Moshi Mjini,
Hebu tujikumbushe KWA upande wa Cuf
wakati wa dk salmini
Juma Duni Haji (Waziri wa Afya) na Hamad Masoud Hamad (Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano.)
Makamu Mwenyekiti wa CUF, Machano Khamis Ali, ndugu wawili Abass Zam na Ali, Said Zam Ali, Pembe Ame Manja, Mohammed Ali Maalim, na Hamad Mmanga Khalfan.
wengine ni Ramadhan Shamna Ali, Hamza Makame Omar, Nassor Seif Amour, Sharif Haji Dadi na wanawake wawili akiwemo Zeleikha Ahmed Mohammed na Zena Juma Mohammed
Wengine ni aliyekuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohammed, Abdallah Said Abeid, Soud Yussuf Mgeni (marehemu) na Hassan Said Mbarouk (marehemu) waliofariki dunia mwaka jana.
JUU YA MISUKO SUKO HIYO, BADO CUF ILIKUWA NA NGUVU NA HAIKUTETEREKA. JEE CHADEMA Mbowe, Ndesamburo wakifungwa Chadema kusambaratika?