Ye Soya
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 237
- 248
Naamini watz wengi bado wamepigwa na butwaa baada ya watu wa cuf waliounga mkono kwa 100% mswada wa kuunda kamati ya katiba bungeni hivi karibuni wanaenda ikulu kumuona Rais JK. Leo akiongea na magic fm radio asubuhi Mtatilo ambaye ni makamu katibu mkuu cuf bara alisema wameenda ikulu ili mapendekezo yao yawe kwenye mabadiliko ya mswada huo yatakayofanyika ktk bunge la mwezi wa february mwakani. Je, kwa kuwa walijua jk kesha saini huo mswada, isingetosha wakasubiri hoja zao wakazipeleka bungeni? Kulikuwa na umuhimu gani wa kwenda ikulu? Au ndio tuseme wamefata mkumbo wa Cdm? Je kila chama kiende kumuona jk? Nawasilisha wanaJF!