CUF hawataweza kushindana na M4C ya CHADEMA kwa sababu zifuatazo...

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Jun 4, 2011
7,789
8,914
CUF wanajitahidi kila namna kuwemo kwenye Kundi la KUMBE WAMO ila kwa bahati Mbaya ni vigumu sana Kufikia mafanikio ya CHADEMA kwa sababu zifuatazo

1. Mafanikio ya CHADEMA hayajaanza leo na yamejengwa kwa miaka mingi sana tofauti na CUF wanavyo zania kwamba watajenga Chama chao ndani ya huu muda Mfupi

2. CHADEMA inapendwa na Wananch Naturay na hii ni kutokana na sababu nyingi Kubwa ikiwemo KUPAMBANA NA UFISANI, NA JINSI WABUNGE WA CHADEMA WANAVYO SHUKA NONDO BUNGENI NA NJE YA BUNGE. cuf hawana watu wa aina hiyo

3. CHADEMA ina watu/ Hazina kubwa sana ya kuweza kuwezesha Uhamasishaji tofauti na CUF, na hapa ndo sehemu zaidi ambayo CHADEMA kinajivunia na ndo sehemu ambayo inaimaliza CUF moja kwa moja, Leo hii John HECHE yuko Kagera akiendeleza M4C na yuko peke yake, Kamanda MAWAZO yuko Mwanza, CUF kiongozi wao wa Vijana hawezi kufanya anayo fanya JOHN HECHE, Mtatiro hawezi kufanya mikutano peke yake ni mpaka apewe sapoti ya Prfesa

- Wananchi Leo hii hata wakisikia kuna DIWANA WA CHADEMA KUTOKA MWANZA ATAFANYA MKUTANO Tanga bado hamasa itakuwa kubwa sana na watu watajitokeza CUF hakuna kitu kama hicho

- CHADEMA hata bila kuwatumia Viongozi wa Juu kama Dr Slaa na Mbowe M4C inaweza fanya vizuri kwani watu kama akina LEMA, SUGU, WENJE, ZITO, NYERERE, MNYIKA, MSIGWA, na makamanda wa sasa MILYA, MAWAZO na wengineo wanaweza leta hamasa ya aina yake kwenye Mikutano ya M4C,

- CUF haina watu wa aina hii na inawategemea LIPUMBA PEKEE NA MALIMU KWA UPANDE WA ZANZIBAR

- Viongozi wengi wa CUF hawajulikana Miongoni mwa wananchi, Zaidi ya Profesa pamoja na Malmu Sefu hao wengine hawajulikana na ni vigumu kufanya Mikutano wakiwa peke yao,


4. CUF wananch wengi wanakitazama kama Chama cha huko Zenj na hii iko wazi kabisa kupitia kwa Viongozi wao na hata wakipanda Jukwaani wengi utasikia ni lafudhi ya Zenji so hii nayo ni tatizo kubwa sana kwa CUF

5. Ndoa yao na CCM nao ni tatizo kubwa sana

6. Umarufu wa CHADEMA umeanzia mbali na unachagizwa na factor nyingi sana ikiwemo ya Majina ya watu Maalufu hapa Tanzania kama Vicent Kiboko Nyerere, Letricia Nyerere na sasa hivi watoto wa WASIRA, hii inachangia kwa kiasi kikubwa sana kuipaisha CHADEMA, haya majina yakitajwa ni Promo tosha kwa CHADEMA

7. vyombo vya Usalama hususani Police wanachania sana kufanikisha M4C

MOD HII THREAD HAINA UHUSIANO NA MKUTANO WA LEO SO ISIUNGANISWE TAFADHALI
 
Mkuu ni kweli kabisa hawa HAKI SAWA KWA WAPEMBA wanazania CHADEMA imeanza leo harakati zao, wao kuku bali kuolewa imekula kwao
 
cuf wanatumiwa tu. me nnauhakika hii ni nguvu ya soda tu. sio mda mrefu sana watashindwa kuendeleza kampeni yao. kuiga ni kazi sana. huwezi kufanikiwa kama aliyebuni
 
Ni kweli ulichangia, lakini umesahau kwamba CHADEMA inabebwa na mfumo Christo ambao uko well organized, ili hali CUF inabebwa na wakina yakhe ambao hawako well organized, hawana media za kutosha, hawana wasomi wengi ukiondoa wachache wakina Prof. Hata hivyo washabiki wa CUF wanaimani na Chama hiko na si rahisi kuhama. Kwa upande wa CDM mashabiki wake ni Oportunist ambao wanaweza kuhama na kuamia chama kingine kinachokaribia kushika dola
 
Hata CUF wanatambua hayo ila wanalazimika kufanya mikutano katika mikoa ambayo ni ngome ya CHADEMA kwani tofauti na hayo ndoa inaweza kuvunjika. Nao wanaogopa kwani bado wanaipenda ndoa yao ambayo bado changa sana.
 
Ni kweli ulichangia, lakini umesahau kwamba CHADEMA inabebwa na mfumo Christo ambao uko well organized, ili hali CUF inabebwa na wakina yakhe ambao hawako well organized, hawana media za kutosha, hawana wasomi wengi ukiondoa wachache wakina Prof. Hata hivyo washabiki wa CUF wanaimani na Chama hiko na si rahisi kuhama. Kwa upande wa CDM mashabiki wake ni Oportunist ambao wanaweza kuhama na kuamia chama kingine kinachokaribia kushika dola

Hivi bila kuingiza udini uwezi changia? Ngoja 2015 Chadema utaisoma namba
 
Ni kweli ulichangia, lakini umesahau kwamba CHADEMA inabebwa na mfumo Christo ambao uko well organized, ili hali CUF inabebwa na wakina yakhe ambao hawako well organized, hawana media za kutosha, hawana wasomi wengi ukiondoa wachache wakina Prof. Hata hivyo washabiki wa CUF wanaimani na Chama hiko na si rahisi kuhama. Kwa upande wa CDM mashabiki wake ni Oportunist ambao wanaweza kuhama na kuamia chama kingine kinachokaribia kushika dola

Mkuu, achana Na udini utakuua!
huwezi toa hoja bila kuchanganya Na udini?
 
MODS tafadhali msaada,

Naomba (kwa idhini ya mleta mada) mrekebishe makosa ya uandishi (spelling errors; but without changing the tone or meaning of the same) ili habari na ujumbe huu muhimu ujadiliwe vizuri na kubaki ktk kumbukumbu kwa usahihi zaidi
 
Ni kweli ulichangia, lakini umesahau kwamba CHADEMA inabebwa na mfumo Christo ambao uko well organized, ili hali CUF inabebwa na wakina yakhe ambao hawako well organized, hawana media za kutosha, hawana wasomi wengi ukiondoa wachache wakina Prof. Hata hivyo washabiki wa CUF wanaimani na Chama hiko na si rahisi kuhama. Kwa upande wa CDM mashabiki wake ni Oportunist ambao wanaweza kuhama na kuamia chama kingine kinachokaribia kushika dola

Wakati nakukanya uache udini.Hembu tuambie unataka washawishi nini akina yakhe kama kila kitu chao hakipo organised?Waachane navyo?Au lengo lako ni lipi?
 
Achaneni na "si yu efu" wakuu, adui mkubwa wa CDM ni mtazania mwenye mawazo mgando na asiyejua chanzo cha matatizo ya nchi hii. Kuhangaika na "si yu efu" ni kupoteza muda na kukubali ushindi wa thithimwewe kupitia ile formula yao ya "divide and rule"
 
maoni yako ukweli umechanganyika na uongo kwahio kimahesabu maelezo yote yanakuwa ya uongo, ila kisiasa unaweza kuonekana mtu ulie andika kitu cha maana sana na ukweli mtupu

baadhi ya uongo katika maoni yako
''3. CHADEMA ina watu/ Hazina kubwa sana ya kuweza kuwezesha Uhamasishaji tofauti na CUF, na hapa ndo sehemu zaidi ambayo CHADEMA kinajivunia na ndo sehemu ambayo inaimaliza CUF moja kwa moja, Leo hii John HECHE yuko Kagera akiendeleza M4C na yuko peke yake, Kamanda MAWAZO yuko Mwanza, CUF kiongozi wao wa Vijana hawezi kufanya anayo fanya JOHN HECHE, Mtatiro hawezi kufanya mikutano peke yake ni mpaka apewe sapoti ya Prfesa''

ukweli hukuzungumza, Mtatiro alikua musoma, na huko kafanya mikutano na alizunguka mikoa mingi na kafanya mikutano mwenyewe, Katani(kiongozi wa vijana Taifa) nae alikuwa mtwara mjini, lindi, na kwao tanadahimba kafanya mikutano kute huko pekeyake. akina Abdul Kambaya, mketo wanafanya mikutano hapo dar wao wenyewe, bado wabunge akina Sakaya, barwan n.k wanafanya mikutano wenyewe bila viongozi wa kitaifa kualikwa. labda sema huoni taarifa hizo ktk magazeti unayo soma.


kama kweli hao ulio sema wanamvuto na wanauwezo wa kuhamasisha na watu kujaa wawasikilize...... waende kufanya mkutano m4c pemba halafu ulete picha.

 
Unategemea nini kiongozi anapanda kwenye stage, anaropoka "CHADEMA NA CCM VIMESAHAU waislamu, sasa mjiunge na Cuf' hii ni kauli ambayo inatosha kukimaliza chama kisiasa. Watalaumu cdm ila wanajimaliza wenyewe.
 
Hivi bila kuingiza udini uwezi changia? Ngoja 2015 Chadema utaisoma namba

Kaka hapo hamna udini ni reality. Jana kwenye mkutano wa CUF, wadau wengi waliochangia walieleza kwamba kwenye mkutano kulijaa watu wengi wenye vibaraka mshehe. Hiyo ni fact na kimsingi ni suala la kihistoria na hapo sio udini ila ni kutokana na Chimbuko la Chama hicho kutokea eneo la Pwani lenye waislam wengi. Ni hivyo hivyo kwa CDM inachimbuko lake kutoka Mkoa wa Kilimanjaro.
 
5`Wewe uko tayari kusema sana CUF inamfumo wa kipwani (kiislam) lakini hautaki kusikia kwamba CDM ina mfumo kristo. Rejea coments zako kuhusu mikutano ya CUF. Kuwa na mfumo fulani kunatokana na waanzilishi wa kile Chama. Kutokana na makuzi na elimu aliyopata mtu anaweza kuona jambo fullani kwake ni muhimu wakati mwingine akaliona si muhimu.

Tuchukulie jambo dogo tu la miziki ya kaswida. Imagine umeenda kwenye ofisi ya umma halafu ukahudumiwa na afisa anaesikiliza kaswida, kuna watu wengi wanaweza kuwa against hilo, lakini hawatajali ikiwa ni kwaya. Aidha ni dhahiri backing ya CUF ni waislam, ambao kwa Tanzania bara so far hawajaweza kusimamia masuala yao mbalimbali, japo suala hilo linachangiwa na historia tulioachiwa na waasisi wa Tanganyika.``
 
Mimi sijafahamu CDM na CUF wanashindania nini? Nafasi ya pili?

majebere labda useme cuf wanashindana na cdm, sidhani kama cdm inashindana na cuf. kwa upande wa mwonekano kwa wananchi, kuna kitu cuf wanachokosea halafu hawajui kama kinawaathiri, muda wote macho yao yako kwa cdm, wamesahau kabisa kuwa walianzisha chama na kwa malengo yapi. sasa wana lengo tofauti kabisa, la kuwaatack cdm, ila hata atack yenyewe hawajui pia kuwa hawawezi kivile, kwa ccm kuona vile basi kwa urahisi tu wanawatumia, kwa hiyo wanaonekana kama wanafarakana na kupoteza meaning ya existance ya upinzani, na wao (ccm) wanaamini kuwa watasonga mbele hawa wawili wakiwa wanapambana, wanawapa kichwa cuf ambacho actually hawastahili wala hawana hiyo advantage kwa wananchi.
lakini sasa, hawafanikiwi pia kwa kuwa cdm wanayaona hayo yote na hawapotezi muda japo wakati mwingine inawabidi wajibu mashambulizi na uongo wa cuf.
 
Unategemea nini kiongozi anapanda kwenye stage, anaropoka "CHADEMA NA CCM VIMESAHAU waislamu, sasa mjiunge na Cuf' hii ni kauli ambayo inatosha kukimaliza chama kisiasa. Watalaumu cdm ila wanajimaliza wenyewe.

pengine anaamini aaminicho ponda hadi akahimiza kususia sensa.Kuwa wapo wengi na kura zao zinatosha wapa CUF ushindi.
 
Hebu tupia picha za mikutano ya mtatiro kanda ya ziwa

maoni yako ukweli umechanganyika na uongo kwahio kimahesabu maelezo yote yanakuwa ya uongo, ila kisiasa unaweza kuonekana mtu ulie andika kitu cha maana sana na ukweli mtupu

baadhi ya uongo katika maoni yako
''3. CHADEMA ina watu/ Hazina kubwa sana ya kuweza kuwezesha Uhamasishaji tofauti na CUF, na hapa ndo sehemu zaidi ambayo CHADEMA kinajivunia na ndo sehemu ambayo inaimaliza CUF moja kwa moja, Leo hii John HECHE yuko Kagera akiendeleza M4C na yuko peke yake, Kamanda MAWAZO yuko Mwanza, CUF kiongozi wao wa Vijana hawezi kufanya anayo fanya JOHN HECHE, Mtatiro hawezi kufanya mikutano peke yake ni mpaka apewe sapoti ya Prfesa''

ukweli hukuzungumza, Mtatiro alikua musoma, na huko kafanya mikutano na alizunguka mikoa mingi na kafanya mikutano mwenyewe, Katani(kiongozi wa vijana Taifa) nae alikuwa mtwara mjini, lindi, na kwao tanadahimba kafanya mikutano kute huko pekeyake. akina Abdul Kambaya, mketo wanafanya mikutano hapo dar wao wenyewe, bado wabunge akina Sakaya, barwan n.k wanafanya mikutano wenyewe bila viongozi wa kitaifa kualikwa. labda sema huoni taarifa hizo ktk magazeti unayo soma.


kama kweli hao ulio sema wanamvuto na wanauwezo wa kuhamasisha na watu kujaa wawasikilize...... waende kufanya mkutano m4c pemba halafu ulete picha.

 
Tatizo la CUF kwa sasa ni kukosa uelewa wa adui wa watanzania kwa sasa ni nani. Adui wa watanzania kwa sasa sio Chadema wala vyama vingine vya upinzani. Adui wa watanzania ni CCM pamoja na sera zake zilizo-fail. Adui wa watanzania ni CCM inayowahadaa watz maisha bora lakini hawatimizi ahadi. Adui wa watz ni CCM iliyogeuka kichaka cha wanaofisadi rasilimali za nchi hii hivyo kuwakosesha watz wengi fursa ya kushiriki faida itokanayo na rasilimali hizi ambazo nchi yetu imejaaliwa na Mwenyezi Mungu. Sasa wao CUF wanapingana na Chadema na matokeo yake wanaonekana kituko kwa mtu yeyote mwenye uelewa wa kawaida tu. No wonder inaonekana wanatumiwa na CCM kwa sababu ni ngumu ku-prove otherwise. Wajipange upya na watapata matokeo mazuri.
 
Back
Top Bottom