mlimbwa1977
Member
- Feb 7, 2011
- 24
- 0
Kwa ujumla hali ya maisha kwa Watanzania walio wengi inaendelea kuwa mbaya kadri miaka inavyokwenda licha ya maliasili zilizopo nchini.Mwaka huu tunasubiri kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika,umri wa miaka hamsini hairandani na maisha duni waliyonayo watanzania walio wengi.Kumekuwa na namna ya kujitetea kwa viongozi wetu kuwa Taifa letu bado changa hivyo kuhalalisha udhaifu uliopo wa maisha duni.Kwamba tunapaswa kuwa na subira mpaka tutakapofikisha labda miaka elfu moja,ndipo tuweze kulingana na wenzetu kimaendeleo kama vile,Africa Kusini,Libya,Misri,Cape verde,Shelisheli,nk.
Hali mbaya iliyopo nchini ya kiuchumi,kiuongozi,kijamii,Kisiasa,nk.itaendelea kudhoofisha mustakabali wa taifa letu kama mabaliko ya haraka hayatafikiwa.Licha ya kuwa na kila aina ya utajiri tumekosa viongozi,viongozi bora ndio mwarubaini wa matatizo tuliyonayo sasa.Viongozi wanapatikana kwa njia ya kuchaguliwa,hatuhitaji viongozi wanaoshindwa kufanya maamuzi,badala yake wanaishia kulalamika kama ilivyo kwa wasio na mamlaka ya kufanya maamuzi (wananchi wa kawaida).
Taifa letu litajiendesha kwa ufanisi tutakapoondokana na ukiritimba wa chama kimoja kujiona ndio wenye haki ya kuongozi taifa letu,tunahitaji ushindabni wa vyama vya siasa katika kuwaletea maendeleo wananchi,chama kinachofanikiwa kuongoza vizuri ndicho kinachopaswa kuchaguliwa kuongoza.Chama cha mapinduzi kimeonyesha kwa vitendo kushindwa kuongoza taifa.Angalia viongozi wa serikali za mitaa hakuna wanachofanya,angalia maofisini hakuna kinachofanyika cha maana (wafanyakazi wanafanyakazi kwa mazoea,hakuna kuwajibishana),wananchi
wameendelea kuishi kwenye nyumba za tembe,matibabu duni,elimu isiyokidhi,miundombinu isiyokidhi,bei za vyakula juu,uzalishaji duni wa bidhaa viwandani,tumeishia kuhemea kutka nje,thamani ya shilingi inaendelea kuanguka,hakuna anaejali.
Umuhimu wa vyama vikuu vya upinzani nchini kuuanzisha ushirikiano kuelekea uchaguzi mkuu ujao ni muhimu sana sasa kuliko wakati mwingine wowote,chama chochote kitakachojiona ni bora kuliko wenzao na kutarajia kushinda peke yake ni kujidanganya.Ushirikiano ni muhimu sana ili kuiondoa CCM madarakani ili tuanzishe mfumo wa kupokezana uongozi,hii italeta ushindani muafaka katika kuwaletea maendeleo wananchi.Nawaomba Chadema,CUF,NCCR,nk.kuacha kiburi,nchi hii ni yetu sote tunawategemea sana kubadilsha mfumo wa uongozi uliopo sasa katika nchi yetu.mlimbwa1977@yahoo.com.
Hali mbaya iliyopo nchini ya kiuchumi,kiuongozi,kijamii,Kisiasa,nk.itaendelea kudhoofisha mustakabali wa taifa letu kama mabaliko ya haraka hayatafikiwa.Licha ya kuwa na kila aina ya utajiri tumekosa viongozi,viongozi bora ndio mwarubaini wa matatizo tuliyonayo sasa.Viongozi wanapatikana kwa njia ya kuchaguliwa,hatuhitaji viongozi wanaoshindwa kufanya maamuzi,badala yake wanaishia kulalamika kama ilivyo kwa wasio na mamlaka ya kufanya maamuzi (wananchi wa kawaida).
Taifa letu litajiendesha kwa ufanisi tutakapoondokana na ukiritimba wa chama kimoja kujiona ndio wenye haki ya kuongozi taifa letu,tunahitaji ushindabni wa vyama vya siasa katika kuwaletea maendeleo wananchi,chama kinachofanikiwa kuongoza vizuri ndicho kinachopaswa kuchaguliwa kuongoza.Chama cha mapinduzi kimeonyesha kwa vitendo kushindwa kuongoza taifa.Angalia viongozi wa serikali za mitaa hakuna wanachofanya,angalia maofisini hakuna kinachofanyika cha maana (wafanyakazi wanafanyakazi kwa mazoea,hakuna kuwajibishana),wananchi
wameendelea kuishi kwenye nyumba za tembe,matibabu duni,elimu isiyokidhi,miundombinu isiyokidhi,bei za vyakula juu,uzalishaji duni wa bidhaa viwandani,tumeishia kuhemea kutka nje,thamani ya shilingi inaendelea kuanguka,hakuna anaejali.
Umuhimu wa vyama vikuu vya upinzani nchini kuuanzisha ushirikiano kuelekea uchaguzi mkuu ujao ni muhimu sana sasa kuliko wakati mwingine wowote,chama chochote kitakachojiona ni bora kuliko wenzao na kutarajia kushinda peke yake ni kujidanganya.Ushirikiano ni muhimu sana ili kuiondoa CCM madarakani ili tuanzishe mfumo wa kupokezana uongozi,hii italeta ushindani muafaka katika kuwaletea maendeleo wananchi.Nawaomba Chadema,CUF,NCCR,nk.kuacha kiburi,nchi hii ni yetu sote tunawategemea sana kubadilsha mfumo wa uongozi uliopo sasa katika nchi yetu.mlimbwa1977@yahoo.com.