CUF, acheni kupotosha watu kuhusu matokeo ya Uchaguzi Wilaya ya Igunga 2010

Mkuu Mag3 na wengineo, takwimu ulizoweka hapa zinadhihirisha kitu kimoja kikubwa ambacho ni kwamba upinzani bado una kazi ya ziada ili kuweza kupenya katika jimbo la Igunga na Tabora kwa ujumla. Badala ya kupoteza muda kuwarihisishia CCM kazi ya kuvipaka matope CUF, CHADEMA, NCCR na wengineo, kwa nini msiweke tofauti zenu kando ?

Ni imani yangu kwamba hakuna chama cha upinzani kitakachoweza kuin'goa CCM madarakani peke yake. Ni vyema tofauti na vijembe visivyo na tija viwekwe pembeni na nguvu zikaunganishwa kuweza kuwashinda hawa watawala wa sasa.

Lengo la vyama vyote vya siasa (ikiwemo CCM yenyewe) ni sharti liwe moja, kuongoza taifa katika dira mbadala na hii ya CCM ambayo imeleta miaka 50 ya majuto.
 
Kuna umuhimu mkubwa sana kwa chadema kusimamisha mgombea igunga. Ofcourse lengo kubwa la kwanza ni kushinda katika uchaguzi huo. Lengo la pili ni kukitangaza na kukijenga chama jimboni igunga na mkoani tabora kwa ujumla. Pamoja na hayo kama kweli chadema wana malengo ya kukamata nchi hapo baadae hawapaswi kuogopa chochote. Wanapaswa kujua kwa wao ndio chama kikuu cha upinzani, hivyo upinzani huo hauishii bungeni tu ni pamoja na kwenye chaguzi mbalimbali kama huo wa igunga.
 
Cdm hawatumii pesa kununua wanachama,wanachama wanafuata sera za kweli.so wakipewa somo kumbe wanaweza kuelewa na hii ni tofauti na nilivyokuwa naamini kuwa cuf wana nafasi kubwa.
 
Nimetafuta data kutoka tume ya uchaguzi za mkoa mzima wa Tabora, pamoja na hiyo mbinu ya kutaka tuamini CUF ni maarufu huko Tabora kuliko chama chochote cha upinzani lakini ukweli uko hivi kutokana na matokeo ya mwaka jana:

Dr. Slaa - 38, 341

Lipumba - 34,374

Tofauti anayozidiwa nayo Lipumba ni 3,977 karibu kura 4000 sasa sijui huo umaarufu na ukwao wa Lipumba unaelezekaje hapa. Kwa kifupi kama alivyosema Mag3, mashabiki wa CUF wanawaongopea watanzania.

Naujuwe hizi ni baada ya wizi! Tunachotaka ikiwezekana CUF ife tubaki na Chadema ili nguvu ya Watanzania iunganishwe pamoja kumtoa huyu Joka chumbani.
 
Back
Top Bottom