CTV: Mdahalo wa wagombea Ubunge Igunga

Great thinkers hii habari siyo ya kweli, binafsi nipo igunga na nilihudhuria mdahalo, na haya ndio matatizo ya hawa CCM B kwa sababu hawana stragegy zaidi ya kurembua kwa mabosi wao, kwanza kabisa ni kichekesho wakati halmashauri inakashfa kibao za mabilioni ya pesa za wananchi, ikiwemo taarifa ya mdhibiti mkuu wa mahesabu iliyowekwa pale wazi, eti watu wanazungumzia shilingi milioni 16 ambazo hata hivyo mgombea wa chadema alikuja kumjulisha mpaka balance iliyobaki na kwamba utendaji wake huo ndio uliompa cheo. tatizo CUF hawajipangi na wanaonekana wazi tatizo lao ni wivu kwa chadema, jamani hii taarifa ni kichekesho mimi ni mwandishi niliyeko huku na kwa bahati nzuri nimesikia tangazo kwamba mdahalo huo utarushwa leo saa tatu mpaka tano usiku star tv angalieni muone, kijana wa cuf sio mbaya lakini sio mzuri kiasi hicho na hilo wanalosema sio kweli.
 
Great thinkers hii habari siyo ya kweli, binafsi nipo igunga na nilihudhuria mdahalo, na haya ndio matatizo ya hawa CCM B kwa sababu hawana stragegy zaidi ya kurembua kwa mabosi wao, kwanza kabisa ni kichekesho wakati halmashauri inakashfa kibao za mabilioni ya pesa za wananchi, ikiwemo taarifa ya mdhibiti mkuu wa mahesabu iliyowekwa pale wazi, eti watu wanazungumzia shilingi milioni 16 ambazo hata hivyo mgombea wa chadema alikuja kumjulisha mpaka balance iliyobaki na kwamba utendaji wake huo ndio uliompa cheo. tatizo CUF hawajipangi na wanaonekana wazi tatizo lao ni wivu kwa chadema, jamani hii taarifa ni kichekesho mimi ni mwandishi niliyeko huku na kwa bahati nzuri nimesikia tangazo kwamba mdahalo huo utarushwa leo saa tatu mpaka tano usiku star tv angalieni muone, kijana wa cuf sio mbaya lakini sio mzuri kiasi hicho na hilo wanalosema sio kweli.

Unaweza ukawa mwandishi lakini si mwandishi sahihi!!! Unaposema kuwa halmashauri ina kashfa kibao za ubadhirifu wa mabilion lakini watu wanaongelea milioni 16 una maana gani? Hizo unazosema milioni 16 siyo sehemu ya mabilion au kwako wewe mabilioni yanaanzia shilingi ngapi? Ufisadi ni ufisadi tu hata uwe wa shillingi moja!! Ngoja nijiandae kuuangalia huo mdahalo iff. Megawat zitakkuwepo
 
Kumbe mgombea wa Chadema ana kashfa ya ubadhirifu. Sasa mbona anaendelea na kampeni?

mbona CCM imeua watu na inaendelea kuua lakini ipo madarakani? Mwita unaichukia CHADEMA kwa kuwa inakuchoma, nahsi huwa ukilala unaiota....inakutorment, inautorture moyo wako, ukiickia moyo unakulipuka....nakuambia na bado....utatapatapa mpaka utakapokubali kuwa CHADEMA ndio yenyewe....na ukishupaza sana shingo UTAKUFA GHAFLA...!
 
Vipi wamepeleka tena pingamizi? maana kila kukicha wanawaza kushinda kwa ma-pingamizi! CCM-B hawana lolote
 
huyo mahona,angepitia Chadema!angekuwa amejihakikishia uheshimiwa!lakini kwa sasa mambo yanavyoenda!nahisi Cuf na Chadema watachukua kura paru paru na magamba wataibuka wasìndi japo kwa kura chache.
 
Huu ndio ukweli CCM itashinda kwa 37 .8 % Igunga huu ndio utabiri wangu na Chadema na CUF wataondoka na kura zisizopungua 56 % ila zitakua ni divided kwa hiyo CCM imejihakikishia ushindi bila ya wasi kwa uzembe wa Upinzani . Igunga ni Tarime ya Wapinzani kumbukeni Chadema na CUF na NCCR mageuzi walivyopata 58% huko Tarime uchaguzi uliopita ila walizigawa kura vipande vipande na CCM kushinda kwa 38.5 % ni below ya 50 %
reference see this link The National Electrol Commission of Tanzania - Homepage
 
Jamani mbona mna wivu, kama alijieleza vizuri na kujenga hoja za msingi kuliko wote kwanini asiwe mshimdi. kushinda mdahalo sio kushinda ubunge hivyo haki yake mpeni.
 
mbona ccm imeua watu na inaendelea kuua lakini ipo madarakani? Mwita unaichukia chadema kwa kuwa inakuchoma, nahsi huwa ukilala unaiota....inakutorment, inautorture moyo wako, ukiickia moyo unakulipuka....nakuambia na bado....utatapatapa mpaka utakapokubali kuwa chadema ndio yenyewe....na ukishupaza sana shingo utakufa ghafla...!

huwezi kuhalalisha kosa kwa kutumia kosa lingine
 
Ni ukweli usiopingika kwamba kosa ni kosa tu na wala si kweli kwamba viongozi wa Chadema they are perfect na hivyo hawafanyi makosa au hawakuwahi kukosa,ikumbukwe kwamba wao si malaika,they are human being like others.Ila hapa kinachotupa shida ni kitu kimoja.
Kwa nini makosaa ni ya CHADEMA tu wakikosa CCM sio makosa na wenzao B wanahesabika wamekosea kidogo tu na hakuna wakuliongelea.
Hivi makosa ni Chadema tu ndo anaejua kukosea na kosa hilo likaitwa kosa?wakikosa CCM-MAGAMBA sio kosa na wala halipashwi kuzungumzia.
Hivi mnatoa wapi ujasiri wa kuandika eti kashfa ya Kashindye mgombea wa Chadema au kuzungumzia hilo wakati kuna kashifa ngapi za wana CCM tena zingine zinatia hata pressure,kabisa,nani msafi ndani ya CCM?kuanzia juu hadi chini,hata huyu mgombea wa CCM dr Kafumu unayajua aliyokuwa akiyafanya wizara ya madini?unajua kama alikuwa kamishina wa madini?kuna madudu ambayo hakushiriki?hata hapo Igunga kishawadhuru,au hujui kama Igunga kuna madini? lakini iweje anagombea?au ni kweli kwamba kosa ni la Chadema tu akikosa wa CCM si kosa?wewe ulietoa post hii napata mashaka na uelewa wako kwani dola hii hujui kama ni chafu kuliko hata choo cha stand ya mabasi?mbona bado inapigana kuendelea kuongoza?
huna hoja hapa,eti unasema Kashindye ana kashifa,kwanza mimi binafsi siamini kwa sababu ni vigumu kugombea kupitia upinzani ukitokea serikali ili hali una tuhuma kama hizo,hali yake ingekuwa tete zaidi ya kile unachodhani. na hata hivyo hatuwezi kumjaji kwa kosa hilo mbona ni dogo?ikumbukwe kwamba makosa yanapimika kwa ukubwa na ndoo maana adhabu haiko flat,kwamba kila kosa ni jela miaka 2,no ndio maana kila kosa lina hukumiwa kwa ukubwa wake na ushahidi utakaotolewa kuthibitisha kosa hilo
Nawasilisha
 
Great thinkers hii habari siyo ya kweli, binafsi nipo igunga na nilihudhuria mdahalo, na haya ndio matatizo ya hawa CCM B kwa sababu hawana stragegy zaidi ya kurembua kwa mabosi wao, kwanza kabisa ni kichekesho wakati halmashauri inakashfa kibao za mabilioni ya pesa za wananchi, ikiwemo taarifa ya mdhibiti mkuu wa mahesabu iliyowekwa pale wazi, eti watu wanazungumzia shilingi milioni 16 ambazo hata hivyo mgombea wa chadema alikuja kumjulisha mpaka balance iliyobaki na kwamba utendaji wake huo ndio uliompa cheo. tatizo CUF hawajipangi na wanaonekana wazi tatizo lao ni wivu kwa chadema, jamani hii taarifa ni kichekesho mimi ni mwandishi niliyeko huku na kwa bahati nzuri nimesikia tangazo kwamba mdahalo huo utarushwa leo saa tatu mpaka tano usiku star tv angalieni muone, kijana wa cuf sio mbaya lakini sio mzuri kiasi hicho na hilo wanalosema sio kweli.

Mijitu mingine inabishia hata the obvious. Kila mtu aliyeangalia mdahalo ule na hata kusoma magazeti ya leo anasema wazi kwamba mgombea wa CUF alifanya vizuri kuliko wote. Tatizo hapa ni kwamba walichotarajia magwanda hakikwenda vizuri na ndiyo maana stori hii imechukiza. Kwa ufupi bwana Kashindye anabebwa na nguvu ya chama chake na siyo uwezo wake. Na Mahona kama angekuwa na chama chenye ushawishi ndiye mgombea bora kuliko wote wanaoshiriki uchaguzi huu mdogo.

Kubali mzee kwamba kwa mdahalo wa jana Mahona aliwika.
 
Mimi nafurahi kuwa demokrasia inakua. Huu ushindani unanipa matumaini kuwa sisi inawekwa roho juu
 
WAGOMBEA ubunge katika Jimbo la Igunga, Leopold Mahona wa CUF na Mwalimu Joseph Kashindye wa Chadema, walimkaba koo mgombea wa CCM, Dk Dalaly Kafumu katika mdahalo uliofanyika mjini Igunga kuwa amehusika na mikataba mibovu ya madini.Walitoa maneno hayo kwenye mdahalo wa uchaguzi mdogo wa Igunga na Tanzania tunayoitaka ambao uliwahusisha wagombea hao watatu uliofanyika katika ukumbi wa Sakawa.

Mahona alimtuhumu Dk Kafumu kuwa ndiye aliyesaini mikataba mibovu ya madini inayoligharimu taifa hadi sasa akidai kwamba katika kila Sh100 ya Tanzania, nchi inapata Sh3.“Hakuna wilaya ambayo mtu anaweza kutembea na kuokota almasi, isipokuwa Igunga. Lakini sekta hiyo iko chini na chanzo ni huyu bwana, nani asiyejua kuwa ndiye aliyesaini mikataba mibovu ya madini?” alihoji Mahona.

“Mikataba ambayo katika kila Sh100, Serikali ya Tanzania na watu wake inaambulia Sh3!”alisema Mahona huku akishangiliwa na watu waliohudhuria madahalo huo.Akijibu hoja hiyo, Dk Kafumu alisema hakuwahi kuingia mikataba ya madini, bali alikuwa msimamizi wa sheria iliyotungwa bungeni.

“Mimi kazi yangu ni kusimamia sheria na si kusaini mikataba. Kazi ya kusaini mikataba inafanywa na waziri na sheria inatungwa bungeni kina Zitto (Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Chadema) wanafahamu,” alisema Dk Kafumu.

Hata hivyo, baada ya majibu hayo mgombea wa Chadema Kashindye, alisimama na kitabu kinachoelezea utafiti wa madini nchini alichoeleza kuwa hakijulikani kwa wananchi wa kawaida na badala yake, kimeuzwa Ulaya kutafuta wawekezaji.

“Katika kitabu cha mgombea wa CCM kinaeleza kuwa Igunga kuna madini ya aina 11, kitabu hiki amekiuza na kukitangaza Ulaya kuvutia wawekezaji, woga wangu ni kuwa ule mpango wa kufukia wananchi katika Mgodi wa Bulyanhulu, unaweza kufanyika hapa Igunga,” alisema Kashindye
 
Dr Kafumu ni chaguo la baadhi ya wanaCCM si chaguo la wananchi wa Igunga. Wananchi wa Igunga hawadanganyiki, ni waelewa, wanataka maendeleo sio propaganda za magamba. Igunga lazima ikombolewe sasa.
 
Wa Tanzania kuweni na subra kwani ukweli sahihi utapatikana wakti wa matokeo ya uchaguzi. Jifunzeni Tambo za kisiasa na majigambo mwishowe ni matokeo ndio yenye kubainisha ukweli wa mambo.

Vile vile mlioko Tz basi kama mdahalo huo utaonyeshwa kwenye TV utatoa mwanga na kila mtu atakuwa jaji wa kile alichokiona.

Kila la kheir wana Igunga. Khatima ya maendeleo yenu ipo katika kikaratasi chako cha kuoigia kura.

nakhenee lolo
 
mgombea wa CUF, Leopold Mahona ameibuka kidedea katika mdahalo wa wagombea ubunge katika jimbo la igunga akiongea kwa kujiamini na kueleza nini atakacho wafanyia wakazi wa jimbo la igunga huku akiwatuhumu wagombea wenzake kukabiliwa na tuhuma za ubadhirifu wakati wakiwa kazini, ambapo alisema kashindye alipokuwa mratibu alikabiliwa na ubadhirifu wa sh 14,000,000. ambapo kashindye alishindwa kukanusha, akijibu maswali kwa ufasaha huku akipigiwa makofi mengi na waliohudhuria.

Hongera sana CCM 'B' kwa kuongea kwa kujiamini
 
mgombea wa CUF, Leopold Mahona ameibuka kidedea katika mdahalo wa wagombea ubunge katika jimbo la igunga akiongea kwa kujiamini na kueleza nini atakacho wafanyia wakazi wa jimbo la igunga huku akiwatuhumu wagombea wenzake kukabiliwa na tuhuma za ubadhirifu wakati wakiwa kazini, ambapo alisema kashindye alipokuwa mratibu alikabiliwa na ubadhirifu wa sh 14,000,000. ambapo kashindye alishindwa kukanusha, akijibu maswali kwa ufasaha huku akipigiwa makofi mengi na waliohudhuria.

Inaonekana lengo lako hapa ilikuwa ni kumshambulia kashindye, kwamba naye ni fisadi. Na kwakuwa cuf mnafanya juhudi za kuwasaidia washirika wenu ccm, hujathubutu hata kumtaja mgombea wao kwamba alifanya nini kwenye huo mdahalo.

Lakini kwakuwa startv wameahidi kuuonyesha, basi tuwaombe tanesco wasifanye mambo yao walau kwa usiku mmoja tu wa leo ili tujionee kilichojiri huko igunga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom