Tanzania kampuni nyingi hazina mafunzo ya kutosha ya biashara na hii ndiyo sababu kampuni nyingi zinakufa.
Kwa Upande wa CRDB: CRDB wanaamini wamefanya kila kitu kuhamisisha watu wa USA kufungua Account ikiwa ni pamoja na kuanzisha Internet Banking na kuruhusu pesa ya Account iwe kwenye Dollars. CRDB Wamejigamba mbona eti wamefanikiwa sana Botswana.
Kwa Upande wa Watanzania wa USA: Wanaona CRDB hawafanyi kazi nzuri na wamejaa uzembe na uswahili hivyo hawawezi kufungua account ya Tanzanite ya CRDB.
Tatizo ni nini hapa? Tatizo ni utamaduni.
CRDB na Watanzania wengi wamesahau kwamba utamaduni wa Watanzania wa USA sio sawa kabisa na utamaduni wa Watanzania wa Botswana au ambao wako Tanzania. Kwasababu wote ni Watanzania haina maana utamaduni wa kufanya vitu ni sawa mfano: Mtanzania wa USA akiandika email ya kuuliza kitu kwenye account anategemea kujibiwa sio zaidi ya siku mbili lakini CRDB Tanzania wanaweza kuchukua hadi wiki mbili kujibu email. Mfano mwingine Watanzania wa USA hawanashida kama ukiwasiliana nao na kuwaambia mfano kufungua account ni wiki nne lakini kama ukiwaambia ni siku mbili halafu ichukue mwezi mzima wanafunga account. Hivyo inabidi kama unafanya biashara na Watanzania wa USA Uwape muda wa ukweli. Hii sio kwasababu yeyote ya kujifanya nani zaidi lakini ni utamaduni waliozoea wa kufanya shughuli za kila siku za kijamii huku USA. Watanzania wa Botswala wanaelekea kuwajua zaidi kiutamaduni Watanzania wanaoishi nyumbani hivyo hawaweweseki kwa mammbo mengi kama wale wa USA. Kama kuna Watu wanaotaka kufanya biashara na Watanzania wa Diaspora mimi ningeshauri kujifunza utamaduni wao au kuajiri mtu aliyeishi kwenye diaspora.
Kwa Upande wa CRDB: CRDB wanaamini wamefanya kila kitu kuhamisisha watu wa USA kufungua Account ikiwa ni pamoja na kuanzisha Internet Banking na kuruhusu pesa ya Account iwe kwenye Dollars. CRDB Wamejigamba mbona eti wamefanikiwa sana Botswana.
Kwa Upande wa Watanzania wa USA: Wanaona CRDB hawafanyi kazi nzuri na wamejaa uzembe na uswahili hivyo hawawezi kufungua account ya Tanzanite ya CRDB.
Tatizo ni nini hapa? Tatizo ni utamaduni.
CRDB na Watanzania wengi wamesahau kwamba utamaduni wa Watanzania wa USA sio sawa kabisa na utamaduni wa Watanzania wa Botswana au ambao wako Tanzania. Kwasababu wote ni Watanzania haina maana utamaduni wa kufanya vitu ni sawa mfano: Mtanzania wa USA akiandika email ya kuuliza kitu kwenye account anategemea kujibiwa sio zaidi ya siku mbili lakini CRDB Tanzania wanaweza kuchukua hadi wiki mbili kujibu email. Mfano mwingine Watanzania wa USA hawanashida kama ukiwasiliana nao na kuwaambia mfano kufungua account ni wiki nne lakini kama ukiwaambia ni siku mbili halafu ichukue mwezi mzima wanafunga account. Hivyo inabidi kama unafanya biashara na Watanzania wa USA Uwape muda wa ukweli. Hii sio kwasababu yeyote ya kujifanya nani zaidi lakini ni utamaduni waliozoea wa kufanya shughuli za kila siku za kijamii huku USA. Watanzania wa Botswala wanaelekea kuwajua zaidi kiutamaduni Watanzania wanaoishi nyumbani hivyo hawaweweseki kwa mammbo mengi kama wale wa USA. Kama kuna Watu wanaotaka kufanya biashara na Watanzania wa Diaspora mimi ningeshauri kujifunza utamaduni wao au kuajiri mtu aliyeishi kwenye diaspora.