CRDB na fees zao...!?

Naomba ufafanuzi kidogo hapo hgarama za internet banking, je hata kwa wale wateja waliyoomba bank statement kwa nia ya barua pepe wanakatwa?
Nilishawahi kuleta hii kero hapa siku za nyuma, nashukuru wadau walitoa mwanga. Kwa hali ilivyo, CRDB iatayumba sana kwa kuwa haya makato yanakera sana. CEO, Sumaye na Wakurugenzi wengine wanapaswa kusoma upepo haraka, kwa kuwa hata kule kwenye hisa bei inapepesuka, wateja wamekuwa wakiibiwa sana
 
Pole sana, but those are normal fees

Card fees huwa ni shilingi 4000 semi annualy, i mean per year utakatwa card fees tsh 8000, na huwa hizo fees zinapita mwezi wa saba na mwishoni mwa december au january mwanzoni. Kama ulikatwa card fees mara mbili inawezekana kabisa either ulirenew card alafu ile ya zamani hukurudisha bank, so kwenye system zao utaonekana we una card mbili, au ukirudisha lakini haikutolewa kwenye system.

Hiyo 1,000 ni monthly maintanance fees, account yoyote inachajiwa maintanance fees ya sh 1,000 except JUNIOR JUMBO ACCOUNT yenyewe haina charges.


Hiyo withholding tax, ukiangalia vizuri kwenye hiyo statement yako utaona credit ina narration inerest applied,hiyo account yako huwa ina accrue interest kila mwaka na normaly huwa inaingia tarehe moja july, na hiyo interest inakatwa withholding tax ya 10% na inaenda direct TRA

Kama hujaelewa hapo uliza tena
 
...Ongeza na hizi:

-Maintenance fee 700/= ( nina hakika hii wameishapandisha!)
- Withdrawal fee 500/= ( pia nadhani imeishapanda!)
- Visa ATM Charges 2000/-
- Mimi binafsi nina cheki ya shs 30,000/- ambayo huingia kila Ijumaa kwenye Account yangu na inapoingia tu jamaa wanachukua 1,500 kama Commission na mimi kubaki na 28,400/= kwa maana hiyo katika 120,000/= ya kila mwezi jamaa wanavuta 6,000/= zangu kama commission yao mbali na makato yote hayo mengine!! Dah. Naanza kufikiria sana kuhusu kuweka hela zangu chini ya Godoro!

-

Umekosea hapo,

maintanance fees ni tsh 1,000 per month,

withdraw charges kwenye ATM ni sh 600, over the counter ni sh 1000

Visa withdraw charges niincase ukiwithdraw kwenye ATM ambayo sio ya CRDB ndo utakatwa sh 2000:A S angry:
 
NMB,for sure am enjoying!!tena nataka nifungue nyingine hapohapo,Fixed accnt

Mkuu mimi ni mteja wa NMB, CRDB na Exim Bank lakini pengine hujuwi vizuri makato ya NBM mkuu. Siku moja nimefika pale Bank house nikakutana na bango kubwa pale mlangoni limeorodhesha makato nilichoka. Nikajisemea "Benki hii si ya makabwela tena". Inawezekana hapo ulipo unapata huduma nzuri lakini kuna watu wako sehemu tofauti na wewe ukiwaambia habari za NMB hawataki hata kusikia. Na kama unataka kufungua fixed akaunti sikushauri ufungue NBM kwani faida zao ni ndogo ukilinganisha na benki zingine kama vile FNB (First National Bank - hawa ndo wanaongoza kwa faida kubwa kwa fixed akaunti) pia Exim ni wazuri kwa fixed akaunti.
 
Mkuu mimi ni mteja wa NMB, CRDB na Exim Bank lakini pengine hujuwi vizuri makato ya NBM mkuu. Siku moja nimefika pale Bank house nikakutana na bango kubwa pale mlangoni limeorodhesha makato nilichoka. Nikajisemea "Benki hii si ya makabwela tena". Inawezekana hapo ulipo unapata huduma nzuri lakini kuna watu wako sehemu tofauti na wewe ukiwaambia habari za NMB hawataki hata kusikia. Na kama unataka kufungua fixed akaunti sikushauri ufungue NBM kwani faida zao ni ndogo ukilinganisha na benki zingine kama vile FNB (First National Bank - hawa ndo wanaongoza kwa faida kubwa kwa fixed akaunti) pia Exim ni wazuri kwa fixed akaunti.

asante mdau,basi ntazitemblea benki hizo kwa fixed!!kwa kweli makato yao nayatambua sana ila nimeona nitulie nao tu maana sioni hata pa kukimbilia!
 
Mabenki yanakimbia kukopesha na kutengeneza pesa kupitia fees/commissions, inaonyesha muelekeo ndio huo kwa wote, sijui Fees elekezi za BoT kama zitasaidia kwenye hili suala.
 
Leo nilikuwa naperuzi account yangu ya CRDB through internet banking na nikashtuka kidogo na fees zao. Nimekutana na kitu kama ifuatavyo:

Monthly maintenance fee ........Tshs. 1,000
Card fee June ........................Tshs. 4,000 (hii transaction ya tarehe 9 July)
Card fee June ........................Tshs. 4,000 (hii transaction ya tarehe 13 July)
Withholding Tax .....................Tshs. 63.39

Nilikuwa sijanotice hivi vitax kwa muda na nashangaa kama huu ni utaratibu mpya. Kama wanamfanyia kila mteja namna hii, basi wanatengeneza faida ya hatari sana

Angalia faida yao.....



pc2RO3K3JMAAAAABJRU5ErkJggg==
 
sina experince na exim bank
hivo nao ni wazuri??

Mkuu nilichojifunza ni kuwa benki zinatofautiana kutoka tawi moja hadi jingine ndani ya benki hiyohiyo kwa ubora wa huduma. Binafsi sijawahi kupata tatizo na hawa Exim. Na cha zaidi gharama za kuendesha akaunti ni ndogo zana ulinganisha na mabenki mengine.
 
Mkuu nilichojifunza ni kuwa benki zinatofautiana kutoka tawi moja hadi jingine ndani ya benki hiyohiyo kwa ubora wa huduma. Binafsi sijawahi kupata tatizo na hawa Exim. Na cha zaidi gharama za kuendesha akaunti ni ndogo zana ulinganisha na mabenki mengine.



thank u mkuuu
 
Back
Top Bottom