Bishanga
JF-Expert Member
- Jun 29, 2008
- 15,323
- 10,050
Kuna Pharmacist kanilipulia bomu akaniambia Condoms za DUREX aina ya FEATHERLITE zenye pakiti ya rangi ya brown zimepigwa marufuku kisa ziko chini ya kiwango. Naomba wadau walio karibu na TFDA watuhabarishe kama ni ya kweli haya,na je usalama wa waliokuwa wanazitumia uko vipi au ndo inabidi kujisalimisha 'angaza'? Kusema kweli inatisha maana leo pitia Pharmacy yoyote mjini aina hiyo ya condoms kweli hazipo madukani! Wadau twafa maana ilianza na metakelfin feki,mara ampicillin feki sasa jamani hawa matapeli wanavamia na idara nyeti?