Facilitator
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 2,280
- 1,763
Kufududua kwa kifudusi. Kiswahili kinazidi kuwa kigumu!
Kufududua kwa kifudusi?? Hii imetulia. Masharobaro waipate hii waipe promo kila mahali. Media zote zitairasimisha tu..
Kufududua kwa kifudusi. Kiswahili kinazidi kuwa kigumu!
wanaharibu maana wanakaa kama kamati na kutafuta neno la kiswahili badala ya kuacha lugha ijipanue yenyewe-mbona tunatumia maneno ya kiarab,kireno n.k
so naon kwa maneno kama kondom,password yaachwe yabakie kama yalivyo-ijulikane ni neno la kigeni tumeazima-kuliko kukaa na kutafuta maneno wanayojua wao wenyewe na kufanya hata sisi waswahili tushindwe kuyafahamu
ikiwa tutakopa kila neno jipya, basi kiswahili kitapoteza usanifu wake kwa vile kitakuwa na msamiati asilia finyu kabisa. Ni vema kuunda istilahi kwa kila dhana mpya ifikapo. tusiwe omba omba. Kati ya Kifudusi na shakoshi, ni lipi bora zaidi?