Computer programing na ma-software jamani!

Chamalama

Senior Member
Dec 12, 2010
131
44
Napenda sana mambo ya kutengeneza programe na software. Kozi gani nisome na Chuo gani? Niko University (PCM A-level) ila nasomea ishu nyingine tofauti na hiyo.Ningependa kuanzia ngazi ya Diploma au Degree.
 
Napenda sana mambo ya kutengeneza programe na software. Kozi gani nisome na Chuo gani? Niko University (PCM A-level) ila nasomea ishu nyingine tofauti na hiyo.Ningependa kuanzia ngazi ya Diploma au Degree.

Kwa kuwa bado uko A -Level tambua kuwa program na software ni kitu kile kile na ili kutengeneza hii kitu itakubidi ufanye kazi kubwa katika masomo yako,ngazi ya diploma sidhani kama unaweza.

Hii kazi ni ngumu sana lakini inayolipa kwa kiwango cha kutisha.Hapa bongo unaweza husipate waliowahi kufanya hii kitu.
kule South Africa wameweza kutengeneza Opetating software ya Ubuntu .wengine mikwara tu.
 
@chamalama

Ushauri wangu kwasababu tayari upo chuo(hujasema unasoma nini na mwaka wa ngapi) haina haja ya wewe kubadili kozi unayosoma. Kama unapenda programming unawezasoma Computer Programming Courses kwa mda wako wa ziada.

Tafuta chuo(eg LearnIT, UCC) kuna short courses ambazo zinaweza kukupa mwangakuhusu Software development.
 
Kwa kuwa bado uko A -Level tambua kuwa program na software ni kitu kile kile na ili kutengeneza hii kitu itakubidi ufanye kazi kubwa katika masomo yako,ngazi ya diploma sidhani kama unaweza.

Hii kazi ni ngumu sana lakini inayolipa kwa kiwango cha kutisha.Hapa bongo unaweza husipate waliowahi kufanya hii kitu.
kule South Africa wameweza kutengeneza Opetating software ya Ubuntu .wengine mikwara tu.

Jamaa kasema yupo chuo ila anasoma inshu nyingine co mambo ya computer.Back to topic,kuweza kuteneza software unaweza hata kama ukiwa na diploma ya IT au COMPUTER SCIENCE,hapa inategemea na mitaala ya chuo unachosoma.Kuweza kutengeza softwares inabidi ujue sana computer languages zake.
 
Unataka ubadili kabisa profession au unataka ujue tu kutengeneza software? Kama ni kubadili profession, maliza degree yako baadae pandishia na postgraduate ya IT, hapo mlimani wanatoa.

Otherwise, kama ni kujua tu kutengeneza software, nenda vyuo vya wahindi mjini, wanatoa short courses kuanzia three weeks hadi three months za Computer programming.
 
Napenda kuwaasa jamaa zangu wanaopenda kuwakatisha wengine tamaa. Ndugu zangu,mimi naamini hakuna somo gumu, ila determination ya anayesoma. Tuondokane na tabia hii.

Ushauri ambao ni + ni huo wa kujiendeleza. Mimi nilisoma arts ila napenda computers, rafiki zangu wananisaidia, nimefika mbali.
 
  • Thanks
Reactions: KXY
Napenda kuwaasa jamaa zangu wanaopenda kuwakatisha wengine tamaa. Ndugu zangu,mimi naamini hakuna somo gumu, ila determination ya anayesoma. Tuondokane na tabia hii.

Ushauri ambao ni + ni huo wa kujiendeleza. Mimi nilisoma arts ila napenda computers, rafiki zangu wananisaidia, nimefika mbali.

No No.Haya mambo ya kutokupenda kuelezwa ukweli ndiyo yanayotuharibu wabongo,mnapenda maelezo matamu matamu ya kutia moyo wakati hali iko tofauti.

ninaposema kuwa kutengeneza software ni kazi NGUMUUUUUU sana na inabidi uwe mzuri sana katika lugha za computer.
Kama unabisha nitajie software 5 tu zilizotengenezwa na wabongo tangu kuumbwa kwa hii dunia na zinatum,iwa na nani.Je si kwamba wataalam wa ICT wanasoma kila kukicha? huo ndiyo ukweli hata kama unaumwa.

unaowaona humu na mikwara yao yoooooote,waambie kuhusu kutengeneza software watatoa maelezo mpaska mwakani.
 
No No.Haya mambo ya kutokupenda kuelezwa ukweli ndiyo yanayotuharibu wabongo,mnapenda maelezo matamu matamu ya kutia moyo wakati hali iko tofauti.

ninaposema kuwa kutengeneza software ni kazi NGUMUUUUUU sana na inabidi uwe mzuri sana katika lugha za computer.
Kama unabisha nitajie software 5 tu zilizotengenezwa na wabongo tangu kuumbwa kwa hii dunia na zinatum,iwa na nani.Je si kwamba wataalam wa ICT wanasoma kila kukicha? huo ndiyo ukweli hata kama unaumwa.

unaowaona humu na mikwara yao yoooooote,waambie kuhusu kutengeneza software watatoa maelezo mpaska mwakani.

Mkuu labda tuelimishane kidogo kuhusu Software.


Software kwa lugha rahisi ni mfumo wa kompyuta ambao umeandikwa kwa lugha ambayo inaeleweka kwa kompyuta kwa ajili ya kuiambia kompyuta nini cha kufanya na kifanyike wakati gani.(kwa maneno yangu)
Kuna aina mbalimbali za software kutokana na vigezo vitakavyo tumika kuzigawa lakini aina mbili ndio zinazofahamika na kutumika zaidi nazo ni System Software na Application Software.


Kwa maelezo yako hapo juu unaongelea aina ya kwanza yani System Software ambazo zinajumuisha operating Systems kama Windows na Ubuntu.
Tukija aina ya pili, Application Software hizi zinatengenezwa kukidhi mahitaji ya sehemu husika kwa mfano hospitali wanaweza kuwa na Hospital Management System, Supermarket zinapatikana na katika ofisi mbali mbali. Aina hii ya Software tuna vijana wetu wa kitanzania wanatengeneza na mfano wa kampuni ni data vision, cats, dflex na nyinginezo kwa kiasi flani wahindi ndio walifungua milango katika kutengeneza hizi software.


Kwa maelezo hayo kwa kifupi nataka kumshauri mtoa mada kwamba 'impossible is nothing', watu wanafanya haya mambo naamini na wewe utaweza ukiamua.
 
Mkuu labda tuelimishane kidogo kuhusu Software.


Software kwa lugha rahisi ni mfumo wa kompyuta ambao umeandikwa kwa lugha ambayo inaeleweka kwa kompyuta kwa ajili ya kuiambia kompyuta nini cha kufanya na kifanyike wakati gani.(kwa maneno yangu)
Kuna aina mbalimbali za software kutokana na vigezo vitakavyo tumika kuzigawa lakini aina mbili ndio zinazofahamika na kutumika zaidi nazo ni System Software na Application Software.


Kwa maelezo yako hapo juu unaongelea aina ya kwanza yani System Software ambazo zinajumuisha operating Systems kama Windows na Ubuntu.
Tukija aina ya pili, Application Software hizi zinatengenezwa kukidhi mahitaji ya sehemu husika kwa mfano hospitali wanaweza kuwa na Hospital Management System, Supermarket zinapatikana na katika ofisi mbali mbali. Aina hii ya Software tuna vijana wetu wa kitanzania wanatengeneza na mfano wa kampuni ni data vision, cats, dflex na nyinginezo kwa kiasi flani wahindi ndio walifungua milango katika kutengeneza hizi software.


Kwa maelezo hayo kwa kifupi nataka kumshauri mtoa mada kwamba 'impossible is nothing', watu wanafanya haya mambo naamini na wewe utaweza ukiamua.


Uko sawa kwa asilimia 100 unachosema.
Lakini mkuu kumbuka kuwa hapa bongo wanachofanya ni Development tu siyo Creation ya software mfano hizo dflex ,data visio ni development tu !

Ebu tazama
1: Unasema datavision soma hapa
2:Unasema dflexsoma hapa
3:Unasema cats somahapa

hivyo kwa ufupi hakuna application software unayoweza kunieleza kuwa imekuwa created na wabongo labda kufanya developments.
labda nipatie elimu kwa kunitajia hiyo software.
 
Uko sawa kwa asilimia 100 unachosema.
Lakini mkuu kumbuka kuwa hapa bongo wanachofanya ni Development tu siyo Creation ya software...hivyo kwa ufupi hakuna application software unayoweza kunieleza kuwa imekuwa created na wabongo labda kufanya developments.
labda nipatie elimu kwa kunitajia hiyo software.
coming soon!
 
unahitaji kuanza na msingi na kuendelea. Shule itakusaidia kupata professional qualification, lakini sio guarantee utakuwa professional SE
 
Uko sawa kwa asilimia 100 unachosema.
Lakini mkuu kumbuka kuwa hapa bongo wanachofanya ni Development tu siyo Creation ya software mfano hizo dflex ,data visio ni development tu !

Ebu tazama
1: Unasema datavision soma hapa
2:Unasema dflexsoma hapa
3:Unasema cats somahapa

hivyo kwa ufupi hakuna application software unayoweza kunieleza kuwa imekuwa created na wabongo labda kufanya developments.
labda nipatie elimu kwa kunitajia hiyo software.

Umenichanganya kidogo.

unamaanisha development inayofanyika ni re-engineering tu na hamna new product au?

1. http://www.datavision.co.tz
2. http://www.dflex.co.tz
3. http://www.cats-net.com

 
Umenichanganya kidogo.

unamaanisha development inayofanyika ni re-engineering tu na hamna new product au?


1. www.datavision.co.tz
2. www.dflex.co.tz
3. www.cats-net.com


hizo link hakuna inayofunguka !

pili mkuu naona hatuelewani kabisa.ninachosema ni kuwa hizo unachosema kuwa zimetengenezwa Tz ni marekebisho tu yaani kama michuzi alivyokuwa akininunua nguo ulaya na kuzipeta Dar na kuzipiga chata ya KP basi. au kwenda kwani ukatengeneza nguo za chata yako.

au ku-repair tv basi hakuna jipya hapo
mfano hiyo cats unayosema ilitengenezwa mwaka 2004 kwa mjibu wa wikipedia soma maelezo haya

CATS (Computer Aided Transcription System) is an EDA software for mask data preparation (MDP) in integrated circuit design and manufacturing.

Originally it was developed by Transcription Enterprises, Ltd, acquired by Numerical Technologies, Inc. (2000), in its turn acquired by Synopsys, Inc. (2003).

As of 2004, it is an industry standard for MDP operations, such as mask fracturing and mask inspection.


Sasa wenzako wa dar wanaanzia hapo na kuingiza mautundu wakitumia ama notice au ujuzi na ujanja tu basi hakuna creation hapo mkuu

Jioni njema
 
Nafikiri nimekuelewa.

Kwanza hizo nilizotaja ni kampuni sio products.
Pili unachozungumzia ni kwamba huku wana customize tu product ambazo zimeshatengenezwa, hili lina ukweli ndani yake lakini kumbuka sio kila product itakidhi mahitaji ya mteja.

Zipo Software zinazotengenezwa hapahapa tatizo ni kwamba zinatengenezwa kwa mahitaji ya mteja husika hivyo haziwezi julikana kama inavyokuwa MS Office kwa mfano.

Sijakataa hoja yako lakini kwamba nyingi wanazi 'pimp' tu
 
coming soon!

Eagery waiting for HT software solutions.

Rutunga M. Mpe ndugu yako moyo kujua wapia aanze, mwenyewe atajipima kama kweli dream yake ya kuwa software developer inawezekana.
Pia sioni ajabu ya software kuwa configurable, kwani kuna njia nyingi tu za kudevelop software, a closed software au open software...
Kama mteja anahitaji kudevelop a given solution, developers wake wataangalia development environments ambazo zipo sokoni na kujua ni ipi/zipi zitaweza kutumika for the solution, hapo basi, huyu developer sio lazima aanze ukurasa wa kwanza kutengeneza the environment, na baadae ndio atengeneze software. Kutokuwepo na the "environment" as a solution iliyotengenezwa Tanzania sio hoja, kwani ki'biashara, haitii akili kuanza square one, katika hili. kutumia development framework/solution mbona is order of the day?!

Kweli Linux imetengenezwa South Africa, au na wenyewe wame-configure a linux variant into Ubuntu...?
 
No No.Haya mambo ya kutokupenda kuelezwa ukweli ndiyo yanayotuharibu wabongo,mnapenda maelezo matamu matamu ya kutia moyo wakati hali iko tofauti.

ninaposema kuwa kutengeneza software ni kazi NGUMUUUUUU sana na inabidi uwe mzuri sana katika lugha za computer.
Kama unabisha nitajie software 5 tu zilizotengenezwa na wabongo tangu kuumbwa kwa hii dunia na zinatum,iwa na nani.Je si kwamba wataalam wa ICT wanasoma kila kukicha? huo ndiyo ukweli hata kama unaumwa.

unaowaona humu na mikwara yao yoooooote,waambie kuhusu kutengeneza software watatoa maelezo mpaska mwakani.

Heshima yako ndugu Rutunga M,
Hakuna kinachoshindikana, tatizo ni watu wenye mawazo kama yako.. Kama havijawahi fanyika, haimaanishi havitafanyika.. Ingependeza kumshauri hatua anazotakiwa chukua..

Binafsi ni Programmer though bado ni medium programmer.. Wakati naanza kusoma Computer science, nilipata changamoto kadhaa, baada ya watu kunishauri kuwa Programming ni ngumu.. Kutokana na Syllabus ya chuo changu, kulikua na mambo ya Programming kibao.. Automatically nimejikuta nimeipenda Programming sana tena sana, kutokana na the way walimu wangu walivonifundisha, na interest niliyo nayo katika Programming.. Sio maeneo hayo tu, hata katika maeneo mengine ya System Analysis, System & Database design and Implementation..

Kuwa Best Programmer sio lazima uweze kutengeneza System softwares kama OS nk. Kuna mambo mengi yanaweza fanyika katika Programming..

Nilichokuja kukigundua katika Programming ni kwamba, inategemea na eneo husika la Programming.. Ila kitu cha msingi sana katika programming ni analytical,creative,Mathematics skills na Logic.. Especially kwenye designing and implementation of a system..

Pia tutambue kuwa, Programming zote zinahusiana.. Mfano ukiangalia Hardware Programming (Programming of Micro Processors), Games Programmings (C/C++ graphics), Robotics, Web Programming, Desktop apps Programming kuna vitu vinavyo bind hizi lugha pamoja... Logic za maeneo haya zinahusiana sana, cha msingi ni basic knowledge..

Dunia ya IT ya sasa, inajitahidi ku implement IDE's ili kuweza kuokoa muda wa ku code Programs (Component Technology, Pattern Technology) na pia sasa tuna-shift kwenda kwenye Distributed Network Objects (eg.. CORBA, etc).. Kwa hiyo ukiwa kwenye realtime, sio lazima uanze coding from the scratch.. IDE's zimetengenezwa, kwa ajili ya ku-implement kutengeneza softwares..

Programming is all about logic.. First, Believe kwambba Program flani inawezekana kutengenezwa... Kitachofata ni namna ya kufanya hicho kitu..

Kwa mtazamo wangu, Programmer wengi wa kibongo sio kwamba hawawezi kufanya mambo makubwa HAPANA, nasema HAPANA.. Shida yetu kubwa wengi tunasoma huku tukifikiria swala la ajira.. Unakuta mtu, anasoma huku akifikilia, je akimaliza shule yake ataweza kuwa placed katika kampuni itakayomlipa??

Kuna hizi wanazoziita Certifications kama (OCA,OCP,CCNA,CCNP) na nyingine kibao.. Kwa mtazamo wangu, zinachangia kwa namna moja nyingine kuua morali ya vijana katika maeneo kama haya ya Programming.. Kwa nini nasema hivi? Kampuni kama CISCO kwa sasa, wanaingiza pesa sana katika mitihani kama hiyo.. Ofcoz, kwa upande mwingine, hizi Certifications ni mhimu kwa sababu zinatumika kama Proof, ila kwa upande mwingine vijana wengine hawa concentrate kufanya vizuri katika maeneo yao kwa sababu wanawaza kufanya tu mitihani hii ili waweze pata kazi nzuri. Maana Kampuni nyingi zina imani kuwa mtu akiwa na certifications, ndio anafaa.. Binafsi sipingi Certifications, ila certification bila Ujuzi ni useless..

Wabongo wengi tunapenda maisha ya mkato katika mafanikio, so hatutaki kutumia skills zetu kufanya innovative activities, kwa sababu tunaona ni wastage of time.. Na hii ni kama nilivosema awali, wengi wanasoma ili wapate kazi, na si kusoma ili Ujue vitu.. But hakuna kinachoshindikana..

Kwa hiyo ndugu mwanzisha thread, kama u really like Programming, ni wewe tu.. Cha msingi jipime kwanza..

Jiulize maswali yafuatayo:

1. Do you have Analytical skills? au je waweza fundishika Analytical skills?
2. Do you have Creative skills? au je waweza fundishika Creative l skills?
3. Do you know Mathematics and Logics??
4. Je, unataka kusoma ili upate kazi(Kwa ajili ya kipato) au unasoma Ujue vitu??
 
vp kaka,if you have serious interest in programming go for it.their is nothing that hard about computers,they are slaves and you are the master.for starters i'll recommend you take up python or ruby programming languages they are quite simple and very powerful languages...usiogopeshwe...by the way i reckon they are softwares been developed/have been developed by tanzanians,this ratunga m guy knows nothing about software engineering...follow you heart
 
Programming is hard and those who persevere can become one!
 
Eagery waiting for HT software solutions.

Rutunga M. Mpe ndugu yako moyo kujua wapia aanze, mwenyewe atajipima kama kweli dream yake ya kuwa software developer inawezekana.
Pia sioni ajabu ya software kuwa configurable, kwani kuna njia nyingi tu za kudevelop software, a closed software au open software...
Kama mteja anahitaji kudevelop a given solution, developers wake wataangalia development environments ambazo zipo sokoni na kujua ni ipi/zipi zitaweza kutumika for the solution, hapo basi, huyu developer sio lazima aanze ukurasa wa kwanza kutengeneza the environment, na baadae ndio atengeneze software. Kutokuwepo na the "environment" as a solution iliyotengenezwa Tanzania sio hoja, kwani ki'biashara, haitii akili kuanza square one, katika hili. kutumia development framework/solution mbona is order of the day?!

Kweli Linux imetengenezwa South Africa, au na wenyewe wame-configure a linux variant into Ubuntu...?

I know you're patient because it takes a lot to release just a buggy alpha. so it comes! bttt, I believe all you need is passion, perseverence and swallow your pride so that you learn from others. and yes ubuntu is Linux distro
 
Back
Top Bottom