COCA-COLA wahujumu biashara ya PEPSI

MAMA POROJO

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
4,974
785
Dar es Salaam na mikoa mingi sasa hivi ni kipindi cha joto kali sana. Kama wewe ni mpenzi wa kinywaji baridi aina ya Pepsi na kwenye mizunguko yako ukaona sehemu wamepanga viti vya rangi nyekundu vya coca-cola, eneo hilo si salama hata kidogo kwa kinywaji cha Pepsi, kwa maana nyingine eneo hilo vinywaji hivyo ni marufuku kabisa kuuzwa.

Yapo maelezo kuwa baada ya kinywaji cha jamii ya coca-cola kukosa soko baada ya kuchakachua vinywaji vyao na vinywaji vya jamii ya pepsi kupendeka zaidi, kampuni ya coca-cola imeingia mkataba na wauzaji wengi wa rejareja kutokuuza vinywaji vya pepsi, na kila mwisho wa mwezi coca-cola wanakulipa fedha taslimu kama faida yako uliyokuwa ukiipata ulipokuwa unauza vinywaji vya pepsi, pamoja na kupewa viti, meza na firiji.

Sina hakika kama tume ya biashara huru wanayo taarifa kuhusu huu uhuni unaofanywa na kiwanda cha vinywaji baridi cha coca-cola,au pengine tume nayo imechakachuliwa na makaburu.
 
Wameanza mchezo wa TBL na SBL!!!

TBL nayo ipo chini ya utawala wa makaburu. Tume ya ushindani huru (jina la tume sina hakika kama nimelipatia au vipi) ilingilia kwa haraka na TBL walionywa kuheshimu biashara za washindani wao na walilipishwa faini kubwa.
 
TBL nayo ipo chini ya utawala wa makaburu. Tume ya ushindani huru (jina la tume sina hakika kama nimelipatia au vipi) ilingilia kwa haraka na TBL walionywa kuheshimu biashara za washindani wao na walilipishwa faini kubwa.

Inabidi na hii kesi ipelekwe hukohuko ili utata uondolewe..........badala ya kushindana kwa kutoa huduma na bidhaa nzuri wao wanaingiza mbinu zao za ajabu!
 
Actualy i cant comment on that b'se in economics sense this products are substitute meaning they both fulfil the same want,lakini kama coca wanafanya hii sio nzuri and they will never win the market kwasababu taste and preference za watu zinabaki palepale
 
pepsi ilivyo ya low quality, i cant buy that idea kwamba coca eti wanaihujumu pepsi! ile soda yenye ladha km magadi au lamba lamba au askirimu eti leo iipige bao the mighty COCA COLA. sijui labda uswazi huko lkn huku kwetu kwa wajanja coke inabamba kichizi
 
pepsi ilivyo ya low quality, i cant buy that idea kwamba coca eti wanaihujumu pepsi! ile soda yenye ladha km magadi au lamba lamba au askirimu eti leo iipige bao the mighty COCA COLA. sijui labda uswazi huko lkn huku kwetu kwa wajanja coke inabamba kichizi

Kumbe coca-cola wanatumia mamilioni ya pesa kuzuia mauzo ya pepsi ili watu wa uswazi wasiendelee kunywa magadi?
 
Majimoto:

Heading ya thread na contents haviwiani!

Andika vizuri ili tuweze kuelewa unachomaanisha
 
hili ni kweli kabisa mkuu, mmoja wa wapenzi wakubwa wa pepsi ni mimi na mara nyingi nikienda sehemu wameweka viti vya COCA COLA ukiuliza PEPSI unaambiwa hamna, sababu ni kwamba COCA wameweka viti na meza zao. lakini naona hii sio biashara nzuri, huwezi kumlazimisha mtu anywe kinywaji ambacho hakipendi. Kama soda yako haiuzi tafuta mbinu ili inunuliwe na sio kuzuia. Kuna siku moja nilikuwa kwenye hotel moja huko bagamoyo, nilikuwa nimelala kwenye kitanda karibu na bwawa la kuogelea. Mle ndani ya bwawa kulikuwa na jamaa wawili wanaoga, basi wakaja hadi pale nilipokuwepo mimi na kuniuliza mbona huna furaha, nikaambiwa nifuahi na nani wakati nipo alone, wakasema kwa sababu hunywi COCA na wakati huo nilikuwa nakunywa PEPSI. ndio niakjua kumbe haya majamaa ni mafanyakazi ya COCA. kwa kweli COCA hainyweki kabisa soko lake kwishney
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom