Clouds FM yasababisha Jide kutoshirikiana na wasanii wa Bongo

Ndi ndi ndi imehit Bila hata clouds kupigwa #Huu mchezo hauhitaji hasira.
 
HII STATION INAENDESHWA KITOTO SANA TANGU NAINZE KUSIKILIZA FM KESI ZA CLOUDS NI NYINGI SANA ZA KUNUNIANA ALOO PALE VP KUNA WANAUME KWELI? YANI WAO NI KUNIANA TU UKIKOSEA HIZO NDO DALILI ZA KUTANGULIZA MASLAHI MBELE SIO KUSAIDIA WATU ETI WANAJIITA REDIO YA WATU WAKATI WANANUNA BALAA BADO KUSUTANA NA MICHAMBO.
 
Hivi hawa anaye wapa jeuri ni nani...

Wana tabia za ajabu ,visasi,sifa za kijinga na
wamechangia sana kudumaza mziki kwa figisu zao.tatizo ni mmoja tu pale ...rug...
ila bi dada kesi yake pale ni tofauti na wengine!

Na ni kipimo kujua aliyempenda kweli ni yupi,huyu anae muandama kwa hasira ile au yule aliyekuja mla akamtapika.!
 
Kama tunavyojua ya kwamba Lady Jay dee komandoo hana mahusiano na redii clouds fm,sasa hali hiyo imefanya huyu dada hata nyimbo zake kutochezwa katika kituo hicho.

Kumbuka clouds washakuwa katika tafrani na wasanii kama Mapacha,Sugu,Rama dee n.k,lakini hao wote waliomba msamaha na walisamehewa na bado nyimbo zao hazichezwi pale wala hata interviews hawapewi wala nini! Sasa huyu dada nadhani anaona aibu kuomba radhi clouds fm kwa kuwa anajua hata akiomba msamaha bado hawatacheza nyimbo zake, kitendo cha Jide kugombana na clouds fm kimemfanya akose ushirikiano na wasanii wote wa tanzania na hico kujikuta hakuna msanii anaeomba kufanya collable na yeye.

Hii inatokana na kwamba wasanii wanaogopa endapo watamshirikisha hii maana yake nyimbo haitapigwa clouds fm na ndio redio kubwa Tanzania nzima,ukitaka wimbo wako uvume ni lazima udili na hawa majamaa,kazi ipo
ukubwa wa Clouds Fm utakuwa ndani kwako tu ..
 
Ni kweli kuwa Clouds fm ina nguvu kubwa kwa wasanii na hii ni kwa sababu inasimamia tasnia nzima ya music na sio tu kupiga nyimbo kama wengine.

Wanafanya promo, wanaandaa matamasha na pia deal nyingi za mziki za nje na ndani zinapitia kwao, hivyo wakiamua kumpandisha msanii watampandisha hata awe mbovu.

Pamoja na hayo zipo njia nyingine nje ya wao na Jide ni mkongwe hivyo anaweza kufanya mambo kama kawaida na wadau wengine na akawa safi.

JIDE NI PAKA MZEE HAWEZI KUPOTEA NJIA
 
Simkubali Jide kwa tabia zake za kulia lia na kulaumu wengine kwa matataizo yake, lakini hapa kwenye ndi ndi nimemkubali.

Naamini hata hao watangazaji clouds wanaisikiliza, alafu wakiingia ofisini "wanafuta midomo" bosi asijue.
 
Hao redio mawingu ndo wanaowanyonya hao wasanii wasiojitambua jide anajitambua ndiyo maana hataki shobo.
 
Hivi inamana hadi wafanyakazi wa clouds media group nao wana beef na Komando jide maana wamebana hadi kwenye brog zao kutoa link ya video ya NDI NDI NDI
 
Ni kweli kuwa Clouds fm ina nguvu kubwa kwa wasanii na hii ni kwa sababu inasimamia tasnia nzima ya music na sio tu kupiga nyimbo kama wengine.

Wanafanya promo, wanaandaa matamasha na pia deal nyingi za mziki za nje na ndani zinapitia kwao, hivyo wakiamua kumpandisha msanii watampandisha hata awe mbovu.

Pamoja na hayo zipo njia nyingine nje ya wao na Jide ni mkongwe hivyo anaweza kufanya mambo kama kawaida na wadau wengine na akawa safi.

JIDE NI PAKA MZEE HAWEZI KUPOTEA NJIA
Mkuu sikubaliani na wewe msanii hata wimbo akiwa na wimbo mbovu akipelekwa kwa hao mawingu atasikika !!!!!...... hapana huo uongo .

kuna jama zangu wawili wanamuziki wachanga wanatoka mbeya siku moja tulikuwa tunabishana kuhusu haya haya mambo ya muziki wakasema kwa Tz hao jamaa ni ndoo wachawi wa muziki wakiamua kitu ndoo wameamua kama wakikata wamekataa huwezi toka kamwe ....

Niliwabishia nikawaambia ukitoa wimbo mzuri lazima mashabiki wa ukubali kwanza ndoo wewe msanii ufahamike alafu uanze kula deal za matamasha ila ukitoa wimbo mbaya utahonga mpaka uchoke hausikiki hata kidogo, waliendelea kunibishia.

Nikaja kuachana na hao jama baada ya kuona ni wale wale wamekuwa brainwashed . Sasa ikafika zamu yao na wenyewe ni wasani inabidi waingie studio watoe wimbo wapeleke pale ...sikia kichekesho wale jamaa walipeleka wimbo pale mwaka 2012 waka honga wee mpaka wakachoka lakini wasikilizaji hawakuzipenda nyimbo zao. Baada ya kuona Ma dj na watangazaji wanawalia hela wakaamua kurudi kulima mbeya.
 
Mkuu sikubaliani na wewe msanii hata wimbo akiwa na wimbo mbovu akipelekwa kwa hao mawingu atasikika !!!!!...... hapana huo uongo .

kuna jama zangu wawili wanamuziki wachanga wanatoka mbeya siku moja tulikuwa tunabishana kuhusu haya haya mambo ya muziki wakasema kwa Tz hao jamaa ni ndoo wachawi wa muziki wakiamua kitu ndoo wameamua kama wakikata wamekataa huwezi toka kamwe ....

Niliwabishia nikawaambia ukitoa wimbo mzuri lazima mashabiki wa ukubali kwanza ndoo wewe msanii ufahamike alafu uanze kula deal za matamasha ila ukitoa wimbo mbaya utahonga mpaka uchoke hausikiki hata kidogo, waliendelea kunibishia.

Nikaja kuachana na hao jama baada ya kuona ni wale wale wamekuwa brainwashed . Sasa ikafika zamu yao na wenyewe ni wasani inabidi waingie studio watoe wimbo wapeleke pale ...sikia kichekesho wale jamaa walipeleka wimbo pale mwaka 2012 waka honga wee mpaka wakachoka lakini wasikilizaji hawakuzipenda nyimbo zao. Baada ya kuona Ma dj na watangazaji wanawalia hela wakaamua kurudi kulima mbeya.
Rudia kusoma post yangu, nimeandika wakiamua na sio wakihongwa
 
Hao redio mawingu ndo wanaowanyonya hao wasanii wasiojitambua jide anajitambua ndiyo maana hataki shobo.
Tatizo wasani wa Tanzania hawajitambui sijui Elimu ila kuna baadhi wanajitambua kama Sugu , Nature , Prof J na Jide.


Huwezi kuambiwa na kituo cha tv au redio" eti usishirikiane na mtu fulani ukikaidi sipigi wimbo wako au sikuandali matamasha ".

Hivi kwenye karne hii wewe msanii wa muziki unategemea kituo cha redio au tv au kikundi cha watu fulani wenye influnce wakuandalie show ????

Umetunga mashairi (hii nikazi kubwa mno) umepeleka studio ( hi pia ni kazi ngumu kwa sababu lazima prodyuza atulie ili kitu kikitoka kiwe kikali )

Haya sasa wimbo umetoka umesambaza redioni bahati nzuri wimbo wako ukapendwa na mashabiki sana mpaka ukawa namba moja kwenye chati za muziki za kila redio hapa nchini.

Haya sasa umefika steji hii unashindwa kujua nifanyeje ???


Watu wanausikia wimbo wako hawajawahi kukuona ......na wewe umebaki umeduwaa tu unasubiri kituo cha redio au tv kikuandalie show

Kazi ngumu zote umeziweza hiii nyepesi inakushindaa ????? Unashindwa kumtafuta meneja akafanya kazi hii mhhhh .

Basi ndoo maana wale jamaa wanawazuia kushirikiana na wanamuziki fulani kwa sababu wameona uzaifu wenu.

1.Elimu
2. Elimu
3. Elimu
 
clouds bana wameona dada wa watu kakomaa na anafanya powa mnakuja kuchek upepo wa mashabiki bado tunaiman nae akomae mtegemea cha nduguye hufa masikini.
kweli mkuu mleta uzi tumemshtukia ni kipele wa clouds,thumbs up lady jd komando...NDI NDI NDI
 
Mtoa mada umechelewa wapi? Siku hizi watu wanatumia Sana internet, kwahiyo hizi redio zipige zisipige muziki unawafikia watu popote walipo
kuhusu hilo la kujitangaza kwa njia ya internet nawapongeza sana wana hiphop one the incredible, songa,Nikki mbishi na wengineo kwa kuitumia fursa hiyo vizuri.
na hao wote nyimbo zao ni agharabu kusikia zinapigwa clouds radio.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom